06 August, 2015

Diamond na Zari wajaliwa mtoto wa kike


Msanii wa Bongo mwenye umaarufu wa kimataifa, Diamond Platnumz, maarufu, Naseeb Abdul, amepata majukumu mapya baada ya kujaliwa mtoto. Mkewe msanii huyo, Zarina Hassan, Zari the boss lady, alijifungua msichana mapema leo na kuipa furaha familia hiyo.
Baada ya kuokota tuzo tofauti kwenye mziki, Diamond hatimaye amepata tuzo kutoka kwa Mungu kwa kufanya juhudi nyingi za kutaka kuwa mzazi.
Diamond alipachika picha ya mtoto wake akibebwa na mamake, Sanura Kassim kwenye ukurasa wake wa Instagram na kupokea pongezi kutoka mashabiki.
Aidha, msanii huyo amemuanzishia mtoto wake ukurasa wa Instagram kwa jina Tiffah Dangote na kuvutia zaidi ya wafuasi elfu kumi na sita.
Diamond mwenye umri wa miaka 25, aliwashangaza wengi kwa kuanza kumfanyia bintiye ununuzi wa vifaa vya watoto kabla ya kuzaliwa.

Utamaduni wa kurejesha mahari marufuku Uganda


Mahakama ya juu zaidi nchini Uganda imesema kuwa utamaduni wa kurejesha mahari baadaya talaka katika ndoa za kitamaduni unakiuka katiba na utamaduni huo unapaswa kupigwa marufuku.
Uamuzi huo wa majaji saba katika mahakama hiyo umetolewa baada ya wanaharakati wa haki za wanawake kuwasilisha kesi mahakamani wakisiema kuwa utamaduni huo unawanyima wanawake haki zao.
Jaji mkuu wa Uganda Bart Magunda Katureebe amesema kuwa ikiwa utamaduni huo utaruhusiwa kuendelea itakuwa na maana kuwa wanawake ni kama bidhaa zinazouzwa sokoni.
Ngombe hutumiwa sana kulipa mahari Uganda
Lakini idadi kubwa ya majaji hao walikubaliana na uamuzi kwamba utamaduni wa utoaji mahari unapaswa kuendelea na kwamba haukiuki katiba.
Hata hivyo mmoja wa majaji hao alisema kuwa utamaduni huo unawadhalilisha wanawake na kwamba mahakama inapaswa kulifanya swala la ulipaji mahari kuwa chaguo na wala sio sharti.

Sudan Kusini:Mazungumzo ya amani yaanza


Mazungumzo mapya yanayolenga kumaliza mgogoro wa vita vya wenyewe kwa wenyewe wa miezi 19 Sudan Kusini yameanza katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Wapatanishi kutoka shirika la IGAD wanajaribu kuwarai rais Salva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar kutia sahihi mkataba wa amani kufikia mwezi Agosti.
Bwana Machar amesema kuwa makataa yaliowekwa ni vigumu kuyaafikia.
Baraza la makanisa lenye ushawishi mkubwa nchini humo limewataka viongozi hao wawili kusitisha vita hivyo mara moja ,likisema haikubaliki kwamba watu wanaendelea kufariki huku wao wakizozania mamlaka.

Kwamujibu wa Forbes, Hawa ndio waigizaji 10 wanaolipwa mkwanja mrefu zaidi duniani

post-feature-imageUsanii wa uigizaji katika filamu hutuacha na hisia tofuati tunapowatazama hasusan waigizaji nguli.
Lakini je, unafahamu kiasi cha fedha wanazolipwa kwa uigizaji wao ?
Jarida la Forbes limezindua orodha ya waigizaji bora na wanaolipwa mshahara wa juu zaidi duniani.
Jarida hilo limeangazia faida wanazopata baada ya kulipa gharama kama vile kodi na ada ya wasimmamizi wao. Kwa mwaka wa tatu mfululizo, muigizaji wa filamu ya Iron Man, Robert Downey Jr anaongoza orodha hiyo.

Downey Jr alitia kibindoni dola milioni $80m . Downey ameshiriki katika filamu za 'Avengers' na 'Age of Ultron'. Na kwa mara ya kwanza, orodha hiyo imewashirikisha waigizaji wanaoigiza nje ya Hollywood.

Hii inamaanisha kuwa wasanii watajika katika filamu nje ya Marekani kama vile Bollywood ya India na wasanii wa Asia pia wamejumuishwa katika orodha hiyo. Muigizaji nyota kutoka Uingereza Daniel Craig aliorodheshwa katika nafasi ya 15 sawa na Chris Hemsworth kutoka Australia.

Wawili hao walizoa takriban dola milioni $27m kwa mujibu wa Forbes. Msanii Jackie Chan wa filamu ya Karate Kid miongoni mwa nyingine nyingi tu, ameorodheshwa katika nafasi ya pili.

Chan alipokea dola milioni 50 mwaka uliopita kwa kazi yake.
Tazama Orodha kamili hapa

Hawa ndio wasanii wanaolipwa vyema kulingana na Forbes.


  1. Robert Downey Jr - $80m
  2. Jackie Chan - $50m
  3. Vin Diesel - $47m
  4. Bradley Cooper - $41.5m
  5. Adam Sandler - $41m
  6. Tom Cruise - $40m
  7. Amitabh Bachchan - $33.5m
  8. Salman Khan - $33.5m
  9. Akshay Kumar - $32.5m
  10. Mark Wahlberg - $32m

Je unamfahamu Edward Lowassa ni nani katika siasa za Tanzania? Huu ndio wasifu wake

post-feature-image
Umoja usio rasmi wa vyama vinne vya upinzani nchini Tanzania unajulikana kwa jina la Katiba ya Wananchi (UKAWA), baada ya kusubiri kwa muda hatimaye umemtangaza Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.
Lowassa anagombea kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), huku vyama vingine vitatu vikimuunga mkono. Hii inatokana na sheria za Tanzania ambayo haitambui umoja wa vyama.
Kabla ya kujiengua chama Tawala chama cha Mapinduzi CCM, Edward Lowassa amekuwa mwanachama wa CCM kwa muda wa miaka 38, ambapo alijiunga na chama hicho mara tu baada ya kumaliza elimu yake ya chuo kikuu mwaka 1977.

Hatua ya mwanasiasa huyo mashuhuri nchini Tanzania kuamua kujiunga na chama cha upinzani Chadema, ikiwa imebaki miezi mitatu tu kuelekea uchaguzi mkuu, kumebadilisha kabisa upepo wa kisiasa nchini Tanzania, na hasa uchaguzi mkuu ujao.

Lowassa alikuwa Maziri Mkuu kati ya mwaka 2005 na 2008 kabla ya kujiuzuLu wadhifa huo kufuatia sakata la kashfa ya rushwa iliyohusisha kampuni ya kuzalisha umeme ya ki-Marekani Richmond Development Company LLC ya Houston Texas.

Hata hivyo wakati anatangaza kuhamia kwake Chadema, Lowassa alikanusha katu katu kuhusika kwa namna yoyote na kashfa hiyo na kudai kuwa yeye alifuata tu amri kutoka kwa ‘wakubwa’ walio juu yake. “Kama kuna mtu yeyote mwenye ushahidi basi na aende mahakamani ama sivyo anyamaze” alisema Lowassa.

Kuhama kwake kunamfanya Lowassa kuwa ndie kiongozi wa kwanza wa ngazi ya juu kabisa wa CCM kukihama chama hicho tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania mnamo mwaka 1992.

Mwanajeshi wa zamani na aliyewahi kupigana wa vita kati ya Uganda na Tanzania mwaka 1978/79, Lowassa aliiambia hadhara kwamba akiwa kama mtu mwenye uchungu na nchi yake isingekuwa rahisi kubaki ndani ya CCM huku akiona chama hicho kimepoteza mwelekeo na sifa ya kuongoza nchi.

Lowassa amekimbilia upinzani baada jina lake kukatwa wakati alipoomba kuwa mgombea urais kupitia chama tawala CCM katika uchaguzi mkuu ujao utakafanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Wakati mchakato wa CCM wa kumtafuta mgombea wao wa urais ulipoanza, Lowassa ndiye aliyekuwa kinara wa wagombea wote 42. Kila kona aliyozunguka, mikutano yake ya hadhara ilivutia maelfu ya watu waliomuunga mkono.

Wakati chama cha CCM kilimtaka kila mgombea apate sahihi za wadhamini 450 lakini Lowassa alipata sahihi za wadhamini zaidi ya 700,000.
Hata hivyo mchujo wa chama ulipofanyika jina lake lilikatwa mapema kabla hata ya kupelekwa kwenye vikao vya vya juu vya chama hicho. Ambapo baadae Waziri wa Ujenzi John Pombe Magufuli ndiye aliyeibuka kidedea na kuwa mgombea kupitia chama tawala CCM.
Lowassa ameushutumu mchakato CCM wa kutafuta mgombea urais akiuita kuwa ulijaa chuki na mizengwe dhidi yake, hali ambayo aliifananisha na ‘ubakaji wa demokrasia’
“Nitakuwa mnafki nikisema bado nina imani na CCM. CCM niliyoiona Dodoma si CCM niliyokulia”, alisema, na kuongeza “kama Watanzania hawapati maendeleo kupitia CCM basi wakayatafute nje ya CCM”
Wakati sakala la Richmond lilipoibuka miaka michache tu iliyopita, Chadema ilimfanya limsakama Lowassa kuwa ni mmoja wa mafisadi wakubwa nchini. Lakini wakati chama hicho kinamkaribisha kuwa mwanachama wao, kiligeuka na kusema hakuna mtu msafi nchini na kwamba hawawezi kuacha kumpokea mwanasiasa mwenye mtaji mkubwa wa wafuasi kama Lowassa.
Wakati akiwa Waziri Mkuu, Lowassa alisifika kama mchapakazi hodari na msimamiaji wa moja kwa moja wa shughuli za serikali. Bado anaendelea kufahamika kwa jina la utani la ‘mzee wa maamuzi magumu’.
Moja ya mafanikio makubwa ya uwaziri mkuu wake ni jitihada kubwa na mafanikio ya upatikanaji wa fedha za kujenga chuo kikuu cha Dodoma. Chuo hiki kikuu cha umma kilichopo katikati ya Tanzania kilianzishwa mwaka 2007.
Lowassa ni mashuhuri pia kwa kusimamia mpango wa serikali uliofanikiwa wa ujenzi wa shule za kata ambazo uliiletea Tanzania sifa kubwa kwa kutoa fursa ya watoto wengi kupata nafasi shuleni.
Mtoto wa Mzee Ngoyai Lowassa, ambaye aliwahi kuwa mtumishi wa serikali ya kikoloni, Lowassa ameanza harakati zake za kuwania urais tangu mwaka 1995 lakini inaarifiwa kwamba rais wa kwanza wa Tanzania Mwl Julius Nyerere alimkatalia kushika nafasi hiyo. Wafuasi wa Lowassa wamekuwa wakiyatupilia mbali madai hayo
Ulipofika uchaguzi wa mwaka 2005, Lowassa hakutaka kuwania urais, lakini badala yake alimnadi rafiki yake wa siku nyingi Rais wa sasa Jakaya Kikwete ambaye alipata ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 80.

Utafiti: Ukila vyakula vilivyotiwa viungo kila siku unajiongezea maisha marefu

post-feature-imageUtafiti mmoja uliofanywa nchini China umebaini kuwa ukila chakula kilichotiwa viungo kila siku unajiongezea maisha marefu.
Utafiti huo haswa umeonesha kuwa ukila chakula hususan pilipili utaishi maisha marefu zaidi duniani.
Watafiti mjini Baijing walidadisi maisha na vyakula wanavyokula wenyeji nusu milioni katika kipindi cha utafiti cha miaka 7.

Utafiti huo ulibaini kuwa wale waliokula chakula kilichojumuisha pilipili walikuwa katika hali bora zaidi kiafya wala hawakuwa katika hatari ya kuaga dunia. Hali yao ya siha ilitofautiana sana ikilinganishwa na wale ambao waliweka viungo katika vyakula vyao chini ya siku moja kwa juma .

Watafiti hao walitoa tahadhari.
Wanasema kuwa utafiti huo ulikuwa wa ushahidi tu lakini wakashauri utafiti zaidi ufanyika kwengineko ilikutilia pondo utafiti wao.
Hata hivyo walibaini kwa uhakika kuwa kiungo kinachopatikana katika pilipili, 'capsaicin' kinauwezo wa kupigana na seli zinazotuma ujumbe kwa ubongo kuwa mtu amezeeka na kusababisha viashiria vya utu uzima.

DEPAY ANAUTAKA MFUPA ULIOMSHINDA DI MARIA, ATAUWEZA?

Depay 1
Nyota mpya wa Manchester United, Memphis Depay unaweza kusema amefanya maamuzi magumu ya kuvaa viatu vizito.
Kuelekea msimu ujao wa ligi kuu England unaoanza Jumamosi hii, Depay ameomba kupewa jezi ya heshima Old Trafford, namba 7.
Di Maria (left) poses with the No 7 shirt last summer upon his £60m arrival to the club from Real Madrid
Mshambuliaji huyo kinda amejitosa kuchukua jezi hiyo ya maana ambayo iliwahi kuvaliwa na masupastaa wa maana waliowahi kucheza Manchester United wakiwemo George Best, Bryan Robson, Eric Cantona, David Beckham na Cristiano Ronaldo na nyota wa sasa anayeondoka, Angel di Maria.
Inafahamika kwamba kocha wa United, Louis van Gaal bado hajatoa namba katika kikosi chake.
The Holland international's (right) request has  been looked favourably upon by United boss Louis van Gaal
Namba 9 pia iko wazi, lakini Van Gaal amevutiwa na maombi ya Depay kwani inaonesha jinsi gani Mholanzi huyo anajiamini.
Depay

Nick Minaj kuja na Mobile game yake

ick Minaj na kampuni iliyotengeneza game la Kim kardashian, Glu Mobile Inc wanashirikiana kutengeneza game jipya la Nick Minaj ambalo litatoka mwaka 2016. Kampuni hiyo imeamua kufanya na kazi na Nick Minaj baada ya mafanikio makubwa iliyopata kutokana na Game la Kim kardashian   ‘Kim Kardashian: Hollywood’  ambalo mpaka sasa ni game iliyonunuliwa zaidi kupitia duka la mtandaoni la Apple Marekani

NEW SONG: KRISH GENIUS – GOOD DIE YOUNG

Christopher-Martin 1Mwimbaji wa Reggae nchini Jamaica maarufu kwa jina la  Christopher Martin ameachia single yake mpya inayoitwa  ‘Good Die Young’ kutoka kwenye album yake ya ‘Music without Rules’ iliyokamilika chini ya ‘Cr2O3 Records. Hivyo basi ukiwa kama shabiki wa muziki wa Reggae chukua time hii kuisikiliza hiyongoma hapa

Messi alivyokasirika akampiga kichwa huyu jamaa wa AS Roma.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina anaeichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania Lionel Messi alishindwa kuzuia hasira zake baada ya kupigwa kikumbo na Mapou Yanga-Mbiwa wa klabu ya AS Roma ya Italia, tukio hilo lilitokea katika mchezo wa kirafiki ambapo timu zote mbili zilikuwa zinautumia mchezo huo kama sehemu ya maandalizi ya mwanzo wa msimu.
Barcelona-v-Roma
Messi akiwa na hasira alimfuata Yanga-Mbiwa na kumpiga kichwa na mwamuzi aliwaonya kwa kuwaonyesha kadi za manjano wote wawili,mchezo ulimalizika kwa FC Barcelona kushinda kwa jumla ya goli 3-0 magoli ambayo yaliwekwa wavuni na wachezaji Neymer dakika ya 26, Messi dakika ya 41 na Rakitic akaitimisha goli la mwisho dakika ya 66 ya mchezo.
Barcelona's Lionel Messi, right, and Roma’s Mapou Yanga-Mbiwa get involved in a scuffle during the Joan Gamper trophy soccer match between FC Barcelona and AS Roma at the Camp Nou stadium in Barcelona, Spain, Wednesday, Aug. 5, 2015. (AP Photo/Francisco Seco)

messi-yanga-barcelona-roma_1008y8l3pt7911gg6266p37hqu
Nimekusogezea video ya tukio lenyewe

05 August, 2015

Wakimbizi wa Somalia warejesha kwao

Wakimbizi wa kwanza 100 wamerejeshwa Somalia kufuatia makubaliano kati ya Shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikia maswala ya wakimbizi,UNHCR na serikali ya Kenya na Somalia.
malia
Uhamisho huo wa kujitolea wa wakimbizi umeafikiwa baada ya Kenya kutishia kuwafurusha wakimbizi wa Somalia baada ya mashambulizi ya kigaidi yaliyotekelezwa na kundi la wapiganaji kutoka Somalia al Shaabab.Awali Kenya ilikuwa inawasafirisha wakimbizi kwa mabasi lakini kutokana na changamoto za kiusalama katika eneo la Kaskazini Mashriki mwa Kenya ,UNHCR imeanzisha safari za moja kwa moja kutoka Daadab kwenda Somalia.
ds
Kiongozi wa UNHCR bwana Raouf Mazou anasema kuwa ”huu ni mwanzo mpya””Ndege za kwanza mbili, zimeondoka Daadab kuelekea Kismaayona miji mingine midogo ya Luuq na Baidoa.”Serikali ya Kenya ilikuwa imetishia kuwafurusha wakimbizi wa Somalia kutoka kwenye kambi ya Dadaab kufuatia ripoti za kijasusi zilizoeleza kuwa njama zote za mashambulizi ya Kundi la wapiganaji wa Kiislamu kutoka Somalia,Al Shabaab yalikuwa yakipangwa na kufanikishwa kutoka Dadaab.
ds2Kenya ilitoa amri hiyo punde baada ya wanamgambo wa kiislamu wa Al Shabaab kuwaua wanafunzi wakristu takriban 150 katika chuo kikuu cha Garissa mapema mwezi Aprili.

The Sexy Idris Elba breaks record on a Solo Cover for Maxim magazine

Your boyfriend is hot hot....oooppss Your's and many other ladies i know,lol...

 This British hottie has broken the record twice within just three months...first, he broke the record by driving a Bentley on sand at a 180.361 mph...i hope i got that info right
 And now,he appears on the cover of Maxim magazine alone..a magazine which has a reputation of using women or couples on their covers...and never a solo male
 And we loooove the photoshoot
Stylish,hot and sexy plus with a British accent...dayuuum,what is there not to like about this man!

Vinywaji vya kusisimua akili, kutia mwili nguvu, vina athari za kiafya

post-feature-imageWatu hupenda kunywa vinywaji mbalimbali ambavyo huongeza nguvu hasa pale wanapojihisi wamechoka lakini wanataka kuona wanaendelea na kazi.
Wengine, hasa madereva, hupenda kutumia vinywaji hivi ili kuondoa uchovu na kuwafanya wasipate usingizi. Hufanya hivyo ili wasisinzie na kusababisha wasababishe ajali.

Kwa upande mwingine pia, wapo wanaokunywa vinywaji hivi vya kuongeza nguvu kama starehe au mbadala pale wanapokuwa hawatumii vilevi.

Duniani kote matumizi ya vinywaji vya kuongeza nguvu kwa sasa yameongezeka kuliko unavyofikiria. Takwimu zilizotolewa katika utafiti uliochapishwa mwaka 2009 katika jarida la ‘Drug Alcohol Dependence’ toleo la 99(1–3), zinaonyesha kuwa mwaka 2006 pekee, takribani aina mpya 500 za vinywaji hivi ziliingizwa sokoni.

Ongezeko hili kubwa la vinywaji vya kuongeza nguvu, linazua mashaka kwa wataalamu wa afya kuhusu usalama wa afya ya jamii. Hii ni kutokana na ukweli kuwa, matumizi makubwa ya vinywaji hivi yanaambatana na madhara ya afya ya mwili na akili kwa watumiaji.

Watanzania wengi hasa vijana kwa sasa wanapendelea kutumia vinywaji hivi kwa wingi. Kwa sasa soko la vinywaji baridi limejaa vinywaji vya kuongeza nguvu. Ni jambo la kawaida kuona watu wazima na watoto wakinywa vinywaji hivi safarini, katika sherehe mbalimbali na katika kumbi za starehe. Vinywaji hivi huuzwa kwa wingi katika maduka makubwa (Super markets), maduka madogo, hotelini na katika migahawa.

Miongoni wa watumiaji wakubwa wa vinywaji hivi ni wanamichezo na madreva hasa wa magari yanayofanya safari za masafa marefu, ambao wanaamini kuwa kwa kutumia vinywaji hivi huongeza nguvu za mwili, kasi ya vitendo, umakini na kupunguza uwezekano wa kupata usingizi. Watu wengi wanapotumia vinywaji hivi pia huvichanganya na pombe.

Vinywaji vya kuongeza nguvu, visivyo na kilevi,  kisayansi vinaelezwa vina kiasi kikubwa cha kafeini, vitamini pamoja na kemikali za taurine, glucuronolactone.

Wakati mwingine pia huongezewa dawa aina ya guarana pamoja na mitishamba aina ya ginseng kwa lengo la kusisimua akili na kuongeza nguvu za mwili.

Mtafiti wa madhara ya dawa za kulevya wa Chuo Kikuu cha Dodoma, Dk Stephen Nsimba anasema kwamba vinywaji hivi vina kiasi kikubwa cha kafeini ambayo ni dawa inayosisimua ubongo na kwa kuvichanganya na pombe athari zake kwenye mfumo wa fahamu za mwili huongezeka.

“Baada ya kuchanganya vinywaji hivi, kafeini katika vinywaji vya kuongeza nguvu, hupunguza athari za kilevi na kumfanya mtumiaji asibaini haraka kuwa amekunywa kiasi kikubwa cha kilevi. Hili ni jambo la hatari” anaonya Dk Nsimba.

Habari mbaya zaidi ni kwamba baadhi ya watengenezaji wa vinywaji hivi huweka kiasi kikubwa cha kemikali kuliko inavyotazamiwa katika hali ya kawaida na hawaonyeshi katika lebo ama karatasi ya maelezo inayobandikwa kwenye kifungashio.

April mwaka jana, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TDFA) ilikamata makopo 1,526 ya vinywaji vya kuongeza nguvu katika soko la Tanzania ambavyo vilikuwa havikidhi viwango vya ubora na usalama kwa matumizi ya binadamu.

Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Mkurugezi wa TFDA, Hiiti Sillo aliyoitoa Aprili  3, 2014 wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Matokeo ya utafiti mmoja yaliyowasilishwa katika mkutano wa mwaka 2013 wa Chama cha Afya ya Moyo cha Marekani (American Heart Association) uliofanyika katika mji wa New Orleans, ilibainika kuwa kunywa kopo moja hadi matatu ya vinywaji vya kuongeza nguvu, kunaweza kusababisha moyo udunde bila mpangilio na kuongeza shinikizo la damu.

Utafiti huo unaongeza kusema kuwa, hali kama hiyo inaweza kusababisha  kifo cha ghafla au magonjwa sugu kama vile shinikizo la damu, kisukari na kiharusi kwa baadhi ya watu.

Dk Gordon F. Tomaselli, ambaye ni msemaji wa American Heart Association (AHA) anasema: “Ingawa jambo hili linaoneka kama dogo lakini linaweza kusababisha madhara makubwa kwa baadhi ya watu. Wale walio na magonjwa ya moyo au historia ya magonjwa hayo katika familia zao, ni lazima wajiepushe na utumiaji wa vinywaji vya kuongeza nguvu.”

Baadhi ya watu wanaokuwa hawana habari kuwa wana magonjwa ya moyo hasa pale, ugonjwa unapokuwa katika hatua za mwanzo, wanaweza kuhatarisha maisha yao kwa kunywa vinywaji vya kuongeza nguvu ambavyo vina kiasi kikubwa cha kafeini.

Kiasi kikubwa cha kafeini kinaweza kusababisha shinikizo la damu, kuweweseka, kukosa usingizi, maumivu ya kichwa na degedege.

Baadhi ya watafiti wanabainisha kuwa vinywaji hivi pia vinaweza kusababisha ugonjwa wa kisukari.

Utafiti wa Dk. D.C. Greenwood na wenzake uliochapishwa katika jarida lijulikanalo kama Europian Journal of Epidemiology, toleo la 25(4) la mwaka 2010, unabainisha kuwa matumizi ya vinywaji vya kuongeza nguvu wakati wa ujauzito, unaweza kusababisha mimba kuharibika, kuzaa mtoto mfu au kuzaa mtoto mwenye uzito pungufu.

Kina mama wanaonyonyesha pia wanapotumia vinywaji hivi huwasababishia watoto wao matatizo ya kiakili ikiwa ni pamoja na kulia kupita kiasi.

Vijana wanaotumia vinywaji hivi, pia wanakabiliwa na hatari ya kutumbukia katika matumizi ya dawa za kulevya, tumbaku na ulevi wa pombe wa kupindukia.

Utafiti wa hivi karibuni nao umebaini kuwa vijana na watoto wanaotumia vinywaji hivi hupata athari za kiakili kiasi kwamba uwezo wao wa kujifunza na kutambua mambo unaathirika.

Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa T. Van Batenburg-Eddes na wenzake uliochapishwa katika jarida la Front Psychology toleo la 5, mwaka 2014.

Utafiti wa jeshi la Marekana uliochapishwa mwaka jana unabainisha kuwa, wanajeshi wengi wanaokunywa vinywaji vya kuongeza nguvu wanakabiliwa na hatari ya kujiua.

Utafiti huo unaongeza kusema kuwa wanajeshi wanaochanganya vinywaji vya kuongeza nguvu pamoja na pombe wanakabiliwa na hatari kubwa zaidi ya kujiua. Hii ni kwa mujibu wa utafiti wa H.B. Mash na wenzake uliochapishwa katika jarida la Social Psychiatry and Psychiatric Epidemiology, toleo la 49(9).

Kutokana na athari za vinywaji hivi kiafya, jamii inashauriwa kupunguza au kujiepusha na matumizi yake.

Ni busara pia mamlaka za kiserikali na kidini zinazohusika na usalama wa afya ya watoto zikasaidia kuielimisha jamii kwamba watoto na vijana walio chini ya miaka 18 wasitumie vinywaji hivi. Ni vyema vinywaji kama hivi vikapigwa marufuku.

Mastaa wa soka na vioja vyao Uwanjani

Wachezaji mpira ni miongoni mwa watu maarufu sana kutokana na kazi yao kupendwa au kuwa na mashabiki wengi kutoka sehemu mbalimbali, miongoni mwa vitu ambavyo huwezi kuvidhania kama unaweza kuviona kwa mastaa wako wa soka ambao umezoea kuwaona wakiwa katika muonekano uliozoeleka kuonekana labda wakiwa katika mechi au matukio ya kawaida.
Katika pitapita zangu mtandaoni nimekutana na hii list ya mastaa wa soka waivyoamua kujiachia kwa vioja kabisa.
Dani Alves
download (1)
Dani Alves aliwahi kuvaa wigi wakati akisherehekea ushindi wa Timu yake ya Taifa
Andrey Arshavin
download (2)
Ni mchezaji wa zamani wa Arsenal anatajwa kuwa sio miongoni mwa watu wanaouchukulia mchezo wa mpira wa miguu serious.. Ndani ya Uwanja akaona afanye kioja kupindisha uso wake.
Mario Balotelli
download (3)
Chochote anachokifanya Balotelli huwa hakiko mbali na headlines za Waandishi wa Habari.
Antonio Cassano
download (4)
Antonio Cassano akishangilia ushindi wa goli 2-0 Italy ilivyoifunga Ufaransa katika michuano ya Euro 2008.
Zlatan Ibrahimovic
download (6)
Zlatan Ibrahimovic wakati alipovua nguo Uwanjani bila hofu kabisa.
Stephen Ireland
download (7)
Kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester City Stephen akishangilia goli kwa staili ya kuvua bukta
David Luiz
download (8)
David Luiz beki ghali wa klabu ya PSG ya Ufaransa akishangilia goli

Meek Mill amdiss tena Drake akiwa kwenye show.

meek mil
Rapa Meek mill amerudi na dis nyingine baada ya Drake kumkalisha na Back To Back, Meek Anasema “wasanii kama Lil Wayne, Tyga, Na Birdman hawampendi, show zake zimejaa wauwaji , kila mtu anapigwa risasi, nikikutana na Drake ntaiweka suruale yake katikati ya makalio [Subii] ” .
Hata hivyo hakuna ushahidi kuwa Wayne ana beef na Drake sababu hivi karibuni walikuwa pamoja kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa ya meneja wao Mack Maine.

ANGEL DIMARIA ATAJUTIA KWA YALIYOTOKEA

DI MARIAWakati Manchester United ikimsajili mchezaji Angel Di maria kutoka Real Madrid msimu uliopita, kila mmoja alidhania kuwa wamepata professional na mchezaji wa kiwango cha dunia.
Real Madrid walijitahidi kadiri ya uwezo wao kumzuia asiondoke mchezaji huyo aliyekuwa uti wa mgongo katika kufanikisha ‘La Dacima’ kombe la kumi la UEFA champions league, lakini tayari Dimaria alikua kaisha itengeneza akili yake kuondoka huku akiviamsha usingizini vilabu vya Manchester United na PSG kuwania saini yake.
PSG ndio waliokuwa kipaumbele kumsaini lakini Real Madrid walikataa kumkopesha baada ya PSG kubanwa na sheria ya matumizi ya pesa ya UEFA, financial fair play. Hatua hiyo ikampa faida Ed Woodward kumleta Old Trafford kwa ada ya pauni 60m. Hapa mambo hayakwenda sawa kwa Dimaria na bila shaka anatamani asahau haraka.
Kwanza, Dimaria alitua Old Trafford na kukabidhiwa jezi namba 7 ambayo katika historia ya klabu ya Manchester United, ina matarajio makubwa sana na Dimaria akashindwa kuitendea haki.
Pili, Dimaria alikuja Old Trafford kwa ada kubwa kabisa ya uhamisho na kuweka rekodi ya klabu na ligi kuu nchini England. Ada ya pauni 59.7m na sasa anaondoka kwa pauni 44.4m ni dhihaka kubwa kwa Dimaria mwenyewe na hasara kwa klabu.

Tatu, ahadi na maneno yake mazuri ya kutua Old Trafford vyote vimeyeyuka. Dimaria aliwahi kusema Manchester United ingekua timu yake ya mwisho kuichezea barani ulaya kabla ya kurudi kwao Argentina. Leo hii amejikuta akichukiwa sana na mashabiki wa Manchester United na pia ni doa katika CV yake.
Mwisho, mashabiki na klabu zinastahili kulipwa fadhira zao kutoka kwa wachezaji. Wachezaji pia wanatakiwa kuishi kiume na kusema wazi wazi hisia zao ili wasijikute wanawakera mashabiki zao na kuzipa hasara klabu. Dimaria anajikuta mnafiki na mtu asiye mueledi kutokana na yote yaliyomtokea katika career yake hadi hivi sasa.
Hatimaye yote niliyoyaandika hapo juu yana madhara makubwa kabisa katika maisha ya Dimaria aidha kiakili ama kimwili. Zaidi ya mashabiki 650m wa Manchester United duniani kote, sasa wanamchukia Dimaria na hilo litamtesa mchezaji huyo. Atajutia sio tu kuondoka United, bali Real Madrid.
Real Madrid ndio wanaoendelea kummiss zaidi kwani alikuwa mmoja wa waliokuwa uti wa mgongo wa timu na hata pengo lake linaonekana tofauti na Manchester United ambako hakua na msaada wowote.

KASEJA, TEGETE KUTUA MWADUI FC

TegeteAliyekuwa golikipa wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na vilabu vya Simba na Yanga Juma Kaseja na mshambuliaji wa zamani wa Yanga Jerryson Tegete huenda wakajiunga na klabu ya Mwadui FC kama mambo ya klabu hiyo yataenda kama yalivyopangwa.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema pamoja na kukamilisha usajili wa wachezaji waliokuwa wanawahitaji, lakini bado nafasi ipo kwa ajili ya Juma Kaseja na Jerry Tegete kwani wakipewa nafasi wanaweza wakaonesha uwezo mkubwa.
“Mimi nimeshamaliza usajili, nimeshasajili wachezaji 26 wanatosha, wachezaji pekee ambao kama mipango yangu itaenda sawasawa basi kuna mpango wa kuwaongeza Juma Kaseja na Jerry Tegete. Kwasababu ni wachezaji ambao nimezungumza nao na wameniambia wanataka kucheza na hawakuweka mbele kipato, mimi wamenivutia kwasababu tunapokuwa na wachezaji kwenye timu tunataka tuwatumie kucheza ili tupate mafanikio kwenye ligi”.
juma-kaseja1“Lakini kunawachezaji ambao hawaperfom inabidi tuwatoe kwenye dirisha dogo la usajili, lakini ukiwa na wachezaji wazuri wenye kuonesha commitment ambao wanataka kucheza kuisaidia timu yao sioni kwanini nisiwachukue kwasababu namba bado inatosha”.
Kwa usajili wa wachezaji wa kigeni unaofanywa na baadhi ya vilabu vya ligi kuu hapa nhini Julio amesema yeye hatishwi na usajili huo kwani yeye ni Kocha mkubwa na anatambua uwezo wa wachezaji wengi na hata pale anapowaita wachezaji haoni kama ni wazee na anatambua kuwa ni wachezaji wenye uwezo mkubwa”.
“Mimi kwanza sitishiki na usajili wa Azam, Simba na Yanga, wao wamevutika na wachezaji wao wa nje kwasababu zao binafsi kwanza wanafedha,Yanga wanatarajia wakiwa na wachezaji wa kigeni watafanikiwa kwasababu wanacheza mashindano ya Afrika wanataka kuingia kwenye ‘Super eight’ ili wafanikiwe. Mimi sidhani kama hilo litafanikiwa”.
Lakini Azam hivyohivyo nao japokuwa juzi wamechukua ubingwa wamefanya vizuri nimeona timu yao sio mbaya sana, Simba wamepoteza ubingwa kwa takribani miaka mitatu kwahiyo wanategemea wakiwa na wachezaji wa nje basi wanaweza wakafanya kile kitu wanachokitarajia na watapata ubingwa lakini sioni kama itafanikiwa vilevile”.
Msikilize Julio hapa chini akieleza nia yake ya kuwasajili Kaseja na Tegete

WASHAMBULIAJI WATANO WANAOTEGEMEWA KUFANYA MAKUBWA EPL 2015/16

dara ya ushambuliaji inawezekana ndiyo idara muhimu sana na inayoangaliwa na watu wengi sana uwanjani, sina maaana kuwa soka linachezwa sehemu ya mbele pekee la hasha…., soka linachezwa klia kona ya uwanja ila wazungu hawakuwa wapuuzi waliposema “Striker life is in the goal scores”, wakiwa na maana kuwa maisha ya mshambuliaji yapo katika ufungaji, ukiwa mshambuliaji bila shaka assist ni kitu cha ziada ila kazi yako wewe ni kufunga tuu. Kutokana na hayo sio vibaya leo tukitazama baadhi ya wachezaji ambao baadhi ya mashabiki na wachambuzi mbalimbali wa soka wanategemea makubwa kutoka kwao kwenye idara ya kutikisa nyavu msimu ambao pazia lake tayari limefunguliwa juzi kwenye mchezo wa ngao hisani kwa “mbwatukaji” kupata kipigo kitakatifu kutoka kwa “Petit” Wenger. Naomba tuungane pamoja hapa chini kutazama washambuliaji watano ambao washabiki wanategemea kupata magoli Zaidi ya 19 kutoka kwao msimu ujao…….
5> Aleksandar Mitrovic
Mitrovic
Mashabiki wengi wa Epl wanatarajia mshambuliaji mpya wa Newcastle aliyesajiliwa kwa Euro 12M kutoka Anderlech ya Ubelgiji, Aleksandar Mitrovic kufanya makubwa kwenye ligi yenye ushindani barani Ulaya, matarajio haya yanakuja kutokana na kiwango alichokionyesha Mserbia huyu kwenye mechi ya Champion League msimu uliopita pale timu yake iliposawazisha magoli matatu dhidi ya Arsenal. Huyu jamaa alianza kupata uzoefu mapema kabisa tangu akiwa na umri wa miaka 20. Msimu uliopita alifunga magoli 20 katika ligi na kuwa mfungaji bora kwenye ligi ya ubelgiji. Pia katika mechi 69 alizocheza amefunga jumla ya magoli 36, ikiwa ni wastani wa karibu goli 1 katika mechi 2. Kutokana na kiwango chake, timu za Roma na Porto zilionyekana kuvutiwa naye sana ila mwisho wa siku alitua Saint James Park.
4> Harry Kane
Tottenham Hotspur's Harry Kane celebrates scoring his side's first goal of the game during the Barclays Premier League match at White Hart Lane, London.
clays Premier League match at White Hart Lane, London.
Hatimaye baada ya Roberto Soldado kuonekana kufanya vibaya katika idara ya ufungaji, Mauricio Pochettino aliamua kumpa nafasi kinda wa kiingereza Harry Kane na kufunga magoli 21 msimu uliopita na miongoni mwa magoli hayo ni yale aliyowafunga wapinzani wao wa London, Chelsea na Arsenal. Kutokana na kiwango chake msimu uliopita ni wazi tayari Kane ameshawafahamu mabeki wa Epl na jinsi ya kukabiliana nao. Idadi ya magoli inatarajiwa kuongezeka msimu ujao kwani utakuwa mnafiki kama ukiambiwa utaje wamaliziaji wazuri kwa sasa pale Epl alafu ukamuacha kinda huyu wa miaka 22. Tottenham itakuwa na ratiba nzuri kwani katika mechi 6 itakazo anza watakutana na timu moja pekee katika zile 8 zilizomaliza juu msimu uliopita. Hapa Kane ndo mahali ambapo anatarajiwa kuwaonea Mabeki wa timu hizi na kuanza kuweka akiba ya magoli mapema kabisa.
3> Wayne Rooney
rooney
Kuondoka kwa Robin Van Persie na Radamel Falcao, kunamfanya Wayne Rooney mpaka sasa kuwa tegemeo la Manchester United kule mbele hasa kutokana na United kutopata mshambuliaji wa kueleweka mpaka sasa japokuwa dirisha la usajii bado halijafungwa. Usajili wa viungo makini Schneiderlin na Schweinsteiger bila shaka utaimarisha idara ya kiungo na kumpa nafasi Rooney kucheza sana pale mbele na kuwa na uwanja mpana sana wa kufanya makubwa katika ufungaji. Tayari LVG ameshampa uhakika wa kuanza kila mechi kutokana na yeye kuwa nahodha wa timu. Kumbuka aliwahikufunga magoli 27 msimu wa 2011/12 na pia alitupia magoli 26 kwenye msimu wa 2009/10, misimu yote hiyo alipewa majukumu ya kucheza kama namba 9. Endapo LVG atafanya hivi ni wazi kuwa mfumo wowote atakao utumia na Rooney kucheza mbele bado atafanikiwa kupata magoli anayo yahitaji ili kuwa mshambuliaji wa pili kuwa na magoli mengi pale Epl.
2> Diego Costa
costa
Mshambuliaji hatari wa Ki Brazil anayecheza timu ya taifa ya Spain, Diego Costa”The governor”, anatarajiwa kumaliza msimu na magoli Zaidi ya 25 kama hatopata majeraha ya mara kwa mara kama msimu uliopita. Msimu uliopita alifunga magoli 20 katika mechi 26 kwenye msimu wake wa kwanza wa Epl, endapo kama sio Majeraha ni wazi hakuna mtu ambaye angemkamata Diego katika ufungaji wa EPL, kumbuka hakuwa na goli hata moja la penati katika magoli yake yote. Kutokana na support atakayo ipata kutoka kwa viungo wakabaji na washambuliaji ambao siku zote wapo nyuma yake, Oscar, Hazard na Willian ni wazi Diego ataendelea kupata huduma nzuri na kutupia nyavu mara kibao, pia assist za Cesc zitazidi kumuweka juu mchezaji huyu ambaye mpaka sasa hajafahamu lugha ya kiingreza licha ya kukaa takribani mwaka mzima pale London. Kumbuka Chelsea itakutana na Man City pamoja na Arsenal katika mechi 6 za mwanzo. Endapo diego atakuwa fiti bila majeraha naamini ataanza vizuri katika mechi hizi
1> Sergio Aguero
aguero
Hatutaweza kushangaa endapo Jamaa lenye nguvu na kasi kutoka Argentina, Sergio Aguero kuwa mfungaji bora wa ligi kwa mara nyingine tena. Amekuwa na mwendelezo mzuri wa kufunga kwenye michuano ya Copa America baada ya kufunga magoli 3 katika mechi 5, kumbuka msimu uliopita alimaliza na magoli 26 katika mechi 33 huku akitoa assist 10. Kutokana na kiwango chake ni wazi Aguero atakuwa na msimu mwingine mzuri hasa kutokana na kuwa mzoefu kwenye Epl kwa muda sasa, kingine pia huyu jamaa ndo mpiga penati za ndani ya uwanja hivo bado ana faida ya kuzidi kuongeza magoli hasa baada ya usajili wa Raheem ambaye anapenda ku drible hadi kwenye box za wapinzani.

Albamu Ya Dr.Dre Ya “Compton” Itatoka Kwa Mara Ya Kwanza Mtandaoni

Albamu ya “The Chronic” rapper Dr. Dre itatoka kwenye mtandao lakini haitakuwa halisi yenyewe lakini kupitia kwenye mitandao ndio itakuwa sehemu ya kwanza kusikiliza mzigo huo.

Albamu hiyo inayokuja ya “Compton” itapatikana kupitia Apple Music kuanzia saa 6pm-9pm PST siku ya Alhamisi Agosti 6, taarifa kupitia Beats 1 radio zimetengazwa na mtangazaji Zane Lowe.

“Listen to the premiere of @drdre new album, Compton,” (August 4). “Uncensored & exclusively on @AppleMusic.” Aliandika Lowe

Dr. Dre alitangaza albamu hiyo siku ya Jumamosi Agosti 1, kupitia kipindi chake cha “The Pharmacy” kupitia radio ya Beats 1, kwenye albamu hiyo ameshirikishwa Eminem, The Game, Kendrick Lamar, Jon Connor, Snoop Dogg, King Mez na wengine, albamu hiyo imepangwa kutoka Jumamosi Agosti 8.

Mwanzilishi huyo wa Aftermath alisema alivutiwa na filamu inayokuja ya N.W.A movie, Staright Outta Compton ndo maana akaamua atengeneza albamu yake ya kwanza baada ya zaidi ya miaka 10, filamu inatarajiwa kutoka Agosti 14.

Wapenda hip hop, movies get ready to hit the bottons na theaters….compton1

Kwenye StoriKubwa >>> Ya MAGUFULI, Rais JK.. Lowassa? mastaa waliokatwa YANGA …

222222MWANANCHI
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli, na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan jana walichukua fomu kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), huku Rais Jakaya Kikwete akisema wapinzani wataisoma namba.
Ofisi ndogo za makao makuu ya CCM zilizoko Lumumba na za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), zilifurika mashabiki waliovalia nguo za rangi ya njano na kijani, ambazo hutumiwa na chama hicho, huku wakazi wengine wanaofanya kazi au kuishi maeneo jirani na barabara za Morogoro, Bibi Titi na Ohio, wakilazimika kusimamisha shughuli zao kwa muda kushuhudia msafara wa wagombea hao ukipita.
Walinzi  wa ofisi za NEC walilazimika kufanya kazi ya ziada kudhibiti wafuasi wa CCM waliosindikiza wagombea hao kutoka ofisi ndogo za CCM kabla ya msafara huo kuondoka baada ya wawili hao kuchukua fomu, kurejea Lumumba, ambako mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete aliupokea.
“Wakwere wanasema chihendo na mwene mwana, yaani shughuli na mwenye mtoto,” alisema Rais Kikwete mara baada ya msafara kuwasili akieleza sababu za yeye kuwapo eneo hilo kwa kutumia maneno ya shughuli za kitamaduni za jandoni, unyagoni na mkoleni za kabila la Wakwere.
“Nimekuja hapa kujiridhisha kama kweli fomu zimechukuliwa. Na kweli nimeziona. Baada ya hatua hii wale wanaodhani kuwa CCM ni chama cha mchezo mchezo, wataisoma namba.”
Huku akikatiza hotuba yake kwa kuitaka bendi ya TOT ya chama hicho kuimba wimbo wa “Shangilia Ushindi Unakuja”, Rais Kikwete alisema kwa kuwa yeye ni baba alilazimika kuja kuangalia kama mwanaye ametekeleza alichotuma.
Kikwete, ambaye alitumia mifano iliyovunja mbavu wafuasi hao, alirusha kijembe kwa wanachama walioihama CCM akisema ni tamaa na kuahidi kufanya mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni.
CCM shangilia ushindi unakuja, tena ushindi wa uhakika na si wa wasiwasi. Baada ya hapa kitakachofuata ni uzinduzi hapo Agosti 22 kwenye mkutano utakaotisha. Hatumwi mtoto siku hiyo, unakuja mwenyewe,” alisema.
“Watu wanasumbuliwa na tamaa na wakati mwingine ni tamaa iliyopitiliza kutaka madaraka.”
Magufuli alitoka ofisi ya CCM Lumumba akiwa amepanda gari aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa wazi juu akiwa na msafara wa magari yapatayo 10 kuelekea ofisi za NEC. Baada ya kufika eneo la makutano ya Barabara ya Ohio na Bibi Titi, alishuka na kupanda gari nyingine iliyokuwa wazi nyuma na kuamsha kelele za shangwe.
Aliwasili ofisi hizo saa 5.22 asubuhi na baada ya kuchukua fomu za kuwania urais, msafara wa kurejea ofisi za chama hicho zilizoko Lumumba ulianza tena na kufika ofisi hizo ndogo za CCM, ambako ulipokelewa na Rais Kikwete.
“Matatizo ya Watanzania nayajua na  ninaahidi kuwa nitakuwa mtumishi wenu mtiifu,” alisema Dk Magufuli baada ya Rais Kikwete kumuomba aketi ili azungumze na wafuasi wa chama hicho.
“Nafahamu kuwa Watanzania wanahitaji ajira na hawataki usumbufu kwenye biashara zao kama mamantilie, wana kero kwenye huduma mbalimbali. Ninawaahidi kuwa nitazishughulikia.
Napenda nimhakikishie mwenyekiti na wananchi mliokusanyika hapa kuwa CCM itashinda na wala simuoni mtu wa kutushinda. Nashukuru kwa moyo mliouonyesha wa kunisindikiza mimi pamoja na Samia. Mmetoa jasho na mmepoteza muda wenu. Napenda kuwahakikishia kuwa muda wenu hautapotea bure.”
Alirudia wito wake wa kuwataka wananchi kuendeleza mshikamano uliopo bila kujali itikadi zao wala makabila ili kuliletea Taifa maendeleo kwa kuondoa kero zinazowakabili.
MWANANCHI
Katibu Mkuu wa CUF na Makamu wa Kwanza Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad amesema ilikuwa kazi kubwa kumshawishi Juma Duni Haji kukiacha chama hicho na kujiunga Chadema ili awe mgombea mwenza wa Edward Lowassa.
Duni, ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF, alitangazwa kujiunga na Chadema jana, ikiwa ni makubaliano ya mkakati maalumu wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wa kukabiliana na kikwazo cha kisheria cha kupata mgombea mwenza kutoka chama tofauti na kilichosimamisha mgombea urais.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inataka Makamu wa Rais kutoka chama kilichoshinda kiti cha urais na hivyo Duni amejiunga na Chadema akiwa mwakilishi wa Ukawa kwenye Serikali iwapo umoja huo, unaoundwa na CHADEMA, CUF, NLD na NCCR – Mageuzi utashinda Uchaguzi Mkuu.
Lakini kabla ya Duni kukubali ushauri huo, Maalim Seif alisema walikuwa na kibarua kigumu.
“Tulimwita Babu Duni, tukamwambia azma hii, akasema; ‘hivi kweli niende Chadema mie?’” alisema Maalim Seif akimnukuu Duni wakati akihutubia Mkutano Mkuu wa Chadema jana kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Nikamwambia kwa hili tunalotaka la mabadiliko, lazima uende Chadema.”
Maalim Seif, ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa waliopewa nafasi ya kuzungumza kwenye mkutano huo ambao ni chombo cha juu cha uamuzi cha Chadema, alisema kikubwa kinachotakiwa ni kuunganisha nguvu kuhakikisha kuwa upinzani unatwaa Dola katika uchaguzi ujao wa Rais, wabunge na madiwani.
Maalim Seif, ambaye alijitangazia ushindi wa kiti cha urais wa Zanzibar, pia alimtangaza Lowassa, ambaye pia aliondoka CCM na kujiunga na Chadema wiki iliyopita, kuwa ameshashinda mbio za urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mgombea mwenza na wanachosubiri sasa ni kuapishwa tu.
“Huu ni wakati wa kujiamini na kuamini kuwa tunaweza kuchukua dola,” alisema Maalim Seif ambaye pamoja na mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba waliiongoza CUF katika kupatikana kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (SUK).
Wakati Maalim Seif akitangaza ushindi kwa Ukawa, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alionya kuwa kazi ya kuiondoa CCM si rahisi na kwamba nguvu ya Watanzania inahitajika kufanikisha azma hiyo.
HABARILEO
Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Ujambazi Mkoa wa Morogoro, Elibariki Pallangyo , amepigwa risasi na kufa papo hapo nyumbani kwake eneo la Yombo jiji Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Andrew Satta alisema kuwa usiku wa kuamkia jana majira ya saa tisa usiku, kundi la watu zaidi ya kumi lilivamia nyumbani kwa Pallagyo eneo la Yombo kwa kuruka ukuta, kisha kuvunja mlango na kuingia ndani walikopora fedha na simu za mabinti wanne waliokuwa ndani kabla ya kufanya mauaji.
“Hili tukio ni la kusikitisha kwani watu hawa wanaonesha walikuwa na lengo la kumuua tu na si kupora mali, kwani wamechukua fedha Sh 130,000 pamoja na simu za mkononi 4 ambazo walikuwa nazo hawa wasichana waliowakuta sebuleni,Satta.
Alisema baada ya watu hao kupora simu na fedha kutoka kwa mabinti, waliekea kwenye chumba cha Pallangyo, wakampiga risasi moja kifuani na kumuua.
Wauaji hao walitokomea kusikojulikana huku wakisahau kifaa kinachotumika katika milipuko. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Temeke na utapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi kabla ya maziko.
HABARILEO
Rais Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kufanya kampeni za kistaarabu, kwakuwa nchi ya Tanzania inayo sifa ya kuendesha mambo yake kwa njia ya amani na utulivu.
Alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati akihutubia mamia ya wakazi kwenye hafla maalumu ya kuwaaga wananchi wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika uwanja wa Mkwakwani jijini hapa.
Katika hafla hiyo, ambayo Rais Kikwete aliongozana na Mama Salma Kikwete alipata fursa ya kupokea zawadi za aina mbalimbali kutoka kwa wawakilishi wa wananchi kutoka wilaya za Tanga, Mkinga, Pangani, Muheza, Korogwe, Lushoto, Handeni na Kilindi ambazo zinaunda mkoa huo.
Alisema kwa kuwa kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi wa Oktoba zitaanza rasmi Agosti 21 mwaka huu ni vyema wananchi kila mmoja kwa nafasi yake, wahakikishe zinafanyika kwa ustaarabu na utulivu ili kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo nchini.
“Tanzania ina sifa ya kuendesha vitu kwa amani na utulivu …naomba kampeni zitakazofanyika za kuwanadi wagombea wa udiwani, ubunge na urais ziwe za kistaarabu hakuna sababu ya kufanya vurugu bali kila mtu apewe nafasi ya kumwaga sera zake, asikilizwe kwa utulivu”, alisema.
Aidha, Rais Kikwete aliwashukuru wakazi wa Tanga kwa kuiunga mkono CCM sambamba na kumuunga mkono kwa kiwango kikubwa kwenye chaguzi zote, zilizomuweka madarakani mwaka 2005 na 2010, ikilinganishwa na baadhi ya mikoa mingine nchini.
“Wito wangu kwenu ichagueni CCM tu katika serikali inayokuja, chama hiki kitawajengea Chuo Kikuu cha Serikali kwa sababu hapa Tanga hamna… naomba wananchi tujiandae vizuri kwa ajili ya kushiriki uchaguzi huo mkuu,” alisema.
Awali, akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Magalula Saidi Magalula alisema “Wananchi wa mkoa huu wameniagiza niwasilishe kwako maombi ya vitu vifuatavyo ujenzi wa daraja la Mligazi linalounganisha wilaya ya Handeni na Miono, pia ujenzi wa barabara ya Tanga- Pangani–Bagamoyo kwa kiwango cha lami, Bandari ya Tanga, kufufuliwa kwa viwanda mbalimbali vya uzalishaji na kufufuliwa kwa reli ya Tanga – Moshi hadi Musoma”.
HABARILEO
Mbunge wa Viti Maalumu Chadema, Chiku Abwao ndiye atakayepeperusha bendera ya ACT kuwania ubunge wa Jimbo la Iringa mjini katika uchaguzi mkuu ujao, huku akitamba kwamba atambwaga mbunge anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema).
Mbali na Abwao aliyejiunga na ACT Wazalendo hivi karibuni, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chadema, Abuu Changawa naye ameiacha Chadema na kujiunga ACT Wazalendo, huku akitangaza kuwania udiwani katika Kata ya Mivinjeni, mjini hapa.
Abwao aliyewahi kuwa mbunge wa NCCRMageuzi, alisema; “Nimeondoka Chadema baada ya kubanwa kila kona na Mchungaji Msigwa akidhani kwamba mimi nilikuwa Chadema kwa sababu ya kutaka cheo.”
Alisema pamoja na kunusurika maisha yake wakati akipigania ushindi wa Mchungaji Msigwa 2010, mahusiano yao kisiasa yamekuwa mabaya kwa kipindi chote kwani kila alilokuwa akijaribu kulifanya kwa niaba ya chama hicho alitafsiriwa analenga kugombea ubunge jimbo la Iringa Mjini.
Alisema ili kumuonesha nguvu yake kisiasa na kwamba yeye sio mwanasiasa anayetaka tu uongozi lakini mwenye dhamira na maono ya dhati ya kusaidia kuleta mabadiliko nchini atagombea ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini kupitia ACT Wazalendo.
JAMBOLEO
Siku mbili baada ya mawaziri watano kushindwa katika kura za maoni ya ubunge ndani ya CCM, waziri mwingine, Gaudentia Kabaka anayeshughulikia Kazi na Ajira, naye amedondoshwa katika jimbo la Tarime Mjini.
Kabaka, kabla ya kujitosa katika siasa za majimbo, alikuwa mbunge wa muda mrefu wa viti maalumu. Aidha, katika kura hizo zilizofanyika kote nchini, zimewaacha katika hali mbaya wabunge wanne, baada ya kushindwa katika kura za maoni majimboni mwao.
Hao ni Nyambari Nyangwine, Gaudence Kayombo, John Lwanji na Salome Mwambu.
Matokeo ya Tarime Mjini na Tarime Vijijini ambako Nyangwine ameanguka, yamethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu Wazazi Wilaya ya Tarime, Mathias Lugola aliyetangaza rasmi matokeo ya majimbo hayo.
Awali, matokeo hayo ya kura za maoni yaliahirishwa kutangazwa kutokana na kuwepo kwa tuhuma za kuwapo kwa wizi wa kura. Kwa jimbo la Tarime Mjini, Lugola alifafanua kuwa Michael Kembaki ndiye aliyeibuka mshindi kwa kura 3,908 akifuatiwa na Kabaka aliyepata kura 2,411.
Katika Jimbo la Tarime Vijijini, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Christopher Kangoye ambaye amejaribu zaidi ya mara tatu kuusaka ubunge, lakini bila mafanikio aliibuka mshindi akivuna kura 15,928 dhidi ya 12,205 za John Gimunta ambaye ni Mweka Hazina wa CCM wilayani Tarime.
Nyangwine na Gimunta, baadaye walilalamikia matokeo hayo wakisema mchakato wa kura za maoni ulitawaliwa na hujuma.
Kayombo azidiwa Mbinga Katika Jimbo la Mbinga Vijijini, matokeo yaliyotangazwa saa 5:45 usiku baada ya mvutano wa kutangaza matokeo unaodaiwa kudumu kwa takribani saa 12, yameonesha kuwa mbunge wa jimbo hilo aliyekuwa amejitokeza kutetea kiti chake, Gaudence Kayombo ameshindwa katika kura za maoni ndani ya CCM.
Aliyeibuka mshindi ni Martin Msuha, aliyepata kura 13,354 dhidi ya 12,068 za Kayombo, ambaye pia kwa mwaka mmoja na nusu kati ya Januari 12, 2007 na Agosti 2, 2008 alikuwa Naibu Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji.
Wengine walioshiriki katika mchakato wa ubunge jimboni humo na kura zao kwenye mabano ni Humphrey Kisika (545), Dk Silverius Komba (1,289), Edesius Kinunda (2,355), Deodatus Mapunda (2,532), Benaya Kapinga (3,941) na Deodatus Ndunguru.
Wabunge Singida hoi MCHUANO wa makada mbalimbali wa CCM kuwania nafasi za ubunge katika mkoa wa Singida umekamilika, huku wabunge waliokuwa wakitetea nafasi zao na baadhi ya vigogo kwenye chama hicho wakiwa wamebwaga vibaya.
Kwa mujibu wa Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Mary Maziku, wabunge wawili waliokuwa wakitetea nafasi zao hawakuweza kupata kura za kutosha kwenye kura za maoni. Nao ni Salome Mwambu wa Jimbo la Mkalama na John Lwanji wa Manyoni Magharibi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai ambaye aligombea jimbo la Mkalama alifanikiwa kushika nafasi ya pili kwenye kinyang’anyiro hicho kwa kupata kura 3,908 nyuma ya Allan Kiula aliyezoa kura 5,823. Jimbo hilo lilikuwa na wagombea 16.
NIPASHE
Rais Jakaya Kikwete, amesaini miswada mitano ya sheria, iliyopitishwa na Bunge la 10 Julai, mwaka huu.
Imo iliyozua tafrani na kusababisha wabunge 45 wa Ukawa kutimuliwa bungeni na wengine kususia mkutano wa 20.
Katika tukio la kihistoria lililofanyika Ikulu, jana na kuhudhuriwa na mawaziri, watumishi wa wizara na wadau wa mafuta na gesi, Rais alisaini miswada hiyo baada ya mawaziri husika kuwasilisha maelezo ya miswada hiyo.
Miswada hiyo ni wa sheria ya mafuta, sheria uwazi na uwajibikaji katika rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia, muswada wa sheria ya mapato yatokanayo na mafuta na gesi pamoja na muswada wa sheria ya Tume ya walimu.
Vile vile muswada wa sheria ya usimamizi wa masoko ya bidhaa yote ya mwaka 2015.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema tukio hilo ni la kihistoria kwa Tanzania kwa miswada mitano kusainiwa katika hadhara kubwa ya watu.
Alisema miswada ya sheria ya gesi na mafuta inaweka utaratibu mzuri wa kimfumo, kisheria na udhibiti mzuri wa kusimamia uchumi wa gesi na mafuta, kujibu kilio cha Watanzania kuwa rasilimali ziwanufaishe na kizazi kijacho.
Balozi Sefue alisema pia watanzania wataunganishwa na ulimwengu wa gesi kwa biashara watakazoanzisha na kutekeleza katika uchumi huo, ikiwa ni pamoja na kuwa na uchumi nyumbulifu katika kulinda mahitaji ya vizazi vijavyo na cha sasa.“Tunafanya walichofanya wengine duniani na kuepuka yaliyoleta matatizo katika nchi nyingine,” alisema Balozi Sefue.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema muswada wa sheria ya mafuta unalenga kuleta sheria mpya ya kusimamia sekta ndogo ya mafuta nchini kwenye masuala ya utafutaji; uendelezaji; uzalishaji; usafirishaji; uagizaji; uchakataji; uhifadhi na biashara ya mafuta na gesi asilia nchini.
“Malengo ya muswada wa sheria ni kuimarisha usimamizi wa sekta ili kuhakikisha maslahi ya nchi katika tasnia ya mafuta yanalindwa kikamilifu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo, kuweka mfumo madhubuti wa kisheria utakaoimarisha usimamizi wa shughuli za mafuta katika mkondo wa juu, wa kati na wa chini kupitia sheria moja,” alisema  na kuongeza:
“Masuala muhimu ni kuweka utaratibu ambao serikali ya Muungano na ya Mapinduzi ya Zanzibar zitashirikiana katika shughuli za utafutaji, uchimbaji na uendelezaji wa vitalu vya mafuta na gesi katika yaliyo kwenye maeneo yanayugusa pande zote mbili,” alibainisha.
Simbachawene alisema sheria hiyo itawezesha kuanzishwa kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (Pura) ambayo itasimamia shughuli zote za udhibiti katika masuala ya kiufundi na kibiashara katika mkondo wa juu.
NIPASHE
Mbunge wa Mkuranga mkoani Pwani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,  Adam Malima, amesema kuwa kura za maoni zilizopigwa jimboni humo hazikuwa huru na haki kwa madai kwamba waliopiga kura walikuwa wachache lakini kura za matokeo zikawa nyingi.
Malima ambaye alisema kuwa hakuridhishwa na mwenendo mzima wa kura za maoni kwa vile umechukua siku tatu bila mawakala kusaini fomu za matokeo.
Matokeo ya kura za maoni katika jimbo hilo yalitangazwa juzi usiku, huku Malima akiwaambia wananchi na wapambe wake wasifanye fujo na kuwataka warudi nyumbani na kwamba vikao vya juu vya maamuzi vitatoa jina la nani apeperushe bendera ya chama.
“Mchakato uligubikwa na udanganyifu mkubwa, kura haziendani na uhalisia, pia mawakala hawakutia saini baada ya kumalizwa kwa upigaji kura katika vituo vyao, lakini ninaviachia vikao vya maamuzi vifanye kazi yake,” Malima.
Alisema kuwa ana nafasi nyingi ndani ya chama na miongoni mwa watu walioaminiwa na Rais Jakaya Kikwete kuandaa ilani ya uchaguzi, na kuwa anashangaa kusikia kuwa hawezi kuwaletea wananchi maendeleo katika jimbo hilo.
“Watu kama hao ni timu za wenzangu ambazo zinatumika kusema eti wataenda upinzani, siwezi kuzuia kambi zisiongee kitu chochote, lakini mimi sihami CCM ingawa kura hizi zina walakini,’” alisema.
Akitangaza matokeo hayo, Mkurugenzi wa  Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Hadija Kusaga, alisema kuwa waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 46,904, kura zilizopigwa ni 26,949 na kwamba kura 904 ziliharibika.
Alisema kuwa katika matokeo ya kura hizo, mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, Abdallah Ulega, aliibuka na ushindi kwa kupata kura 16, 294 huku Malima akipata kura 8, 212.
NIPASHE
Mgombe urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Magufuli jana alichukua fomu za kuwania nafasi hiyo huku Mwenyeti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akiwaasa wanachama wa chama hicho wasimpuuze adui yeyote katika uchaguzi mkuu mwaka huu na kutamba watafunga magori uwanjani huku wapinzani wakiwatazama.
Magufuli alichukua fomu hizo katika ofisi za Tume ya Taifa ya  Uchaguzi (Nec) kwa mbwembwe akiwa kwenye msafara wa magari, pikipiki, matarumbeta na muziki.
Akizungumza na wanachama wa CCM jana mchana katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, Rais Kikwete aliwasihi wanachama wa chama hicho kutodharau adui yeyote watayepambana naye katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Licha ya Rais Kikwete kutofafanua kauli yake hiyo, katika uchaguzi mkuu ujao CCM inatarajia kupambana vikali na mgombea urais kupitia Ukawa, Edward Lowassa aliyehama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hivi karibuni.
Lowassa alikihama CCM huku akisema kwamba ameamua kufanya hivyo kutokana na kubakwa kwa demokrasia ndani ya chama hicho kikongwe nchini.
Kikwete alisema katika uchaguzi wa mwaka huu, chama hicho kitafunga magori uwanjani huku upinzani ukitazama na kwamba kitapata ushindi wa kishindo na hilo hana wasiwasi nalo.
Rais Kikwete jana alionekana mwenye furaha muda wote huku akiomba kikundi cha kwaya cha TOT, kimuwekea wimbo wa ‘acha waseme CCM kina wenyewe, shangilia ushindi unakuja’.
Wakati wimbo huo ukipigwa, Kikwete aliamua kuucheza akiwa jukwaani huku akishangiliwa na wananchi waliokusanyika katika ofisi za CCM.
Hata hivyo, Rais Kikwete hakuzungumzia juu ya kuondoka  Lowassa ndani ya CCM, na kwenda kujiunga na Chadema kisha kuteuliwa kugombea urais kupitia umoja huo.
Alisema dunia nzima inajua maendeleo mazuri yaliyofikiwa kupitia utawala wake na kwamba katika kampeni watakwenda kuwaeleza wananchi mambo mazuri yaliyofanywa.
Alijivunia maendeleo makubwa yaliyopatikana katika utawala wake na kusisitiza kuwa anaondoka madarakani huku akiiacha nchi ikiwa na amani, umoja na mshikamano.
Wakati wa kwenda kuchukua fomu ya kugombea urais, Dk. Magufuli jana aliambatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), huku wakisindikizwa na viongozi mbalimbali waandamizi wa CCM.

04 August, 2015

For Men- The Jaeger A/W '15 Campaign

Among the best brands to follow and purchase from, is Jaeger. Their classic cloth lines includes the usage of the world's finest cashmere and even camel hair! I like their 1880's fabric and the consistency in their designs


For the Autumn/ Winter 2015 collection, Jaeger stocks its tweed blazers and their signature camel coat, among others
Clean cuts,amazing!
Tanzanian Designers on male clothes, be Inspired

For more, visit their site Jaeger.co.uk 

NEW AUDIO: MAYUNGA NICE COUPLE

RadekArtPhoto-5780Yule mshindi wa Airtel Trace Music Star Mayunga ametuletea audio yake iitwayo NICE COUPLE chukua time yako adhim kuidowload nakushare na wana DOWLOAD HAPA

Ripoti ya TFDA kuhusu idadi na thamani ya vipodozi vilivyoteketezwa 2014/15…(Audio)

fekiiii
Mmlaka ya chakula na Dawa TFDA imeatoa ripoti ya mwaka wa fedha kuhusu bidhaa mbalimbali zilizokamatwa na kuteketezwa kwa mujibu wa sheria na hatua zilizochukuliwa.
Mkurugenzi wa TFDA Hitti Sillo amesema  katika mwaka wa fedha wamekamata na kuteketeza vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku tani 16.61 ambazo thamani yake ni shilingi milioni 44.2.
‘Vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku vilivyoingizwa tumekamata vikiwa vinaingizwa nchini na vingine vimekutwa katika soko vikiwa tayari vimeingizwa na vingine vikiwa njiani  kuingizwa nchini, mara nyingine tumekamata mabasi yakiwa na vipodozi vinavyoingizwa nchini  kinyume cha sheria vyote hivyo thamani yake kwa mwaka wa fedha uliopita ni shilingi milioni 44″ Sillo.
Amesema kazi hiyo ni endelevu kwa kuwa TFDA ipo sehemu mbalimbali nchini na wakaguzi wake wapo kuanzia bandarini na katika viwanja vya ndege ambapo ndipo hukamataa bidhaa nyingi.
Amesema miaka mitatu iliyopita udhibiti umeimarika sana ndio maana matukio mengi ya kukamatwa kwa watu ambao wanaingiza vipodozi hatari kinyume cha sheria wanakamatwa wakiwa mipakani.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...