01 August, 2015

KUELEKEA MCHEZO WA NGAO YA JAMII MOURINHO AMPA TANO TERRY

John TerryKocha wa Chelsea Jose Mourinho amemsifia beki wake John Terry kuwa ni beki bora wakati wa maandalizi kuelekea mchezo wa ngao ya jamii uatakaopigwa kesho.
Terry (34) alikuwa ni nguzo imara ya Chelsea wakati wa msimu uliomalizika akikiongoza kikosi hicho kutwaa ubingwa wa ligi ya England (EPL) kwa mara ya kwanza tangu walipofanya hivyo kwa mara ya mwisho mwaka 2010.
Ubora aliouonesha Terry ulimfanya atajwe kuwa kwenye kikosi cha PFA kwa msimu uliopita ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipotajwa kwenye kikosi hicho kwa mara ya mwisho msimu wa 2005-06.
“Nilipokuja, nilikuja na swali: Nitamkuta John wa aina gani? Atafanya nini? Ataimarika? Atamkaribia John yule ninaemfahamu mimi?” Mourinho aliuambia mtandao wa ESPN.
Kabla ya ujio wa Mourinho 2013, hatma ya Terry ilikuwa mashakani ndani ya Stamford Bridge na alikuwa na wakati mgumu wakati wa utawala wa Rafa Benitez.
Mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha England alianza kwenye mechi 24 kati ya 69 ambazo Chelsea ilicheza kwenye mashindano yote kwa msimu wa 2012-13. Mourinho akaongeza kuwa hakujua kuwa, ubora wa beki huyo ulikuwa uko mikononi mwake.
“Hususan kabla sijaja wakati wa kipindi cha Rafael Benitez nilidhani huyu mtu amekwisha kwasababu alikuwa hachezi mechi kubwa nikafikiri atakuwa kwenye matatizo”.
Chelsea wanaanza mapambano ya msimu mpya mwishoni mwa juma hili kwenye dimba la Wembley, wakati watakapopambana na Arsenal kuwania taji la kwanza la ngao ya jamii.
Chelsea imepata nafasi hiyo ya kucheza mchezo wa ngao ya jamii baada ya kushinda taji la ligi kuu ya England wakai Arsenal wao walishinda kombe la FA.

TUSIJIDANGANYE, HAKUNA FREE LUNCH DUNIANI

Mwanauchumi mashuhuri duniani, hayati Milton Friedman (1912-2006) aliwahi kusema kuwa hakuna kitu kama lanchi ya bure (there's no such thing as a free lunch). Ingawa hakuna uthibitisho kama Friedman ndio mtu wa kwanza duniani kutumia hiyo sentesi katika hotuba yake, watu wengi sana walimhusisha na huo usemi kwa muda mrefu wakati wa maisha yake. Milton mwenyewe aliwashangaza wasikilizaji wake wa taasisi ya CATO (CATO institute) nchini marekani (tarehe 6 May, 1993) aliposema kuwa vitu vizuri maishani vinapatikana bure (the best things in life are free). Hizi sentensi mbili zinapingana kwa kiasi fulani ingawa zinaelezea kitu kimoja. Si ajabu wanauchumi wengi duniani walipokea habari za kifo cha Friedman mwezi uliopita kwa masikitiko makubwa sana.
Tafadhali marafiki zangu wa-jamaa (socialists) msianze kubeza uamuzi wa kutumia mifano ya Friedman katika makala hii. Nimeamua kutumia hotuba za Friedman ambaye wengi wenu mnamuita bepari (capitalist), kwa sababu kubwa mbili. Kwanza, matokeo ya mechi kati ya ubepari na ujamaa ni kwamba mabepari wameshinda 5-2. Pili, watanzania wengi sasa wameutambua uongo wenu wa-jamaa kwa sababu ya mali za nchi mnazojilimbikizia kila siku huku mkituambia watanzania wenzenu tufunge mikanda. Friedman alifafanua usemi wake kwa kusema kuwa; hakuna mtu anayetumia pesa za mwenzake kwa makini zaidi ya anavyotumia pesa zake mwenyewe (nobody spends somebody else's money as carefully as he spends his own).
Ni ukweli uliothibitishwa sasa, hakuna kitu cha bure duniani. Hakuna chakula (lanchi) cha bure duniani. Kwa miaka mingi sasa nchi maskini za kiafrika zimekuwa zinapokea misaada kutoka kwa nchi tajiri duniani kwa ajili ya shughuli za maendeleo. Ukweli wa mambo unaonyesha kuwa misaada hiyo haijabadili hali zetu za maisha na badala yake siku hadi siku watanzania na waafrika kwa ujumla tunazidi kuwa masikini. Ninadhani kuwa ni wakati muafaka kwa waafrika kusoma tena hotuba za Friedman ili kutambua kuwa hakuna kitu kama lanchi ya bure. Hili lundo la misaada tunayoletewa sio ya bure kama wanavyoiita wafadhili wetu. Hizi lanchi za bure tunazopewa hazitasaidia kabisa juhudi zetu za kuondokana na umasikini. Wanauchumi wengi walishang'amua hili; hizi lanchi za bure zinatudumaza na zitatuponza milele.
Kama huamini hebu jiulize maswali yafuatayo. Karne nyingi zilizopita wakati wa mapinduzi ya viwanda (industrial revolution), ni misaada gani ya nje ambayo wazungu wa Ulaya walipokea ili kufanikisha mapinduzi hayo? Je ni fedha kiasi gani za kigeni benki ya dunia iliwapa wazungu waliohamia Amerika na Australia kujiendeleza? Ni misaada kiasi gani ilitakiwa ili kuwawezesha wazulu kujenga falme zenye nguvu kabla ya ukoloni? Je, wamisri walipokea mikopo kiasi gani ili kujenga mapiramidi? Majibu ya maswali yote hayo ni HAKUNA. Misaada ya nje inadumaza badala ya kuendeleza. Misaada inayoitwa ya bure inafanya watu kuwa wategemezi badala ya kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo. Misaada ya nje inawapa viongozi wetu nafasi ya kuifuja kwa sababu hakuna uhakika wa ni lini na ni wapi ilitolewa. Ukweli wa mambo ni kwamba; hakuna msaada wowote tunaopewa na hawa wanaojiita wafadhilli wetu. Hii ni njia mpya inayotumiwa na wanaojiita wafadhili wetu kutudumaza.
Tuseme ukweli; nchi za kiafrika hazihitaji misaada ya nje ili kuendelea au kutokana na umasikini. Nchi zetu hazihitaji mipango ya wafadhili na wakopeshaji ili kufanikiwa. Nchi zetu zinahitaji uhuru wa fikara (free minds) na juhudi zetu wenyewe badala ya lanchi za bure. Nitamnukuu tena Friedman hapa; ni kweli hapa duniani kuna lanchi ya bure, lanchi huru, lanchi isiyopimika, Lanchi yenyewe ni soko huria na vitu binafsi (in the real economic world, there is a free lunch, an extraordinary free lunch, and that free lunch is free markets and private properties). Sina nia ya kuchanganya madesa hapa (nikitumia lugha ya mlimani) kwa kuongelea soko huria na misaada ya nje katika makala moja. Nia kubwa hapa ni kusisitiza umuhimu wa kupunguza ushawishi wa nje (iwe wa serikali au wa wafadhili) katika kuleta maendeleo ya Afrika.
Watanzania na waafrika inabidi tujifunze kutoka katika historia ambayo inaonyesha kuwa maendeleo ya kweli ni yale yanayozalishwa ndani ya nchi na wananchi wenyewe. Maendeleo ya kweli yataletwa na sisi wenyewe na watoto wetu na wala sio wanauchumi wa Benki ya dunia na shirika la fedha-IMF. Misaada ya nje ni sumu ya maendeleo yetu na inatudumaza. Makala hii pia inawalenga wale vijana wanaokaa vijiweni bongo bila kazi huku wakilalamika kuwa serikali haijawasaidia. Hakuna hata siku moja serikali yetu itakuwa na pesa za kutosha za kumsaidia kila mmoja wetu awe tajiri. Ni wakati wa kujishughulisha wenyewe ili kujiletea maendeleo. Makala hii inawalenga baadhi ya viongozi serikalini wanaofuja mali zetu huku wakisingizia kuwa tuko masikini kwa sababu hatupati misaada ya kutosha kutoka nje. Tunaweza kupata na ni vizuri tukipata wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuleta ushindani wa kimaendeleo (nguvu ya soko huria). Lakini Kama tutakaa chini na kusubiri kupiga wafadhili virungu (kuomba lanchi za bure na misaada), basi tutazidi kuwa masikini milele zote.

“Kuacha Aina Ya Muziki Uliokutambulisha Unakuwa Haupo Loyal Kwa Mashabiki Wako” – Mansuli

man 
Msanii wa hip hop, “Kina kirefu” rapper Mansuli amefunguka na kusema kwamba msanii kuacha aina ya muziki uliokutambulisha wakati unaanza kufanya unakuwa haupo loyal kwa mashabiki wako unakuwa hauwatendei haki watu wako, ingawa kila mtu anakuwa na uhuru wa kufanya kitu ambacho anakipenda.
Mansu,I ni moja ya wasanii wanaofanya hip hop halisi, ameendelea kufanya hivyo toka alipoingia kwenye game, toka ngoma ya “Kina kirefu” ilipomtambulisha katika gemu, ameendelea kupewa heshima ndani ya gemu la hip hop.
Kwa sasa Mansulii amerudi rasmi baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu kutokana na masomo, leo Jumamosi ameachia ngoma mpya inayokwenda kwa jina la “Usiku Mmoja” feat Maulo, ngoma ambayo imefanywa na producer Pala kutoka Tatoo Records Masaki Dar es salaam.
Anafanya mipango ya kufanya video ya ngoma na mkali Director Hanscana, akiamini kwamba directors 1a Tanzania pia wao wanaweza, akiongelea kuhusu video kupigwa Tv za kimataifa kwa nyimbo za Kibongo amesema ni kitu kizuri.

Zama za ujasiriamali zilizoufukia ujamaa (MAKALA)

Nyerere2
Na FRANCIS MAWERE
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliamua kuanzisha mfumo wa kiuchumi wa Ujamaa na Kujitegemea miaka michache baada ya Tanganyika kujipatia uhuru wake.
  Kwa kufanya hivyo alikuwa ameamua kufuata mawazo ya akina Adam Smith, David Ricardo, Milton Friedman, Fredrich Hayek, Ayn Rand Robert Owen, Pierre Leroux na Karl Marx kwa kuwataja kwa uchache; ambao wanatajwa kama waasisi na watetezi wa Ujamaa.
Hii ni kwamba aliamua kusimama kinyume na mawazo ya ubepari ya akina  Stuart Mill, Albert Einstein, George Bernard Shaw, Leo Tolstoy na Emma Goldman ambao katika anga za uchumi wanaheshimika kuwa waasisi na watetezi wa ubepari.
Mwalimu Nyerere alitumia muda, akili na nguvu nyingi sana kuwasilisha na kuwashawishi Watanzania kuupokea na kuukubali Ujamaa na Kujitegemea.
Mambo hayakwenda vizuri katika pande mbili. Mosi, kutokana na hali ya uchumi wa kidunia na nafasi ya Ujamaa kwa wakati huo duniani; utekelezaji wa sera za Kijamaa ulikuwa ni wa kutoa jasho mno. Pili, Watanzania wengi waliupokea Ujamaa na Kujitegemea kwa shingo upande na wale walioupokea kwa moyo mweupe inaonekana hawakumuelewa vizuri Mwalimu Nyerere.
 Upande wa kwanza ni nafasi ya Ujamaa duniani wakati Mwalimu Nyerere alipokuwa anauleta Ujamaa uliokolezwa mapambo (Ujamaa na Kujitegemea) hapa Tanzania. Ukweli ni kwamba hadi kufika miaka ya 1950 tayari Ujamaa ulishakuwa kwenye hali mbaya ya kumalizikia kuanguka. Hii ina maana Mwalimu Nyerere alikuwa anajaribu “bahati” ya kuijenga Tanzania imara kiuchumi kwa kutumia mfumo wa uchumi ambao ulishakuwa katikati ya changamoto kali sana za kushindwa.

 Ushahidi wa kushindwa kwa Ujamaa katika miaka hiyo, tunaupata kutoka kwa mataifa ambayo tunaweza kuyaita waasisi na miamba wa Ujamaa duniani. Gazeti la Urusi liitwalo Pravda, Mei 1988 liliandika habari ya kitafiti kuhusu hali tete ya uchumi wa Umoja wa Nchi za Urusi (USSR) kutokana na kufuata sera za Ujamaa.
 Katika habari hiyo, Pravda ilithibitisha kuwa matarajio ya Wajamaa yanazidi kuyeyuka kutokana na matokeo mabaya kwenye uchumi. Kwa mfumo, ilielezwa kuwa kati ya sekta 170 zilizoainishwa kuboreshwa na Ujamaa wao hakukuwa hata na moja iliyofanikisha malengo walau kiasi cha kuridhisha. Gazeti hilo lilihitimisha kwa kusema kuwa mfumo wa Ujamaa ni sawa na machafuko yaliyokusudiwa.

 Si hivyo tu, bali nyuma kabisa hapo mwaka 1920 wakati wa utawala wa Lenins Bolsheviks kule Urusi, tayari wanauchumi wengi akiwamo mwanauchumi wa Kiaustralia, Ludwig von Mises, walieleza kwa kina kuwa Ujamaa ulishakuwa umeanguka.
 Kwenye machapisho yake mawili maarufu sana, Economic Calculation in the Socialist Commonwealth  na Socialism, An Economic and Sociological Analysis, Mises anasema kuwa kutokana na tabia, tamaduni, mazoea na asili ya mwanadamu; kufanikisha Ujamaa ni sawa na kutengeneza sanamu kisha kutaka uipe uhai.

 Tunafahamu kuwa vita kubwa ya wafuasi wa Ujamaa na wale wa ubepari chimbuko lake kubwa ni mgawanyo wa rasilimali zilizopo katikati ya wanajamii. Ubapari wenyewe unasifa ya kuruhusu watu binafsi kuendesha uchumi kwa watu binafsi kumiliki njia kuu za uzalishaji.
 Kwenye ubepari, serikali inatakiwa kubaki kama mwangalizi tu na inapaswa kuliacha soko kuamua. Wakati Ujamaa wenyewe unasisitiza kuwa njia kuu za uchumi ni lazima zimilikiwe kwa pamoja na serikali iwe na mamlaka kamili ya kuingilia chochote katika mwenendo wa kiuchumi.
 Hapa ndipo penye kasheshe kubwa. Wale wapinzani wa Ujamaa huwa wanaenda mbali na kumnanga Karl Marx na kusema kuwa hakuwa na sababu za kiuchumi kuasisi Ujamaa. Marx yeye aliona kuwa ubepari ulikuwa ukilinyonya tabaka la wafanyakazi hivyo alipofikiria Ujamaa alisema utakuwa ni mfumo ambao utamlipa kila mtu kwa kadiri ya anavyofanya kazi.

Pengine tuanzie hapa kuutazama Ujamaa wa Mwalimu Nyerere hasa tukiangalia ule upande wa pili wa namna ambavyo ulipokewa kwa shingo upande na namna ambavyo haukueleweka. Mwalimu Nyerere alipoibuka na mfumo wa Ujamaa aliuongezea viungo kwa kuuita “Ujamaa na Kujitegemea”, lengo lake lilikuwa ni kuona Tanzania kama taifa likisimama na kumudu mahitaji yake na ya watu wake pasipo kutegemea fadhila, kuombaomba ama misaada.

Yakafanyika mambo mengi lakini makubwa mawili ni kuanzishwa kwa Vijiji vya Ujamaa na kutaifishwa kwa mali binafsi kuwa za umma. Nia ilikuwa nzuri lakini matokeo ya hatua hizi mbili hayakuwa mazuri pengine kwa sababu wananchi hawakuuelewa vema huu Ujamaa na Kujitegemea.
Kutokana na hili, maelfu ya wananchi hasa wale waliohamishwa makazi, waliopoteza mifugo yao, waliotakiwa kuacha mashamba na mazao yao na kwenda kwenye vijiji vya ugenini waliuchukia Ujamaa na Kujitegemea katika hatua za awali kabisa. Hata ubinafsishaji wa mali binafsi zikiwamo hospitali, shule, viwanda, kampuni na mashirika ulileta kizaazaa kwa sababu wamiliki wake walikuwa na wafuasi wengi na kama hawakuridhika basi na wafuasi wao waliuchukia Ujamaa na Kujitegemea ungali unaanza.

Pamoja na hilo inaonekana wananchi walioupokea Ujamaa na Kujitegemea walielewa kipengele kimoja tu cha Ujamaa lakini hiki cha Kujitegemea inaonekana hakikueleweka kabisa. Ili useme taifa linajitegemea ina maana kuwa wananchi wanajitegemea. Kwenye Ujamaa na Kujitegemea serikali ilihodhi njia kuu za uchumi na miundombinu ya kijamii, huku wananchi wakibaki kufanya kazi “kijamaa”.
 Suala hili lilisababisha wananchi wengi kama si wote kuitegemea serikali kwa mambo mengi ikiwamo upatikanaji wa elimu, huduma za afya, miundombinu na mengineyo. Serikali iliendelea kufurukuta kuwapa wananchi bure huduma za kijamii hadi ikafika mahali ikajikuta haina ujanja tena. Ndipo pale mahali Mwalimu Nyerere alipoamua kung’atuka na ghafla bin vuu nchi ikawa haina ujanja zaidi ya kujisalimisha kwenye makucha ya Benki ya Dunia (WB) na Shirika na Fedha (IMF).
 Ilikuwaje Taifa la Ujamaa na Kujitegemea likashindwa kujitegemea? Jibu ni rahisi. Ni kwa sababu wananchi wake katika ngazi ya mtu mmoja mmoja walikuwa hawajitegemei. Badala yake walikuwa wakiitegemea Serikali kwa kila kitu. Jambo hili halikutokea kwa bahati mbaya na wala halikutokana na ubovu wa uongozi wa Mwalimu Nyerere, isipokuwa una chimbuko lake kutoka katika saikolojia na tabia za kibinadamu kama alivyosema mwanauchumi Mises.

Kosa kubwa lililofanyika katika mfumo wa Ujamaa na Kujitegemea ilikuwa ni kutafuta usawa wa kijamii na kiuchumi kwa watu wote. Kiasili kila mwanadamu ameumbwa tofauti na kupewa upeo, vipawa, karama, uwezo, matarajio na maono yanayotofautiana. Tena kiasili mwanadamu hutafuta kuwa tofauti, kufanya lile alipendalo na kutambuliwa na kujulikana kwa yale ayafanyayo.
Hapa kwenye karama, maono, vipawa ndipo mahali ambapo humuwezesha mwanadamu kusoma mazingira yake, kuangalia matatizo yaliyopo na kuyatafutia ufumbuzi kwa kutumia karama, vipawa, maono na uwezo wake. Namna hii ya utatuzi wa matatizo na changamoto ndiyo msingi na chimbuko la ujasiriamali (Intrinsic Entrepreneurship).

 Mchumi na mwanasaikolojia wa kale, John Stuart Mill, katika kitabu chake cha Principles of Political Economy (1848) anasema, “Ukimlazimisha mwanadamu awe sawa na wengine, afanye kila kitu kwa kuamuliwa na mamlaka, basi atakuwa na hulka zifuatazo: Atakuwa mtu anayefanya mambo nusunusu (passive), hatafanya mambo makubwa zaidi ya yale wanayofanya wenzake hata kama ana uwezo na kubwa kabisa hataona umaana wa kujipambanua katika kazi kwa sababu iwe atafanya sana ama atafanya kidogo, maslahi anapata yale yale.”
Hapa ndipo mahali Ujamaa na Kujitegemea ulipoua vipawa vingi vya kijasiriamali. Wafanyakazi hawakuona umuhimu wa kufanya zaidi, wananchi hawakuwa na sababu ya kufanya zaidi kwa sababu Serikali ilitoa kila kitu na vile vile ilikuwa na utaratibu unaobana unapotaka kufanya biashara. Mathalani, ule mtindo wa kumbana mtu na kutaka ajieleze namna alivyofanikiwa hata akajenga nyumba ama kununua kitu cha thamani ulizalisha woga miongoni mwa Watanzania wengi.
 Kivuli cha woga ule kinatutafuna hadi sasa, ndiyo maana nchi hii mtu anapofanikiwa kiuchumi watu hawamuamini, wanamtilia shaka; eidha watasema ni fisadi ama ni mshirikina ama ni mwizi. Ujamaa na Kujitegemea ingawa haukuandika katika maandishi ya sera zake, lakini ulihesabu mtu kuwa na utajiri kama “dhambi na unyonyaji”.

 Kule Magharibi walianza kutumia msamiati wa ujasiriamali miaka ya 1700! Sisi Tanzania msamiati huu ndiyo kwanza unavuma miaka hii ya 2000. Dhana ya ujasiriamali iliasisiwa na ubepari. Tulipokuwa tunacheza ngoma ya Ujamaa na Kujitegemea tuliuita ubepari ni unyama. Kwa lugha nyepesi ni kuwa Ujamaa na Kujitegemea ulipenyeza imani vichwani mwa Watanzania; ya kuamini kuwa “ujasiriamali ni unyama”.
 Hili tunaweza kulithibitisha kwa kutazama kile ambacho Watanzania tunafahamu kuhusu ujasiriamali. Wengi wa Watanzania bado wanashangaa-shangaa, wanasikiasikia tu lakini wanahisi kuwa ujasiriamali si kitu kinachowahusu. Jirani zetu Wakenya ambao wamekuwa wabepari nyakati zote; hadi watoto wa shule za msingi wananunua hisa katika soko lao la hisa Nairobi. Sisi hapa Tanzania wasomi wetu wanahitimu vyuo vikuu hawajui hata ABC hisa achilia mbali uwezo wa kutumia maarifa waliyopata kujiajiri.

 Nihitimishe kwa kusema kuwa kushindwa kwa Ujamaa na Kujitegemea hakuwezi kuhesabiwa moja kwa moja kama ni kushindwa kwa Mwalimu Nyerere; kwa sababu Ujamaa ulishakuwa umeshindwa kabla hata Mwalimu Nyerere hajabuni Ujamaa na Kujitegemea.
Wachumi wanatuthibitishia kuwa miundombinu ya Ujamaa ndiyo chimbuko la kuanguka kwake. Na moja ya sababu za kudondoka kwa viwanda na mashirika mengi ya umma ilikuwa ni kushindwa kuzalisha kwa kuangalia mahitaji na matakwa ya watumiaji (soko).
Watanzania tunahitaji ushindi wa kiuchumi tunapoendelea kumuenzi Mwalimu

NEW: MAKOMANDO FT. M- RAP – TANZANIA (OFFICIAL MUSIC)

MAKOmandoKundi moja la wasanii wa muziki hapa Tz maarufu kwa jina la ‘Makomando’ ambao wanafanya vizuri kwenye muziki wa Bongo fleva, kwa sasa wamekuletea ngoma nyingine ambayo wamemshirikisha rapper M-rap inaitwa ‘Tanzania’ imetengezwa katika studio ya Uprise Music chini ya mikono ya Producer ‘Dupy’

MAN U YATAMBULISHA UZI MPYA ULIOVUNJA REKODI YA ‘MKWANJA’ DUNIANI

Manchester KitManchester United imekuwa miongoni mwa klabu ambazo zimetambulisha jei zao zitakazotumiwa kwa ajili ya msimu ujao. Klabu hiyo imevunja rekodi kwa kuwa ni klabu inayopiga pesa nyingi duniani kutoka kwa watengezaji wa jezi ambapo jezi zao zitakuwa zikitengenezwa na kampuni ya Adidas baada ya kusaini dili la pauni milioni 750.
Kabla ya Adidas Nike ndio walikuwa watengenezaji wa jezi za mashetani wekundu na wamedumu kwa muda wa miaka 13 kabla ya Adidas kuchukua dili hilo baada ya mkataba wa Nike na Man U kumalizika.
Wakongwe hao (Adidas) wa kutengeneza vifaa vya michezo wanaamini wnaweza kutengeneza kiasi cha pauni bilioni 1.5 kutokana na mauzo ya jezi za Man U kwa muda wa miaka 10 ijayo.
Dili hilo kati ya Manchester United na Adidas linayapiku madili mengine ya klabu ambazo zinatengenezewa jezi na kampuni hiyo ikiwa ni pamoja na klabu Bayern Munich (pauni milioni 645) na Chelsea (pauni milioni 300).
Jezi hizo mpya zitakuwa na muonekano kama ule wa zamani enzi za Ryan Giggs zikiwa na shingo ya V yenye rangi nyeupe na michirizi mitatu kwenye mikono yake.
Manchester Kit 1

KING OF DISTRESSED JEANS :KANYE WEST

kanye2
Kanye ni mvaaji mzuri wa distressed jeans na sio distressed jeans tu hata t shirt zake huwa zina matb ya risasi au zimechanwa basi kaazii mradi tu awe tofauti.
kanye3
Kama huu mshati umechanwa mikononi na kukunjwa but ni swaggger,Hizi sneakers ni yeye kadesign akishirikiana na Adidas zaitwa yeezy boost
kanye5
k kaanye KANYE333 KANYE8478

Jul 26, 2015; Toronto, Ontario, CAN; Recording artist Kanye West performs during the closing ceremony for the 2015 Pan Am Games at Pan Am Ceremonies Venue. Mandatory Credit: Matt Detrich-USA TODAY Sports *** Please Use Credit from Credit Field ***

HUYU NDIO ROONEY UNAEMJUA WEWE…ANGALIA PICHA ZAKE NYINGINE AKIWA BADO KINDA

Wayne Rooney enzi za utoto wake

Wayne Rooney ni mchezaji wa Manchester United mwenye heshima kubwa kwenye klabu yake, taifa lake na dunia kwa ujumla kutokana na uwezo wake mkubwa awapo uwanjani.
Kutoka kushoto: John Rooney (7), Graeme Rooney (10) na Wayne Rooney (12)
Kutoka kushoto: John Rooney (7), Graeme Rooney (10) na Wayne Rooney (12)
Leo nimekuwekea picha kadhaa za Rooney wakati akiwa mdogo, kumbe huyu jamaa na yeye ni kama wachezaji wengine wenye majina makubwa duniani, alianza kucheza mpira akiwa na umri mdogo sana na kitu cha kufurahisha ni kwamba wadogozake pia walikuwa wanacheza mpira japo hawakufanikiwa kuvuma duniani kama yeye.
Wayne Rooney wakati akiwa na umri wa miaka 10
Wayne Rooney wakati akiwa na umri wa miaka 10
Duncan Ferguson akimkabidhi Wayne Rooney kitambaa cha unahodha wakati anatoka nje ya uwanja
Duncan Ferguson akimkabidhi Wayne Rooney kitambaa cha unahodha wakati anatoka nje ya uwanja

Linah ‘No Stress’ (Video)

linahMawa dada LINAH SANGA leo hii katuletea Kideo chake kipya  ‘No Stress’ Alichokifanya na Godfather ndani ya South Africa na hii itakuwa ni video ya pili ya Linah kutengenezwa chini ya usimamizi wa Godfather, Ole Themba ilikuwa ni video ya kwanza ya Linah kusimamiwa na Director huyo mwenye heshima kubwa kwenye kazi yake Africa.LINAH BABEchkua time yako murua kukitazama Kideo hicho cha ‘No Stress’ kutoka kwa ndege MNANA LINAH. Bonyeza PLAY kukitazama

31 July, 2015

Ben Pol kufanya collabo na Jason Derulo kutoka Marekani

Mfalme wa R&B Tanzania, Benard Michael Paul a.k.a Ben Pol ameweka wazi mipango yake ya kuupeleka muziki wake kimataifa kwa kutafuta collabo na wasanii wakubwa wa kimataifa.

Ben Pol ambaye kwa sasa yuko nchini Kenya alikoenda kushiriki kwenye msimu mpya wa kipindi cha Coke Studio Africa, amesema kuwa miongoni mwa wasanii ambao anategemea kufanya nao collabo ni pamoja na hit maker wa “Wiggle”, Jason Derulo kutoka Marekani.

Hit maker wa “Sophia” ameweka wazi mpango huo alipokuwa katika session ya kuulizwa maswali na mashabiki kupitia ukurasa wa Facebook wa Coca Cola.

Shabiki alimuuliza Ben pol endapo akipata nafasi ya kuchangua msanii wa kufanya naye collabo wa kimataifa atamchagua nani?

“Kwa sasa nafikiria kufanya collabo na Jason Derulo, kwa sababu ni msanii mchapakazi na anayezidi kukua na kuvuka mipaka siku hadi siku, Menejimenti yangu inaendelea kumtafuta, natumai tutafanikiwa.” alijibu Ben Pol.

Hadi sasa Ben Pol tayari amefanya collabo na Nameless na Rabbit wa Kenya.

Hii ndio taarifa kamili ya BASATA kuhusu kumfungia shilole mwaka mmoja kutojihusisha na kazi za sanaa


Balaza la sanaa Tanzania (BASATA) limetangaza kumfungia mwanamziki wa Kike shilole kutojihusisha na kazi za sanaa kwa mwaka mmoja ndani na nje ya nchi.  Adhabu hii imetolewa kufuatia shilole kupigwa picha za aibu wakati akitumbuiza nchini ubeligij mname tarehe 09/05/2015 .
“Tarehe 9 May 2015 ukiwa katika onyesho lako la muziki Ubelgiji ulicheza uchi mbele ya hadhira ya wapenda sanaa za Tanzania hivyo kudhalilisha utu wako na jamii ya kitanzania kimaadili
BASATA ilipata habari zako, kumbuka pia October 2013 BASATA lilikuonya na ukakiri kwa kuomba msamaha tabia yako ya kucheza bila kuzingatia maadili uwapo jukwaani, BASATA ilikupa nafasi ya kutoa maelezo kwanini usichukuliwe hatua za kinidhamu kwa kitendo chako lakini umekaidi kutoa maelezo yako
Baraza limejiridhisha kwamba ulikiuka maadili ya kazi ya sanaa kwenye onyesho lako huko Ubelgiji makusudi na umekiuka sheria kwenye ibara ya 30 (2) ya katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kwa kuvunja maadili ya jamii ya Mtanzania hivyo baraza linakusimamisha kujishughulisha na kazi za sanaa nchini na nje ya nchi kwa mwaka mmoja, kufanya kinyume na hayo kutapelekea kupewa adhabu zaidi pamoja na yeyote utakaeshirikiana nae”
Hii ndio barua yao

Hii ni moja ya picha zilizomponza shilole Shilole 2

HII NI STORI MPYA KUHUSU ANGEL DI MARIA

di-maria-manchester
Kimsingi kuna stori nyingi sana kuhusu dili la Angel Di Maria kujiunga na PSG kutokea Manchester United, lakini leo kuna jipya limeibuka.
Kwa mujibu wa Gazeti la  L’Equipe dili h ilo limeshakamilika na nyota huyo wa zamani wa Real Madrid anakaribia kuthibitishwa kusajiliwa.
Ingawa ada ya uhamisho bado haijathibitishwa, inafahamika kwamba United hawataweza kufikia mzigo waliotumia kumnunua wa paundi milioni 59.7 majira ya kiangazi mwaka jana.

OLYMPIC GAMES: NI BEIJING TENA 2022

001ec94a26ba0a1c636309
Wakati Urusi ikijiandaa kuandaa mashindano ya kombe la dunia mwaka
2018, marafiki wa Urusi kisiasa nchi ya China, imechaguliwa kuandaa
mashindano mengine makubwa duniani ya Olympic mwaka 2022. Jiji la
Beijing ndio limechaguliwa kuandaa mashindano hayo kwa mara nyingine
tena kwani mwaka 2008 pia walipata nafasi hiyo.
Beijing itafanya hivyo kwa mara nyingine huku ikiwa ya kwanza kuandaa
mashindano hayo nyakati zote mbili {majira ya baridi na kiangazi}.
Beijing ililishinda jiji la Almaty la nchini Kazakhstan.
Mashindano ya Olympic yaliyopita nchini china yalilaumiwa kutokana na
hali ya hewa kutokuwa nzuri, hata hivyo kamati ya maandalizi ya
michuano hiyo imedai mashindano yajayo yatakuwa bora Zaidi pengine
kuliko mashindano yoyote yaliyo wahi kufanyika.
Beijing ilipata kura 44 dhidi yakura 40 za Almaty, Thomas Bach rais wa
kamati ya Olympic alitangaza matokeo hayo mapema leo Ijumaa.

Global Fashion News- Cindy Crawford to debut new Fashion Show, Kyle and Kendall Jenner to launch new Shoe collection

The 80's model sensation, Cindy Crawford is about to debut her new TV Show on modeling, which will show the modelling wars in the ’80s between Ford Modelling Agency and Elite Model Management. Are you as excites as we are?! The show is called The Icon!

In other news, the Jenner/Kardashian girls are set to launch their new shoe collection.
Kyle and Kendall Jenner have teased us with the below monochrome set, which shows platforms and a range of strap-shoes which are part of their new Shoe collection
What do you think?

30 July, 2015

Download na sikiliza wimbo mpya wa mpiganaji Edu Boy Ft Baraka’Ni Wewe’.

edu+boyyyyyHuu imbo mpya wa Rapa Edu Boy Ft Baraka ‘Ni Wewe’ Download na usikilize hapa

Mshindi wa airtel trace “Mayunga” kwa mara kwanza video yake kutambulishwa Trace

Aliekua mshindi wa aitel Trace mwaka 2015 Mayunga kutoka Tanzania ameanza vizuri kwani siku ya ijumaa kituo kikubwa cha kimataifa “Trace” itazindua video yake aliyo ishoot South Africa.
Mayunga-trace

Tiwa Savage azawadiwa Microphone ya thahabu na almasi

Mbunifu wa mapambo Nigeria Micheal Awujola Aka Malivelihood amemzawadia Tiwa Savage Microphone iliyopambwa na thahabu na almasi ikiwa na jina la TIWA.
Hii ni zawadi ya Tiwa kwa kujifungua hivi karibuni na alifahamisha mashabiki wake kwa kuandika “Malivelihood Custom made Gold Sennheiser Microphone with Diamond Sleeve for the Mavin First Lady. Congratulations on the new born #Gold #Diamond #malivelihood.”
Wasani wengi waliowahi kupewa zawadi na mbunifu huyu ni Annie Idibia, Wizkid na Rahama Babangida .Tiwa-Savage1

New Video: Hemedy PHD – Imebaki Story

papiiiMoja kati ya video ambazo Hemedy PHD ukimuuliza alizo ingia gharama zaidi ni hii hapa.Cha kwanza video imefanyika mikoa mitatu na maeneo tofauti pia hata vifaa ni vingi zaidi tofauti na video za mwanzo.Video imeongozwa na Msafiri Musaa wa Kwetu studio ITAZAME HAPA

KALI: “ANGEL DI MARIA AMEPOTEA, ATAYEMPATA KUZAWADIWA £30

angel-di-maria
Nyota aliyevunja rekodi ya usajili ya Manchester United, Angel Di Maria anaonekana kukaribia kujiunga na PSG.
Winga huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 27 hakuwepo katika kikosi cha Man United kilichofanya ziara ya maandalizi ya msimu mpya nchini Marekani, huku Louis van Gaal akidai kwamba hajui lolote kuhusu alipo Di Maria.
Van Gaal alizungumza hayo na waandishi wa habari baada ya United kufungwa 2-0 na PSG alfajiri ya leo.
Mwandishi wa talkSPORT,  Alan Brazil ameleta kali baada ya ku-post tangazo huko Manchester akitangaza kumtafuta Di Maria akitania kwamba amepotea.
Jamaa huyo amesema atakayemuona Di Maria popote pale alipo ampigie simu Van Gaal kwa namba inayoonekana pichani chini na atapewa zawadi ya paundi milioni 30.

UZI MPYA WA SIMBA SC WATOKA KWA KASI….

simba-sports-club-231-768x403
Jezi za Simba zimeanza kuuzwa rasmi leo tarehe 30 – 7 – 2015 kwa mashabiki na wapenzi wa klabu ya hiyo na wapenda mpira wa soka wote Tanzania.
Kama walivyoahidi simbasports.co.tz imewapatia zawadi mashabiki wa Simba wawili wa kwanza kununua jezi hizo, ambapo washindi ni Fabiani Mayenga na Amina Hussein.
Simbasports.co.tz ilifanya mahojiano na mmoja wa washindi, Fabiani Mayenga na kusema “najisikia vizuri sana kwa kuwa ndani ya klabu inayonijali sana, leo hapa nimekuja kununua uzi mpya wa Simba na kupewa zawadi hakika nimefurahi sana na ninaishukuru klabu yangu kwa kutujali wapenzi wake “.
Mayenga pia amewataka wapenzi na mashabiki wa Simba kujitokeza mapema kununua jezi kwa TSH 15,000 ili nao waweze kuichangia klabu yao kwani kununua jezi hizo na kuongeza mapato kwa klabu tofauti na awali ambapo klabu ilikuwa haifaidiki na jezi feki.
Kwa wakazi wa Dar es Salaam wanaweza kupata jezi hizi makao makuu ya Simba pamoja na kwenye maduka ya Uhl Sports yaliopo mtaa wa Sinza na Jamhuri, kwa wakazi wa mikoani kwa sasa wanaweza kupata jezi hizi kupitia kwenye duka mtandao la Jumia www.jumia.co.tz .
Simbasports.co.tz itaendelea kutoa Jezi pamoja au tiketi ya VIP bure kwa wateja wawili wa kwanza kwenda kushuhudia mechi zitakazochezwa siku ya Simba Day tarehe 8 – 8 – 2015.

29 July, 2015

Chege Chigunda amezungumza haya kuhusiana na kupost picha za mpenzi kwenye mitandao ya kijamii

Wapenzi wengi kwa sasa wanaamini juu ya suala la kuwekwa au ku post picha ya mpenzi wake kwenye account yake ya Instagram, Facebook au DP kwenye Whatsapp kuwa ndio kupendwa na kuamini kuwa hakuna mwingine zaidi yake.

Kwa msanii Chege Chigunda yeye alikuwa na mtazamo wake pale alio hojiwa na T-Bway 360 kwenye show ya 5Selekt kinacho rushwa na EATV kila siku ya Jumatatu hadi Ijumaa saa 10 Jioni hadi saa 12 Jioni baada ya kuobwa achangie hoja 'Je kuna umuhimu wa ku post picha ya mpenzi wako kwenye mtandao wa kijamii?'.

Chege alisema kuweka au ku post picha ya mpenzi wako kwenye account yako sio kuonyesha mapenzi japokuwa inaweza kuongeza mapenzi. Kwake yeye amesema anweza hata ku post mara moja kwa mwaka au zaidi ila ni kutokana na vile atakavyo jisikia na sio kwamba ndio itaonyesha mapenzi yake ya dhati kwa mpenzi wake.

Chege Chigunda pia amezungumzia kuhusiana na shughuli zake za kimuziki kwa sasa na kuwataka Watanzania kuakaa tayari kwa ngoma zake mbili ambapo moja kaifanya na msanii wa Afrika Kusini na nyingine kaifanya na msanii wa Nigeria.

Chege ni moja wa wasanii ambao wametuza heshima yao kwa muda kwakuto sikika kwenye skendo mbaya nakusababisha heshima ya muziki wake kuzidi kusimama vyema.

MANULA AIPELEKA AZAM FC NUSUFAINALI KAGAME CUP

Wachezaji wa Azam FC wakimpongeza golipa wao Aishi Manula baada ya kudaka penati iliyopigwa na Hajji Mwinyi na kuivusha timu yake hadi kwenye hatiua ya nusu fainali ya Kagame
Timu Azam FC ‘Wanalambalamba’ wamefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mihuano ya Kagame baada ya kuitupa nje ya mashindano timu ya Yanga kwenye mchezo war obo fainali uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa.
Timu hizo zililazimika kufika hadi kwenye hatua ya mikwaju ya penati kufuatia kumalizika kwa mchezo huku timu hizo zikiwa sare ya bila kufungana. Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya Kagame,hatua ya robo fainali inapomalizika ndani ya dakika 90 bila imu kufungana zinakwenda moja kwa moja kwenye changamoto ya mikwaju ya penati.
Aishi mManula alipangua penati ya Haji Mwinyi ambayo ilikuwa ni penati ya tatu kwa upande wa Yanga na kufanikiwa kuivusha timu yake hadi kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Kipre Tchetche, John Bocco, Himid Mao, Pascal Wawa na Agrey Morris walifunga mikwaju yao kwa upande wa Azam wakati Salum Telela, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Godfrey Mwashiuya walifunga penati zao huku Hajji Mwinyi yeye penati yake ikidakwa na mlinda mlango wa Azam FC Aishi Manula.
Mpira ulianza kwa kasi sana dakika za mwazo za kipindi cha kwanza, huku Azam wakifanya shambulizi kali dakika hiyohiyo ya kwanza ambapo Kipre Tchethe alishindwa kufunga goli baada ya….kupiga krosi iliyowapita walinzi wa Yanga na kumkuta yeye ambae aliukosa mpira.
Azam hawakuishia hapo waliendelea kufanya mashambulizi lakini wachezaji wa Azam hawakuwa makini kwani hadi kipindi cha kwanza kinamalizika walikuwa wamekosa takribani nafasi nne za kufunga.
Kwa upande wa Yanga, kipindi cha kwanza hakikuwa kizuri sana kwao kwasababu hawakufanya mashambulizi mengi ambayo yaliwashtua Azam. Shambulizi lililofanywa na Yanga lilitokana na mpira wa kurusha ambapo Mbuyu Twite alirusha mpira uliookolewa kwenye mwamba wa pembeni wa goli na mlinda mlango Aishi Manula.
Wachezaji wa Azam walikuwa wakitumia nguvu nyingi sana kuwakaba wachezaji wa Yanga hali ilyopelekea mwamuzi kuwatuliza kwa kuwapa kadi za njano. Kheri Abdullah Salum, Frank Domayo, Jean Mugiraneza  na Ame Ally walioneshwa kadi za baada ya kuwachezea vibaya wachezaji wa Yanga. Wakati kwa upande wa Yanga Juma Abdul na Mbuyu Twite walioneshwa kadi za njano.
Kipindi cha pili kianza kwa Azam kufanya mabadiliko kwa kumtoa Kreri Abdullah Salum na nafasi yake ikachukuiwa na Said Morad wakati Frank Domayo ‘Chumvi’ alipumzishwa na nafasi yake kuchukuliwa na Ame Ally ‘Zungu’. Yanga wao wakamuingiza Salum Telela kuchukua nafasi ya Deus Kaseke wakati Juma Abdul alitoka kumpisha Joseph Zutah na Malimi Busungu akaingia baada ya Amis Tambwe kupumzishwa.
Kipindi cha pili bado Azam waliendelea kukosa magoli kwani Kipre Tchetche, Ame Ally na Shah Farid Mussa walikosa goli baada ya kujichanganya wao kwa wao na mpira kunyakwa na mlinda mlango Ally Mustafa ‘Barthez’
Kwa matokeo hayo, Azam FC inakamilisha timu nne zilizofuzu kucheza hatua ya nusufai naili ya michuano ya Kagame kwa mwaka 2015 ambapo Ijumaa itakutana na KCCA ya Uganda iliyofuzu kucheza hatua ya nusu fainali leo mchana kwa kuibanjua timu ya Al Shandy ya Sudan kwa goli 3-0 huku Yanga wakiwa wameyapa mkono wa kwaheri mashindano ya Kagame kwa mwaka 2015.

JAROME BOATENG AKAMILISHA DILI NA JAY Z

COVERBeki wa Bayern na mshindi wa kombe la dunia Jarome Boateng amekua mchezaji wa kwanza kutoka Ulaya kusaini mkataba na kampuni ya Jay Z Roc Nation Sport.
Boateng mwenye miaka 26 ameungana na mastaa wengine kwenye michezo ambao wapo chini ya Roc Nation Sport kama Le Bron James na wengine.
Boateng alikamilisha dili hilo kwenye Sports Bar ya Jay Z huko Brooklyn na baadae wakaendelea kwenye private party na Jay Z.
2AE3864100000578-0-image-a-37_1438086482923

C PWA – WASANII WA HIPHOP WANASHINDWA KUVUKA BODA KWASABABU YA UWOGA WA KUWEKEZA

.
Msaii wa hiphop C pwa  amefunguka  kuwa wasanii wengi wa hiphop wa bongo wanashindwa kufika level za kimaita kutokana na kutowekea katika mziki .C Pwa amesema “Kuna wasanii wachae sana wa  hiphip ambao wamewekeza katika mziki na matunda wanayaona , nikisema kuwekeza namaanisha Good video ,good music production n.k . But ki bongobongo wasanii wengi wanaogopa kuwekeza kitu kinachowafanya wasivuke boda”CPWAA

Video: MeekMill azomewa na wakazi wa mji anaotoka drake ‘Toronto’

meek-nicki-all-eyes-7Mbali na MeekMill kufanikiwa kuingia Toronto japo meya wa mji huyo alimpiga marufuku  kukanyaga lakini amekiona cha mtemakumi baada ya Wakazi wa mji huo ambao anaotoka Drake wamemzomea Meek Mill wakati anaperfom kwenye moja ya show ya “PinkPrint Tour” iliyofanyika mjini humo.
Meek Mill na Drake wameingia kwenye beef baada ya Meek kuibuka na kudai kuwa drake huwa anaandikiwa mistari na drake kuachia diss track inayomlenga meek mill moja kwa moja.

Birdman azungumzia ugomvi wake na Lil Wayne kwa mara ya kwanza,tuhuma za mauaji pia.

lilbaby
Boss wa Cash Money Record na baba wa rapa Lil Wayne amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu kesi ya madai ya dola milioni 51 na kuchonga njama za kumua Lil Wayne.
Birdman anasema  “Waye ni mwanangu milele na hakuna cha kupinga au kubadilisha swala hilo, nitafanya chochote anachotaka nifanye ila ayabaki kuwa mwanangu tu, yote anayotaka kufanya niko naye sawa , nampenda hadi kufa na nimempa baraka zangu kwa lolote analofanya ” .
Birdman anasema bado anazungumza vizuri na Lil Wayne na kwamba vyombo vya habari vimekuza jambo hili, akiongelea kuacha Wayne atoke Cash Money, Birdman anasema , hajamzuia Wayne akisema baba nataka kutoa niendelea atakubali kumwachia “.
Birdman amekanusha kumrushia chupa ya pombe Lil Wayne na kusema hawezi fanya hivyo kwa mwanae, kuhusu njama za kumpiga risasi, birdman anasema ni kitu cha kijinga sana alichowahi kusikia”.
Birdman amethibitisha kuwa Nicki Minaj na Drake hawawezi kuondoka Cash Money.

28 July, 2015

MOURINHO: HAZARD NI BORA KULIKO RONALDO

Eden Hazard
Winga wa Chelsea Eden Hazard ni lazima azingatiwe kuwa miongini mwa wachezaji watatu bora wa dunia- yaani juu ya Cristiano Ronaldo kwa sasa, hayo ni maneno ya kocha Jose Mourinho .
Ronaldo na Lionel Messi wamekuwa wakipokezana tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Ballon d’Or), kwa miaka ya hivi karibuni, huku wakiwa wanafunga mamia ya magoli huko ligi kuu nchini Uhispania, lakini bosi huyo wa ‘The Blues’ amesema kitendo cha Ronaldo kukosa kombe lolote msimu uliopita ndio sababu ya kuwa nyuma ya Hazard.
Hazard alichukua tuzo ya mchezaji bora wa ligi ya Uingereza msimu wa 2014-15 huku Chelsea wakitwaa ndoo hiyo, hivyo Mourinho anasema hii ndio sababu ya winga wake kupewa mazingatio makubwa katika hili.
“Ni dhahiri inategemeana na msimu walionao”, aliwaambia waandishi. “Wanatakiwa kushinda makombe tu, au sio? Mpira bila ya makombe ni sawa na hamna kitu”.
“Messi alishinda makombe matatu. Ameshinda michuano mitatu mwaka jana, vile vile amefika fainali ya Copa America. Alikuwa na msimu bora kabisa na kwa timu yake pia. Sipendi wachezaji au mameneja wanajishindia tuzo binafsi bila ya timu.
“Msimu uliopita, ndio”, Mourinho aliendelea wakati alipoulizwa kama Hazard alikuwa na msimu bora kuliko Ronaldo”, bila kujali kwamba Ronaldo alikuwa yuko vizuri. Alikuwa yuko vizurri sana. Alifunga idadi ya magoli ya kutosha tu.
“Sina shaka kwamba ni mchezaji wa kiwango cha juu. Ninachosema ni kwamba, kwa mtazamo wangu, kila mcheza soka duniani lazima aelewe kwamba timu lazima iwe mbele ya makombe (timu kwanza, mchezaji baadaye)
“Eden anakuja kwa kasi sana sasa na alipaswa kuwa moja ya wachezaji bora Ulaya mwaka uliopita. Lakini kwa mtazamo wangu ni kwamba anatakiwa kuwa kwenye tatu bora na sio kumi bora.
“Nadhani Eden ni mchezaji bora wa nchi yetu. Mchezaji bora wa Uingereza. [Chama cha Waandishi wa Habari za Soka] walimpigia kura pia, mchezaji bora wa EPL.Kama ilivyo ada EPL ni ligi bora duniani, Nadhani ni miongoni mwa wachezaji wa kiwango cha juu duniani”.

Ma-star kwenye Series ya Empire “Grace Gealey na Trai Byers”wamevalishana pete.


Ma star ambao wametamba katika series iliyotamba ulimwenguni ya Series ya Empire ambapo mwanzo walikuwa wakiyaficha mahusiano yao lakini kwa sasa imekuwa si siari tena kwani wameamua kuweka wazi na kuvishana pete.
grace-gealy-trai-byers-engaged-ftr
Trai mwenye umri wa miaka 31 aliamua kufanya engagement katika sherehe ya Grace ya siku ya kuzaliwa iliyofanyika katika mji wa Chicago ambapo Grace alifanyiwa suprise na jamaa na kuanza kumuuliza maswali kama yupo tayari.Kutokana na the source “New York report”ime ripoti kuwa Trai ali-share picha ya wawili hao ikionyesha baadhi ya watu,chakula pamoja na pete.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...