30 September, 2016

Exclusive Download: Sinasi - Masai Wa Kigoma

ikiliza wimbo mpya wa Masai Wa Kigoma - SINASI #UswahiliFlavor! Bofya DOWNLOAD hapo chini kuupakua wimbo Huo. Enjoy

Wenger: Wachezaji wa Afrika wamenifaa sana katika soka

Arsene Wenger ameongoza Arsenal kwa miaka 20
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameiambia BBC kuwa wachezaji kutoka nchi za Afrika wamekuwa wenye umuhimu mkubwa katika taaluma yake ya miaka 20.

Wenga alikuwa akizungumza wakati wa mkutano wake wa kawaida na waandishi wa habari kabla ya mechi ambapo pia alitunukiwa kwa kukiongoza klabu hicho kwa miongo mwili.Nwankwo Kanu wa Nigeria alikuwa mmoja wa wachezaji waliokuwa wenye umuhimu mkubwa kwa Arsene
Akiwa mwenye uso uliotabasamu, Wenger amesena kuwa wachezaji kutoa Afrika wana moyo, wenye ubunifu na nguvu, masuala ambayo ni vigumu kuyapa kwenye mchezo.

Aliwataja wachezaji akiwemo Nwanko Kanu wa Nigeria, Kolo Toure wa Ivory Coast na gwiji raia wa Liberia George Weah, ambaye alikuwa meneja wake katika klabu ya Monaco nchini Ufaransa, kama wachezaji watatu waliokuwa na uswawishi mkubwa katika taaluma yake.

Samsung Galaxy A8 yazinduliwa Rasmi,

Hatimae zile tetesi ya kwamba Samsung wataachia Samsung Galaxy A8 mwezi huu zimekuwa za kweli. 
 Ifahamike kwamba Samsung kwa kipindi hichi cha karibuni walipata msala kupitia Note7 mara baada ya Kugundulika kwamba simu hizo zinalipuka hovyo hata kuzuiliwa Katika viwanja tofauti tofauti vya ndege ulimwenguni. Safari hii wameachia mzigo mpya huu hapa ulikanao kwa Jina la Samsung Galaxy A8. Mzigo utaanza kuingia Sokoni ifiikapo tarehe 1 mwezi ujao.

 Na zifuatazo ni SPECIFICATIONS zake.

Release date:  September 2016
Form factor:   Touchscreen 
Dimensions (mm): 156.60 x 76.80 x 7.20

Weight (g)           :  182.00


Battery capacity (mAh):  3300


Removable battery:  No



SAR value            : NA 

 DISPLAY 

 Screen size (inches): 5.70 
 Touchscreen          :Yes 
 Resolution            : 1080x1920 pixels 

HARDWARE 

Processor          : 1.5GHz  octa-core 
Processor make Exynos :  7420 
RAM                           :3GB 
Internal storage                          :32GB 
Expandable storage                    : Yes 
Expandable storage type             : microSD 
Expandable storage up to (GB)   : 256 

CAMERA

 Rear camera    : 16-megapixel 
 Flash              :Yes 
 Front camera    : 8-megapixel 

 SOFTIWARE 

Operating System Android 6.0.1 

CONNECTIVITY

Wi-Fi        :Yes
Wi-Fi standards supported : 802.11 a/ b/ g/ n/ ac
GPS          :Yes
Bluetooth  :Yes, v 4.20
NFC          :Yes
Infrared     :No
USB OTG   :Yes
Headphones  :3.5mm
FM               :Yes
Number of SIMs :2


SIM 1

     
SIM Type     :Nano-SIM
GSM/ CDMA  :GSM
3G              :Yes
4G/ LTE       :Yes

SIM 2     
SIM Type    :Nano-SIM
GSM/ CDMA :GSM
3G             :No
4G/ LTE      :Yes









 Sensors

Compass/ Magnetometer  :Yes
Proximity sensor             :Yes
Accelerometer                :Yes
Ambient light sensor       :No
Gyroscope                      :No
Barometer                      :No
Temperature sensor         :No

 

Lenovo Unveils New 'Hello Moto' Boot Animation; Will Come on New Moto Phones


Lenovo acquired Motorola Mobility from Google in 2014 for $2.9 billion. Since then, Lenovo has almost killed the brand's identity, retaining just the 'Moto' bit. However, the Chinese smartphone and PC manufacturer wants to run its loyal users through a nostalgia of 'Hello Moto' boot animation.

If you remember, Motorola under Google used to ship firmware that had 'Hello Moto' boot animation for Moto X smartphones. These animations were frequently updated as well. After Lenovo took possession of Motorola Mobility, however, things were expected to change. However, it's now evident that Lenovo is aware of Motorola's popularity as a brand that used to make some durable and wonderful smartphones back in time.

Therefore, Lenovo on Thursday posted a video of the 'Hello Moto' boot animation, and said it will be "the power-up on new Moto phones." The YouTube video shows the famous 'Hello Moto' signature line followed by a series of colourful patterns and images, and finally ending with a Lenovo logo.

Lenovo has not given any official word as to which Moto phones will get the boot animation, but if following tradition, it should become available on the Moto X family. The update may soon be rolled out via OTA to the users. We are also not sure if the update will reach the 2015 range of Moto phones such as Moto X Gen 2.

Do you like Lenovo's efforts to revive Motorola's resonance as a brand in the market? Let us know in the comments below.

All the way Up Rmx- Diamond Plutnum Part 2


Diamond ameachia verse nyingine ya Remix yake ya ‘All the way Up’ , amejibu tetesi za kuchepuka, jina la Simba na mpinzani wake, Alikiba.
Kulikuwa na tetesi kuwa muimbaji huyo wa ‘Salome’ amerudiana na Wema sepetu kimyakimya, pia kuna tetesi kuwa amechepuka na Hamisa mobetto ambaye pia ametokea kwenye video yake mpya, Jibu ndio hili


“Mara nakula hamisa mobetto, ati Sepenga kaja magetho, ilimradi Zari apate mchecheto, Tale waambie waache unambinambi hata nikila wote dini yangu sio dhambi” 
Diamond na Alikiba ni washindani wakubwa kimuziki na maneno ya hapa na pale hayakosekani, Huku Diamond akiwa amesaini dili kubwa zaidi la kuwa balozi wa Vodacom, Alikiba na yeye alipata dili la kuwa Balozi wa Wild Aid, inayopinga mauaji ya tembo. Diamond nalo kaliongelea


“Siachi pengo hadi waombe poo, wao wakipost tembo si tunapost show”
Kama unajiuliza Tilalila ni nani, basi jua kuwa ni Mr.Blu jina limetokana na wimbo wake wa ‘Tilalila’ wa muda kidogo, Mr. Blu na Diamond waliwahi kuingia kwenye mgogoro wa jina la ‘Simba’, Chibude nalo hajaliacha lipite,
Mwambie na tilalila, kamwe kanzu haifanani na dera”
Enjo All the Way Up rmx

Europa League: Manchester United waichapa Zorya Luhansk

Zlatan Ibrahimovic
Manchester United wameondoka kwenye mkia kundi lao la ligi ndogo ya Ulaya, Europa League, baada ya kupata ushindi dhidi ya Zorya Luhansk.

Zlatan Ibrahimovic alifunga bao la pekee dakika ya 69, baada ya kombora la nguvu mpya Wayne Rooney kugonga mlingoti wa goli.

Hilo ndilo bao la kwanza la Ibra katika mechi tano, na lilitokana na kombora la kwanza la United lililolenga goli kwenye mechi hiyo.

United walitawala pakubwa mchezo huo uliochezewa Old Trafford, ingawa Sergio Romero alihitajika kufanya kazi ya ziada kuzima kombora la Paulinho muda mfupi kabla ya Ibrahimovic kufunga.

Mashetani hao Wekundu walitarajiwa kufanya vyema Europa League lakini walianza kampeni yao kwa kulazwa 1-0 na klabu ya Feyenoord ya Uholanzi mechi yao ya kwanza.

United sasa wamo nambari tatu kundini, wakiwa na alama sawa na Feyenoord na moja nyuma ya viongozi Fenerbahce wa uturuki ambao watazuru Old Trafford 20 Oktoba.Wayne RooneyUnited watarejea uwanjani Jumapili Ligi ya Premia ambapo watacheza dhidi ya Stoke City dimba la Old Trafford.

Utafiti: Chunusi humfanya mtu kuonekana mdogo

Chunusi huwanfanya vijana kuonekana wadogo kwa muda mrefuwapo wewe ni kijana ambaye ana chunisi ,unaweza kujihisi kana kwamba ni mwisho wa dunia. Lakini utu uzima wako utakusaidia.

Utafiti mpya kutoka chuo cha Kings mjini London,kilichowachunguza mapacha wa kike 1,205,unasema kuwa kijana aliye na chunusi huishi masha akionekana mdogo ukilinganisha na watu wa umri kama wake ambao wana ngozi nzuri.
Wataalam wanasema kuwa ni kwa sababu watu waliio na acne wana kinga ya mwilini dhidi ya uzee.

Hiyo inamaanisha kwamba vitu kama vile ngozi iliojikunja na ilikonda huonekana baadaye katika maisha.
Kwa nini?

Utafiti huo umechunguza seli nyeupe zilizchokuliwa kutoka kwa mtu mwenye chunusi na kubaini kwamba zina kofia zenye kinga katika mwisho wa kromosomu zake zinazowasaidia kutozeeka haraka.

28 September, 2016

New AUDIO Aslay - Kidawa


Pakua nyimbo mpya ya Aslay inayokwenda kwa jina la Kidawa.

List ya wasanii wa Hip-Hop watakao wania Tuzo za BET

Hii ndiyo list kamili ya wasanii na DJs watakao wania Tuzo za BET 2016. Sherehe za utoaji tuzo hizi zitafanyika kwenye ukumbi wa Cobb Energy Performing Arts Centre jijini Atlanta, Georgia, na zitaoneshwa na kituo cha BET (DStv channel 129) Alhamisi ya October 6, 2016.


Best Hip-Hop Video
2 Chainz – Watch Out
Desiigner – Panda
DJ Khaled F/ Jay Z & Future – I Got the Keys
Drake – Hotline Bling
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
Kanye West F/ Rihanna – Famous
 
Best Collabo, Duo or Group
DJ Khaled F/ Drake – For Free
DJ Khaled F/ Jay Z & Future – I Got the Keys
Drake & Future – Jumpman
Drake F/ Wizkid & Kyla – One Dance
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
 
Best Live Performer
Drake
Future
Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Lyricist of the Year
Chance the Rapper
Drake
Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Video Director of the Year
Benny Boom
Colin Tilley
Director X
Hype Williams
Kanye West
 
DJ of the Year
DJ Drama
DJ Envy
DJ Esco
DJ Khaled
DJ Mustard
 
Producer of the Year
DJ Mustard
Dr. Dre
Metro Boomin
Mike WiLL Made-It
Pharrell Williams
 
MVP of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Track of the Year
All the Way Up – Produced By Cool & Dre and Edsclusive (Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared)
Controlla – Produced By BOI-1DA (Drake)
Hotline Bling – Produced By Nineteen85 (Drake)
I Got the Keys – Produced By Southside (DJ Khaled F/ Jay Z & Future)
Panda – Produced By Menace (Desiigner)
Album of the Year
DJ Khaled – I Changed A Lot
Dr. Dre – Compton
Drake – Views
Fetty Wap – Fetty Wap
Future -DS2
Kanye West – The Life of Pablo
 
Best New Hip-Hop Artist
Anderson .Paak
Bryson Tiller
Chance the Rapper
Desiigner
Tory Lanez
 
Hustler of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Jay Z
Kanye West
 
Made-You-Look Award (Best Hip Hop Style)
A$AP Rocky
Drake
Future
Kanye West
Nicki Minaj
 
Best Hip Hop Online Site/App
Allhiphop.Com
Complex.Com
Hotnewhiphop.Com
Worldstarhiphop.Com
XXLMag.Com
Best Mixtape
Chance the Rapper – Coloring Book
French Montana – Wave Gods (Hosted By Max B)
Future – Purple Reign
Lil Uzi Vert – Lil Uzi Vert VS. The World
Young Thug – Slime Season 3
 
Sweet 16: Best Featured Verse
2 Chainz – No Problem (Chance the Rapper F/ Lil Wayne & 2 Chainz)
Drake – Work (Rihanna F/ Drake)
Kendrick Lamar РFreedom (Beyonc̩ F/ Kendrick Lamar)
Kodak Black – Lockjaw (French Montana F/ Kodak Black)
Nicki Minaj – Down In the DM – Remix (Yo Gotti F/ Nicki Minaj)
 
Impact Track
Cole – Love Yourz
Jay Z – Spiritual
Jidenna – Long Live The Chief
Raury F/ Key – Trap Tears
Sir The Baptist F/ ChuchPeople – Raise Hell
 
People’s Champ Award
Desiigner – Panda
DJ Khaled F/ Drake – For Free
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
O.T. Genasis F/ Young Dolph – Cut It
Travis Scott – Antidote
Young Thug – Best Friend

Video: Feza Kessy – Walete (Official Video)

Ni mwezi mmoja umepita tangu mwanadada Feza Kessy aiachie audio ya ngoma yake mpya inayoitwa “Walete” katika media tofautitofauti. 
Na huu ameona ndio wakati mzuri wa kuiachia video ya ngoma hiyo. Itazame hapa chini

Ratiba ya Mechi za UEFA leo September 28



Baada ya hapo jana michezo 8 kuchezwa katika viwanja tofautitofauti barani Ulaya ikiwa ni katika ligi ya mabingwa barani humo, leo pia kuna muendelezo wa ligi hiyo.


Ikiwa ni timu 16 ambazo zitamenyana katika viwanja 8 ili kukamilisha ratiba ya kucheza mechi 2 kwa kila timu kwa makundi A,B,C na D kama ilivyokuwa hapo jana kwa makundi E mpaka H. Ratiba ya mechi za leo ipo kama ifuatavyo.
Group A
  1. Arsenal vs Basel
  2. Ludogorets Razgrad vs Paris Saint German
Group B
  1. Besiktas vs Dynamo Kyiv
  2. SSC Napoli vs Benfica
Group C
  1. Borussia Monchengladbach vs Barcelona
  2. Celtic vs Manchester City
Group D
  1. Atletico Madrid vs Bayern Munich
  2. FC Rostov vs PSV Eindhoven

Simba v Yanga Jumamos Rekodi zitaongea


JUMAMOSI ya wiki hii, yaani Oktoba 1, 2016, nyota wa zamani wa soka ulimwenguni, Mliberia George Opong Weah, atakuwa akisherehekea miaka 50 tangu kuzaliwa kwake, lakini kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, kutakuwa na habari nyingine wakati mahasimu wakuu wa soka Tanzania, Yanga na Simba, watakapokuwa wakivaana kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

George Weah ndiye mchezaji wa kwanza kutoka barani Afrika kutunukiwa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, yaani tuzo ambayo mpaka leo hii hakuna mchezaji yeyote wa Kiafrika aliyewahi kuipata.

Nakumbuka ilikuwa mwezi Desemba, mwaka 1995, ambapo FIFA iliitangazia dunia ya soka kuwa Weah amechaguliwa kwa kupigiwa kura kuwa mwanasoka bora wa dunia.

Ni katika mwaka huo, George Weah akawa Mwanasoka Bora wa Ulaya na haikuishia hapo, akatangazwa pia kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika! Ndani ya mwaka mmoja, akajikusanyia mataji matatu.

Hapana shaka haya ni mafanikio yasiyo na mifano katika historia ya soka barani Afrika. Weah ni alama ya soka ya Liberia. Aliwahi kutoa misaada kwa timu ya taifa ya Liberia iliyokuwa na hali duni ili iweze kucheza michuano ya Kombe la Dunia na Kombe la Mataifa ya Afrika, hii ilichangia kumfanya aheshimiwe zaidi na wananchi wa nchini humo.

Nakumbuka mara baada ya kutunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa dunia, Weah aliwahi kuibeba timu yake ya Taifa akiwa ndiye nahodha wa kikosi hicho kwa gharama zake yeye mwenyewe, ambapo aliambatana na kikosi hicho kwa ajili ya mchezo wa kimataifa dhidi ya timu ya Taifa ya Tanzania.

Watanzania wengi walikuwa wagumu sana kuamini kuwa yeye ndiye hasa alikuwa George Weah. Kila alichokuwa akikifanya pale Sheraton Hotel (sasa Serena Hotel), kilionekana kushuhudiwa na Watanzania wengi waliokuwa wakimshangaa.

Ukiachana na stori ya Weah ambaye Jumamosi anatimiza umri wa miaka 50, Simba na Yanga zitakutana siku hiyo ikiwa ni siku ya 275 ya mwaka kati ya siku 366, lakini ni baada ya siku 237 tangu zilipopambana mara ya mwisho Februari 20, 2016 katika mchezo wa marudiano msimu uliopita ambapo Simba ililala kwa mabao 2-0.

Kabla ya hapo, Septemba 26, 2015 kwenye uwanja huo huo, Yanga pia waliibuka na ushindi wa mabao 2-0, wakilipa kisasi cha kufungwa ‘bao la kizembe’ na pekee Machi 8, mwaka huo, lililopachikwa kimiani na Emmanuel Okwi.

Kinachosubiriwa na mashabiki wa soka hapa nchini ni kuona ni timu ipi kati ya Yanga na Simba itakayosherehekea ushindi na kuungana na Weah kwenye ‘birthday’ yake Jumamosi hii, ni jambo lililo gumu kutokana na rekodi ya timu hizo mbili, ambazo kimsingi ndizo zilizoleta mwanga wa soka nchini.

Tangu Simba ilipozinduka kutoka katika kufanya vibaya kwenye ligi na hatimaye kukalia usukani mpaka sasa, kumekuwa na mhemko mkubwa baina ya timu hizo mbili, mashabiki na wanachama wake wakitambiana kwamba timu yao itaibuka na ushindi.

Lakini kelele hizo zitahitaji pia kuangalia matokeo ya uwanjani yakoje, vinginevyo upande mmoja unaweza kuzizima.

Matokeo baina ya mechi hizo daima huwa hayatabiriki na tangu Simba walipoibamiza Yanga kwa mabao 5-0 Mei 6, 2012, wamevuna ushindi mmoja tu wa Machi 8, 2015 wakati Okwi alipopachika bao la pekee, huku kipa wa Yanga, Ali Mustafa Barthez akiwa ametoka langoni.

Itakumbuka kwamba, baada ya kipigo kile cha aibu kwa Yanga, timu hizo zilikutana mara nane, Yanga ikishinda mara tatu na Simba mara moja, huku zikitoka sare mechi nne.

Zilipokutana Oktoba 3, 2012 zilitoka sare 1-1, mechi ya Mei 18, 2013 Yanga wakashinda 2-0, Oktoba 20, 2013 timu zikatoka sare ya 3-3, Aprili 19, 2014 sare ya 1-1 na Oktoba 18, 2014.

Machi 8, 2015 ndipo Simba iliposhinda, lakini Septemba 26, 2015, Yanga ikapata ushindi wa 2-0 kama ilivyofanya tena Februari 20, mwaka huu.

Simba inaingia uwanjani ikiwa na washambuliaji wapya ambao wamekuwa moto wa kuotea mbali, akina Laudit Mavugo, Shiza Kichuya na Ibrahim Ajib, lakini Yanga inao wachezaji wake wote wawili walioipa ushindi Februari 20, ambao ni Donald Ngoma na Amis Tambwe.

Yanga, ambao ni mabingwa watetezi, ndio wana kibarua kigumu zaidi kwa sababu licha ya kupitwa mchezo mmoja na Simba, inahitaji kushinda mechi hiyo ili iweze kurejesha matumaini ya kuutetea ubingwa wao baada ya kupoteza mechi moja mwishoni mwa wiki, ilipofungwa na Stand United bao 1-0 kwenye Uwanja wa Kambarage, mjini Shinyanga.

Simba ina pointi 16, baada ya kushuka dimbani mara sita na kushinda mechi tano, huku ikitoka sare mechi moja wakati Yanga imecheza mechi tano, ikishinda mechi tatu, sare moja na kupoteza mechi moja.
Kupoteza mechi hiyo kuna maana moja kwa Yanga, itakuwa imejeruhiwa vibaya katika kampeni yake na kuwapa matumaini zaidi Simba, ambao hawajawahi kutwaa taji la ubingwa tangu mwaka 2012.

Matokeo ya sare bado hayatainufaisha Yanga, lakini itakuwa ni faida kwa Simba ambayo itakuwa na uhakika wa kufanya vizuri katika mechi zake zote ngumu msimu huu.

Mechi baina ya timu hizi mbili kongwe katika historia ya soka nchini huwa zinatawaliwa na vituko vingi mno. Kuvunja nazi, kuoga maji ya maiti, kuruka ukuta, kuingia uwanjani kinyumenyume na mengine kama hayo hutajwa kwamba ni sehemu ya kuhanikiza ushindani.

Hata hivyo, kwa sasa hawawezi kuruka ukuta kama ilivyokuwa miaka ile ya zamani, wala hawawezi kuoga maji ya kuoshea maiti au kuvunja nazi hadharani, kwa sababu sheria za soka haziruhusu ushirikina na timu hizo mbili zimekwishawahi kutozwa faini kwa vitendo hivyo.

Hii itakuwa mechi ya 82 kuzikutanisha Simba na Yanga kwenye Ligi Kuu tangu mwaka 1965 ilipoanzishwa Ligi ya Taifa na aliyekuwa kocha wa Taifa Stars, Milan Celebic.
Katika kipindi chote hicho, msisimko wa kuelekea mechi hizi umekuwa mkubwa, bila kujali nani anawania kitu gani.

Hata hivyo, katika mechi 81 zilizopita, Watanzania wameshuhudia Yanga ikitawala zaidi kwa kushinda mara 31, wakati Simba imeshinda mara 23.

Jumla ya magoli 168 yamefungwa tangu kuanza kwa Ligi Kuu mwaka 1965, Yanga ikiongoza kuifunga Simba magoli mengi zaidi.

Timu hiyo imeishindilia Simba magoli 91, huku Simba ikitumbukiza nyavuni kwa Yanga magoli 77.
Faraja pekee yaliyokuwa nayo wanachama na mashabiki wa Simba ni kwamba timu yao inaongoza kwa kuifunga Yanga tangu kuingia kwa karne ya 21.

Kwa mujibu wa rekodi, tangu kuingia mwaka 2000, Simba imeifunga Yanga mara 11, zikiwa zimetoka sare mara 15, huku Yanga ikishinda mechi nane kwenye mechi za Ligi Kuu tu.

Watani hao wamekutana mara 34 kwenye mechi za Ligi Kuu Bara. Katika mechi hizo zote, magoli 65 yamefungwa, Simba ikiwa imefunga magoli 35 dhidi ya 32 ya Yanga.

Yanga imeweza kuifunga Simba mara mbili kwa msimu mmoja kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1991.
Ikumbukwe kuwa kabla ya Ligi Kuu kubadilishwa na kuanza kuchezwa kwa mfumo wa msimu kama England, ilikuwa ikichezwa mwanzoni mwa mwaka hadi mwisho, hivyo timu zilikuwa zikikutana mwaka mmoja mara mbili, tofauti na sasa zinapokutana msimu mmoja, lakini miaka tofauti.

Mfano mechi ya kwanza Simba iliyofungwa mabao 2-0 msimu uliopita ilichezwa Septemba 26, mwaka jana.
Hii ni tofauti na mwaka 1991, Yanga ilipoifunga Simba mara mbili kwa msimu mmoja, lakini pia ilikuwa mwaka huohuo.

Ilikuwa ni Mei 18, Yanga ilishinda bao 1-0 lililofungwa na Said Sued ‘Scud’ dakika ya saba na mechi ya marudiano mzunguko wa pili ikashinda tena bao 1-0, mechi iliyochezwa Agosti 31, mfungaji akiwa ni yuleyule Scud.

Katika mechi zote 81 zilizopita na kuzaa mabao hayo 168, winga machachari wa Yanga, Omar Hussein ‘Keegan’ wa Yanga ndiye anayeongoza kwa kufunga magoli mengi katika historia ya timu hizo, akiwa amezifumania nyavu mara sita, akifuatiwa na straika Abeid Mziba pia wa Yanga, aliyefunga magoli
matano kwenye mechi zinazoihusisha timu hizo.

Mastraika wengine wa Yanga, Idd Moshi na Jerry Tegete wa Yanga, pia wao wamepachika mabao manne kila mmoja.

Hata hivyo, Simba nayo imeingiza wachezaji waliofunga magoli manne kwenye mechi za watani ambao ni marehemu Edward Chumila na Musa Hassan ‘Mgosi’.

Rekodi zinasema kuwa tangu kuingia karne ya 21, yaani kuanzia mwaka 2000 wachezaji wanaoongoza kwa kufunga magoli mengi kwenye mechi za watani ni Mgosi na Tegete, ambao kila mmoja amefunga magoli manne, idadi ambayo haijafikiwa na mchezaji yeyote yule karne hii.

Wachezaji waliopachika mabao matatu kwenye mechi za watani wa jadi kwa upande wa Yanga ni Kitwana Manara, Maulid Dilunga, Said Mwamba na Mohammed Hussein ‘Mmachinga’ na kwa upande wa Simba ni Abdallah Kibadeni na Emmanuel Okwi.

Orodha hiyo inaonyesha waliofunga mabao mawili kwa upande wa Yanga ni Salehe Zimbwe, Juma Mkambi, Rashid Hanzuruni, Said Sued ‘Scud’, Makumbi Juma ‘Homa ya Jiji’, Issa Athumani, Idelfonce Amlima, Sekilojo Chambua, Ben Mwalala, Sunday Manara na Amis Tambwe.

Kwa upande wa Simba ni Jumanne Hassan ‘Masimenti’, John Makelele ‘Zig Zag’, Malota Soma ‘Ball Jugler’, Nicodemus Njohole, Dua Said, Steven Mapunda ‘Garincha’, Madaraka Selemani, Ulimboka Mwakingwe na Athumani Machupa.

Moja ya tukio litakalobaki kumbukumbu kwa muda mrefu kwa wanachama na mashabiki wa Simba ni mwamuzi wa kike, Jonisiya Rukyaa kumtoa mapema beki Abdi Banda wa Simba dakika ya 20 na kuwafanya kucheza pungufu kwa muda mrefu, huku ikilazimika kubadilisha mbinu ilizokuwa nazo awali.
Tukio hili lilionekana kulalamikiwa sana na mashabiki wa Simba, ambao awali waliamini kuwa timu yao itaibuka kidedea.

Walidai kuwa rafu ya Banda ilikuwa nyepesi mno na mwamuzi hakupaswa kutoa kadi nyekundu, hasa ikizingatia mechi kubwa kama ya watani wa jadi.

Wakati Yanga wakitoka na nderemo na vifijo, Simba walitoka uwanjani wakilia na mwamuzi Rukyaa.
Hii inakumbusha miaka 42 iliyopita kwenye mechi ya Ligi Kuu (Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara wakati huo) iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana, mjini Mwanza.

Ni mechi ambayo haitasahaulika kirahisi na kizazi cha soka kilichokuwa hai wakati huo.
Katika mechi hiyo iliyochezwa Agosti 10, Yanga iliifunga Simba mabao 2-1 kwenye pambano kali, tata na lililokuwa na matukio ya kukumbukwa.

Simba ilielekea kuwa bingwa na kushinda mechi hiyo kwa bao 1-0 lililofungwa na Adam Sabu dakika ya 16.
Dakika ya 87 marehemu Gibson Sembuli aliisawazishia Yanga bao. Dakika saba za nyongeza, Sunday Manara (baba yake mzazi Haji Manara, msemaji wa Simba) akaiandikia Yanga bao la pili na kutwaa ubingwa.

Simba ilimlalamikia sana mwamuzi, marehemu Manyoto Ndimbo kwa madai alikuwa amezidisha muda. Mchezaji Saad Ali wa Simba alianguka na kuzirai na mpaka sasa zipo simulizi kuwa eti sehemu ile aliyoangukiwa hapaoti tena majani hadi leo hii, na wengine wakidai kumeota kichuguu.

 SOURCE: DIMBA

Chuo Kikuu cha Oxford chaongoza ubora wa vyuo vikuu duniani

CHUO kikongwe zaidi katika ulimwengu wa nchi zinazozungumza Kiingereza na kilichotoa viongozi mashuhuri nchini Uingereza cha Oxford, kwa mara ya kwanza kimeongoza katika orodha ya vyuo vikuu duniani, lakini Makamu Mkuu wa chuo hicho ameonya kwamba Brexit inaweza kuharibu mategemeo yake ya muda mrefu.
 
Chuo hicho cha Oxford kimepiku chuo kilichokuwa kikiongoza orodha hiyo kwa miaka mitano iliyopita, cha California Institute of Technology,  ambacho kimeshika nafasi ya pili. Pia orodha hiyo imeshuhudia vyuo vikuu vya China vikipanda kwa haraka zaidi katika orodha hiyo ya vyuo vikuu bora duniani. 

Oxford, walikosoma mawaziri wakuu wane kati ya sita waliopita wa nchi hiyo, kimepiku chuo cha Marekani baada ya bajeti yake ya utafiti kuongezeka kufikia paundi bilioni 1.4 ($1.83bn), wakati matokeo ya utafiti wake ukiongezeka, anasema Phil Baty, mhariri wa orodha hiyo. 

Lakini Baty anasema kujitoa kwa Uingereza kutoka katika Jumuiya ya Ulaya “ni hatari kubwa kwa mafanikio yetu” kwa kufanya kuwa vigumu zaidi kuwavutia wanataaluma wa juu zaidi na kuwaweka katika miradi ya utafiti. 

Brexit inahatari ya kuwaondoa wanafunzi, wafanyakazi na fedha, Makamu Mkuu wa Oxford, Profesa Louise Richardson, aliiambia redio ya BBC. 

Richardson alisema kuwa vyuo vikuu vingine vimeongeza jitihada zake katika kuchukua asilimia 17 ya wafanyakazi wake ambao ni wananchi wa Jumuiya ya Ulaya, na ambao hadhi yao katika Uingereza haiwezi kuhakikiwa baada ya kura ya Juni 23. 

“Vipo vyuo vikuu vingi duniani ambavyo vitafurahi kuwa nao na vimekuwa vikijaribu kuwafuata ili kuwachukua na kuwauliza kama wanaweza kujiunga na vyuo vyao badala ya kuendelea kubaki,” alisema.
Serikali pia imeshindwa kutoa uhakika kama itafidia kiasi cha paundi milioni 67 kwa mwaka ambazo chuo hicho kimekuwa kikipokea kutoka kwa Baraza la Utafiti la Ulaya ambazo hutumika kufanya kazi za utafiti, alisema. 

“Kusema ukweli, tuna wasiwasi juu ya hilo.”
Wakati Oxford, University of Cambridge na London’s Imperial College vya Uingereza vikiwa ndani ya vyuo kumi bora duniani pamoja na chuo kikuu cha ETH Zurich, orodha hiyo imetawaliwa na vyuo vikuu vya kutoka nchini Marekani. 

Chuo Kikuu cha Stanford cha Marekani kimeshika nafasi ya tatu, wakati Massachusetts Institute of Technology, MIT kikishika nafasi ya tano, Havard nafasi ya sita, Princeton saba na Chuo Kikuu cha California, Berkeley na Chuo Kikuu cha Chicago vikifungana katika nafasi ya kumi. Vyote hivi vinatokea nchini Marekani. 

Cambridge cha Uingereza kimeshika nafasi ya nne, wakati Imperial College kikiwa cha nane na ETH Zurich nafasi ya 9.

Chuo Kikuu cha St. Andrews cha Scotland na Chuo Kikuu cha Sheffield vimeporomoka kutoka vyuo vikuu 100 bora duniani. 

Katika Ulaya, nchi za Ujerumani na Uholanzi zimeshika nafasi ya tatu na nne, ambapo Ujerumani ina vyo vipatavyo 41 katika vyo vikuu 200 bora na Uholanzi ikiwa na vyuo vikuu 13 katika orodha hiyo. 

Nchi za Ulaya Kusini kama Hispania na Italia hazijafanya vizuri kutokana na uhaba wa fedha na matatizo katika kuwapata wafanyakazi bora, Baty alisema.

Kwa upana zaidi, orodha inaonyesha taasisi katika bara ya Asia zimepiga hatua, kukiwa na vyuo viwili kutoka barani humo – Chinese University of Hong Kong na Korea Advanced Intitute of Science and Technology – vikiwa ndani ya vyuo 100 bora na vingine vinne vikiingia katika vyuo bora 200. 


Peking University kimepanda hadi nafasi ya 29 kutoka 42, na Tsinghua kikishika nafasi ya 35, kutoka nafasi ya 47 ya mwaka 2015. 

Vyuo vya Asia vinapanda, alisema Baty, wakati serikali ya China ikiingiza mabilioni ya dola katika vyuo vyake wakati huo huo, nchi za magharibi zikikabiliwa na uhaba ya bajeti. 

 Source: RAIA MWEMA

Download: Mungu Wa Ajabu - Ritha Komba

Msanii wa Injili Ritha Komba ameachia rasmi wimbo wake mpya "Mungu Wa Ajabu" ambao unabeba jina la albamu yake mpya itayokuwa sokoni siku za usoni! 
"Nimeita album yangu Mungu wa  ajabu kwasababu katika hali ya kawaida hakuna MTU anae weza kumtoa mwanae kwaajili ya kuiponya nafsi ya MTU mwingine, leo hii tumewekwa huru  na kusamehewa dhambi kwaajili yake pale alipomtoa mwanae wa  pekee na kumleta kwetu sisi wanadamu hiyo ni ajabu." - Ritha Komba
BOFYA DOWNLOAD HAPO CHINI KUUPAKUA WIMBO HUO.

Leicester City washinda mechi Ligi ya Mabingwa Ulaya

Islam Slimani scores for Leicester
Leicester walicharaza Porto bao moja kwa bila mechi yao ya kwanza nyumbani katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya na kuendeleza mwanzo wao mwema katika dimba michuano hiyo mikuu ya Ulaya.

Islam Slimani, ambaye ana sifa nzuri ya kuwafunga Porto alipokuwa akichezea Sporting Lisbon, alifunga bao lake kwa kichwa dakika ya 25 kutokana na krosi ya Riyad Mahrez.

Nguvu mpya wa Porto Jesus Corona alifunga mlingoti kwa kombora lake lakini Leicester walikwamilia uongozi wao na wakaondoka na ushindi.
Slimani alinunuliwa na Leicester £29m siku ya mwisho sokoni. Ana sifa za kuwahangaisha Porto akiwa Sporting Lisbon hivi kwamba alikuwa amepewa jina la utani "the Dragon Slayer" (Mwuaji wa Zimwi)
Leicester wanaongoza Kundi F wakiwa alama mbili mbele ya FC Copenhagen walio nambari mbili.

Klabu hizo mbili zitakutana tarehe 18 Oktoba.
Leicester walioshangaza wengi kwa kushinda ligi kuu Uingereza msimu uliopita, wameanza vibaya msimu Ligi ya Premia, ambapo wameshindwa mechi tatu kati ya sita walizocheza kufikia sasa. Walifungwa mabao manne na Liverpool na Manchester United.

Yet the template that brought success last season - a deep, solid backline and pacey counter-attacks - was once again employed with success at a raucous King Power Stadium.

After seeing his side leak three goals to corners at Old Trafford on Saturday, Leicester boss Claudio Ranieri preferred Luis Hernandez to Danny Simpson at right-back, but it was centre-halves Wes Morgan and Robert Huth who impressed.

At the other end, Mahrez caused trouble on the right in the first half, Vardy explored the channels and Slimani barely stopped running.

Snapchat imezindua miwani yenye kamera

miwani ya kamera
Kampuni ya Snapchat imezindua miwani ya aina yake yanayomuezesha mtu kupiga video na kuisambaza katika mtandao huo wa kijamii.

Inasema miwani hiyo iliyopewa jina 'Spectacles', ina nasa kumbukumbu za watu kupitia kamera ndogo.

Snapchat imejiongezea sifa kwenye mitandao ya kijamii inayotumiwa kutuma ujumbe, zikiwemo picha na video ambazo hufutwa baada ya kuonekana mara moja.

Lakini kifaa hicho kipya na kampuni hiyo kubadilisha jina kutoka Snapchat na kujiita Snap, zinadhihirisha azma ya kampuni hiyo kupita kiwango cha kuwa mtanadao wa ku chati.

Katika tangazo lake la biashara, Snap inasema miwano hiyo ya kutuma video ina lensi ya ukubwa wa digri 115, iliyo na upana zaidi kuliko kamera za kwenye simu za kisasa.Miwani ya kamera
Na ina uwezo wa kurekodi video kwa hadi sekundi kumi kwa mara moja.
Picha hizo zinaweza kutumwa moja kwa moja kwenye mtandao huo wa kijamii ili mtu aweze kuzisambaza kwa wafuasi wengine wa mtandao huo.

Mkurugenzi mkuu wa Snap mwenye umri wa miaka 26, Evan Spiegel, ametaja miwani hiyo kama chombo kinachomuezesha mtu kuona kumbukumbuku nzuri kama walivyoiptia kwa mara ya kwanza.

Mtoto azaliwa kutoka kwa mbegu za watu watatu

Dkt John Zhang akiwa na mtoto huyo
Mtoto wa kwanza aliyetengezwa kwa kutumia mbinu ya uzazi wa mbegu za watu watatu amezaliwa, jarida la kisayansi la New Scientist limetangaza.

Mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miezi mitano ana chembe chembe za DNA kutoka kwa mamake, babake pamoja na jeni za mfadhili.

Madaktari wa Marekani walichukua hatua hiyo kuhakikisha kuwa mtoto huyo wa kiume atakuwa huru kutokana na hali ya jeni ambayo mamake kutoka Jordan anabeba katika jeni zake.

Wataalam wanasema kuwa hatua hiyo ni mwamko mpya wa kimatibabu na inaweza kusaidia familia nyingine zilizo na hali za jeni zisizokuwa za kawaida.
Lakini wameonya kuwa uchunguzi wa mara kwa mara wa mbinu hiyo mpya ya kiteknolojia inayoitwa ufadhili wa Mitochondrial unahitajika.

Mitochondria ni vyumba vidogo vidogo ndani ya kila seli ambavyo hubadili chakula kuwa nguvu inayotumika mwilini.

Baadhi ya wanawake hubeba jeni zilizo na kasoro na wanaweza kupitisha jeni hizo hadi kwa watoto wao.

Wanasayansi waliohusika katika shughuli hiyo walisafiri hadi Mexico kwa sababu huko hakuna sheria za kuzuia shughuli kama hiyo ya kimatibabu.
Walichukua sehemu muhimu za chembe za kinasaba (DNA) kutoka kwa yai la mama, na DNA ya mitochondria kutoka kwa yai la mfadhili na kuunda yai lenye afya ambalo lilitungshwa mbegu kutoka kwa baba.

Matokeo yake ni kuzaliwa kwa mtoto mwenye 0.1% ya DNA kutoka kwa mfadhili na jeni nyingine zote, zinazoamua sifa kaa vile rangi ya nywele na macho kutoka kwa mama na baba.Teknolojia mpya ya uzazi ndio iliotumika kumtengeza mtoto huyoDkt John Zhang, mkurugenzi wa kimatibabu katika hospitali ya New Hope Fertility Centre jijini New York City, anasema yeye na wenzake walitumia njia hiyo kupata viinitete vitano, lakini wakastawisha kimoja tu.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...