09 September, 2016

Video: Pipi ft Nikki wa Pili – Hafai

Msanii Pipi mwenye sauti tamu katika mziki wa Bongo fleva ameachia video yake mpya ya wimbo “Hafai”, amemshirikisha mkali wa Hiphop Nikki wa Pili. Video imeongozwa na kampuni ya Blue Image. Unaweza Kuupakua wimbo huo(Audio) kwa kubonyeza DOWNLOAD hapo chini

AudioMPYA:Bushoke- Mpita Njia

Ni Headlines za msanii kutoka Bongoflevani, Bushoke ambae ametuletea hii single yake mpya iitwayo ‘Mpita Njia’, wimbo umetayarishwa na producer Ema The Boy na Alan Mapingo. Bofya Download hapo chini kuupakua waimbo huo.

Video: Malaika "Rarua"

Hii ni time nyingine tena ya kuenjoy na mdundo mpya kutoka kwa staa wa bongo flavour Malaika ambaye alishawahi kumiliki mdundo wa ‘salesale‘ aliomshirikisha producer Mensen Selekta na sasa kaileta hii ya ‘Rarua

Video: TID ft Joh Makini – Confidance

Video mpya kutoka kwa msanii TID ya wimbo “Confidance”, amemshirikisha Joh Makini. Video imeongozwa na kampuni ya Kwetu Studios. Downlaod Audio hapo chini

Serena Williams atupwa nje kwenye michuano ya US Open

Serena Williams ameendelea kuharibu kwenye mashindano ya tennis baada ya hapo jana kuondolewa kwenye nusu fainali ya michuano ya US Open na mchezaji wa Jamhuri ya Czech, Karolina Pliskova.
381880bc00000578-0-image-a-4_1473382194216
Kwenye mchezo huo Karolina alifanikiwa kushinda kwa seti 6-2, 7-6 (3) katika mchezo uliofanyika kwa muda wa saa moja na dakika 26. Kwa sasa Pliskova atakutana na Kerber kwenye mchezo wa fainali siku ya Jumatatu.
38188a3e00000578-3780869-image-a-22_1473382710662
Mapema mwezi Agosti mwaka huu Serena na ndugu yake Venus Williams walitolewa kwenye raundi ya kwanza ya mchezo wa tennis wa wanawake wawili wawili kwenye michuano ya Olimpiki.
38187ad500000578-3780869-image-a-19_1473382609664
Serena alikuwa anatarajia kufikisha mataji 23 ya grand slam kwenye michuano hiyo na kuvunja rekodi ya Steffi Graf ya mataji 22 ambayo wanafanana kwa sasa.

06 September, 2016

New AUDIO: Chibau Mtoto Wa Pwani Ft.Nay TrueBoy - KAWIMBO

Chabai mtoto wa Pwani ni moja wa wasanii wa bongo flava ambao wamekaa kimya kwa muda mrefu, ila safari hii kaja na ngoma ijulikanayo kwa jina la KAWIMBO akiwa amemshirikisha rapper Nay TrueBoy, ngoma imetengenezwa na Producer Mr T-Touch. Bofya DOWNLOAD hapo chini kuupakua wimbo huo.

Wayne Rooney akerwa na mjadala juu yake

kaptein  
Nahodha wa timu ya Uingereza Wayne Rooney amesema kuwa majadiliano yanayoendelea kuhusu shughuli zake ndani ya timu hayana maana.

Rooney ambaye amecheza mechi yake ya 116, akicheza kama kiungo siku ya jumapili walishinda 1-0 dhidi ya slovakia, ambayo ilikuwa ni mechi ya kwanza chini ya meneja mpya Sam Allardyce's.Allardyce amesema kuwa mechi iliyopita hakuwa na la kusema kuhusu nafasi ya Rooney ilikuwa ipi na kucheza alivyotaka.
Rooney mwenye miaka 30 alisema " Nilicheza kwa nafasi yangu ili kusaidia timu yangu kushinda mchezo, japo mengi yalifanyika juu yake"
Akiongea na Sky Sport, kapteni wa timu ya Manchester United aliongeza kuwa" Nimekuwa nikifanya kazi yangu yote na ghafla ikawa habari kubwa, si jambo kubwa na nadhani kuna kutoeleweka kwa kiasi kikubwa juu ya hilo"
Nafasi ya Rooney kwenye Klabu yake na nchi imekuwa ikijadiliwa kwa kiasi kikubwa msimu huu na kwa rekodi ya wafungaji nchini Uingereza.

E! News; Lil-Wyne haja staafu Muziki- ni msongo wa mawazo!

 
Ni siku chache tuu baada ya rapper Lily wyne kutangaza kupita account yake ya Twitter kwamba anastaafu Muziki.Wayne aliteka vichwa vya habari kwa maneno haya “I AM NOW DEFENSELESS AND mentally DEFEATED & I leave gracefully and thankful I luh my fanz but I’m dun,” Kauli yake hiyo ilitafsiriwa na wadau mbali mbali kwamba Mkali huyo kaacha Muziki rasmi.

 0903-sub-lil-wayne-tmz-01 Kipindi cha E! News Marekani kimesema rapa Lil Wayne haja staafu muziki ila tweet zake kuhusu kuchoshwa na muziki zilitokana na msongo wa mawazo na mambo yake kutokwenda sawa hivi karibuni,

E! News imeripoti kuwa maneno hayo ya Lil Wayne yalitokana na msongo wa mawazo anaopitia kwa sasa rapa huyu na kwamba bado anapenda muziki na hana mpango wa kuacha kuimba, ameshaanza kurekodi kazi mpya.

Tecno kutoa Phantom 6 Septemba hii, itathibitisha ubora wake?


Tecno1.PNGSio suala jipya kwamba Bara la Afrika limegubikwa kwa kishindo na ulimwengu wa Smartphone (vijana wa mjini wanaziita simu janja). Ulimwengu huu umeshuhudia mapinduzi makubwa ya kiteknojia kwenye simu za mkononi. Urahisi huu umeonekana kwenye manunuzi, mahusiano, ajira, kupata taarifa kwa haraka zaidi n.k. Kampuni kubwa ya kutengeneza simu, TECNO, imegusia mwendelezo wa simu zake kali za PHANTOM mwezi wa Septemba.

Nimefuatilia kwa makini matoleo ya PHANTOM na kugundua kwamba bidhaa zao zimekuwa zikiwalenga watumiaji wa maisha ya kati. Sasa wanagusia kwamba toleo lao jipya litawalenga watumiaji wa maisha ya juu.

Swali linakuja... Je! Wataweza kuliteka soko Septemba hii? Kwa jinsi mambo yanavyoonekana, lengo hili linaweza kufikiwa au kuvukwa.

TECNO PHANTOM 6 itakuwa nit oleo jipya la TECNO lenye vitu vingi vya kuangaliwa katika teknolojia nzima ya utengenezaji wa Samrtphone

Betri inayochaji kwa haraka
Huu umekuwa ni wimbo wa taifa kwa watumiaji wa Smartphone. Sawa, kuna vitu vingi vya kufurahia lakini tatizo linakuja kwamba simu haikai na chaji sana. Inapokuja kwenye PHANTOM 6, port yake ya Type-C 2.0 USB ina uwezo wa kuchaji simu yako kutoka 0% mpaka 35% ndani ya dakika 10 tu.

Kamera ya mbele (13MP) + Kamera ya nyuma (5MP) 
  Sasa hapo ni mwendo wa kutwanga selfies na picha kali ukiwa na kamera zenye uwezo wa hali ya juu mbele na nyuma. Picha hizi zenye ubora wa kipekee zinazoongeza rangi na uhai kwenye matukio yako ya kukumbukwa huku zikikutoa mwakemwake kama vile haujapatwa na jua.
Muundo wa chuma
Habari nilizozipata kutoka kwenye vyanzo vya kuaminika ni kwamba, TECNO Phantom 6 itakuwa na ‘kava’ la chuma lilitengenezwa kwa umahiri wa hali ya juu na watu wanaoipenda kazi yao.

Umbo Jembamba


Inasemekana kuwa TECNO Phantom 6 itakuwa miongoni mwa simu nyembamba zaidi kutengenezwa duniani. Yaani utafikiri aliyekuwa anabuni muundo alikuwa kwenye ‘diet’

Bei
Ingawa TECNO Phantom 6 inategemewa kuwa ni miongoni mwa Smartphone zenye ubora wa hali ya juu, wataalamu wa mambo wanasema kwamba bei yake haitapishana na mfuko wa mwananchi.

cc TECNO TZ

05 September, 2016

Music: Moni Central Zone ft Geof Master – Vanilla & Strawberry

 
Ukiachana na kuwa ni mji mkuu wa taifa la Tanzania tu, Dodoma vilevile ndio makao makuu ya kundi la muziki la Central Zone, kundi ambalo anatoka mkali Moni. Bofya Download hapo chini kuupakua wimbo huo.

Nicki Minaj Drops “The Pinkprint Freestyle”

Video Image of Nicki Minaj in Bebe Rexha's' "NO BROKEN HEARTS" Video
Its been a minute since Nicki Minaj blessed us with a freestyle. Well here it is, inspired by Young M.A. “Ooouuu” got the New York reigning rap queen for close to six minutes (with a few breaks). And just when you think its over, she flips it on some Caribbean club ish (shout out to Shabba Ranks). So far the response has been overwhelmingly positive.
Check out the “The Pinkprint Freestyle” below:


loading...

Afcon 2017: Uganda yafuzu mara ya kwanza tangu 1978

Farouk Miya

Uganda imefuzu kwa mara ya kwanza kucheza katika fainali za Kombe la Mataifa Bingwa Afrika kwa mara ya kwanza tangu 1978 baada ya kulaza Comoros Jumapili.

Ushindi wao wa 1-0 uliwawezesha kufuzu kwa fainali zitakazochezewa Gabon mwaka ujao kama mojawapo wa mataifa mawili bora yaliyomaliza ya pili katika makundi.

Wapinzani wao Kundi D Burkina Faso pia walifuzu kwa ushindi wa dakika za mwisho wa 2-1 dhidi ya Botswana, ushindi uliowawezesha kuongoza kundini.

Tunisia na DR Congo pia zilifuzu baada ya kuongoza katika makundi yao.
Mataifa 16 yatashiriki michuano hiyo itakayoandaliwa 14 Januari hadi 5 Februari. Waliofuzu ni viongozi wa makundi yote 13, mataifa mawili bora yaliyomaliza ya pili hatua ya makundi, na wenyeji Gabon.

Algeria, Cameroon, Egypt, Ghana, Guinea-Bissau, Ivory Coast, Mali, Morocco, Senegal na Zimbabwe walijihakikishia nafasi kabla ya mechi za Jumapili.

Katika kufuzu, Uganda pia walifikisha alama 13, kupitia bao la dakika ya 35 la Farouk Miya mjini Kampala, lakini wakaorodheshwa wa pili kwa sababu walilemewa na Burkina Faso klabu hizo mbili zilipokutana.
Mara ya mwisho Uganda kucheza fainali za Kombe la Mataifa Bingwa Afrika ilikuwa miaka 38 iliyopita ambapo walimaliza wa pili baada ya kushindwa fainali an Ghana.

loading...

04 September, 2016

#Exclusive | Download Taswira - Emma Mopao

Emma Mopao ni mmoja wa wasanii wachache kufanya Afro Jazz Tanzania na huu ni wimbo wake mpya #Taswira unaobeba jina la album yake ambayo nayo ipo Mkito! #AfroJazz. Bofya DOWNLOAD hapo chini Kuupakua wimbo huo.

Mkutano wa mataifa ya G-20 waanza Uchina

Viongozi wa mataifa yenye uwezo mkubwa duniani wakongamana nchini Uchina
Mkutano wa mataifa yenye uwezo mkubwa duniani, G-20 umeanza rasmi siku ya Jumapili mjini Hangzhou huko China, huku viongozi wa mataifa hayo wakianza kuhutubu.
Katika misururu ya mikutano ya leo itakuwa tu hotuba kutoka kwa viongozi wa mataifa wanachama.
Maswala yanayojadiliwa ni pamoja na swala muhimu la usalama katika maeneo ya bahari ya kusini mwa China.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, kucheleweshwa kwa swala la kifedha, katika harakati za kufufua uchumi hususan miongoni mwa mataifa madogo madogo yanayokuwa kiuchumi.
Aidha amesifu Marekani na Uchina kwa kuridhia muafaka wa Paris kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa.
China imefanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa mkutano huo unafaulu.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...