27 February, 2016

Official AUDIO | Engine - I miss u[Make Me Sing RMX] | Download

Official AUDIO | Engine - I miss u[Make Me Sing RMX] | Download
 
Sikiliza wimbo wa kwanza wa Dogo Janja baada ya kurudi kundini TipTop #MYLIFE

GIANNI INFANTINO RAIS MPYA WA FIFA

Gianni
Raia wa Switzerland Gianni Infantino amechukua mahala pake Sepp Blatter kama rais wa shirikisho la soka duniani Fifa.
Katibu huyo mkuu wa Fifa alipata kura 115 katika raundi ya pili ikiwa ni kura 27 zaidi ya mpinzani wake wa karibu Sheikh Salman bin Ebrahim al-Khalifa.
Mwanamfalme Ali bin al-Hussein alikuwa wa tatu akiwa na kura nne huku Jerome Champagne akishindwa kupata hata kura moja.
Tokyo Sexwale alijiondoa kabla ya kura kuanza kupigwa mjini Zurich.
Raundi ya kwanza ya upigaji kura ilishindwa kum’baini mshindi wa moja kwa moja.
Wingi wowote wa kura[zaidi ya aslimia 50] katika raundi ya pili ya uchaguzi huo ulikuwa unaweza kumwezesha mgombea kutangazwa mshindi katika raundi ya pili.
Infantino ni wakili mwenye umri wa miaka 45 kutoka eneo la Brig jimbo la Valais nchini Switzerland ,ikiwa ni eneo lililopo chini ya maili sita kutoka nyumbani kwa Blatter.
Blatter ambaye aliliongoza shirikisho hilo tangu mwaka 1998 alijiondoa mwaka uliopita kabla ya kupigwa marufuku katika shughuli zozote za kandanda kwa kipindi cha miaka sita.
Baada ya kutangazwa mshindi, Infantino aliwaambia wajumbe waliopiga kura kwamba hakuweza kujielezea kutokana na hisia alizokuwa nazo.
Lakini aliwaambia wajumbe kwamba ”kwa pamoja wataweza kuirudisha sura ya Fifa na heshima ya Fifa”.
Chanzo: BBC Swahili

Habari zilizopo katika magaeti ya leo Jumamosi Feb 27

26 February, 2016

Rais wa Misri 'auzwa' mtandaoni

Sisi
Raia wa Misri wamekuwa wakimkejeli rais wao Abdul Fattah al-Sisi mtandaoni baada yake kusema kwamba anaweza kujiuza ili kusaidia uchumi wa taifa hilo.
"Ingeliwezekana mimi niuzwe, ningejiuza,” alisema Bw Sisi alipokuwa akihutubu kupitia runinga ya taifa.
Muda mfupi baadaye, ukurasa uliundwa kwenye mtandao wa kuuza bidhaa mtandaoni wa Ebay wa “kumuuza” Bw Sisi.
Kwenye ukurasa huo, uliofunguliwa dakika chache baadaye, mwuzaji alisema akiuza “jemedari ambaye amemaliza muda wake wa kutumia” na kuweka picha ya rais huyo hapo.
Bei ilizidi $100,000 (£72,000) baada ya saa kadha. Ukurasa huo baadaye ulifutwa.
Bw Sisi alikuwa pia amependekeza Wamisri watoe “pauni 10 ($1.2; £0.9) kwa Misri kupitia ujumbe wa simu” kusaidia kupunguza mzigo wa kiuchumi unaokumba taifa hilo.
Alisema hayo alipokuwa akizindua mpango wa ukuaji wa kiuchumi wa 2030.
Alikejeliwa pia kwenye Twitter huku watu wakifanyia mzaha tamko lake. Kwa muda, kitambulisha mada #Ebay kilivuma sana kwenye Twitter nchini humo.
Matatizo yanayokabili Misri kwa sasa ni pamoja na kupungua kwa uwezekaji kutoka nje pamoja na kupungua kwa watalii.
Kiwango cha mfumkko nchini humo kimepanda sawa na ukosefu wa ajira.
Hivi vimetokana na miaka kadha ya machafuko.
Bw Sisi ameapa kuendelea kujenga nchi hiyo “hadi mwisho wa maisha yangu au muhula wangu” na kuwahimiza Wamisri wamsikize yeye pekee iwapo wanaipenda Misri kwa dhati.
"Msiwasikize wengine, nisikizeni mimi,” amewahimiza.

Man United yaichapa Midtjylland Europa


Mechi za Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya Uefa Europa Ligi imeendelea tena usiku wa Alhamisi kwa michezo mbali mbali .
Baadhi ya matokeo ya mechi hizo Manchester United imevuna ushindi mnono wa mabao 5-1 dhidi ya Midtjylland , Liverpool wakiwa nyumbani dhidi ya Fc Ausbarg imechomoza na ushindi wa bao 1-0, Loco motiv Moscow na Fenerbahçe zimefungana bao 1-1.Debutant Marcus Rashford celebrates after scoring  his second goal of the night on what was an impressive night for the teenager
Mechi nyingine Schalke 04 imechapwa na Shakt Donsk, Rapid Vienna imechapwa na Valencia bao 4-0, Lazio imeichapa Galatasaray bao 3-1, Tottenham imeshinda dhidi ya Fiorentina bao 1-0, Bayer Levkusen imeibugiza Sporting ba0 3-1, Ath Bilbao imetoka sare na Marseille bao 1-1.

PICHA Debutant Rashford celebrates after scoring on his Manchester United debut — the 18-year-old was originally named on the benchRashford showed his composure to slot the ball home to level the scoreline on aggregate in front of Manchester United's home fansMemphis Depay (left) celebrates with Manchester United new boy Rashford after the teenager scored his first goal of the eveningManchester United playmaker Juan Mata squandered an opportunity to put his side in the lead by missing a first-half penaltyPione Sisto (left) celebrates in front of the Old Trafford faithful after putting his side in the lead within the opening 27 minutesSisto opens the lead for away side Midtjylland after wriggling his way past United's makeshift defence before shooting at goal

Magazeti ya Leo Ijumaa February 26.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...