13 February, 2016

Ratiba: Ligi kuu England Leo Feb,13,2016


Hii hapa ratiba kamili ligiu kuu Uingereza leo Jumamosi Feb 13,2016


England: Premier League
15:45
Sunderland
-
Manchester United
18:00
Bournemouth
-
Stoke
18:00
Crystal Palace
-
Watford
18:00
Everton
-
West Bromwich
18:00
Norwich
-
West Ham
18:00
Swansea
-
Southampton
20:30
Chelsea
-
Newcastle

Naibu Rais wa Kenya William Ruto amepata ushindi Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC)

Ruto
Naibu Rais wa Kenya William Ruto amepata ushindi muhimu kwenye kesi yake inayosikizwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) baada ya majaji wa rufaa kukubali rufaa yake ya kupinga kutumiwa kwa ushahidi wa mashahidi waliojiondoa.
Hii ina maana kwamba ushahidi ulioandikishwa awali na upande wa mashtaka hauwezi kutumiwa dhidi ya Bw Ruto na mwanahabari Joshua Sang.
Uamuzi huo ni pigo kubwa kwa upande wa mashtaka unaoongozwa na Fatou Bensouda.
Upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi sita waliokuwa wanahusisha Bw Ruto na ghasia za baada ya uchaguzi za mwaka 2007-08, vilivyosababisha vifo vya watu 1,200, walioondoa ushahidi wao.
Upande wa mashtaka unasema walitishiwa au wakahongwa.
Majaji wa rufaa wamebatilisha uamuzi wa awali wa majaji uliosema upande wa mashtaka unaweza kutumia ushahidi uliowasilisha na mashahidi hao kabla yao kubadili nia.
"Ushahidi ulioandikisha awali uliwasilishwa bila washtakiwa kupewa fursa ya kuwahoji na kuwauliza maswali mashahidi hao,” amesema jaji wa mahakama ya rufaa Piotr Hofmanski.
Bw Sang amefurahia uamuzi huo na kusema maombi yake yamejibiwa.

Magazeti ya Leo Jumamosi Feb 13,2016

12 February, 2016

When You Thought It Was Over: Martin Shkreli Has Words For Kanye West

Martin-ShkreliLast year, Martin Shkreli purchased the Wu-Tang Clan’s Once Upon A Time In Shaolin. For $2 M, the pharmaceutical kingpin bought the sole copy. And now — the “fake Batman villian” — has a sinister plan against Hip-Hop.
What are the details of that evil plot? Last night (Feb. 11), the pricey drug-pusher hopped onto his official Twitter account and sent out a few tweets that could change the course of Hip-Hop history! Backed by his bank account, he  offered Yeezy $10 M to sell The Life of Pablo to him — and only him.
Shkreli’s proposition is legally binding. By law, both Kanye and Def Jam must present the offer to its Board of Directors. Even if this nefarious maneuver is unsuccessful it may potentially “delay the album by a few days.”
Since sending out the initial tweets Shkreli has been appalled by the backlash. The pharm-bro has declared his good intentions. “The point is NOT to keep music from people, it’s to remind everyone how important and central it is in our lives,” he wrote.

video mpya ‘Make me Sing’ Diamond Plutnum ft AKA

Baada yakungojea ngama hilo kwa muda mrafu, leo wakali hao wawili wame tudondoshea mzigo mpya kabisi unaokwenda kwa jina la ‘Make me Sing’. Play hapo chini upate uhondo

New Audio ;Ben Pol na Jux "NAKUCHANA"

Wakali wawili wa muziki wa RNB, Ben Paul na Jux wametuletea ngoma mpya inayokwenda kwa jina la NAKUCHANA chukua time yako kuusikiliza hapo chini
Pia Download HAPA

Ligi kuu Tanzania Bara kuendele tena wikiendi hii


Mshikemshike wa ligi kuu Tanzania bara utaendelea tena wikiendi hii ambapo jumamosi kutapigwa jumla ya michezo mitano.
Stand United watakua wenyeji wa Wekundu wa msimbazi Simba Sport klabu, huku Mgambo Jkt wakipimana ubavu na African Sport.
Mbeya City wao watakua katika dimba lao la sokoine mjini Mbeya, kuwaalika wanakishamapanda timu ya Toto Afrikans toka Mkoani Mwanza.
Majimaji watakuwa wageni wa Ndanda Fc mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Nangwanda sijaona huko mkoani mtwara, Jkt Ruvu watakipiga na Kagera Sugar.
Ligi hiyo itaendelea tena siku ya jumapili kwa michezo miwili kuchezwa Mwadui Fc watapima ubavu na Tanzania Prisons, huku Coastal Union wakiwaalika Azam Fc.

ICC kuamua juu ya William Ruto Leo


Mahakama ya jinai ya kimataifa -ICC leo inatarajiwa kutoa uamuzi ambao huenda ukakuwa na athari kwa kesi inayomkabili naibu rais wa Kenya William Ruto. Bwana Ruto na mushtakiwa mwenzake, mwana habari Joshua arap sang wameshatkiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.
Mashtaka kama hayo yaliyomkabili rais Uhuru Kenyatta yalifutiliwa mbali na mwendesha mkuu wa mashataka ya ICC, Fatou Bensouda kwa ukosefu wa ushahidi.

TRA yakamata shehena kubwa ya bidhaa za magendo

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukamata bidhaa za magendo kwenye maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na mipakani.
Taarifa hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo wakati akifanya mahojiano na Mwandishi wa Idara ya Habari (MAELEZO) ofisini kwake Jijini Dar es Salaam kuhusu juhudi za operesheni ya kutokomeza bidhaa za magendo nchini.
Bw. Kayombo ameeleza kuwa, mkoani Lindi TRA imefanikiwa kukamata mashua katika bandari ya Lindi ambayo ilisheheni bidhaa za magendo zenye thamani ya shilingi 159,361,046.
Ameongeza kuwa katika operesheni hiyo, TRA imefanikiwa kukusanya kodi ya jumla ya shilingi 10,500,678 kutoka katika bidhaa zilizokuwa katika nyaraka za forodha (manifest) ambapo pia inategemea kukusanya kodi ya shilingi 19,529,500 kutoka katika bidhaa ambazo zilikuwa katika nyaraka za forodha lakini thamani yake ilikuwa chini ya bei halisi.
Akitaja bidhaa hizo za magendo zilizokamatwa katika mashua hiyo ni mifuko 3,725 ya sukari yenye thamani ya shilingi 127,070,562, betri katoni 50, mchele mifuko 3,087, mafuta ya kula madumu 80, majokofu manne ya mtumba, baiskeli 4 za mitumba pamoja na katoni 20 za hamira.
“Mashua hiyo ilikamatwa katika bandari ya Lindi tarehe1 Februari, 2016 baada ya wasamaria wema kutoa taarifa ya kuwepo bidhaa za magendo ndani ya mashua hiyo ambapo upakuaji wa shehena hiyo ulianza mara moja.’’Alisema Kayombo.
Ameongeza kuwa, Jijini Dar es Salaam, TRA kwa kushirikiana na kikosi cha doria cha Jeshi la Wanamaji wameweza kukamata Jahazi lenye jina la ‘Takbiri’ lenye usajili wa namba Z-875 likiwa limesheheni lita 19,700 za dizeli ambapo thamani yake bado haijapatikana kwakuwa imepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kwa ajili ya Uchunguzi zaidi.
Aidha, majahazi mengine matatu yamekamatwa katika eneo la Kigombe mkoani Tanga ambayo yalikuwa na bidhaa za magendo yenye thamani ya shilingi 99, 682, 273, 48 ambapo ndani kulikuwa na magunia ya sukari, mchele, mafuta ya kula, matairi ya magari, nyavu za kuzuia mbu, jokofu, jiko la umeme, rangi za kupuliza, betri na biskuti.
Majahazi hayo yalitaifishwa baada ya wahusika kujitosa ndani ya maji na kutoroka.
TRA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi inafanya doria saa 24 kila siku katika maeneo yote yaliyoshamiri upitishaji wa bidhaa za magendo pia imeunda Kanda Maalum katika maeneo ya Mbweni, Msasani, Kunduchi pamoja na Kigamboni.

Magazeti ya Leo Ijumaa FEB 12,2016

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...