Showing posts with label Documentaries. Show all posts
Showing posts with label Documentaries. Show all posts
02 June, 2016
25 May, 2016
Abert Mangwea Mkali wa Free-style aliye ondoka na Kipaji chake.
Hakika hujafa hujaumbika, na Mwanadamu ni uvumbi na atarudi mavumbini, Kifo na mauti havitokwepeka kwa mwanadamu/ama kiumbe chochote chenye Uhai hapa ulimwenguni.
Ikiwa week hii ni week ya kumkumbuka mkali Albert Mangea(a.k.a Mimi), yapo meengi yamepita tangu kuondoka kwake, na hasa katika game hili la Muziki wa Bongo Flava, wapo wasanii wapya pia katika game hili na muziki huu umekua na kukua kweli kweli na natamani mkali huyu ange kuwako katika enzi hizi, sipati picha.
Historia yake Kwa ufupi..
Alizaliwa na jina la Albert Keneth Mangwair mnamo tar. 16 Novemba, 1982, Mbeya, Tanzania. Kiasili, ni mtu wa Ruvuma, yaani, ni Mngoni. Lakini alizaliw mjini Mbeya na akiwa na umri wa miaka 5, familia yake ilihamia mjini Morogoro kikazi na hatimaye kuanza masomo ya msingi hukohuko mjini Morogoro hadi darasa la 5 na kupata uhamisho wa kwenda Dodoma ambapo aliweza kujiunga na shule ya msingi ya Mlimwa. Kisha baadaye shule ya Sekondari ya Mazengo na Chuo cha Ufundi cha Mazengo.
Katika ngazi ya familia, yeye ni mtoto wa mwisho (kwa baba akiwa mtoto wa 10) - na (kwa mama akiwa mtoto wa 6). Albert alifariki dunia mnamo tar. 28 Mei katika mwaka wa 2013 kwa hicho kinachoaminiwa kwamba alizidisha kipimo cha dawa za kulevya huko nchini Afrika Kusini. Ngwair aliacha mtoto mmoja.
Kazi na Muziki..
Ngwair alikuwa akiishi jijini Dar es Salaam, Tanzania ambako alikokutana na mtayarishaji mahiri wa mziki P. Funk Majani na kuanza kufanya naye kazi. Hiyo ilikuwa ni mwaka 2003 ambapo alitoa kibao cha kwanza kiitwacho 'Ghetto Langu,' wimbo uliompatia umaarufu mkubwa sana.
Mangwair pia aliwahi kushinda tuzo ya Kilimanjaro Music Awards kama mwana Hip Hop Bora wa mwaka 2005. Mwaka wa 2007 akatokea kwa wimbo wa kimya kimya akiwa na wana chemba. Katika Kimya Kimya anapagawisha.Zipo nyimbo nyingi ambazo Mangwea alitisha nazo kama Vile Gheto langu, Mikasi, CNN, she got gwan, Dakika moja, Mungu Nisamehe, na pia alipata colabo zilizo hit kama ile ya May Baby yake Quick Raka, na nyingine kibao.
Kifo na mauti...
Albert Mangwair alifariki tarehe 28/5/2013 akiwa huko Afrika ya Kusini. Taarifa zinasema alifariki baada ya kutumia madawa ya kulevya lakini kuna utata kuhusu kilichosababisha kifo cha marehemu, licha ya baadhi ya mitandao mbali mbali kuandika chanzo cha kifo cha mkali huyu ila baadae iligundulika kwamba alilewa kupindukia ilhali hakua amekula.(Rest in peace Mangwea).
Pengo la mangwea katika Bongo Flava/Jamii...
Hakika itachukua Muda mrefu kwa pengo lake kuzibika ama hata Pengo lake kutozibika daima maana kipaji chake na mtazamo wake ulikuwa ni wa hali ya juu mno. Mashairi yake yaliburudisha, Kuelimisha jamii. Mchango wako utakumbukwa na wengi wakubwa ama wadogo, Muziki wa bongo Flava utakukumbuka kwa mchango wako mkubwa uliokua ukiutoa ili mradi tuu uone muziki huo ukisonga mbele na kukua.
Tizama Moja kati ya Video ambayo mimi naipenda kutoka kwa Mkali huyu wa free style( Kimya kimya)
Utakumbukwa na wana kibao, washkaji zako wakina J-Moe, Wana Chemba, T.I.D, Bongo Records na wengine kibao ambao walikuepo kipindi ukiwa china na hata kipindi ukiwa nazo(Marafiki wa dam dam). Mashabiki zako Tutakukumbuka kwa ngoma zako za kinyamwezi na Flow zenye mautam na zaidi ya yote tutazikumbuka zile shows zako.
Naamini ngoma zako zikipigwa club yeyote bado mzuka utakua ule ule daima.
PUMZIKA KWA AMAN MANGWEA, MBELE YAKO NYUMA YAKO.
21 May, 2016
Ladha ya Muziki wa Dance Tanzania Inazidi kupotea.
Ni wazi kwamba miaka ya nyuma MUZIKII huu ulitamba sana na kila mahali ulipokua ukikatiza basi sikio lako haikosi kusikia muziki huu ila miaka hii yakizazi kipya MUZIKI WA DANCE umeonekana ukipotea licha ya BENDI tofauti tofauti kuendelea kurudishia uhai muziki huu.
MARA nyingi nimekuwa nikijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu pale
ninapowasikia watu ambao naamini hasa ni mashabiki wa muziki wa dansi
wakilalamika juu ya kupotea kwa muziki huo, licha ya kuwepo kwa bendi
ambazo zinajinadi kupiga aina hiyo ya muziki hivi sasa.
Pengine
wafuatialiji hasa wa muziki huu wanaweza kutambua ukweli wa jambo hili
hasa kwa kulinganisha zama hizi na zile za Dar International, Moro Jazz,
Cuban Marimba Bend ,Kimulimuli JKT, Tabora Jazz, Nyanyembe Jazz na
nyingine nyingi ambapo wanamuziki mahiri kama Marijani Rajabu, Mbaraka
Mwinshehe, Juma Ubao,Salum Abdalah, walitamba na kuufanya muziki wa
Tanzania kujulikana kimataifa.

Jambo la kujiuliza hapa ni kwa nini muziki wetu wakati huo ulikuwa
unakubalika na jamii yote licha ya kuwa kulikuwa na upinzani mkali
kutoka kwa muziki wa Zaire (sasa DRC Congo) ambayo nayo wakati huo
ilikuwa na wanamuziki vigogo kama Tabu Ley, Luambo Lwanzo Makiadi
(Franco) , Abeti Maskini, Mbilia Mbel, Mpongo Love, n.k.
Ukweli wa hili utaujua ukigundua kuwa wanamuziki wa Tanzania kipindi hicho walikuwa hawapendi kuiga kutoka kwa wageni badala yake walisimama imara kupiga na kuulinda muziki wao, ndiyo maana ilikuwa vigumu kutekwa kimuziki na wageni.
Ukirudi nyuma kidogo miaka ya 80 na 90 kulikuwa na msururu wa bendi za muziki huo hapa nchini ambapo licha ya wingi wake, zilisimama imara na kuendelea kutangaza muziki huu kimataifa zaidi ya ilivyokuwa mwanzo.
Hakuna asiyefahamu ubora wa Bendi za Vijana Jazz wakati huo ikiwa na
Hemed Maneti , Super Matimila chini ya gwiji la muziki Dk Remmy Ongara,
DDC Mlimani Park ya Cosmas Chidumule, Juwata Jazz ya TX Moshi William,
Tancut Almasi ya Kasaloo Kyanga na Kyanga Songa, Bima Lee ya kina Jerry
Nashon ‘Dudumizi’ n.k, bendi ambazo kila moja ilipiga muziki wa dansi wa
Tanzania kwa mtindo wa wake lakini bado ukawa juu kuliko ule wa kutoka
nje.
Lengo letu hapa si kuzitaja bendi hizo lakini kiukweli
nyingi kati ya hizo zilikuwa hazifanyi hata matangazo ya barabarani,
lakini wapenzi wake walikuwa wanajua mahali ambapo zilikuwa zinafanya
maonyesho na kwenda kufurahia burudani ya muziki halisi wa dansi ambao
leo haupo tena.
Iko wapi leo Njata Njata , au ni wapi iliko
Mwenge Jazz ‘Paselepaa’, Bantu Group ‘Kasimbagu’, Tancut Almas
‘Kinyekinye kisonzo’ ni wazi ukikumbuka haya kama ulikuwa mpenzi wa
kweli wa burudani wakati huo lazima chozi litakutoka hasa ukiiona
Sikinde ya sasa iliyobaki jina tu, huku ikishuhudiwa muziki wake kumezwa
na aina ya muziki kutoka Congo DRC.
Kwa sasa asilimia kubwa
muziki wa Tanzania imemezwa na muziki wa Kikongo, kwani kila bendi hivi
sasa baada ya wimbo kuisha kinachofuata ni rap ambazo zinachukua nafasi
kubwa huku zikiwa hazina ujumbe wowote zaidi ya kusifia watu
Hii
ni tofauti na siku za nyuma ambapo mbali na kupata wimbo wenye mashairi
mazuri yenye mafunzo kilichokuwa kinafuta baada ya wimbo kumalizika ni
kuachia ufundi wa wapiga vyombo kumalizia burudani na kuwafanya
mashabiki walioshiba ujumbe vichwani mwao kujimwaga ukumbini kuserebuka.
Hakika
hii ilikuwa maana halisi ya dansi. Hebu tuambizane ukweli ni nani ama
ni bendi ipi leo inafanya haya niende ukumbi gani ambapo sitakutana na
makelele ya rapu za kumsifia mfanyabiashara fulani wa magari ambaye hana
anachokijua katika muziki zaidi ya kumwaga hela ukumbini ah ah! Kazi
kwli kweli!
Hakika miaka hiyo ilikuwa ya ukweli kwa
dansi la Tanzania kwani mbali na ubora wa bendi na wanamuziki waliokuwa
hodari wa utunzi na upigaji vyombo wakati huo pia kulikuwa na
Mashindano ya kutafuta bendi bora Tanzania yaliyojulikana kama
(MASHIBBOTA), mashindano ambayo kwa kiasi fulani yalikuwa nguzo ya
muziki huo ambayo kwa sasa yamebaki historia.
09 May, 2016
Josee Chemelion ni nani?
Jina lake kamili anajulikana kama Joseph Mayanja na alizaliwa mnamo mwaka 1979 Huko nchini Uganda. Josee Chamelion alianza kazi za sanaa mnamo mika ya 1990 nakuendelea wakati akiwa sekondary na alianza kama Mc na Dj kwenye Night clubs..
Baadae alijiunga na Ogopa Djs nchini kenya na Ngoma yake ya kwanza kufanya ilikuwa ikijulikana kama "BAGEYA" mabayo alimsha Mkali mwingine kutoka kenye anaekwenda kwa jina la Red-son.
Aina ya muziki anayoimba Josee ni muunganiko wa ladha za muziki aina zouk, Rumba, na ragga na muziki kidogo kutoka pale Uganda kidogo.
Mpaka ilipo fika mwaka 2013 Chamelion alikuwa teyari ana album zipatazo 12 na album hizo ni Bageya-2000, “Mama Mia” - 2001, “Njo Karibu”- 2002, “The Golden Voice”- 2003, “Mambo Bado”-2004 “Kipepo” - 2005, "shida za dunia"-2006, "sivyo ndivyo"-2007, "Bayunga"-2009, "Vumilia"-2010, "Valu valu"-2012, Badilisha-2013.
Ni Raisi wa Ugandan Music label inayojulikana kwa jina la "Leone Island" ambayo ndani yake kuna wasanii kama Mosses Radio, Wheezle, AK 47 na wakali wengine wengi.
Ni member katika kundi la wasanii nchini Uganda ambalo wasanii hao hutumia majina yao na umaarufu wako kupinga na kupambana na umasikini pamoja na HIV/AIDS,
Tuzo alizo wahi kutwaa ni kama ifuatavyo:-
- Beffta Awards UK – Best International Act
- 2003 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year, Best Male Artist, Best Contemporary Artist & Song of the Year ("Mama Mia")
- 2004 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year & Song of the Year ("Jamila")
- 2005 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group & Best Afro Beat Single ("Kipepeo")
- 2004 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Bei Kali")
- 2005 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Jamila")
- 2006 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group
- 2006 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Mama Rhoda) & Best Ugandan Music Video (Mama Rhoda)
- 2007 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Sivyo Ndiviyo with Professor Jay)
- 2011 Ugandan Radio Dotcom Music Awards – Artiste of The Year
- 2013 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Valu Valu"
- 2014 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Tubonge"
- 2014 HiPipo Music Awards – Song of the Year "Badilisha"
- 2014 HiPipo Music Awards – Best Male ZOUK Song "Badilisha"
- 2015 AFRIMA Awards - Africa Song Writer of the year 2015
Enjoy video mpya kutoka kwa Josee Chemelion inayokwenda kwa jina la Agatako.
03 May, 2016
Huyu ndiye Gerald Levert
Nafahamu fika vijana wengi wanaotamba huku mitandaoni ni wale waliozaliwa miaka ya 90 nakuendelea, na naku-hakikishia ni Asilimia chache sana ya vijana walio katika kundi hili wano mfahamu huyu jamaa aliye julikana kwa jina la Gerald Levert ila kama wewe ni wale walio zaliwa miaka ya 80 basi haswaaa utakua na mimi sanjari.( ha ha haaa natania tuu bhana) but any way Jokes aside now tuje kwenye Mada yetu ya leo.
Linapo tajwa jina la wimbo Cassanova ama Baby Hold On to Me, basi hutoacha kumskia Gerald Levert hapo kati amakundi zima la O’Jays. Huyu jamaa alizaliwa mnamo July 13, 1966 huko Canton katika jimbo la Ohio nchini Marakani.Alikua ni mwana muziki na muigizaji. Na ali-zaliwa katika familia ya muziki ambapo mdogo wake Sean Levert ndie aliye husika katika kuundwa kwa kundi Lililo julikana kwa jina la LeVert.
Akiwa High school mnamo mika ya 1984, ndipo alipa amua kujiingiza moja kwa moja kwenye mziki ambapo aliungana na Mdogo wake Sean Levert akiwa na rafiki yake Marc Gordon na kuunda kundi la muziki walilolipatia jina la R&B trio LeVer.
Kundi hilo lilifanikiwa kuingia studio nakurekodi album saba ambazo me mimi naziita "five scoring gold/platinum success" na Album hizo ni kama vile “I Get Hot” (1985), “Bloodline” (1986), “The Big Throwdown” (1987),
“Just Coolin” (1988), “Rope A Dope Style” (1990), “For Real Tho” (1993)
“The Whole Scenario (1997) pamoja na ngoma kali kama vile “(Pop, Pop, Pop, Pop) Goes My Mind”, “Casanova”, “My Forever Love”,
“Just Coolin” (featuring Heavy D), “Baby I’m Ready” and “ABC-123″ In
1991 the Group hit again with “Livin For The City”
Mnao mwaka 1991 Gerald aliondoka katika kundi hilo na kuamua kufanya kazi zake akiwa kama solo artist na alifanikiwa kutengeneza album ambayo ilichukua namba moja katika chart za Bilbord album hiyo ilijulikana kwa jina la Private Line, na mwaka ulio fuatia aliachilia hit nyingine alomshirikisha baba yake na wimbo huo ulijulikana kwa jina la 'Baby Hold On to Me'. Gerald aliendelea kutoa album nyingi mpaka alipo fikia miaka ya 1990s na mwanzoni mwa miaka ya 2000s ambapo alipata collabo ya wimbo kama vile “Thinkin’ About It ulio achililiwa 1998 Funny”, “Mr. Too Damn Good to You”, “U Got That Love”, and a remake of R. Kelly’s
“ I Believe I Can Fly”,
Gerald aliandika, kuproduce na kufanya kazi na wasanii kama vile Barry White, Stephanie Mills, Anita Baker, Eugene Wilde, Teddy Pendergrass, James Ingram, Freddie Jackson, Chuckii Booker, The Winans, Troop and The O’Jays. Na aliwahi kuonekana katika movies kama vile “Just Don’t Do It” pamoja na ile ya Always and Forever” zote hizo zilikua chini ya mkali Jamie Foxx.
Mnamo November 10, 2006, Gerald alikutwa akiwa amekufa kitandani mwake ambapoa aliyegundua kifo chake alikua ni binamu yake ambaye alikwenda kumuamsha. Kwa mara ya kwanza ili riptiwa kuwa kilicho muua nguli huyo ni matatizo ya moyo(heart attack) lakini taarifa kamili ya kifo chake ilitoka mwaka 2007 mwezi February ikieleza kua Gerald Aliji-overdoze na madawa. Na mwishoni ikafahamika kuwa ni sumu ya dawa hizo ili zidi kwenye damu. Alifariki na maika 40 tuu na aliacha mke na watoto watatu.
Aliacha albu yake ilokwenda kwa jina la “In My Songs” ikiwa bado jikoni iliyo achiliwa mwaka 2007 chini ya familia yake. Pamoja na Manaement iliyo kuwa ikimsimamia.
Tizama moja ya kazi zake huyu jamaaakiwa na kundi la LSG.
Kwa kifupi hiyo ni historia ya nguli huyo wa muziki aliye wahi kuishi ila teyari keshatangulia mbele za haki ambako mimi na wewe tutakwenda siku moja (R.I.P).
Unaweza kujipatia makala hii na makala zetu moja kwa moja kwenye simu yako kila ifikapo week-end Bure kabisa. Unacho takiwa kukifanya ni kujaza Fomu unayo iona hapo chini...
>> unalifahamu-kundi-la-ub40?
>> Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'
Linapo tajwa jina la wimbo Cassanova ama Baby Hold On to Me, basi hutoacha kumskia Gerald Levert hapo kati amakundi zima la O’Jays. Huyu jamaa alizaliwa mnamo July 13, 1966 huko Canton katika jimbo la Ohio nchini Marakani.Alikua ni mwana muziki na muigizaji. Na ali-zaliwa katika familia ya muziki ambapo mdogo wake Sean Levert ndie aliye husika katika kuundwa kwa kundi Lililo julikana kwa jina la LeVert.
Akiwa High school mnamo mika ya 1984, ndipo alipa amua kujiingiza moja kwa moja kwenye mziki ambapo aliungana na Mdogo wake Sean Levert akiwa na rafiki yake Marc Gordon na kuunda kundi la muziki walilolipatia jina la R&B trio LeVer.
Mnao mwaka 1991 Gerald aliondoka katika kundi hilo na kuamua kufanya kazi zake akiwa kama solo artist na alifanikiwa kutengeneza album ambayo ilichukua namba moja katika chart za Bilbord album hiyo ilijulikana kwa jina la Private Line, na mwaka ulio fuatia aliachilia hit nyingine alomshirikisha baba yake na wimbo huo ulijulikana kwa jina la 'Baby Hold On to Me'. Gerald aliendelea kutoa album nyingi mpaka alipo fikia miaka ya 1990s na mwanzoni mwa miaka ya 2000s ambapo alipata collabo ya wimbo kama vile “Thinkin’ About It ulio achililiwa 1998 Funny”, “Mr. Too Damn Good to You”, “U Got That Love”, and a remake of R. Kelly’s
“ I Believe I Can Fly”,
Gerald aliandika, kuproduce na kufanya kazi na wasanii kama vile Barry White, Stephanie Mills, Anita Baker, Eugene Wilde, Teddy Pendergrass, James Ingram, Freddie Jackson, Chuckii Booker, The Winans, Troop and The O’Jays. Na aliwahi kuonekana katika movies kama vile “Just Don’t Do It” pamoja na ile ya Always and Forever” zote hizo zilikua chini ya mkali Jamie Foxx.
Mnamo November 10, 2006, Gerald alikutwa akiwa amekufa kitandani mwake ambapoa aliyegundua kifo chake alikua ni binamu yake ambaye alikwenda kumuamsha. Kwa mara ya kwanza ili riptiwa kuwa kilicho muua nguli huyo ni matatizo ya moyo(heart attack) lakini taarifa kamili ya kifo chake ilitoka mwaka 2007 mwezi February ikieleza kua Gerald Aliji-overdoze na madawa. Na mwishoni ikafahamika kuwa ni sumu ya dawa hizo ili zidi kwenye damu. Alifariki na maika 40 tuu na aliacha mke na watoto watatu.
Aliacha albu yake ilokwenda kwa jina la “In My Songs” ikiwa bado jikoni iliyo achiliwa mwaka 2007 chini ya familia yake. Pamoja na Manaement iliyo kuwa ikimsimamia.
Tizama moja ya kazi zake huyu jamaaakiwa na kundi la LSG.
Kwa kifupi hiyo ni historia ya nguli huyo wa muziki aliye wahi kuishi ila teyari keshatangulia mbele za haki ambako mimi na wewe tutakwenda siku moja (R.I.P).
Unaweza kujipatia makala hii na makala zetu moja kwa moja kwenye simu yako kila ifikapo week-end Bure kabisa. Unacho takiwa kukifanya ni kujaza Fomu unayo iona hapo chini...
PITIA NA HIZI:-
>> Oliver Mtukudzi picha Halisi ya Muziki wa Kiafrica.>> unalifahamu-kundi-la-ub40?
>> Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'
27 April, 2016
Oliver Mtukudzi picha Halisi ya Muziki wa Kiafrica.
Linapotajwa jina la wimbo wa "Neria" basi kila mmoja wetu atakua na mawazo mawili tofauti ambayo yote humuongelea Nguli wa muziki wa Kiafrica na sio mwingine ni Oliver Mtukudzi kutoka kule Zimbabwe kwa mbabe Robert Mugabe.
Jina la utani huwa wanamuita "TUKU" ambapo jina hilo limetokana na jina Mtukudzi hivyo akaamua kufupisha jina lake hilo na kupata hiyo a..ka. amezaliwa mnamo 22 Septemba 1952 mjini Highfield, Harare) ni mwanamuziki wa Kizimbabwe. Oliver ni miongoni mwa wanamuziki walio maarufu kwa muda mrefu sana katika nchi hiyo ya Zimbabwe. Na alianza shughuli za muziki kunako miaka ya 1977 pale alipojiunga na bendi ya Wagon Wheels, ambayo pia alikuwemo na mwanamuziki wa zamani Bw. Thomas Mapfumo.
Nyimbo ya kwanza ilikuwa "Dzandimomotera" iliyoheshimika sana, na hapo ndipo Tuku alipotoa albamu yake ya kwanza, nayo pia ilileta mafanikio makubwa kabisa. Mtukudzi nae pia ni mmoja wa wanakundi la Mahube, kundi la muziki la nchi za Afrika ya Kusini.
Oliver pia ni baba wa watoto watano na wajukuu wawili, wawili hao pia ni wanamuziki. Ana dada zake wanne na kaka mmoja ambaye tayari amekwisha fariki. Anafurahia kuogelea katika bwawa lake la kuogelea (swimming pool) ambalo lina umbo la gitaa. Oliver ametoa zaidi ya albamu 40 na amepata kushinda tuzo nyingi mno na hata zingine hawezi kuzikumbuka.
Filamu alizoshiriki:
- Jit (mwong. Michael Raeburn , 1990)
- Neria (mwong. Goodwin Mawuru, imetungwa na Tsitsi Dangarembga, 1993). Mtukudzi ndiyo alikuwa nyota wa filamu na yeye ndiye aliotengeneza nyimbo ya filamu.
- Shanda (mwong. John na Louise Riber, 2002, rev. 2004)
- Tuzo ya KORA kwa ajili ya matayarisho mazuri ya nyimbo yake ya Ndakuwara mnamo mwaka wa 2002
- Tuzo ya National Arts Merit (NAMA) mnamo mwaka wa 2002 na 2004 kama kundi bora la muziki/ mwanamuziki bora wa kiume
- Tuzo ya KORA kama mwanamuziki bora wa kiume wa Africa na tuzo ya Lifetime Achievement mnamo mwezi Agosti wa mwaka wa 2003
- Tuzo ya Reel kama lugha bora ya Kiafrica mnamo wamaka wa 2003
- An honorary degree from the University of Zimbabwe in Desemba 2003
- Tuzo za M-Net Best kama nyimbo bora ya filamu mnamo 1992, kwa ajili ya filamu ya Neria.
Tafadhali pitia na Hizi zifuatazo.
1.Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'
2. Sababu tano ni kwa nini Bongo flava ya Awali ilikuwa bora kuliko ya bongo
24 April, 2016
Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'
Well! well! well!.. Leo nmepanda hapa MTOKAMBALI kivingine kabisa japo bado niko kule kule kwenye Burudani na Leo nitawapatia angalao Biography ya wakali hawa wa dance ulimwenguni. Linapotajwa jina la 'Kizomba' basi kila mmoja haachi kumfkiria Albir Rojas na Sara Lopez maana wakali hawa ndio wenye KIZOMBA DANCE.
Nianze na Albir Rojas:-
Ni dancer, choreographer, actor na ni professor.
Alizaliwa mnamo 25th mwezi October 1979 huko PANAMA na mama yeke kumpatia jina la Albir ambalo hakutaka mwanae kuchakachua jina hilo kamwe, na mama yake aliamua hivyo sababu kuna siku mama yake huyo alikwenda nchini India nakumkuta mama mmoja akimwita mwanae wa kiume "Albir" kisha akamuuliza mama huyo wa kihindi jina hilo lina maana gani? basi mama yule wa kihindi akajibu "BRAVE" na ndipo mama yake dancer huyu akaamua kumpatia jina hilo.
Wakati akiwa mdogo wa umri mika 12, mama yake alikua akimfundisha dancing japokua wakati huo jamaa huyu alikua havutiwi na dancing na badala yake alikua akivutiwa na Video games na akaendelea na video games pamoja na dancing mpaka akiwa na umri wa miaka 14 wakati alipokuwa High school.
Akiwa high school alialikwa kushiriki kwenye choreography na hapo ndipo Albir akaamua kuikubali DANCING na kuanza kuifanyia kazi. Akiwa na umri wa mika 16, alijiunnga na darasa ladance katika funky dance school na huko alikua akijifunza mambo mengi kuhusiana na choreography.
Albir alimaliza high school akiwa na umri wa miaka 18 na lifanikiwa kutoka na Bachelor of Commerce degree (Accounting).
Baada ya kumaliza masomo yake alipata kazi akiwa kama accountant na huku alikua pia akisoma masomo yake ya shahada ya uzamivu katika maswala hayo hayo ya biashara. Albir alikua akiutesa mwili wake kwa kazi mno maana hasubuhi alikua akienda kazini na jioni alikua akihudhuria darasani na usiku alikua akifanya mazoezi ya dance jambo ambalo mwili wake kuna muda uluonekana kuchoka.
Licha ya hivyo jamaa huyo hakukata tamaa na aliamua kuacha kazi ofisini na kuamua Kuifanya sanaa kwa ujumla kipindi chote cha cha maisha yake.
Albir alikua katika dancing mwaka hadi mwaka na aliwahi kuonekana katika kazi kama Grease, the King and I, Fame, West Side Story na Fantastics, kote huko alikua kama Actor na dancer.
Aliamua kwenda Madrid kwa ajili ya masomo yahusuyo Communication, Advertising, Film making and Sound Technician na alimaliza na akamua kuishi Madrid tangu mwaka 2001 mpaka leo.
Albir amekua akifundisha dancing styles kama cuban salsa, salsa in line, bachata dominicana, bachata madrid, hip hop, popping, KIZOMBA, TARRAXINHA, SEMBA and ballroom dances ambazo yeye ni MASTER wa Style hizo.
Albir anapenda anachokifanya na hua anapenda kushirikisha feelings zake kwa watu wapenda dancing mfano Mimi ( ha ha ha haa).
Nije kwa bibie Sara López:-
Mwana dada huyu ni mzaliwa Madrid, Spain na alizaliwa mnamo mwaka 1986. Alianza dancing akiwa na umri mdogo wa miaka 5 na alitumia miaka 7 kujifunza dance katika ballet, contemporary dance, modern dance, hiphop. na akiwa na umri wa miaka 16 alinza na Latin dances, Salsa, Bachata pamoja na Kizomba.
Akiwa na umri wa mika 18 tuu, akawa amemaliza elimu yake ya Sekondary na akaamua kwenda Madrid kwa ajili ya kujifunza classical ballet. Huko alikaa kwa muda wa mika mitatu zaidi akiwa akijifunza tena Latin rhythms.
Alipata dancing partner wake wa kwanza nchini humo aliyejulikana kama Ronald Jara ambaye alionekana nae katika mashindano ya dancing Madrid in Africadançar (Lisbon Ureno) mnamo mwaka 2012.
na baadae akatambulishwa kwa Mkali Albir ambaye walionekana kufanya kazi kwa pamoja hadi mwaka 2014 walipo achana.
Ikumbukwe kuwa Dancers hawa hawakuwahi kuwa wapenzi kamwe licha ya watu wengi ulimwenguni kufahamu kuwa walikua wapenzi. Nikupatie angalao video moja ya wakali hawa wakifanya vitu vyao katika KIZOMBA.
Mpaka hapo sina la ziada nikutakie siku njema na tukutane tena Juma lijalo hapa hapa MTOKAMBALI,
Mtokambali |
Nianze na Albir Rojas:-
Ni dancer, choreographer, actor na ni professor.
Alizaliwa mnamo 25th mwezi October 1979 huko PANAMA na mama yeke kumpatia jina la Albir ambalo hakutaka mwanae kuchakachua jina hilo kamwe, na mama yake aliamua hivyo sababu kuna siku mama yake huyo alikwenda nchini India nakumkuta mama mmoja akimwita mwanae wa kiume "Albir" kisha akamuuliza mama huyo wa kihindi jina hilo lina maana gani? basi mama yule wa kihindi akajibu "BRAVE" na ndipo mama yake dancer huyu akaamua kumpatia jina hilo.
Akiwa high school alialikwa kushiriki kwenye choreography na hapo ndipo Albir akaamua kuikubali DANCING na kuanza kuifanyia kazi. Akiwa na umri wa mika 16, alijiunnga na darasa ladance katika funky dance school na huko alikua akijifunza mambo mengi kuhusiana na choreography.
Albir alimaliza high school akiwa na umri wa miaka 18 na lifanikiwa kutoka na Bachelor of Commerce degree (Accounting).
Baada ya kumaliza masomo yake alipata kazi akiwa kama accountant na huku alikua pia akisoma masomo yake ya shahada ya uzamivu katika maswala hayo hayo ya biashara. Albir alikua akiutesa mwili wake kwa kazi mno maana hasubuhi alikua akienda kazini na jioni alikua akihudhuria darasani na usiku alikua akifanya mazoezi ya dance jambo ambalo mwili wake kuna muda uluonekana kuchoka.
Licha ya hivyo jamaa huyo hakukata tamaa na aliamua kuacha kazi ofisini na kuamua Kuifanya sanaa kwa ujumla kipindi chote cha cha maisha yake.
Albir alikua katika dancing mwaka hadi mwaka na aliwahi kuonekana katika kazi kama Grease, the King and I, Fame, West Side Story na Fantastics, kote huko alikua kama Actor na dancer.
Aliamua kwenda Madrid kwa ajili ya masomo yahusuyo Communication, Advertising, Film making and Sound Technician na alimaliza na akamua kuishi Madrid tangu mwaka 2001 mpaka leo.
Albir amekua akifundisha dancing styles kama cuban salsa, salsa in line, bachata dominicana, bachata madrid, hip hop, popping, KIZOMBA, TARRAXINHA, SEMBA and ballroom dances ambazo yeye ni MASTER wa Style hizo.
Albir anapenda anachokifanya na hua anapenda kushirikisha feelings zake kwa watu wapenda dancing mfano Mimi ( ha ha ha haa).
Nije kwa bibie Sara López:-
Akiwa na umri wa mika 18 tuu, akawa amemaliza elimu yake ya Sekondary na akaamua kwenda Madrid kwa ajili ya kujifunza classical ballet. Huko alikaa kwa muda wa mika mitatu zaidi akiwa akijifunza tena Latin rhythms.
Alipata dancing partner wake wa kwanza nchini humo aliyejulikana kama Ronald Jara ambaye alionekana nae katika mashindano ya dancing Madrid in Africadançar (Lisbon Ureno) mnamo mwaka 2012.
na baadae akatambulishwa kwa Mkali Albir ambaye walionekana kufanya kazi kwa pamoja hadi mwaka 2014 walipo achana.
Ikumbukwe kuwa Dancers hawa hawakuwahi kuwa wapenzi kamwe licha ya watu wengi ulimwenguni kufahamu kuwa walikua wapenzi. Nikupatie angalao video moja ya wakali hawa wakifanya vitu vyao katika KIZOMBA.
Mpaka hapo sina la ziada nikutakie siku njema na tukutane tena Juma lijalo hapa hapa MTOKAMBALI,
Mtokambali |
22 April, 2016
ELIMU YA TANZANIA YENYE MFUMO WAKIKOLONI
Mara nyingi ukimkuta mzazi mtaani akiwa na mwanae hupenda sana kumhusia maswala ya elimu. Ni jambo jema kwa mzazi kumuasa mwanae juu ya elimu ya dunia hii maana hata vitabu vitakatifu vilivyo andika maneno ya Mwenyezi Mungu yanasema Mkamate sana elimu usimwache aende zake kwa maana ndie mkombozi wa maisha yako. Haya yote ni mwanzo ama utangulizi wa mada yetu ya leo ambayo nimekwisha itambulisha kwako wewe mdau wangu.
Tanzania ni moja ya nchi
zilizowahi kutawaliwa na waingereza enzi zile za ukoloni
na hivyo kuifanya kuwa nchi hii
kuwa moja kati ya nchi
za jumuia ya madola(common wealth). Kiuhalisia nchi hizi huchukua
mfumo wa
kiuongozi pamoja na mifumo yakielimu kutoka kwa waingereza.
Tanzania ni moja kati ya
nchi zinazochukua mfumo huo wa
elimu kutoka kwa waingereza tangu miaka ya
nyuma ambapo Tanzania ikijulikana kama Tanganyika.
Ni elimu
ambayo kwa
lugha yakigeni inaitwa formal education na wala sii ile ambayo
wazee wetu waliipatia chini ya miti yaani informal eduction.
Elimu ya Tanzania imekua ikionekana kuyumba kutokana na kuingiliwa na wazimu siasa ambapo
kipindi cha miaka ya nyuma, elimu
hii ilionekana yenye thamani na iliyodhamiria kuijenga jamii nakubadili ama kukuza uchumi
wa nchi yetu
kwani elimu hiyo ilijikita katika maendeleo ya jamii kwa ujumla
wake. Tizama masomo yaliyo pata kufundishwa
kipindi cha nyuma katika shule za
msingi na hata ufundishaji wake ni tofauti na wa
sasa. Watoto wa Mjini wanasema
wamechakachua, yawezekana hayo yanasababishwa na utandawazi lakini bado elimu hii
ya sasa hapa
kwetu ni taabu tupu kulinganishwa
na hapo awali.
Elimu ya mwanzoni ilikua
ikimjengea kijana mazingira yakuweza kujiajiri nakujikomboa mwenyewe katika umaskini na taabu
lakini hii ya sasa imekua
ni tofauti kwani kwa asilimia
kubwa imekuwa ikimjengea mwanafunzi mazingira yukuajiriwa ofisi jambo ambalo
limekua ngumu na tatizo kuu hapa
nchini mwetu na vijana wengi hubaki
bila ajira na kurudi nyuma kimaendeleo
binafsi na hata maendeleo ya jamii kwa
ujumla.
Vijana wengi ambao hawana
ajira wamezidi kuongezeka mitaani ni sababu
ya msingi mibovu ya elimu
yetu hapa nchini. Kijana anasoma mpaka anahitimu
lakini mwisho wa siku anabaki pale pale akiranda randa mitaani na bahasha yenye vyeti kibao
akitafuta kazi maofisini. Elimu iliyowahi kutolewa
miaka ya nyuma ilikua ikimjenga
kijana katika mazingira ambayo pindi kijana atakapokua
amehitimu masomo yake unakuta teyari
kijana huyo anaweza kufanya kitu pasipo kuajiriwa
ofisini nikimaanisha kujiajiri.
Kiukweli mfumo huu wa elimu tulio nao
ni mbovu na naweza kusema umepitwa
na wakati kwani ni wazi kwamba
unamjenga kijana katika mazingira yakutegemea kuajiriwa maofisini kitu ambacho hakitakiwi.
Kwa upande wa sekondari nako ni majanga
matupu kwani vijana wengi hapo
ndipo ndoto zao huzima mazima.
Kwa elimu yetu ni kwamba mwanafunzi akiwa shule ya
msingi masomo yake yote kutoa
kiingereza hufundishwa kwa Kiswahili lakini pindi anapofikia kuingia sekondari mfumo wa masomo
unabadilika na masomo yote kutoa somo
lakiswahili ambalo huendeshwa kwa kiswahi na mengine yote ni kiingereza
kitupu. Halii hii inakua kigezo
kikubwa kinachomfanya mwanafunzi kushindwa kuendena na mfumo
huo nakushindwa kufanya vyema katika
masomo hayo. Jambo hili linamfanya
mwanafunzi kuishia kukariri pasipo kuelewa ni
nini anachokifanya.
Kwa upande mwingine Gharama za elimu
hii ni
ghali kiasi kwamba wapo baadhi
ya watoto wetu kushindwa kuendelea na masomo yao. Jambo hili
limekua kama
chambo chakuvulia kura katika majukwaa
ya siasa. Wanasiasa wengi wamekua wakitamba majukwaani kwamba endapo wakiingia madarakani watatoa elimu hii bure,
jambo ambalo kiukweli wananchi wanashawishika kuwapigia kura lakini
mwisho wa siku hali inabaki
pale pale. Siasa za nchi hii
ndio zimeharibu kabisa mfumo wa elimu yetu kiasi kwamba
haifai tena katika nchi hii.
Wito wangu kwa serekali na wadau mbali mbali
wa elimu hapa nchini ni
wakae pamoja na kutafuta suluhisho kamili ambalo litaokoa
elimu yetu na kuondoa tatizo hili la ajira kwa
vijana. Vijana wapewe elimu wajiajiri
na sio kungojea
kupata kazi maofisini kitu ambacho hata kwenye
nchi zilizoendelea Hakipo
123ContactForm | Report abuse
MISITU YETU TANZANIA TUNAFAIDIKAJE NAYO?
Kwanza napenda
kuchukua fursa hii kumshukuru sana Mwenyezi
Mungu, muumba wa mbingu na dunia
na vyote vilivyomo tukiwamo sisi wanadamu,
kwa mema mengi mno anayonitendea
na hasa kwa kutujalia uhai hadi leo hii.
Kwa vyovyote vile bila ya Mwenyezi Mungu
kutuwezesha na kututia nguvu sisi
wenyewe hatuwezi, bali hali ilivyo
ya kimazingira na kimaumbile tutakwama tu, hata hao
wanaokwenda angani na kufanya wanayoyafanya huko si kwa
uwezo wao tu, bali pia
ni kwa mapenzi
yake Mola
Nipende kuchua nafasi
hii kukukaribisha
katika makala yetu leo . Leo nitapenda kuzungumzia swala hili
la Rasilimali
ya Misitu
tuliyojaliwa na Mwenyezi Mungu.
Katika hali ya kawaida ni
kwamba Misitu
tulionayo inatosha
kukidhi mahitaji yetu sote tuliopo
karibu na Misitu
katika mambo ya uhifadhi wa wanyama
pori, kupata vyanzo vya maji,
upatikanaji wa mbao kwa ajili
ya ujenzi na hata kupatikana kwa kuni kwa
ajili ya kupikia kwa wale wengi wetu tunayotumia
nishati
hii ya kuni.
Misitu ya asili ni matokeo ya kazi nzuri
iliyofanywa na Mwenyezi Mungu tangu alipouumba
ulimwengu, ikiwamo sayari hii tunayoishi
sisi wanadamu. Kwa maneno mengine,
misitu au maliasili zote tulizonazo ikiwa ni pamoja
na madini, wanyamapori, samaki na viumbe wengine waishio baharini, ardhi (kwa maana ya
udongo), maji (kwa maana ya
vijito, mito, maziwa, mabwawa, bahari na ardhioevu), nishati mafuta na gesi asilia ni
zawadi tuliyopewa na Mwenyezi Mungu.
Kwa bahati nzuri Tanzania Bara imebahatika kuwa na eneo
kubwa lenye misitu ya asili
pamoja na mapori mazuri yenye utajiri
mkubwa wa wanyamapori. Kwa takwimu za mwaka
1998 (ambazo sasa zimeboreshwa na matokeo ya mradi
wa kitaifa wa kupima na kutathmini
misitu ya asili), Tanzania ilikuwa na eneo la misitu ya asili la takribani
hekta milioni 33.5.
Kati ya hizo, hekta milioni
13 ni eneo
la misitu lililohifadhiwa kisheria (misitu ya hifadhi ya
Serikali Kuu (Central
Government Forest Reserves) takribani misitu 600 na misitu 200 ikimilikiwa na Serikali za Mitaa (Local Authority Forest
Reserves) chini ya halmashauri
za wilaya); na zaidi ya hekta
milioni 20 ya misitu ya asili
bado haijahifadhiwa na kusimamiwa kisheria.
Kwa kipindi cha miaka 10 iliyopita, vijiji vichache vimeweza kutenga sehemu ya misitu katika
vijiji vyao na kuitangaza kuwa
misitu ya hifadhi ya vijiji
yenye jumla ya hekta zaidi
ya milioni saba. Hatua hiyo
ni ya
kupongezwa maana vijiji husika sasa
vina nguvu ya kisheria kusimamia
na kutumia misitu husika ipasavyo na hatimaye kunufaika na usimamizi huo, kwa kuongozwa na Sheria ya Misitu
na kanuni zake.
Vilevile, vijiji vinayo fursa
ya kujiwekea sheria ndogo ndogo
kwa lengo
la kuimarisha zaidi utekelezaji wa shughuli za kulinda
msitu kwa faida yao na Taifa
kwa jumla. Pamoja na mafanikio
hayo, bado sehemu kubwa ya
misitu ya asili ambayo haijahifadhiwa
kisheria inapatikana katika maeneo ya
vijiji na haitumiki ipasavyo kuviletea vijiji maendeleo endelevu.
Miaka zaidi ya 20 Serikali
imekuwa ikitekeleza mpango wa
Usimamizi Shirikishi wa Kutunza na Kuendeleza
Misitu nchini
(Participatory Forest Management-PFM). Dhana ya Ushirikishwaji ni mbinu
ya uongozi inayowezesha kupata mchango wa mawazo
na ushiriki mzuri kutoka kwa wadau
mbalimbali, hasa katika utekelezaji wa shughuli za
kujiletea maendeleo endelevu
kwa kutumia rasilimali za asili
tulizonazo.
Ushirikishwaji husaidia watu kubadilishana
mawazo na kufahamu vizuri nini kinaendelea au kinatekelezwa kwa faida yao. Hivyo
kwa kuwashirikisha
wanavijiji katika masuala yanayohusu maendeleo yao vijijini ni
suala muhimu sana na huondoa lawama, pia huongeza
motisha wakati wa kutekeleza jambo
lililoamuliwa.
Isitoshe, ni wajibu
wa kila mdau
kuhakikisha kuwa anawajibika ipasavyo katika kutoa mawazo
na kufikia uamuzi sahihi ili lengo
na madhumuni ya mipango ya maendeleo katika sehemu yao
iweze kufanikiwa. Ili wanakijiji au jamii katika ujumla wake waweze kufanya hivyo, ni
lazima waelimishwe vya kutosha na kuwajengea uwezo (capacity) wa kusimamia na kutumia kwa misingi
endelevu rasilimali na fursa zilizopo ikiwamo misitu ya asili.
Swali lililopo ni je tunafaidika
vyema na hizi faida zitokanazo na misitu tulio nayo?
Zipo faida nyingi zitokanazo na Misitu
hii tuliyo nayo na faida hizo
na kama vile kutumika katika maswala
ya ufugaji wa nyuki, hifadhi
za wanyama, upatikanaji wa nishati ya kuni
na upatikanaji wa mbao ambazo tunatumia
katiaka maswala ya ujenzi na maendeleo hapa nchini.
Ni
ukweli ulio wazi na usiopingika
ya kwamba rasilimali hii haitufaidishi ipasavyo na nathibitisha ukweli huu kwa kutumia
mfano mdogo tuu wa upungufu
wa MADAWATI mashuleni mwetu hasa zile
za msingi. Kimsingi tusingetarajia kuona fedheha na aibu hii kubwa
inayotukumba sisi
leo hii Hapa
nchini Kwetu. Kuna wakati nilikua natazama taarifa ya habari nikaona
habari inayo onyesha watu wa Jamhuri ya watu wa
SWITZILAND wakitoa msaada wa MADAWATI katiaka shule Fulani ya msingi huko Dar-es-salaam. Jamani hivi ni kweli tumekosa miti yakuweza kutupatia
hayo madawati ambayo watoto wetu
wanalizimika kukaa kwenye sakafu na juu ya mawe wakati
wakiwa madarasani waifundishwa?
Huo ni mfano
mdogo tuu unaonyesha ni jinsi
gani bado rasilimali za misitu
hapa nchini hatufaidiki nazo ipasavyo.
Maoni yangu na
mapendekezo yangu ni haya juu ya
swala la ukosefu wa madawati mashuleni.
Kwa sasa zipa shule nyingi
za UFUNDI hapa Tanzania ambazo zinamilikiwa na serekali na baadhi
ya nyingine zinamilikiwa na taasisi binafsi na point ni kwamba Kuna baadhi ya misitu mikubwa
ambayo imekomaa na ambayo inaweza kutupatia mbao kwa ajili ya
kutengeneza madawati yakutosha.
Kwa nini serekali isivune miti hiyo kwa
mujibu washeria na ki sha kutumia
ile sera ya “KATA MTI PANDA
MITI” ili kurudisha miti ambayo imevunwa
kwa ajili yakutengeneza madawati?
Inawezekana kabisa kufanya hivyo na kisha mbao kupatikana ambapo mbao hizo
zitipelekwa katika vyuo vya ufundi
ambapo wanafunzi wanaojifunza ufundi seremala watatengeneza madawati hayo kama
sehemu ya somo lao darasani. Ni matumaini yangu kila mkoa
vyuo hivi vya ufundi vinapatikana
na jambo hili
linaweza kufanikiwa kwa kiasi Fulani.
Serekali Kwa kupitia wataalamu wa mambo ya
misitu waandae miche yakutosha kwa ajili yakupanda
sehem zitakazokua zimevunwa miti hiyo.
Kwakufanya hivyo tutaondoa aibu na tatizo
hili la ukosefu wa madawati Katika
shule zetu.
Yasije yakawa yale
ya “Penye miti mingi hapana
wajenzi.”
Nichukue nafasi hii kukushukuru wewe ulie chukua
nafasi na muda wako kupitia
makala zetu. Tafadhali ungana nami tena katika
makala zetu zinazotoka kila Mwisho wa
wiki.
MAKALA HII IMEANDIKWA NA:-
Francis Mawere
Subscribe to:
Posts (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...

-
Mshambuliaji huyo wa umri wa miaka 26 ambaye amekuwa akichezea klabu ya Corinthians ya Ugiriki amechezea taifa lake mechi 27 na kuwafungi...
-
Brit Awads 2016 zimefanyika huko London ambapo mwanamuziki Adele ameondoka na tuzo nyingi zaidi katika nomination alizo kuwepo. Hizi hapa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...