Showing posts with label Afya. Show all posts
Showing posts with label Afya. Show all posts

28 September, 2016

Mtoto azaliwa kutoka kwa mbegu za watu watatu

Dkt John Zhang akiwa na mtoto huyo
Mtoto wa kwanza aliyetengezwa kwa kutumia mbinu ya uzazi wa mbegu za watu watatu amezaliwa, jarida la kisayansi la New Scientist limetangaza.

Mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miezi mitano ana chembe chembe za DNA kutoka kwa mamake, babake pamoja na jeni za mfadhili.

Madaktari wa Marekani walichukua hatua hiyo kuhakikisha kuwa mtoto huyo wa kiume atakuwa huru kutokana na hali ya jeni ambayo mamake kutoka Jordan anabeba katika jeni zake.

Wataalam wanasema kuwa hatua hiyo ni mwamko mpya wa kimatibabu na inaweza kusaidia familia nyingine zilizo na hali za jeni zisizokuwa za kawaida.
Lakini wameonya kuwa uchunguzi wa mara kwa mara wa mbinu hiyo mpya ya kiteknolojia inayoitwa ufadhili wa Mitochondrial unahitajika.

Mitochondria ni vyumba vidogo vidogo ndani ya kila seli ambavyo hubadili chakula kuwa nguvu inayotumika mwilini.

Baadhi ya wanawake hubeba jeni zilizo na kasoro na wanaweza kupitisha jeni hizo hadi kwa watoto wao.

Wanasayansi waliohusika katika shughuli hiyo walisafiri hadi Mexico kwa sababu huko hakuna sheria za kuzuia shughuli kama hiyo ya kimatibabu.
Walichukua sehemu muhimu za chembe za kinasaba (DNA) kutoka kwa yai la mama, na DNA ya mitochondria kutoka kwa yai la mfadhili na kuunda yai lenye afya ambalo lilitungshwa mbegu kutoka kwa baba.

Matokeo yake ni kuzaliwa kwa mtoto mwenye 0.1% ya DNA kutoka kwa mfadhili na jeni nyingine zote, zinazoamua sifa kaa vile rangi ya nywele na macho kutoka kwa mama na baba.Teknolojia mpya ya uzazi ndio iliotumika kumtengeza mtoto huyoDkt John Zhang, mkurugenzi wa kimatibabu katika hospitali ya New Hope Fertility Centre jijini New York City, anasema yeye na wenzake walitumia njia hiyo kupata viinitete vitano, lakini wakastawisha kimoja tu.

08 July, 2016

Faida 9 za kula mboga za Spinach kwa mama mjamzito

Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu mwilini na madini mbali mbali ambayo huhitajika na Mwili. Mboga za Spinach ni moja kati ya mboga maarufu mno katika jamii zetu na hizi ndizo faida zake kwa wanawake wajawazoto:-
 1. Huzuia mtoto kuzaliwa na matatizo kama mgongo wazi na mdomo na pua kuwa na uwazi uliongana( mdomo sungura)
2. Hupunguza uwezekano wa mtoto kuzajiwa njiti yaani kuzaliwa kabla hajafikisha mienzi 8 tumboni kwa mama. kutokana na kutokuwa na madini ya chuma ya kutosha mama anaweza pata tatizo ili ila kwa sababu spinach ina madini ya chuma ya kutosha yaani folic basi huweza kuzuia shida hii.
3. Huzuia kupata tatizo la upungufu wa damu  hii ni kutokana na spinach kuwa na madini ya folic na chuma yanayoongeza damu mwilini.
4. Husaidia katika utengenazi wa mapafu ya mtoto. inakemikali inayoitwa beta-carotene ambayo hubadilishwa kuwa vitamini A hii ndiyo hutumika kwa ajili ya uundaji wa mapafu ya mtoto.
5. Hutibu tatizo la haja kubwa kuwa ngumu kwa kuwa spinach ina nyuzi nyuzi kiitaamu huitwa fiber ambazo hulainisha choo na kupunguza maumivu.
6. hupunguza maumivu kwa kutumia chemicali yake inayoitwa glyco-lipid ambayo huzuia maumivu katika sehemu za miguu na misuli.
7.  Huwastanisha msukumo wa damu mwilini kwa kutumia kemikali yake inayoitwa nitrate.
8. Huweka kinga ya mwili wa mama mjamzito imara kwa spinach ina vitamin C  hivyo hutapata yale maradhi ya lazima kwa mama mjamzito.
9. Huwezesha utengenezaji  bora kwa mifupa ya mtoto kwa sababu spinach ina madini ya kalishamu ambayo hujenga mifupa ya mama na mtoto.

21 June, 2016

Health tips: What To Eat During Pregnancy?

Are you wondering how to keep you and baby healthy in these nine months? Here are the few tips on what to eat during your pregnancy and what to limit and avoid for the next 40 weeks(Infographics),precision-nutrition-pregnancy-nutrition-2

25 February, 2016

Ebola ina madhara ya muda mrefu


Kikundi cha watafiti wa wahanga wa ugonjwa wa Ebola nchini Liberia wamebaini kuwa wengi kati yao walisumbuliwa na tatizo la akili baada ya kuathirika na virusi vya Ebola.
Watafiti kutoka serikali ya marekani wanatafiti juu ya athari za muda mrefu ambazo wamezimeangalia kwa watu 82 waliopona ugonjwa wa Ebola na kubaini kuwa mbili ya tatu wamesumbuka na tatizo la kudhoofika,kuumwa kichwa,kupoteza kumbukumbu na kuwa dalili za kuwa na huzuni.

03 February, 2016

Kisa nadra cha Zika charipotiwa Marekani

Zika
Kisa nadra sana cha virusi vya Zika kuambukizwa kupitia kushiriki ngono, badala ya kuumwa na mbu, kimeripotiwa nchini Marekani.
Mgonjwa aliyeambukizwa virusi hivyo Dallas, Texas, sana huenda aliambukizwa kupitia kufanya mapenzi, Kituo cha Udhibiti wa Maradhi (CDC) kimeambia BBC.
Mtu huyo hakuwa amesafiri maeneo ambayo yana virusi hivyo lakini mpenzi wake alirejea majuzi kutoka Venezuela.
Virusi vya Zika vinaenezwa sana na mbu na vimehusishwa na visa vya watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo na ubongo kudumaa.
Vinaenea kwa kazi Amerika na Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza hali ya tahadhari duniani.Zika
Shirika la msalaba mwekundu nchini Marekani limewahimisha watu waliotoka maeneo yaliyoathirika na Zika, na ambao wanataka kutoa damu, wasubiri angalau siku 28, kabla ya kutoa damu.
Ushauri huu umeelekezwa kwa watu waliorejea Marekani kutoka Mexico, visiwa vya Caribbean au Amerika ya Kati na Kusini katika kipindi cha wiki nne zilizopita, shirika hilo limesema kupitia taarifa.
Katika tukio jingine, visa viwili vya maambukizi ya Zika vimethibitishwa Australia.
Maafisa wanasema wakazi wawili wa Sydey waliopatikana na virusi hivyo walirejea kutoka Caribbean majuzi.
Kisa hicho cha maambukizi ya Zika Dllas, kitakuwa ndicho cha kwanza kuthibitishwa kutokea Marekani bara, ingawa jimbo la Texas limeripoti visa vingine ssaba, vyote kwenye watu waliorejea kutoka nje.
Anne Schuchat, naibu mkurugenzi mkuu wa CDC amesema hicho ndicho kisa cha kwanza kinachohusisha mtu ambaye hakusafiri.
"Hatudhani aliambukizwa baada ya kuumwa na mbu, lakini tunaamini aliambukizwa kupitia kushiriki ngono.”
Taarifa ya CDC imesema njia bora zaidi ya kujikinga na “kujikinga usiumwe na mbu na kutokumbana na manii kutoka kwa mtu aliyekumbana na virusi vya Zika”.
Kisa hicho hata hivyo sicho cha kwanza kabisa cha maambukizi kupitia ngono kuripotiwa.
Shirika la CDC linasema kwenye tovuti yake kwamba mwaka 2013 kulilipotiwa kisa cha maambukizi kupitia kushiriki mapenzi katika jimbo la French Polynesia.
Shirika hilo linawashauri wanawake wajawazito kutosafiri mataifa mengi yaliyoathiriwa sana na virusi hivyo.

CHANZO: BBC

08 January, 2016

Wavutaji sigara waonywa wasipuuze kikohozi, Yadaiwa kuwa dalili za ugonjwa hatari wa COPD usio na tiba

post-feature-imageWavuta wa sigara wameshauriwa wasipuuze kikohozi kwani inaweza kuwa ishara ya ugonjwa mbaya zaidi unaoweza kudhoofisha na hata kuhatarisha maisha ya wavutaji sigara.
Katika kampeini mpya ya kuhamasisha wavutaji sigara kuhusu athari za uvutaji sigara kwa afya yao, idara ya afya ya umma nchini Uingereza inaonya kuwa wavutaji sigara wengi hawajui hatari ya ugonjwa sugu wa pingamizi ya mapafu ama chronic obstructive pulmonary disease (COPD).

COPD, ainalaumiwa kwa kusababisha mishipa ya hewa kuwa nyembamba mno na hata kufanya wahasiriwa kukosa pumzi wanapotekeleza majukumu mepesi kama kupanda ama hata kushuka ngazi.
Takwimu zinaonyesha watu zaidi ya milioni moja nchini Uingereza wanaishi na hali hiyo.
Vilevile visa 9 kati ya 10 vinavyopatikana vinasababishwa na sigara.

COPD ni mwavuli unaoashiria jumla ya maradhi yanayotokana na kudhoofika kwa mapafu ikiwa .


Hakuna tiba

Watu wenye ugonjwa huu wanamatatizo ya kupumua, hasa kutokana na kupungua kwa uwezo wao wa kupumua na uharibifu wa mapafu.
Dalili ya kawaida ni pamoja na kukosa pumzi hawa wakati unapotekeleza majukumu mepesi, kikohozi kisichosikia dawa na maambukizi ya mara kwa mara kifua.
Idara ya Afya ya Umma nchini Uingereza (PHE) imeanzisha kampeini hii mpya yenye matangazo na kuonya kuwa wavuta wachukulie kikohozi kuwa dalili mbaya na dalili ya kwanza wa maambukizi mabaya ya mapafu.
Hakuna tiba ya maradhi haya,ila iwapo mvutaji ataacha kuvuta sigara,mipango lengwa ya zoezi na dawa zinaweza kupunguza kasi ya maambukizi ya COPD.
Ili kuongeza uelewa juu ya ugonjwa huo, PHE imeandaa filamu fupi inayotumiwa katika kampeini hiyo kwenye mitandao.
Filamu hiyo inamhusisha bingwa wa zamani wa Olimpiki Iwan Thomas, ambaye mamake alipatikana hivi karibuni na ugonjwa wa COPD.
Thomas anafanya majaribio na wavutaji sigara kuona iwapo COPD inaweza kupunguzwa miongoni mwa wavutaji sigara.
Thomas alisema: "Sijawahi kueleweka kikamilifu COPD au athari yake katika maisha ya kila siku, lakini wakati mambo rahisi kama kupanda ngazi, na kutengeneza kikombe cha chai au kutembea kutoka kituo cha mabasi inaanza kuwa vigumu kwangu ndipo ilinifanya nikatahamaki.''

'Mwaka wa kuacha sigara'

"Baada ya uvutaji sigara wa miaka mingi , mamangu mzazi ameamua kuwa mwaka wa 2016 ndio mwaka atakaoacha kuvuta sigara!''
Ningewasihi wale wote wanaovuta sigara wafanye maamuzi kama hayo kwaajili ya kunusuru mapafu na afya yao wenyewe'' alisema Thomas.
Profesa Sally Davies, ambaye ni afisa mkuu wa matibabu,nchini Uingereza aliongeza kusema kuwa : "COPD ni ugonjwa mbaya licha ya kuwa haujulikana sana''.
"Jambo la busara kwa mvutaji sigara ni kutathmini afya ya mapafu yake mapema kisha kuchukua hatua zinazohitajika za kitabibu ilikunusuru maisha yao ikiwa ni pamoja na kuacha uvutaji wa sigara.''

Dondoo za Lishe Wakati wa Ujauzito

Dondoo za Lishe Wakati wa Ujauzito

Unakula nini wakati wa ujauzito? Lishe wakati wa ujauzito ni muhimu kwa ajili ya afya yako na maendeleo mazuri ya mtoto anayekua tumboni. Zifuatazo ni dondoo za kukuwezesha uwe na lishe nzuri wakati wa ujauzito:
  • Jitahidi upate mlo kamili kila siku kwa kupata vyakula vya wanga, protini, mafuta, vitamini, madini na maji ya kutosha.
  • Fanya nusu ya mlo wako uwe ni mchanganyiko wa matunda na mboga za majani.
mjazito akipata mlo wenye mgoga za majani
  • Tumia nafaka zisizokobolewa kama unga wa dona au mtama, mchele usiokobolewa, mikate ya brown au whole grain cereals.
  • Tumia maziwa yenye fafi kidogo( skimmed milk) au maziwa na vinywaji vya soya.
  • Chagua vyanzo vyako vya protini zaidi katika samaki, kuku, mayai, jamii ya maharage, soya na karanga.
  • Tumia zaidi mafuta ya mimea katika mapishi yako kama mafuta ya alizeti, pamba au mizeituni (Olive oil).
    mafuta ya alizeti
  • Punguza vyakula vyenye sukari za kuongeza (hasa artificial sugars) na mafuta kama biskuti, pipi, soft drinks, soda, pipi, ice creams, vyakula vya kukaanga na hot dogs.
  • Kunywa maji mengi, zisipungue lita 2.5 kwa siku.
  • Mazoezi mepesi kama kutembea kwa dakika 30 kwa siku.
  • Epuka matumizi ya pombe kwani yataathiri afya ya mtoto wako.
    usinywe pombe
  • Tumia virutubisho ziada (supplements) utakazopata kliniki.


The human body is made up of cells. Inside a human cell, you will find certain irons such as sodium, potassium, calcium, magnesium and phosphorous. Irons inside our cells are also known as electrolytes and are necessary for the normal functioning of our organs. They regulate bodily aspects such as hydration, heart rate, and the nervous system. An imbalance of electrolytes may cause or increase chances for cell and organ disfunction. This can result in conditions such as irregular heartbeats, headaches, muscle weakness, etc. For human organs to function normally, cells need to be hydrated and nourished with an appropriate diet. Luckily, coconut water is composed of the same irons found in a healthy human cell. Making it an ideal refreshment to simply hydrate the body or for replacing electrolytes lost during sweat and heat. Credit-FAS Magazine

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
The human body is made up of cells. Inside a human cell, you will find certain irons such as sodium, potassium, calcium, magnesium and phosphorous. Irons inside our cells are also known as electrolytes and are necessary for the normal functioning of our organs. They regulate bodily aspects such as hydration, heart rate, and the nervous system. An imbalance of electrolytes may cause or increase chances for cell and organ disfunction. This can result in conditions such as irregular heartbeats, headaches, muscle weakness, etc. For human organs to function normally, cells need to be hydrated and nourished with an appropriate diet. Luckily, coconut water is composed of the same irons found in a healthy human cell. Making it an ideal refreshment to simply hydrate the body or for replacing electrolytes lost during sweat and heat. Credit-FAS Magazine

Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu

10 December, 2015

Madaktari kupandikiza uume Marekani ili kumuwezesha mgonjwa kufanya tendo la ngono

post-feature-imageUpasuaji umepangwa kufanyika kwa mara ya kwanza kupandikiza uume nchini Marekani, kwa lengo la kuwasaidia mpiganaji wa zamani. Upasuaji huo wa saa 12- utahusisha ushonaji wa neva muhimu na mishipa ya damu kwa ajili ya kutunza mkojo na kumuwezesha mgonjwa kufanya tendo la ngono.

Upasuaji huu unafuatia mafanikio ya kwanza kabisa ya upandikizaji wa uume nchini Afrika kusini mwaka jana. Jopo la madaktari kutoka Hospitali ya chuo kikuu cha Hopkins (JHU) wanapanga kumfanyia upasuaji huyo mwanajeshi wa zamani mwenye umri wa miaka 60kama sehemu ya majaribio.

Hatua ya kwanza ya upasuaji huo itaanza kwa kuondoa uume kutoka kwa kijana aliefariki ambaye alijitolea kutoa uume wake kwa ruhusa ya familia yake. Kwa mujibu wa jopo la madakatari katika JHU matumaini ya mwanajeshi huyo wa zamani ni kwamba hisia za uume wake zitarejea katika muda wa miezi 12.

Uwezekano wa mgonjwa kupata watoto, utategemea kiwango cha jeraha na mafanikio ya upasuaji huo. Lakini Wanasayansi wanasema kutokana na kwamba ni upasuaji mmoja wa kupandikiza uume uliofanyika, madaktari watakua makini kuhakikisha kuna matumaini ya kweli.

08 December, 2015

Utafiti uliofanywa umeonyesha Unene wa mwanaume huathiri mbegu za kiume

post-feature-image
Utafiti uliofanywa nchini Denmark umeonyesha uzani wa mwanamume huathiri seli za mbegu za kiume na huenda ukachangia katika kuwafanya watoto wanaozaliwa kuwa wanene

Seli za mbegu za kiume za wanaume wembamba na wanaume wanene zilikuwa na taarifa tofauti za kijenetiki, jambo ambalo huenda linaathiri utendaji wa chembe za kijenetiki.

Dkt Romain Barres, aliyesaidia katika utafiti huo alisema awali ilikuwa imebainika kwamba: “Mwanamke anapokuwa mjamzito anafaa kujitunza vyema. Lakini utafiti huu unaonyesha wanaume wanafaa pia kuangalia uzani wao.”

Utafiti huo ulifanywa kwa wanaume sita walionenepa kupindukia na ambao walikua wakisaidiwa kupunguza uzani. Watafiti walichunguza mbegu za kiume za wanaume hao kabla na baada ya kupunguza uzani baada ya mwaka mmoja.

Dkt Romain Barres mtafiti mkuu wa ripoti hii amesema waligundua tofauti iliyokuwepo kwa wanaume hao. Utafiti unasema kwamba zeli za mbegu za wanaume walionenepa husababisha mabadiliko ya tabia.

Aidha ripoti imeonya wanawake walio na mimba kuwa waangalifu sana hasa ikiwa walitunga mimba hizo wakiwa na wanaume walionenepa sana. Dkt Barres amesema wanaume walionenepa sana husababisha jeni zao kuanza kutamani kula chakula kila mara.

Ameongeza kwamba uzani wa mtu pia unaambatana na ukuaji wa akili. Utafiti huu uliochukua miaka mitano pia ulitofautisha wanaume 13 wenye uzani wa kadiri na 10 walionenepa zaidi. Hapo ikagunduliwa kwamba, wote walikua na tabia tofauti na zilizochochewa na mabadiliko ya seli kwenye mbegu za kiume.

Utafiti pia unasema uzani wa baba unaweza kusaidia, wanawe. Utafiti unasema kwa kula sana baba watoto pia huwahimiza wanawe kula sana ili wakue kwa haraka. Prof Allan Pacey amesema utafiti huu umebainisha kwamba baadhi ya tabia za watoto zimechangiwa na zilizokua mbegu za kiume za baba yao


04 December, 2015

Mwanamke aliyekataa matibabu ya figo kuokoa maisha yake akidai amepoteza mng’ao afariki

post-feature-imageMwanamke aliyekataa matibabu ya figo kuokoa maisha yake nchini Uingereza, akisema ameshapoteza mng’ao, amefariki. Mwanamke huyo wa umri wa miaka 50 aliyetambuliwa tu kama C, aligonga vichwa vya habari baada ya jaji kuamua kwamba ana haki ya kukataa kupokea matibabu ya kusafisha damu.

Figo za C ziliharibika baada yake kunywa dawa kupita kiasi akitaka kujiua. Mahakama iliambia kwamba katika maisha yake, C aliangazia zaidi "sura yake, wanaume na vitu vya thamani.”

Mmoja wa bindi zake aliambia mahakama: “Kupona kwake si kwamba figo zake zianze kufanya kazi tena pekee, bali atahitaji kupata ‘mng’ao’, jambo ambalo anaamini hawezi kuapata tena kutokana na umri wake.”

Mwaka uliopita, C alikuwa amepatikana na saratani ya matiti lakini akakataa matibabu akisema matibabu hayo yangemfanya kuwa mnene.

Baada ya kupata matatizo ya figo, wakfu wa Huduma ya Taifa ya Afya Uingereza katika hospitali ya King’s College ulitaka alazimishwe kupokea matibabu. Lakini Jaji MacDonald, kwenye uamuzi alioutoa Novemba 13, alisema C ana uhuru wa kufanya uamuzi.
House of Entertainment, News, Gossip, Music and Videos!

31 October, 2015

Wewe ni mtumiaji wa vilevi? haya ni mambo ya muhimu unayopaswa kufahamu kuhusiana na Vilevi


“Haiuzwi kwa wenye umri chini ya miaka 18, kunywa kistaarabu” ujumbe huu unapatikana katika matangazo yote ya vilevi, na nadhani hilo linatambulika kwamba pombe si ya vijana chini ya miaka 18. Unywaji wa pombe ni kawaida kwa watu wengi lakini unakunywa kistaarabu? Sina mpango wa kukufundisha kunywa pombe wala kukushawishi uanze kunywa Pombe wote tunajua madhara yanayoletwa kwa unywaji wa pombe wa kupindukia. Leo tuongelee upande wa pili wa shilingi, faida za unywaji wa pombe kwa wastani. Narudi unywaji wa pombe kwa wastani.
Magonjwa ya Moyo.
Utafiti kutoka  Harvard University  Marekani, umegundua unywaji wa pombe kwa kiasi cha wastani kinasaidia mzunguko mzuri wa damu,hii inasaidia kuzia matatizo ya moyo na magonjwa ya kiharusi na kupooza (stroke)
Urefusha Maisha
Utafiti uliofanywa na Catholic University  huko Campobasso, waligundua kuwa kunywa chupa chini ya 4 au 2 kwa siku kwa mwanamme au mwanamke,  kwa asilimia  18 inaongeza muda wa kuishi kama  ililipotiwa na Reuters. Dr. Giovanni de Gaetano  wa Catholic University  pia alisema sio mbaya kama unaweza kunywa pombe kidogo wakati wa kula. Makala nyingine iliyoandikwa na Mediterranean diet, kuwa mvinyo (wine) ni kinywaji safii wakati wa chakula cha mchana na cha jioni. Lakini usinywe tu pombe wakati wote.
Inasaidia kuamsha Hisia za Mapenzi
Kama ilivyo Red Wine inasaidia kupunguza kasi ya magonjwa ya moyo, Mwaka 2009 jarida lililotambulika kama Sexual Medicine, liliandika kwa utafiti waliofanya  asilimia 25 – 30 wanywaji wa pombe hawapati matatizo ya kushindwa kushiriki tendo. Mkuu wa utafiti , Kew-Kim Chew Mtaalamu wa magonjwa ya mlipuko kutoka University of West Australia alifanya utafiti kwa wanaume  1,770 wa Australia,  Chew aliwashauri pia wanaume hao wasitumie pombe kupitiliza sababu bado wanafanya utafiti juu ya swala hilo kwa kina zaidi.

Pombe huamsha Akili
Utafiti uliohusisha watu zaidi ya 365,000 toka mwaka 1997 iliripotiwa na jarida la Neuropsychiatric Disease and Treatment watu wanaokunywa kwa wastani wanauwezo wa kuzuia ugonjwa wa Alzheimer na magonjwa mengine ya akili. Kiwango kidogo cha pombe kinafanya seli za ubongo ziwe hai (fit/active) alisema Edward J. Neafsey, Ph.D mwandishi wa Science Daily. alisema pia hawashauri watu wasiokunywa pombe waanza kunywa pombe. Na akasema kama wale wanaokunywa wanakunywa kwa wastani basi itawasaidia.
Husaidia Tatizo La Mawe kwenye Kibofu
Kwa wanywaji wa wastani kuna uwezekano wa kupunguza uwezekano wa kupata  tatizo la mawe kwenye kibofu huo ni  utafiti uliofanywa na University of East Anglia, watafiti walisema faida zinaonekana kwa wale wanywaji wa kawaida na sio waywaji wa pombe kupinduki  sababu unywaji wa pombe kupitiliza huleta matatizo ya kiafya
Ugonjwa wa Sukari
Tafiti zilizofanywa uholanzi,  watu wenye afya wanao kunywa glass moja au mbili kwa siku wanapunguza uwezekano wa kupata aina ya pili ya kisukari ukiachilia mbali wale wasiokunywa hata kidogo, wale wanaokunywa kidogo wana afya zaidi, walisema watafiti hao kupitia Reuters.
Angalizo kujua faida hizi za pombe haina maana kama hujaanza kunywa pombe uanze sasa na kama wewe unatumia kilevi basi kunywa kwa kiwango kidogo sababu ni faida kwa afya yako kuliko unywaji wa kupindukia. Kunywa kistaarabu.

30 August, 2015

Fahamu kuhusiana na Ugonjwa wa Kipindupindu, Dalili zake na jinsi ya kujikinga

Kipindupindu ni ugonjwa wa kuharisha na  kutapika unaosababishwa na vimelea vya bacteria vinavyoitwa kwa lugha ya kitaalam “Vibrio cholera”.

CHANZO CHA UGONJWA


  • Vimelea vilivyomo kwenye kinyesi na matapishi ya mgonjwa wa kipindupindu.
  • Vimelea vilivyomo kwenye kinyesi cha mtu bila yeye binafsi kuonyesha dalili zozote za ugonjwa.


DALILI ZA UGONJWA WA KIPINDUPINDU.

Mgonjwa wa Kipindupindu huwa na dalili zifuatazo:

  • Kuharisha mfululizo au mara kwa mara bila tumbo kuuma ambako kunaweza kuambatana na kutapika.
  • Kinyesi au matapishi huwa ya maji maji yasiyo na harufu, yanayofanana na maji yaliyooshewa mchele.
  • Kusikia kiu sana, macho kudidimia na ngozi kusinyaa ambavyo hutokana na upungufu wa maji mwilini.
  • Kuishiwa nguvu, kuhema haraka haraka na kulegea. Hali hii hutokana na upungufu wa maji na madini mwilini.


KIPINDUPINDU KINAVYOENEA.


  • Kula chakula au kunywa kinywaji chochote kilicho na vimelea vya ugonjwa wa kipindupindu kwa mfano:-


  1. Kunywa maji yasiyochemshwa.
  2. Kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira ambayo siyo safi.
  3. Kula matunda yasiyooshwa kwa maji safi na salama.
  4. Kunywa pombe za kienyeji zilizoandaliwa katika mazingira machafu au kunywea katika vyombo vichafu.
  5. Kula mboga za majani, kachumbari na saladi bila kupikwa au kuziosha kwa maji safi na salama.


  • Kula chakula au kumlisha mtoto bila kunawa mikono kwa sabuni na maji safi na salama yanayo tiririka.
  • Kuosha au kuhudumia mwili wa mtu aliyekufa kwa ugonjwa wa kipindupindu bila kujikinga.
  • Kunawa mikono kwenye chombo kimoja kwa mfano ndani ya bakuli au beseni kabla ya kula chakula.
  • Kutotumia choo au utupaji ovyo wa kinyesi.
  • Kutonawa mikono baada ya kutoka chooni.
  • Kuweka mazingira katika hali ya uchafu mfano kutupa taka ovyo bila kuzingatia kanuni za afya..
  • Kula vyakula vilivyopoa na visivyofunikwa.
  • Kutiririsha maji ya chooni ardhini na hivyo kusababisha uchafuzi wa vyanzo vya maji na chakula.

Inzi huchangia kueneza ugonjwa wa kipindupindu kwa tabia zake za kutua chooni kwenye kinyesi, uchafu na hata vyakula na vinywaji.

MADHARA YA KIPINDUPINDU


  1. Hofu miongoni mwa jamii katika sehemu yenye mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
  2. Kifo kutokana na ukosefu wa maji na madini mwilini baada ya kuharisha na kutapika sana.
  3. Kushuka kwa uchumi kutokana na familia/jamii kuacha shughuli za uzalishaji mali ili kumuhudumia mgonjwa na kushiriki katika misiba.
  4. Serikali hutumia fedha nyingi kwa ajili ya dawa, posho kwa watumishi katika kukabiliana na ugonjwa wa kipindupindu.


JINSI YA KUJIKINGA NA KIPINDUPINDU


  • Kujenga choo bora na kukitumia Ipasavyo
  • Kufunika tundu la choo na kufunga mlango baada ya matumizi yake.
  • Kunawa mikono kwa maji safi na salama kwa kutumia sabuni baada ya:.

-      kutumia choo.
-      kumtawaza mtoto na kabla ya kula au kumlisha motto.

  • Kula chakula kikiwa bado moto na kufunika chakula kilichoandaliwa tayari kwa kuliwa.
  • Kunywa maji yaliyochemshwa na kuhifadhiwa katika chombo kisafi na salama.
  • Kusafisha vyakula vinavyoliwa vibichi (kama vile matunda na mboga) kwa kutumia maji safi na salama yanayotiririka.
  • Kuhakikisha usafi wa mazingira ya vilabu/baa, wahudumu na vyombo vitumikavyo. Pombe za kienyeji ziandaliwe kwa maji yaliyochemshwa.
  • Weka mazingira katika hali ya usafi.
  • Kumbuka, kuchuja maji yaliyochemshwa kunaweza kuchafua maji kwa kuingiza vimelea.Hivyo, chuja maji kabla ya kuyachemsha.


KUHUDUMIA MGONJWA

Mgonjwa wa kipindupindu hupoteza maji mengi na madini muhimu mwilini anapoharisha na kutapika. Ili kuokoa maisha ya mgonjwa ni muhimu kuchukua hatua zifuatazo:

  • Mpe mgonjwa dawa ya mchanganyiko wa sukari na chumvi(ORS), maji, uji mwepesi, supu nk. mara kwa mara.
  • Mpeleke mgonjwa haraka iwezekanavyo katika kituo cha afya/zahanati/ hospitali au kituo cha kutibu kipindupindu kilicho karibu nawe.
  • Matapishi na kinyesi cha mgonjwa ni hatari kwa afya yako. Kwa hiyo nguo na vitu vingine vilivyochafuliwa na mgonjwa vilowekwe kwenye kemikali maalumu (mfano Jik) au vichemshwe ili kuua vimelea vya kipindupindu na kasha visafishwe kwa sabuni.
  • Ndugu waliokuwa wakiishi na mgonjwa au wale wanaomhudumia wahakikishe wanapata dawa za kinga dhidi ya kipindupindu.

Angalizo:

Ni lazima wakati wote kuwa msafi ili kuzuia vimelea vya ugonjwa visiingie kinywani kwako kwa njia zilizotajwa hapo juu.

Tahadhari:

Maiti ya mgonjwa wa kipindupindu ni hatari, usijishughulishe na kuosha maiti hiyo bali izikwe haraka kwa kufuatwa ushauri wa wataalam wa afya.

Madhara ya kula Mayai yasipoiva vizuri kwa Afya

Mayai ni moja ya vyakula vyenye viini lishe muhimu kwa ajili ya afya ya mwili wa binadamu. Kwa kawaida mayai kabla ya kuliwa, huandaliwa kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchemshwa, kukaangwa au kuchanganywa na vyakula vingine kama vipande vya viazi mviringo ambavyo ni maarufu kwa jina la chips.

Pia, kuna baadhi ya watu wanaopendelea kula mayai mabichi kama dawa ya tiba mbadala, kwa ajili ya kulainisha sauti na wengine hupendelea kula mayai ya kukaanga ambayo hayakukaushwa vizuri.
Ukitembelea migahawa mingi utabaini kuwa watu wanakuwa na mitazamo tofauti na wanavyopenda kula mayai.

Mfano kuna wanaoagiza watengenezewe mayai kwa mtindo unaojulikana kama ‘macho ya ng’ombe.’ Ukiagiza namna hiyo, mpishi atataka kuuliza kama ni ‘macho ya ng’ombe’ ya kugeuza.

Ina maana kuwa ‘macho ya ngombe’ ya kugeuzwa ni yale yanayoivishwa pande zote lakini yale ambayo siyo ya kugeuza, huwa linaifa nusu. Upande mmoja unabaki ukiwa mbichi, na ndiyo raha ya baadhi ya watu.

Hata ukienda kwa wakaanga chipsi, utakuta wanawauliza wateja wao kama wanapokaanga na mayai wakaushe au wasikaushe. Hii inaashiria kuna watu wanataka wale chipsi zikiwa na mayai ambayo halijaiva sawasawa.

Kuna watu wengine wanaamini kwamba kula mayai mabichi kunafanya sauti inakuwa nyororo, hivyo wale waimbaji huwalazimu kufanya hivyo ili kufanya nyimbo zao zivutie.

Si hivyo tu, kuna baadhi ya watu huamini pia dawa ya kikohozi ni kunywa yai bichi lililochanganywa na asali. Hizi ni imani ambazo zimejengeka kwenye jamii na watu hufanya hivyo ili kufikia malengo waliyokusudia.

Katika siku za karibuni, imevuma kuwa mayai ya kwale yanatibu magonjwa sugu kama vile kisukari, shinikizo la damu, saratani na kifua.

Katika mpango huo, wanapendekeza wahusika kula mayai mabichi ya kwale tena kwa kutafuna hadi kaka lake, yaani ganda la nje.

Hali hii imesababisha biashara ya mayai ya kwale kuwa kubwa na hata wafugaji wameongezeka mara dufu.

Wataalamu wanasemaje?

Baadhi ya tafiti za sayansi ya lishe na afya ya jamii, zinabainisha kuwa ulaji wa mayai katika hali ya namna ya ubichi, unaweza kuhatarisha afya.

Wakati mwingine, hali ya namna hii, huwa chanzo cha mlipuko wa magonjwa ya tumbo katika jamii. Katika milipuko ya magonjwa hayo, hali inaweza kuwa mbaya zaidi hasa kwa watoto wadogo, wazee, wajawazito na watu wenye upungufu wa kinga mwilini.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba mayai mabichi yanaweza kusababisha maradhi ya kuharisha na homa ya matumbo kutokana na kubeba vimelea vya magonjwa aina ya Salmonella Enteritidis PT4. Vimelea hivi hatari kwa afya, vinaweza kuwa ndani ya yai au juu kwenye ganda la yai bila kuonekana kwa macho. Mgonjwa aliyepata uambukizo wa bakteria wa Salmonella kutokana na kula mayai, anaweza kuwa na homa kali, maumivu makali ya tumbo pamoja na kuharisha ndani ya saa 72 baada ya kula mayai.

Ugonjwa huu unaweza kudumu kwa siku nne hadi saba na baadhi ya watu huwa na hali mbaya kiasi cha kuhitaji matibabu ya kulazwa hospitalini.

Kwa baadhi ya watu ambao kinga ya miili yao si imara, vimelea vya Salmonella vinaweza kuingia katika mfumo wa damu na kusambaa mwili mzima. Jambo hilo linaweza kusababisha kifo kwa muda mfupi kama mgonjwa hatapewa matibabu sahihi na kwa haraka.

Nchini Uingereza ingawa, ugonjwa utokanao na kula mayai yenye uambukizo wa Salmonella umepungua sana, lakini angalizo la watu kuepuka ulaji wa mayai mabichi bado linadumishwa.

“Ni swala la kujua kwamba hatari bado ipo katika jambo hili, hata kama ni ndogo,” anasema Bob Martin ambaye ni mfanyakazi wa Wakala wa Viwango vya Ubora wa Chakula (The Food Standards Agency) nchini Uingereza.

Utafiti uliofanyika mwaka 2004-2005 katika maeneo mengi ya Ulaya ulibaini kuwa asilimia 20 ya mashamba makubwa ya kuku wa mayai, yalikuwa na kuku waliokuwa na uambukizo wa Salmonella. Hii ni kwa mujibu wa Richard Lawley katika makala yake yaliyochapishwa Februari mwaka 2013 katika tovuti ya Food Safety Watch.

Utafiti mwingine uliofanywa na Q.T. Bura na Henry B. Magwisha kutoka katika Wakala wa Maabara za Mifugo Tanzania (TVLA) kwa kushirikiana na profesa Robinson H. Mdegela wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), nao ulibaini kuwa ndege wengi wanaotaga mayai wana maambukizi ya vimelea vya Salmonella. Utafiti huo ulifanyika katika Jiji la Mwanza kati ya Desemba 2013 na Januari 2014.

Tukiachilia mbali uambukizo wa Salmonella, ulaji wa muda mrefu wa mayai mabichi au yale yasiyoiva vizuri hasa kwa akina mama wajawazito, unaweza kusababisha wazae watoto wanye ulemavu wa viungo vya mwili katika maumbile yao. Utafiti wa Lawrence Sweetman na wenzake uliochapishwa mwaka 1981 katika jarida la Paediatric toleo la 68(4), unabainisha kuwa ulaji wa mayai mabichi au yasiyoiva vizuri, unaweza kusababisha watoto wasiwe na nywele kichwani.

Utafiti wa Timothy D. Durance wa Chuo Kikuu cha British Columbia nchini Canada, uliochapishwa mwaka 1991 katika jarida la Sayansi za Vyakula (Journal of Food Sciences) toleo la 56(3), unabainisha kuwa ute mweupe wa mayai unaweza kusababisha upungufu wa Biotin mwilini.

Dr. Durance anaongeza kusema kwamba, ute mweupe wa mayai mabichi una protini aina ya avidin ambayo huzuia Biotin kusharabiwa (kufyonzwa) kutoka katika chakula kinapokuwa tumboni. Utafiti huo pia ulibaini kuwa hata mayai yaliyochemshwa au kukaangwa vizuri, bado ute mweupe huwa na Avidin yenye nguvu kwa asilimia 40.

Utafiti wa Profesa Hamid Said wa Chuo Kikuu cha California nchini Marekani, nao uliripoti kuwa ute wa mayai yasiyoiva, unasababisha upungufu wa Biotin mwilini. Utafiti huo ulichapishwa katika jarida la sayansi ya lishe katika tiba (American Journal of Clinical Nutrition) toleo la mwaka 2002. Utafiti mwingine ulioongozwa na Donald Mock na kuchapishwa katika jarida la sayansi ya lishe katika tiba la nchini Marekani toleo la 75(2) mwaka 2002, nao ulibainisha kuwa takribani asilimia 50 ya wanawake wajawazito, wana kiwango fulani cha upungufu wa Biotin mwilini hasa katika miezi mitatu ya mwanzo wa mimba.

Hali hii inafanya wajawazito wanaokula mayai mabichi au yasiyoiva vizuri katika kipindi hiki, kuhatarisha afya zao na za watoto wao walioko tumboni kwa kiasi kikubwa.

Utumiaji wa mayai ya namna hii kwa muda mrefu, pia unaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini na ugonjwa wa mzio wa chakula hasa kwa watoto. Lakini pia utumiaji wa mayai yasiyoiva vizuri kwa muda mrefu, unaweza kusababisha ugonjwa wa kukatika katika kwa ulimi kutokana na upungufu wa vitamini B mwilini.

Hali ambayo husababisha shida wakati wa kula vyakula vyenye uchachu au vilivyokolezwa viungo vingi vya aina mbalimbali.

Tahadhari kubwa inahitajika wakati wa kuandaa mayai ili kuhakikisha kuwa chakula hiki muhimu hakigeuki kuwa chanzo cha madhara ya kiafya. Ni vizuri kutunza, kuchagua na kusafisha mayai vizuri kabla ya kuyachemsha au kuyavunja kwa ajili ya maandalizi mbalimbali ya mapishi.

Vyombo vinavyotumika kukorogea mayai mabichi ni lazima visafishwe kwa maji ya moto na sabuni kabla ya kutumika kwa ajili ya maandalizi ya chakula. Kwa namna yoyote ile mayai yasiliwe ikiwa hayakuiva vizuri au yanapokuwa katika hali ya ubichi.

Ni wakati kwa jamii kubadili mwelekeo kwa kula mayai ambayo yamepikwa hadi kuiva na kuepuka kula yakiwa mabichi.

Ni vyema pia ikaeleweka wapikaji wanapaswa kuwaelimisha wateja wao juu ya athari hizi ili kuwafanye wawe na uchaguzi sahihi wa vyakula watakavyotumia.


Katika jamii yetu, wapika chipsi huwa hawaoshi lile bakuli la kukorogea mayai kabla hayajakaangwa. Hii ni hatari kwa sababu chombo hicho kinaweza kikawa sababu ya kusambaza maradhi kwa watumiaji wa mayai.

10 August, 2015

Ugonjwa wa sukari ni chimbuko la chakula kisichofaa

Ni vigumu kujua aina ya chakula kinachokufaa, bila kujua jinsi mwili wako unavyokichakata. Kimsingi watafiti wamebaini makundi makuu matatu ya watu kuhusiana na jinsi miili inavyochakata chakula.

Chakula ambacho ni bora kwa mtu mmoja, kinaweza kuwa sumu baridi kwa mtu mwingine na kumletea madhara endelevu katika maisha yake. Kwa muktadha huu basi hakuna chakula bora kwa kila mtu. Chakula ni bora kwa mtu kama baada ya kukitumia mwili utakipokea vizuri, ukafyonza virutubisho na kikasaidia kuimarisha afya ya mlaji.

Ni vigumu kujua aina ya chakula kinachokufaa, bila kujua jinsi mwili wako unavyokichakata. Kimsingi watafiti wamebaini makundi makuu matatu ya watu kuhusiana na jinsi miili inavyochakata chakula.

Kundi la kwanza ni la wachakataji wa protini. Hawa miili yao inakubaliana zaidi na vyakula vya protini. Kwa watu wa kundi hili vyakula vya wanga na hususan vile vilivyochakatwa na kuchujwa kwa kiwango kikubwa (highly processed and refined), ni sumu baridi ambayo itawapelekea kuugua maradhi mengi ya kimfumo.

Kundi la pili ni la wachakataji wa wanga. Hawa miili yao inakubaliana zaidi na vyakula vya wanga. Kwa watu wa kundi hili la vyakula vya protini, hususan vile vilivyochakatwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kuwa na muda mrefu wa matumizi, ni sumu baridi ambayo itasababisha kuugua maradhi mengi ya kimfumo.

Kundi la tatu ni la wachakataji wa vyakula vya protini na wanga kwa viwango sawa. Kundi hili kidogo lina bahati, kwa maana, halidhuriwi kwa wepesi na vyakula vilivyoko katika yale makundi mawili ya mwanzo.

Moja ya magonjwa yanayosababishwa na mkanganyiko huu katika kula ni ugonjwa wa kisukari. Mchakataji wa protini anapokula chakula cha wanga, kasi ya kuchakata wanga huo ni kubwa mno ikilinganishwa na mlaji mwenzake ambaye ni mchakataji wa wanga.

Kasi hiyo husababisha kiwango cha sukari kinachoingia katika mzunguko wa damu ndani ya muda mfupi kuwa kikubwa sana. Kutokana na hali hii kongosho hulazimika kufanya kazi ya ziada kuzalisha kiwango kikubwa cha kichocheo kinachojulikana kama insulini ili kuondoa sukari kwenye damu na kuipeleka kwenye seli ili itumike kutengenezea nishati.

Hali hii ikijirudiarudia, kongosho huchoka na kuanza kufanya kazi chini ya kiwango au wakati mwingine vipokezi vya sukari katika seli (receptors) hushindwa kuendana na kasi ya kuletewa sukari kwa ajili ya matumizi ya seli hivyo huishia kuikataa sukari hiyo.

Hali hii kitaalamu hujulikana kama insulin resistance, au pingamizi dhidi ya insulini kwa tafsiri isiyo rasmi. Kuna baadhi ya nyakati, vyote hutokea kwa wakati mmoja, yaani kongosho linafanya kazi chini ya kiwango, na pia mgonjwa anakabiliwa na pingamizi dhidi ya insulini.

Hivi karibuni imebainika kuwa moja ya sababu kubwa sana zinazosababisha vipokezi vya seli kushindwa kupokea sukari inayoletwa ni kitu kinachoitwa mfuro (inflammation). Mfuro ni uvimbe kama lengelenge hivi. Mfano wa mfuro ni pale unapojikwaa au kujigonga usoni na mwili ukaumuka na kutengeneza nundu.

Vichocheo vya kusababisha mfuro kwenye seli viko vingi lakini baadhi ya hivi ni vyakula tunavyokula kila siku. Vyakula hivi ni pamoja na sukari na wanga uiliochakatwa kwa kiwango kikubwa.

Athari za ugonjwa

Kisukarini ni ugonjwa ambao unasababisha mololongo wa matatizo mengine ya kiafya mwilini. Matatizo haya ni pamoja na uharibifu wa macho, unaotambulishwa na magonjwa kama glaucoma ambao husababisha uharibifu wa neva za jicho.

Matatizo mengine ni ugonjwa ujulikanao cataracts ambao unatokana na ukungu kwenye lenzi ya jicho na retinopathy unaosababisha uharibifu katika retina ya jicho.

Matatizo mengine ni ya miguu yanayotambulishwa na magonjwa kama neurapathy ambayo ni maumivu yatokanayo na uharibifu wa mishipa ya fahamu, vidonda sugu vya tumbo na gangrene ambao ni mkusanyiko wa tishu zilizokufa kutokana na kutofikiwa na mzunguko wa damu.

Matatizo mengine ni yale ya magonjwa ya ngozi na magonjwa ya moyo.

Mpango mzuri wa kuudhibiti ugonjwa wa kisukari ni kuufuatilia kwa makini. Hii ina maana kuwa ni muhimu kufanya kipimo kila siku, ikiwezekana hata mara mbili au tatu kwa siku. Kutokana na hali hii gharama za kuufuatilia ugonjwa huu ni kubwa na huathiri kwa kiasi kikubwa hali ya kiuchumi ya mgonjwa.

Kwa mfano tu, hivi sasa katika zahanati na vituo vingi vya afya, gharama za kupima kisukari kwa mara moja ni kati ya Sh2,000 na Sh2,500.00. Unapomwambia mtu apime mara tatu kwa siku maana yake atumie kati ya Sh6,000 na Sh7,500.00 kila siku.

Ugonjwa wa kisukari kwa sasa kinaonekana kunyemelea hadhi ya kuwa ni janga la kijamii. Katika pande zote za dunia kisukari kinaongezeka badala ya kupungua. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), dunia inatarajiwa kuwa na wagonjwa wa kisukari milioni 366 mwaka 2030 kutoka wagonjwa milioni 171 waliokuwepo mwaka 2000.

Mwaka 2000 Tanzania ilikuwa na wagonjwa 201,600 na mwaka 2030 inatarajiwa kuongezeka maradufu na kufikia 605,000. Hili ni sawa na ongezeko la asilimia 66.7.

Hata hivyo janga la kisukari linaoonekana kuzikumba zaidi zile nchi ambazo raia wao wanapendelea mno vyakula vya wanga katika mitindo tofauti.

Vyakula hivyo ni soda, pasta, doughnut, keki, mikate, lambalamba, nakadhalika. Nchi kama Italy uwiano kati ya Wataliano wanaoumwa kisukari na wale ambao hawaumwi ni mtu mmoja kati ya 14. Inawezekana sababu kubwa ikawa ni ulaji wa piza, pasta na spaghetti. Hivi ni vyakula vinavyotengenezwa kwa ngano na Wataliano wanapenda kuvila kwa wingi.

Marekani uwiano wao ni mtu mmoja kwa kila watu 17. Hii nayo ni jamii ambayo inatumia soda, doughnut, chips, pizza, na vyakula vingine vya wanga vilivyochakatwa kwa kiwango cha juu. India uwiano wao ni mtu mmoja kati ya 39. Hawa nao ni mabingwa wa vitu vitamu. Wahindi wanapenda tamutamu za kila aina na sifa kuu ya vitu hivyo ni wingi wa sukari, ngano, mafuta na rangi.

Tanzania ina uwiano wa mtu mmoja kati ya 238. Huu ni uwiano mzuri sana ukilinganisha na nchi tulizotangulia kuzitaja. Sababu ya uwiano huu mzuri ni nini? Kimsingi sehemu kubwa ya Watanzania ni wala wanga zaidi kutokana na hali zao za kiuchumi?

Nadhani sababu kubwa ni ukweli kwamba Watanzania wengi ni wakaazi wa vijijini na kimsingi pamoja na kwamba sehemu kuwa ya chakula chao ni wanga, lakini kutokana na sababu za kiuchumi, wanalazimika kuula wanga huo katika mfumo ambao haujachakatwa.

06 August, 2015

Utafiti: Ukila vyakula vilivyotiwa viungo kila siku unajiongezea maisha marefu

post-feature-imageUtafiti mmoja uliofanywa nchini China umebaini kuwa ukila chakula kilichotiwa viungo kila siku unajiongezea maisha marefu.
Utafiti huo haswa umeonesha kuwa ukila chakula hususan pilipili utaishi maisha marefu zaidi duniani.
Watafiti mjini Baijing walidadisi maisha na vyakula wanavyokula wenyeji nusu milioni katika kipindi cha utafiti cha miaka 7.

Utafiti huo ulibaini kuwa wale waliokula chakula kilichojumuisha pilipili walikuwa katika hali bora zaidi kiafya wala hawakuwa katika hatari ya kuaga dunia. Hali yao ya siha ilitofautiana sana ikilinganishwa na wale ambao waliweka viungo katika vyakula vyao chini ya siku moja kwa juma .

Watafiti hao walitoa tahadhari.
Wanasema kuwa utafiti huo ulikuwa wa ushahidi tu lakini wakashauri utafiti zaidi ufanyika kwengineko ilikutilia pondo utafiti wao.
Hata hivyo walibaini kwa uhakika kuwa kiungo kinachopatikana katika pilipili, 'capsaicin' kinauwezo wa kupigana na seli zinazotuma ujumbe kwa ubongo kuwa mtu amezeeka na kusababisha viashiria vya utu uzima.

05 August, 2015

Vinywaji vya kusisimua akili, kutia mwili nguvu, vina athari za kiafya

post-feature-imageWatu hupenda kunywa vinywaji mbalimbali ambavyo huongeza nguvu hasa pale wanapojihisi wamechoka lakini wanataka kuona wanaendelea na kazi.
Wengine, hasa madereva, hupenda kutumia vinywaji hivi ili kuondoa uchovu na kuwafanya wasipate usingizi. Hufanya hivyo ili wasisinzie na kusababisha wasababishe ajali.

Kwa upande mwingine pia, wapo wanaokunywa vinywaji hivi vya kuongeza nguvu kama starehe au mbadala pale wanapokuwa hawatumii vilevi.

Duniani kote matumizi ya vinywaji vya kuongeza nguvu kwa sasa yameongezeka kuliko unavyofikiria. Takwimu zilizotolewa katika utafiti uliochapishwa mwaka 2009 katika jarida la ‘Drug Alcohol Dependence’ toleo la 99(1–3), zinaonyesha kuwa mwaka 2006 pekee, takribani aina mpya 500 za vinywaji hivi ziliingizwa sokoni.

Ongezeko hili kubwa la vinywaji vya kuongeza nguvu, linazua mashaka kwa wataalamu wa afya kuhusu usalama wa afya ya jamii. Hii ni kutokana na ukweli kuwa, matumizi makubwa ya vinywaji hivi yanaambatana na madhara ya afya ya mwili na akili kwa watumiaji.

Watanzania wengi hasa vijana kwa sasa wanapendelea kutumia vinywaji hivi kwa wingi. Kwa sasa soko la vinywaji baridi limejaa vinywaji vya kuongeza nguvu. Ni jambo la kawaida kuona watu wazima na watoto wakinywa vinywaji hivi safarini, katika sherehe mbalimbali na katika kumbi za starehe. Vinywaji hivi huuzwa kwa wingi katika maduka makubwa (Super markets), maduka madogo, hotelini na katika migahawa.

Miongoni wa watumiaji wakubwa wa vinywaji hivi ni wanamichezo na madreva hasa wa magari yanayofanya safari za masafa marefu, ambao wanaamini kuwa kwa kutumia vinywaji hivi huongeza nguvu za mwili, kasi ya vitendo, umakini na kupunguza uwezekano wa kupata usingizi. Watu wengi wanapotumia vinywaji hivi pia huvichanganya na pombe.

Vinywaji vya kuongeza nguvu, visivyo na kilevi,  kisayansi vinaelezwa vina kiasi kikubwa cha kafeini, vitamini pamoja na kemikali za taurine, glucuronolactone.

Wakati mwingine pia huongezewa dawa aina ya guarana pamoja na mitishamba aina ya ginseng kwa lengo la kusisimua akili na kuongeza nguvu za mwili.

Mtafiti wa madhara ya dawa za kulevya wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Dk Stephen Nsimba anasema kwamba vinywaji hivi vina kiasi kikubwa cha kafeini ambayo ni dawa inayosisimua ubongo na kwa kuvichanganya na pombe athari zake kwenye mfumo wa fahamu za mwili huongezeka.

“Baada ya kuchanganya vinywaji hivi, kafeini katika vinywaji vya kuongeza nguvu, hupunguza athari za kilevi na kumfanya mtumiaji asibaini haraka kuwa amekunywa kiasi kikubwa cha kilevi. Hili ni jambo la hatari” anaonya Dk Nsimba.

Habari mbaya zaidi ni kwamba baadhi ya watengenezaji wa vinywaji hivi huweka kiasi kikubwa cha kemikali kuliko inavyotazamiwa katika hali ya kawaida na hawaonyeshi katika lebo ama karatasi ya maelezo inayobandikwa kwenye kifungashio.

April mwaka jana, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TDFA) ilikamata makopo 1,526 ya vinywaji vya kuongeza nguvu katika soko la Tanzania ambavyo vilikuwa havikidhi viwango vya ubora na usalama kwa matumizi ya binadamu.

Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Mkurugezi wa TFDA, Hiiti Sillo aliyoitoa Aprili  3, 2014 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Matokeo ya utafiti mmoja yaliyowasilishwa katika mkutano wa mwaka 2013 wa Chama cha Afya ya Moyo cha Marekani (American Heart Association) uliofanyika katika mji wa New Orleans, ilibainika kuwa kunywa kopo moja hadi matatu ya vinywaji vya kuongeza nguvu, kunaweza kusababisha moyo udunde bila mpangilio na kuongeza shinikizo la damu.

Utafiti huo unaongeza kusema kuwa, hali kama hiyo inaweza kusababisha  kifo cha ghafla au magonjwa sugu kama vile shinikizo la damu, kisukari na kiharusi kwa baadhi ya watu.

Dk Gordon F. Tomaselli, ambaye ni msemaji wa American Heart Association (AHA) anasema: “Ingawa jambo hili linaoneka kama dogo lakini linaweza kusababisha madhara makubwa kwa baadhi ya watu. Wale walio na magonjwa ya moyo au historia ya magonjwa hayo katika familia zao, ni lazima wajiepushe na utumiaji wa vinywaji vya kuongeza nguvu.”

Baadhi ya watu wanaokuwa hawana habari kuwa wana magonjwa ya moyo hasa pale, ugonjwa unapokuwa katika hatua za mwanzo, wanaweza kuhatarisha maisha yao kwa kunywa vinywaji vya kuongeza nguvu ambavyo vina kiasi kikubwa cha kafeini.

Kiasi kikubwa cha kafeini kinaweza kusababisha shinikizo la damu, kuweweseka, kukosa usingizi, maumivu ya kichwa na degedege.

Baadhi ya watafiti wanabainisha kuwa vinywaji hivi pia vinaweza kusababisha ugonjwa wa kisukari.

Utafiti wa Dk. D.C. Greenwood na wenzake uliochapishwa katika jarida lijulikanalo kama Europian Journal of Epidemiology, toleo la 25(4) la mwaka 2010, unabainisha kuwa matumizi ya vinywaji vya kuongeza nguvu wakati wa ujauzito, unaweza kusababisha mimba kuharibika, kuzaa mtoto mfu au kuzaa mtoto mwenye uzito pungufu.

Kina mama wanaonyonyesha pia wanapotumia vinywaji hivi huwasababishia watoto wao matatizo ya kiakili ikiwa ni pamoja na kulia kupita kiasi.

Vijana wanaotumia vinywaji hivi, pia wanakabiliwa na hatari ya kutumbukia katika matumizi ya dawa za kulevya, tumbaku na ulevi wa pombe wa kupindukia.

Utafiti wa hivi karibuni nao umebaini kuwa vijana na watoto wanaotumia vinywaji hivi hupata athari za kiakili kiasi kwamba uwezo wao wa kujifunza na kutambua mambo unaathirika.

Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa T. Van Batenburg-Eddes na wenzake uliochapishwa katika jarida la Front Psychology toleo la 5, mwaka 2014.

Utafiti wa jeshi la Marekana uliochapishwa mwaka jana unabainisha kuwa, wanajeshi wengi wanaokunywa vinywaji vya kuongeza nguvu wanakabiliwa na hatari ya kujiua.

Utafiti huo unaongeza kusema kuwa wanajeshi wanaochanganya vinywaji vya kuongeza nguvu pamoja na pombe wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kujiua. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa H.B. Mash na wenzake uliochapishwa katika jarida la Social Psychiatry and Psychiatric Epidemiology, toleo la 49(9).

Kutokana na athari za vinywaji hivi kiafya, jamii inashauriwa kupunguza au kujiepusha na matumizi yake.

Ni busara pia mamlaka za kiserikali na kidini zinazohusika na usalama wa afya ya watoto zikasaidia kuielimisha jamii kwamba watoto na vijana walio chini ya miaka 18 wasitumie vinywaji hivi. Ni vyema vinywaji kama hivi vikapigwa marufuku.

17 July, 2015

Je,mbu hutambua vipi mwili wa mwanadamu usiku?


Utafiti mpya umebaini kwamba mbu hutafuta kitu cha kula kwa kutumia vigezo vitatu,harufu,macho na joto.
Utafiti huo unasema kuwa mbu anaweza kufahamu aliko mwanadamu kupitia hewa ya kaboni ambayo watu hupumua nje.
Inasemekana mbu hunusa hewa hii kiasi cha mita 50.
Wanasayansi wamesema kwamba walimfuatilia mbu mwenye njaa, ndani ya mtaro uliofunikiwa.
Kisha waligundua kwamba mbu hao walianza kunusa nusa hewa ya kaboni, na kutema mapovu yenye matone meusi yaliowekwa na watafiti hao sakafuni.null
Imebainika kwamba wakati mbu yuko mita chache karibu na kile anacholenga, huvutiwa sana na joto.
Hii imebainisha kwamba hata hufuata joto hilo na kisha kumshambulia mwanadamu.
Huenda ukapata Malaria au ukaponea lakini utakua na vipele pale vya mbu anapokuuma.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...