29 July, 2015

MANULA AIPELEKA AZAM FC NUSUFAINALI KAGAME CUP

Wachezaji wa Azam FC wakimpongeza golipa wao Aishi Manula baada ya kudaka penati iliyopigwa na Hajji Mwinyi na kuivusha timu yake hadi kwenye hatiua ya nusu fainali ya Kagame
Timu Azam FC ‘Wanalambalamba’ wamefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mihuano ya Kagame baada ya kuitupa nje ya mashindano timu ya Yanga kwenye mchezo war obo fainali uliopigwa kwenye uwanja wa Taifa.
Timu hizo zililazimika kufika hadi kwenye hatua ya mikwaju ya penati kufuatia kumalizika kwa mchezo huku timu hizo zikiwa sare ya bila kufungana. Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya Kagame,hatua ya robo fainali inapomalizika ndani ya dakika 90 bila imu kufungana zinakwenda moja kwa moja kwenye changamoto ya mikwaju ya penati.
Aishi mManula alipangua penati ya Haji Mwinyi ambayo ilikuwa ni penati ya tatu kwa upande wa Yanga na kufanikiwa kuivusha timu yake hadi kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Kipre Tchetche, John Bocco, Himid Mao, Pascal Wawa na Agrey Morris walifunga mikwaju yao kwa upande wa Azam wakati Salum Telela, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Godfrey Mwashiuya walifunga penati zao huku Hajji Mwinyi yeye penati yake ikidakwa na mlinda mlango wa Azam FC Aishi Manula.
Mpira ulianza kwa kasi sana dakika za mwazo za kipindi cha kwanza, huku Azam wakifanya shambulizi kali dakika hiyohiyo ya kwanza ambapo Kipre Tchethe alishindwa kufunga goli baada ya….kupiga krosi iliyowapita walinzi wa Yanga na kumkuta yeye ambae aliukosa mpira.
Azam hawakuishia hapo waliendelea kufanya mashambulizi lakini wachezaji wa Azam hawakuwa makini kwani hadi kipindi cha kwanza kinamalizika walikuwa wamekosa takribani nafasi nne za kufunga.
Kwa upande wa Yanga, kipindi cha kwanza hakikuwa kizuri sana kwao kwasababu hawakufanya mashambulizi mengi ambayo yaliwashtua Azam. Shambulizi lililofanywa na Yanga lilitokana na mpira wa kurusha ambapo Mbuyu Twite alirusha mpira uliookolewa kwenye mwamba wa pembeni wa goli na mlinda mlango Aishi Manula.
Wachezaji wa Azam walikuwa wakitumia nguvu nyingi sana kuwakaba wachezaji wa Yanga hali ilyopelekea mwamuzi kuwatuliza kwa kuwapa kadi za njano. Kheri Abdullah Salum, Frank Domayo, Jean Mugiraneza  na Ame Ally walioneshwa kadi za baada ya kuwachezea vibaya wachezaji wa Yanga. Wakati kwa upande wa Yanga Juma Abdul na Mbuyu Twite walioneshwa kadi za njano.
Kipindi cha pili kianza kwa Azam kufanya mabadiliko kwa kumtoa Kreri Abdullah Salum na nafasi yake ikachukuiwa na Said Morad wakati Frank Domayo ‘Chumvi’ alipumzishwa na nafasi yake kuchukuliwa na Ame Ally ‘Zungu’. Yanga wao wakamuingiza Salum Telela kuchukua nafasi ya Deus Kaseke wakati Juma Abdul alitoka kumpisha Joseph Zutah na Malimi Busungu akaingia baada ya Amis Tambwe kupumzishwa.
Kipindi cha pili bado Azam waliendelea kukosa magoli kwani Kipre Tchetche, Ame Ally na Shah Farid Mussa walikosa goli baada ya kujichanganya wao kwa wao na mpira kunyakwa na mlinda mlango Ally Mustafa ‘Barthez’
Kwa matokeo hayo, Azam FC inakamilisha timu nne zilizofuzu kucheza hatua ya nusufai naili ya michuano ya Kagame kwa mwaka 2015 ambapo Ijumaa itakutana na KCCA ya Uganda iliyofuzu kucheza hatua ya nusu fainali leo mchana kwa kuibanjua timu ya Al Shandy ya Sudan kwa goli 3-0 huku Yanga wakiwa wameyapa mkono wa kwaheri mashindano ya Kagame kwa mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...