Showing posts with label Ughaibuni. Show all posts
Showing posts with label Ughaibuni. Show all posts

07 August, 2016

Mwanasayansi anyongwa kwa kosa la usaliti huko Iran

Mwanasayansi kutoka Iran Shahram Amiri ameuawa
Iran imethibitisha kwamba imemuuwa mwanasayansi wa nyuklia, ambaye alituhumiwa kwamba aliipa Marekani habari muhimu kuhusu mpango wa kinyuklia wa Iran.

Shahram Amiri alitoweka mwaka wa 2009 alipokwenda kuhiji katika mji mtukufu wa Mecca .
Alipojitokeza mwaka uliofuatia alikuwa nchini Marekani , akisema kuwa alitekwa nyara na CIA.
Kupitia kwa mitandao ya kijamii alidai kuwa alikuwa ametekwa na kuwa aalikuwa akijificha kutoka kwa majasusi wa Marekani.
Lakini alidai kwamba aliweza kutoroka, na alikaribishwa kama shujaa aliporudi Iran.

Video tatu za Shahram Amiri

Lakini baadaye, Bwana Amiri alifikishwa mahakamani.
Marekani imesema bwana Amiri alikwenda Marekani mwenyewe, na kwamba aliwapatia habari muhimu.
Habari za kuuawa kwake ziliibuka jumamosi mamake mzazi aliposema kuwa alipokea mwili wake uliokuwa na alama za kunyongwa shingoni.

Msemaji wa mahakama aliwaambia waandishi wa habari kuwa ''Shahram Amiri alikuwa amewapa maadui wa Iran habari nyeti kuhusiana na mpango wake wa kinyuklia.''
Gholamhossein Mohseni Ejei alinukuliwa akisema.

Awali Amiri alipokewa kwa shangwe na taadhima aliporejea nyumbani.
Iran imekuwa ikitafuta maarifa ya kuunda silaha za kinyuklia japo imekuwa ikipinga kufanya hivyo na badala yake ikisema kuwa inatafuta nguvu mbadala za umeme.

ata hivyo majuzi ilikubaliana na mataifa yenye nguvu zaidi duniani kusitisha mpango huo wa kisiri na badala yake ipokee msaada kutoka kwa mataifa hayo yenye nguvu za kinyuklia.

loading...

29 July, 2016

Wauawa kwa kushindwa kulipa deni la biskuti India



Mtu mmoja na mkewe kutoka jamii ya Daliti inayobaguliwa tangu jadi nchini India wameuawa, mmoja akiwa amekatwa kichwa na mwengine kunyongwa kwa kushindwa kulipa deni la Rupee kumi na tano ambalo ni karibu senti ishirini na mbili tu.

Polisi kaskazini mwa taifa hilo wamethibitisha kisa hicho ambapo yasemekana mfanyi biashara anayetokea jamii ya hadhi ya juu,aliwaua wanandoa hao kwa kushindwa kulipa deni la biskuti walizokuwa wamewachukulia watoto wao.
Mfanyi biashara huyo amekamatwa.

Ubaguzi kwa misingi ya kijamii umeenea sana nchini India, huku watu wa jamii ya Daliti waliokuwa wamebadikwa jina la 'the untouchables' wakiwekwa kwenye daraja la chini kabisa kwenye sera hiyo ya kibaguzi nchini India iitwayo 'caste' ambapo wananyimwa fursa nyingi za kimaendeleo na hivyo kubaki katika lindi la umaskini .

Hata hivyo Visa vya ukatili wa kibaguzi dhidi ya jamii ya Dalit katika jimbo la Gujarat vimeongezeka mnamo siku za hivi karibuni na vimesababisha wimbi la maandamano kutoka watu wa jamii hiyo.

24 February, 2016

Wagombea urais wa chama cha Republican washindania jimbo la Nevada

Trump
Wagombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani wanakabiliana kwenye uchaguzi wa mchujo katika jimbo la Nevada katika kinyang’anyiro cha nne cha kuamua mgombea wa chama hicho.
Mfanyabiashara Donald Trump, ambaye amekuwa akiongoza kwenye kura za maoni kitaifa, anaongoza pia kwenye kura za maoni jimbo hilo, na anatarajia kupata ushindi wa tatu mtawalia baada ya kushinda New Hampshire na South Carolina.
Nevada, ambalo ni jimbo lisilo na mbabe na lenye watu wengi wa asili ya Amerika Kusini, ni muhimu sana katika uchaguzi.
Upigaji kura kwa sasa unaendelea na kuna foleni ndefu vituoni.
Kura ya maoni ya karibuni CNN/ORC imeonesha Trump ana uungwaji mkono 45% akifuatwa na Seneta Marco Rubio 19% naye Seneta Ted Cruz akiwa na 17%.
Ingawa Nevada ina wajumbe wachache, inatarajiwa kuwa mtihani kwa Trump kutokana na matamshi yake dhidi ya wahamiaji ikizingatiwa kwamba ina watu wengi wa asili ya Amerika Kusini.
Hillary Clinton alishinda kwenye jimbo hilo katika chama cha Democratic Jumamosi.
Alimshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa kumpita kwa asilimia tano na wagombea hao wawili sasa wanaangazia jimbo la South Carolina lenye watu wengi weusi.
Uchaguzi wa mchujo wa chama cha Republican katika jimbo la South Carolina utafanyika Jumamosi.
Uchaguzi wa mchujo hutumiwa kuchagua wagombea wa vyama viwili vikuu kwenye uchaguzi mkuu wa urais ambao utafanyika mwezi Novemba

 SOURCE: BBC

20 February, 2016

Marekani yashambulia kambi ya IS Libya

Maafisa wa Marekani wamethibitisha kuwa ni ndege za Marekani zilizofanya mashambulio huko Libya wakiwalenga wanamgambo wa IS. Hata hivyo shambulio hilo la karibu na mji wa Sabratha,lililonuiwa kumlenga hasa mpiganaji mmoja wa Tunisia limeripotiwa kuwauwa watu 30 .
Mpiganaji huyo wa Tunisia anasemekana ndiye aliyefanya shambulio la mwaka jana katika kumbukumbu za Bardo na hoteli ya ufuoni mwa bahari ya Sousse huko Tunisia ambako watu zaidi ya 10 waliuawa.
Mashambulio hayo yalilenga kambi moja ya wapiganaji wa Islamic State na kumuua kiongozi mmoja mwenye itikadi kali ,maafisa wa Marekani wamesema. Noureddine Chouchane anahusishwa na mashambulio mawili nchini Tunisia mwaka uliopita ,ikiwemo shambulio lililowaua raia 30 wa Uingereza.
Kundi la IS limekuwa likifanya oparesheni zake nchini Libya kwa kipindi cha mwaka mmoja na Marekani inakadiria kwamba lina hadi wapiganaji 6,000 nchini humo.Libya inasalia katika machafuko ya wenyewe kwa wenyewe miaka minne baada ya kupinduliwa kwa aliyekuwa kiongozi wake Muammar Gaddafi,na inapiganiwa na makundi tofauti ikiwemo kundi la IS.

12 February, 2016

ICC kuamua juu ya William Ruto Leo


Mahakama ya jinai ya kimataifa -ICC leo inatarajiwa kutoa uamuzi ambao huenda ukakuwa na athari kwa kesi inayomkabili naibu rais wa Kenya William Ruto. Bwana Ruto na mushtakiwa mwenzake, mwana habari Joshua arap sang wameshatkiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa 2007.
Mashtaka kama hayo yaliyomkabili rais Uhuru Kenyatta yalifutiliwa mbali na mwendesha mkuu wa mashataka ya ICC, Fatou Bensouda kwa ukosefu wa ushahidi.

10 February, 2016

Donald Trump na Bernie Sanders wamepata ushindi katika mchujo wa jimbo la New Hampshire.

Trump
Seneta wa Vermont Bernie Sanders, aliyemshinda Hillary Clinton, amesema ushindi wake unaonesha watu wanataka “mabadiliko kamili”.
Bw Trump na Seneta Sanders wote wawili wamekuwa wakiwataka watu wapige kura dhidi ya watu ambao tayari wamekuwa kwenye mfumo wa utawala.
Maafisa wa jimbo walikadiria kwamba watu wengi wangejitokeza kushiriki kura za mchujo huo wa New Hampshire.
Gavana wa Ohio John Kasich alimaliza wa pili katika chama cha Republican, mbele ya gavana wa Florida Jeb Bush, Texas Seneta Ted Cruz na Seneta wa Florida Marco Rubio wote ambao wanang’ang’ania nafasi ya tatu.
Bi Clinton tayari amempongeza Bw Sanders, lakini akasema ataendelea kupigania kira kura kwenye kinyang’anyiro hicho cha kumtafuta mgombea urais wa chama cha Democratic.
Mchujo huo wa New Hampshire umewapa washindi nguvu mpya wanapoelekea kwa michujo ijayo South Carolina na Nevada.Trump
Ushindi wa Trump New Hampshire ndio wa kwanza mfanyabiashara huyo kutoka New York, ambaye hajawahi kuwania wadhifa wowote wa siasa, na ambaye amekuwa akiongoza kwenye kura za maoni.
Akitangaza ushindi wake, bilionea huyo amempongeza mshindi wa Democratic Bw Sanders lakini akamshambulia akisema “anataka kuuza taifa letu, jameni!”
Baada ya asilimia 50 ya kura kuhesabiwa, Seneta Sanders anaongoza kwa zaidi ya asilimia 10 ya kura dhidi ya Clinton.
Aliongoza kwenye kura za maoni New Hampshire kwa miezi kadha, na ilitarajiwa kwamba angeshinda, lakini bado ni ufanisi mkubwa.
Wengi wanaamini huenda ushindi wake umechangiwa na hali kwamba anatoka jimbo jirani la Vermont.Sanders
"Kile watu hapa wamesema ni kwamba ukizingatia mgogoro wa kiuchumi unaokabili nchi yetu kwa sasa, muda umepita kwa watu wale wale, ambao wamekuwa kwenye mfumo wa siasa na uchumi,” Bw Sanders alisema akiwahutubia wafuasi wake kwenye hotuba ya ushindi baadaye Jumanne.
Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 74 ameahidi kumaliza pengo kati ya matajiri na maskini, kutoa elimu ya vyuo vikuu bila malipo na ‘kuvunja’ benki kubwa kubwa

07 February, 2016

Tetemeko kubwa la ardhi limekumba Taiwan Kusini,


Tetemeko hilo la kipimo cha Ritcher 6.4 lilitokea karibu na mji wa Tainan.
Zaidi ya watu 200 wameokolewa kutoka kwa jengo hilo, ingawa waokoaji wangali wanajaribu kuwafikia watu wengine ambao inadhaniwa wangali wamekwama katika mabaki ya jengo hilo.
Tetemeko hilo liligonga usiku wa manane wakati watu wengi walikuwa wamelala.
Kumetokea matetemeko mengine madogo matano mda mfupi baada ya tetemeko hilo kuu.
Idara ya kusimamia maswala ya chini ya radhi inasema kuwa tetemeko hilo lilitokea sehemu ya juu pekee, hali ambayo husababisha madhara makubwa zaidi.

04 February, 2016

Makamanda wa juu wa wanamgambo wa Islamic State wameingia nchini Libya


Makamanda wa juu wa wanamgambo wa Islamic State wameingia nchini Libya miezi ya karibuni wakitokea Iraq na Syria,Afisa wa maswala ya intelijensia nchini Libya ameeleza.
Afisa huyo ameliambia Shirika la utangazaji la uingereza  BBC kuwa wapiganaji wa kigeni wameingia mjini Sirte.
Wawakilishi kutoka nchi 23,wakiwemo wa kutoka Marekani na Uingereza wamekutana Rome siku ya jumanne kujadili tishio la wanamgambo wa IS nchini Libya.
Hali ya kutokubaliana kwa serikali hasimu nchini humo imesababisha jitihada za kupambana na IS kugonga mwamba.
IS iliudhibiti mji wa Sirte mwaka jana.mji huo ulikuwa makazi ya aliyekuwa Kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Kundi la IS linaaminika kuungwa mkono na wale waliokuwa watawala wa utawala uliopita.
Lakini Ismail Shukri, mkuu wa idara ya intelijensia mjini Misrata, ameiambia BBC kumekuwa na wapiganaji wengi wa kigeni miezi ya karibuni.
Wengi wa wapiganaji wa IS ni wageni kwa asilimia 70. Wengi wao ni raia wa Tunisia,wakifuatiwa na Misri, raia wa Sudan na wachache kutoka Algeria.
Pia Raia wa Iraq na Syria, raia wengi wa Iraq wanatoka kwenye jeshi la Saddam Hussein.
Shukri amesema makamanda wa IS wamekimbilia Libya,kutokana na matukio ya mashambulizi ya anga nchini Iraq na Syria.
Mamlaka mjini Misrata zimesema zinajiandaa kupambana na IS mjini Sirte.

02 February, 2016

Seneta wa Texas Ted Cruz amemshinda Trump mchujo wa Iowa

Trumpeneta wa Texas Ted Cruz ameshinda mchujo wa uchaguzi wa mgombea wa uchaguzi wa Republican katika jimbo la Iowa, Marekani.
Huo ndio mchujo wa kwanza katika uchaguzi wa urais wa 2016 ambao utafanyika baadaye mwezi Novemba.
Mfanyabiashara Donald Trump alikuwa akiongoza kwenye kura za maoni kabla ya kura kupigwa lakini sasa dalili zinaonyesha kwamba atakuwa wa pili.
Seneta wa Florida Marco Rubio anaonekana kufanya vyema kuliko ilivyotarajiwa, na huenda akamaliza nambari tatu.
Kura za mchujo wa chama cha Democratic bado zinahesabiwa.
Asilimia 85 ya kura ambazo zimehesabiwa zinaonyesha pengo kati ya Hillary Clinton na mshoshialisti wa chama cha Democratic Bernie Sanders ni 1% pekee.
Akizungumza baada ya matokeo kujulikana, Marco Rubio amempongeza Bw Cruz na kusema ndiye mgombea ambaye anaweza kuunganisha chama cha Republican ambacho kimegawanyika.CruzWagombea wawili wamejiondoa kinyang’anyironi.
Duru za karibu na mgombea wa Democratic Martin O'Malley, aliyekuwa gavana Maryland, zimeambia BBC kwamba atasitisha kampeni yake, na kufanya ushindani mkali sasa kuwa kati ya wagombea wawili.
Upande wa Republican, gavana wa zamani wa Arkansas Mike Huckabee ameandika kwenye Twitter kwamba atasitisha kampeni yake.

01 February, 2016

Muungano wa Afrika AU hautatuma kikosi cha walinda amani hadi pale serikali ya rais Burundi


Msemaji wa Muungano wa Afrika AU, amesema kuwa umoja huo hautatuma majeshi ya kulinda amani nchini humo hadi pale watakapopokea mwaliko kutoka kwa taifa hilo la kanda ya Afrika Mashariki.
Kauli hiyo ni kinyume na pendekezo la awali la umoja huo ambao uliibua taharuki kuhusu uhalali wake na wajibu wake wa kulinda maisha ya wananchi.
Mjumbe maalum wa umoja huo kanda ya maziwa makuu Ibrahima Fall, anasema kuwa haijawahi kuwa nia ya AU kutuma walinda amani, bila ya idhini ya taifa husika.
Mkutano wa viongozi na marais wa Afrika huko Ethiopia ulishindwa kupitisha mswada uliohitajika ilikuwatuma wanajeshi wapatao 5000 kulinda amani nchini Burundi kufuatia mauaji ya mamia ya wapinzani wa rais Nkurunziza.
Machafuko nchini humo yalitibuka baada ya Nkurunziza kutangaza nia ya kuwania uchaguzi katika muhula wake wa tatu.
Wapinzani wake walisema Nkurunziza alikuwa anakiuka katiba ya taifa na kisha maandamano yakaanza kukotokea hata jaribio la mapinduzi ambayo ilizimwa na kisha rais huyo akaibuka mshindi katika uchaguzi ambao ulisusiwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa wa upinzani.
Kulikuwa na pendekezo la kutuma kikosi cha wapiganaji 5,000 wa muungano wa Afrika ilikuokoa maisha ya wapinzani wa rais huyo.
Awali rais Nkurunziza alionya kuwa majeshi yake yangewakabili vikali jeshi hilo ''Vamizi'' akisema kuwa nchi hiyo iko salama na kuwa ni vitongoji vichache tu vya Bujumbura ambavyo ni ngome ya upinzanani.
Kauli ya mwaka jana wa Nkurunziza kuamua kuwania urais kwa muhula wa tatu ilisababisha vurugu nchini humo, ambapo mamia ya watu wameuwawa na wengine wengi wakitorokea mataifa jirani.

Marekani kutowa msaada zaidi kwa Ethiopia kukabiliana na ukame

Mkulima nchini Ethiopia katika eneo la Megenta  Afar, Ethiopia, Januari,  2016.
Idara ya misaada ya maendeleo ya Marekani USAID, imetangaza kutowa dola millioni 97 ya msaada wa dharura kwa Ethiopia kusaidia kukabiliana na mzozo unaoendelea wa kibinadam, ulosababishwa na athari za mfumo wa El Nino.
Serikali ya Marekani inasaidia waethopia kukabiliana na athari za El Nino na msaada wetu wa ziada utasidia kujenga juhudi za kushugulikia hali hiyo inayoendelea, alisema mratibu wa USAID Gayle Smith, katika taarifa ilotolewa jana.
Idara ya USAID inaeleza kuwa hali ya jotojoto ilotanda katika bahari ya Pacific, imeathiri kwa kiasi kikubwa mifumo ya hali ya hewa , na  kuharibu uzalishaji wa kilimo, na kufanya maisha kuwa magumu, na kadhalika usalama wa chakula miongoni mwa watu masikini na dhaifu.
USAID inaeleza kuwa msaada huo unajumlisha zaidi ya tani elfu 176 ya chakula ambacho kitasambazwa kwa waethiopia na wakimbizi takriban millioni nne.
Katibu mkuu wa umoja mataifa Bw Ban Ki Moon, alionya jana kuwa Ethiopia inakumbwa na ukame mbaya kuwahi kutokea katika kipindi cha miaka 30. Alisema, kiwango cha dharura kinachokabiliwa na Ethiopia ni kikubwa mno kwa taifa moja kuweza kukabiliana nayo pekee yake.
Umoja mataifa unaeleza kwamba watu millioni 10 wanahitaji chakula huko Ethiopia, na kuongezea kuwa, idadi hiyo inaweza kuongezeka maradufu katika kipindi cha miezi 9.

29 January, 2016

Wagombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani wamemkejeli Donald Trump baada yake kususia mdahalo

Trump
Wagombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani wamemkejeli Donald Trump baada yake kususia mdahalo wa kupeperushwa runingani katika jimbo la Iowa.
Aliamua kusususia mdahalo huo wa shirika la Fox News baada ya shirika hilo kukataa kumuondoa msimamizi wa mdahalo Megyn Kelly, ambaye Bw Trump amemtuhumu kwa kuwa na mapendeleo.
Mfanyabiashara huyo tajiri badala yake aliandaa hafla ya kuchangisha pesa, za kuwasaidia wanajeshi wastaafu.
Wapiga kura jimbo la Iowa watapiga kura Jumatatu kuchagua mgombea wao katika kila chama.
Lakini kutokuwepo kwa Trump katika mdahalo huo mjini Des Moines kulijitokeza wazi, na wagombea saba wanaoshindana naye walihisi kutokuwepo kwake.
Seneta wa Texas Ted Cruz aligusia hilo kwa ucheshi dakika za kwanza za mdahalo na kuwakejeli wapinzani wake.
"Mimi ni wazimu na kila mtu katika jukwaa hili ni mjinga, mnene na asiyevutia, na Ben [Carson], wewe ni daktari mbaya wa upasuaji,” alisema, huku akijaribu kumuiga Trump, ambaye hakuwepo.
Gavana wa zamani wa Florida Jeb Bush pia alimchokoza mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York, ambaye amekuwa akimshambulia Bw Bush midahalo ya awali.
"Kwa kiasi fulani namkosa Donald Trump; alikuwa mwanasesere wa dubu kwangu,” alisema huku akitabasamu.
Mengine makuu yaliyojitokeza:
  • Seneta wa Florida Marco Rubio alitetea msimamo wake wa awali wa kufunga misikiti ambayo inatumiwa kueneza itikadi kali
  • Pia aliahidi kuvunja mkataba wa nyuklia na Iran siku ya kwanza akiwa rais.
  • Seneta wa Texas Ted Cruz alisema: "Nitawawinda Isis [IS] popote walipo na kuwaangamiza "
  • Gavana wa New Jersey Chris Christie alisema hajui lolote kuhusu misongamano ya magari ambayo inadaiwa kusababishwa makusudi na wasaidizi wake
  • Gavana wa zamani wa Florida Jeb Bush amesema wanajeshi wa Marekani waliowahi kupigana vijani wanafaa kupata heshima zaidi kuliko wanavyopata sasa chini ya utawala wa Obama
  • Seneta wa Kentucky Paul alieleza wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa mchango wa Marekani kijeshi nchini Syria
Kwingineko mjini Des Moines wakati uo huo, Bw Trump ameongoza mkutano mkubwa wa kutoa heshima kwa wanajeshi wa Marekani waliostaafu
“Unaponyanyaswa, lazima usimame na kutetea haki zako,” amesema, akirejelea mzozo wake na Fox News.
“Lazima tusimame kidete kama watu na kutetea taifa letu iwapo tunanyanyaswa.”
Wengi katika mitandao ya kijamii walionekana kukubali kwamba mdahalo huo wa Fox News ulimkosa sana Trump.
Lakini wengine walisema kukosekana kwake kulisaidia wagombea wengine, ambao hawajakuwa wakisikika kutokana na ‘ubabe’ wa Trump, kusikika.
Uchaguzi wa Iowa Jumatatu ijayo utakwua mtihani wa kwanza kamili kwa wagombea, na mwanzo tu wa msururu wa uchaguzi wa kuwachagua wajumbe wa vyama vya Republican na Democrats.
Kinyume na uchaguzi wa kawaida wa wagombea, ambapo kura za siri hupigwa, uchaguzi wa Iowa huwa ni mkutano wa wagombea wa vyama waliosajiliwa ambao kwanza huwajadili wagombea na kisha kupiga kura zao.
   Source:BBC

27 January, 2016

Elimu dhidi ya Ebola yawaponza vijana


Watu watatu wamepelekwa hospitali kaskazini mwa Siera leone wakiwa na majeraha yaliyotokana na kupigwa risasi baada ya kulumbana na askari juu ya mambo gani wanapaswa kuzingatia ili kuepukana na Ebola.
Polisi wamesema walirusha mabomu ya machozi baada ya vijana hao kuvamia kituo chao huko mjini Barmoi,eneo ambalo mtu mmoja alikufa kutokana na Ebola wiki iliyopita.la Nchi ya Siera leone ilitangaza kuwa iko huru na ugonjwa huo kabla ya kifo hicho kutokea.
Vijana walikuwa na hasira juu ya kufungwa kwa soko katika mji mmoja nchini humo lakini utawala ulitanabahisha kwamba ulisimamisha shughuli hizo za kibiashara kuendelea sokoni ili waweze kubaini watu watatu walipotea huku wakiwa wameathirika na ugonjwa huo.

21 January, 2016

Zimbabwe yaharamisha ndoa za watoto


Mahakama ya kikatiba nchini Zimbabwe imeharamisha ndoa za kitamaduni za watoto, ikisema kuwa watu walio chini ya umri wa miaka 18 hawaruhusiwi kuoa au kuolewa.
Watoto wamekuwa wakilazimishwa kwa ndoa za mapema kwa misingi ya kidini sehemu kadha za zimbabwe.
Serikali inasema kuwa asilimia 31 ya wasichana huolewa wakiwa chini ya miaka 18 licha ya hilo kuwa kinyume na katiba iliyotekelezwa mwaka 2013.

20 January, 2016

Donald Trump ameungwa mkono na gavana wa zamani wa Alaska Sarah Palin,


"Mko tayari kumuunga mkono Trump?” Bi Palin aliwauliza wafuasi waliokuwa wakimshangilia katika mkutano wa kampeni Iowa.
Alikuwa mgombea mwenza wa John McCain mwaka 2008 waliposhindwa na Barack Obama.
Licha ya kustaafu kutoka kwenye siasa na kujitosa katika bahari ya vyombo vya habari, yeye bado ana wafuasi wengi hasa miongoni mwa wahafidhina.
Akitangaza rasmi kumuunga mkono Bw Trump, Bi Palin amesema mgombea huyo ni mtu ambaye yuko tayari kuwawezesha wanajeshi wa Marekani kuangamiza kundi linalojiita Islamic State.
"Tuko tayari kwa mabadiliko,” amesema katika mkutano huo mjini Ames, Iowa.
"Yeye anatumikia “sisi raia”, hatumikii mtu mwingine. Yuko kwenye nafasi nzuri sana ya kuirejeshea Marekani hadhi yake tena.”Palin
Bi Palin alikuwa amehudumu kama gavana wa Alaska miaka miwili alipoteuliwa na John McCain kuwa mgombea mwenza wake.
Alikuwa akivutia umati mkubwa wa watu mikutanoni na kuangaziwa sana na vyombo vya habari.
Baada ya uchaguzi mwaka 2009, alijiuzulu wadhifa wa ugavana na akaanza kufanya kazi kama mwandishi wa habari na mdadisi wa masuala ya kisiasa.
Kabla ya kutangaza kumuunga mkono Bw Trump, Bi Palin alikuwa amesambaza makala ya mtandaoni iliyoandikwa na bintiye Bristol ambayo inamshambulia mpinzani mkubwa wa Trump katika jimbo muhimu la Iowa, Ted Cruz.
Jimbo hilo ndilo litakalokuwa la kwanza kupiga kura za kuamua mgombea.
Bw Cruz hata hivyo amemsifu Bi Palin akisema "bila uungwaji mkono wake, singekuwa katika bunge la seneti”, akirejelea uungwaji mkono aliopata wakati wa duru ya pili ya uchaguzi wa useneta mwaka 2012.
"Bila kujali atakayofanya 2016, nitabaki kuwa mfuasi wake mkuu,” ameandika kwenye Twitter.

Umoja wa Mataifa waiombea Somalia msaada

Miongoni mwao wakiwa zaidi ya watoto 310,000 ambao wanakabiliwa na tishio kubwa na kuangamia kutokana na baa la njaa na utapia mlo ikiwa hawatapata misaada ya dharura.
Shughuli za kusambaza misaada zimeathirika pakubwa kutokana na ukosefu wa fedha za kutosha, usalama na mvua ya el nino inayoendelea kushuhudiwa katika sehemu kadhaa.
Mratibu wa umoja wa mataifa anayehusika na masuala ya misaada ya kibinadamu nchini Somalia Peter De Clrecq, amesema wito huo ni muhimu sana na utasaidi watu wengine milioni moja nukta moja waliokimbia vita nchini Somalia.
Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi ni pamoja na Baido, Bossaso, Gaalkayo, Kiismayo na mji mkuu wa Mogadishu.

19 January, 2016

Polisi nchini Kenya wamenasa noti bandia za jumla ya $693m (£485m) baada ya kufanya msako katika nyumba moja jijini Nairobi.

Polisi
Watu wawili, mmoja kutoka Cameroon na mwingine kutoka Niger, wamekamatwa kuhusiana na pesa hizo.
Mkuu wa polisi Joseph Boinett akitangaza kupatikana kwa pesa hizo, amewaambia wanahabri kwamba hicho ni “kiasi kikubwa sana” cha pesa.
Amesema noti bandia za euro 369 milioni pia zimepatikana, pamoja na mitambo ya kutengeneza noti bandia.
Polisi walifanya msako baada ya kupokea habari za mfanyabiashara aliyetapeliwa Sh40 milioni za Kenya baada ya kuhadaiwa kwamba zingeongezwa mara tatu na kuwa Sh120 milioni.
Kwa jumla, pesa hizo zilizopatikana katika mtaa wa South C, zikibadilishwa na kuwa shilingi za Kenya zinafikia Sh110 bilioni ambazo ni sawa na shilingi trilioni 2.3 za Tanzania.

18 January, 2016

Mamlaka nchini Marekani zimesema zinajaribu kuwatafuta raia wa Marekani waliopotea mjini Baghdad nchini Iraq.


Watu watatu waliopotea wanahofiwa kutekwa nyara na wanamgambo, chombo cha habari cha al-Arabiya, kimenukuu vyanzo vyake.
''tuna taarifa kuhusu kupotea kwa raia wa Marekani nchini Iraq''. Maafisa wameeleza.
Msemaji wa Ubalozi wa Marekani nchini Iraq Scott Bolz amesema wanashirikiana na mamlaka za Iraq kuwatafuta.
Tukio hilo limetokea baada ya muda wa wiki moja paliposhuhudiwa kuzorota kwa hali usalama mjini Baghdad.
Wanamgambo wa Islamic state walikiri kutekeleza mashambulizi kadhaa mjini Baghdad na Dyala wiki iliyopita ambapo zaidi ya watu 50 walipoteza maisha.

17 January, 2016

Rais wa Burkina Faso amesema takriban watu 21 wameuwawa katika shambulio kwenye hoteli moja mjini Ogadugu na wanamgambo waliovamia hotel hiyo.

Roch Mark Christian Kabore amesema washambuliaji wanne waliovamia hotel hiyo waliuliwa ambapo wawili kati yao ni wanawake. Shambulio hilo lililotokea kwenye hotel ya Splendide kwenye mji mkuu wa Ouagadougou sasa limemalizwa.
Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo amesema wanamgambo hao wameuwa watu kumi na nane kutoka mataifa mbalimbali. Zaidi ya watu mia moja na ishirini walikimbia hotel hiyo maarufu kwa watalii.
walionusurika wanasema wanamgambo hao walianza kupiga risasi kwenye jengo hilo na kisha kuliwasha motoKundi la Kigaidi la Al Qaeda kwenye ukingo eneo jangwa imesema lina husika na shambulio hilo.
Watu 126 waliokuwa mateka waliachiliwa huru katika hoteli ya Splendid iliopo katika mji mkuu wa taifa hilo la Magharibi mwa Afrika Ouagadougou, kwa mujibu wa waziri wa maswala ya ndani.
Wapiganaji wanne waliuawa aliongezea huku watu 21 wa mataifa 18 tofauti wakifariki wakati wa shambulio ambalo pia liliulenga mgahawa huo.
Vikosi maalum vya Ufaransa vinasaidia wanajeshi wa taifa hilo katika oparesheni hiyo.Mnamo mwezi Novemba shambulio la AQIM katika hoteli moja ya Bamako nchini Mali liliwauwa watu 19.

16 January, 2016

Mahakama moja nchini Burundi imewahukumu majenerali wa jeshi walioongoza mapinduzi dhidi ya rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kifungo cha maisha.


Mahakama hiyo pia imewahukumu watu wengine tisa miaka 30 jela kwa jukumu lao katika jaribio hilo la mapinduzi .
Wanne hao watakaohudumia kifungo cha maisha jela ni aliyekuwa waziri wa ulinzi Cyrille Ndayirukiye,Jenerali Zenon Ndabaneze, Juvenal Niyungeko na Hermenegilde Nimenya aliyekuwa kamishana wa polisi.
Upande wa mashtaka uliiagiza mahakama kuwafunga washtakiwa wote kifungo cha maisha baada ya kukiri kushiriki katika jaribio hilo la mapinduzi mnamo mwezi Mei. .

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...