Showing posts with label TECHNOLOGY. Show all posts
Showing posts with label TECHNOLOGY. Show all posts

05 January, 2016

Laptop iliyovunja rekodi kwa 2016, nyembamba


Kampuni ya watengenezaji wa laptop za Lenovo kutoka China wamethibitisha kwamba mwaka 2016 wanakuja kuiandika rekodi mpyampya Duniani.
Lenovo wanakuja na aina nyingine ya Laptop kwa mwaka huu 2016, mzigo ni Lenovo Yoga 900 ambapo hii itakuwa ndio laptop nyepesi zaidi Duniani, ina upana wa nusu inch tu upana ambao wanaufananisha na ule wa simu ya iPhone… kingine ni kwamba inaweza kukunjwa kwa namna yoyote bila kuvunjika na wala haina mwisho, yani unaweza kuikunja mpaka sehemu ya nyumba ya kioo na sehemu ya chini vikakutana na bado iko on bila kuzimwa !!
Uwezo wake pia inaweza kukaa na chaji kwa zaidi ya saa 10, na matarajio yaliyopo ni kuziingiza sokoni mwezi March 2016.. bei itagusa kama dola 1,100 ambazo ni sawa na Milioni 2.3 za Kitanzania.
Video hii hapa na muonekano wa Laptop hizo mpyampya.

01 January, 2016

Mambo ni rahisi zaidi.. utaweza kupima chakula kwa simu yako kabla ya kula, hapo vipi?.. (+Video)


Tunasema asante kwa teknolojia kila siku kwa sababu ya vitu vizuri ambavyo tunakutana navyo vikikufikia na kurahisisha mambo mengi kwa sababu tu wataalam wamekaa na wamebuni kitu kizuri !!
Unaambiwa ni suala la kukaa tayari wakati wowote kuanzia sasa tutakuwa na simu zenye uwezo wa kufanya scanning chakula na kutoa majibu kwamba kwenye chakula kuna nini na nini…
scio_results_2-100264526-orig
Kwa sasa kuna kifaa kinaitwa SCiO scanner ambacho ni kidogo tu hivi na kina uwezo wa kufanya scanning kugundua vitu vingi kama kiasi cha sukari kwenye chakula, au mafuta, chumvi, kemikali na vitu vingine… hiki kifaa kimeingizwa kwenye list ya ugunduzi mkubwa uliofanywa kwa mwaka 2015.
Ukiwa na SCiO scanner kama ni mtu mwenye tatizo la kisukari au presha inaweza kumsaidia pia kwa ajili ya kuweza kudhibiti kula vyakula ambavyo havitakiwi kwa wakati akiwa kwenye hali ya kuumwa.

Video ya kifaa chenyewe hii hapa.


31 December, 2015

Mwanaanga apiga ‘wrong number’ kutoka angani

Peake
Mwanaanga Tim Peake, ambaye ndiye Mwingereza wa kwanza kwenda kituo cha kimataifa cha anga za juu, ameomba msamaha baada ya kupiga nambari ya simu isiyo sahihi kutoka anga za juu.
Mwanaanga huyo aliandika ujumbe wake wa kuomba msamaha kwenye Twitter baada ya kumpigia simu mwanamke na kusema: "Hello, is this planet Earth?" (Hujambo, hii ni sayari ya dunia?).
Bw Peake amesema kwenye Twitter kwamba simu hiyo haikuwa ya mzaha.
Hata hivyo, hakusema ni nani hasa aliyekuwa akimpigia simu.
Peake, baba wa watoto wawili anayetoka Chichester, Sussex Magharibi, alitua katika kituo cha kimataifa cha anga za juu (ISS) Jumanne 15 Desemba.
Atakaa katika kituo hicho miezi sita akifanya utafiti wa kisayansi.
Mapema wiki hii, aliwasaidia wanaanga wenzake wawili kutoka nje ya kituo hicho.
Wanaanga Tim Kopra na Scott Kelly, kutoka kituo cha Nasa cha Marekani walihitaji kutoka nje ya kituo hicho kukarabati kifaa kilichokuwa kimeharibika.

15 December, 2015

Ijue smartphone inayokaa chaji siku 15.. (+Video)


Mawasiliano muhimu sana mtu wangu, ndio maana watu wengi wanaona umuhimu wa kuwa na smartphone ili mawasiliano ya njia nyingi yaweze kumfikia.
Wataalam wa mambo wakaingia kazini na kubuni kitu kinaitwa powerbank… ambayo kama smartphone yako ikiisha chaji basi hiyo inakusaidia uendelee kubaki hewani, lakini simu+powerbank ni sawa na mizigo miwili ya kubeba mkononi, usijali… Wachina wanajali mahitaji yako.
CHINA
Kwa sababu unahitaji kitu nafuu, usipitwe na stori kwamba Wachina wameingia chimbo na kuja na mzigo wa smartphone ambazo zinaweza kukaa chaji kwa siku 15, hesabu hiyo kwa lugha nyingine ni kwamba inakaa na chaji kwa wiki mbili kamili !!
Simu yenyewe inaitwa Oukitel K10000 ambayo Wachina wenyewe wamesogezewa tayari sokoni ndani ya nchi yao na pia inapatikana Marekani kwa bei ya kama dola 239 ambazo kwa TZ inasomeka kwa shilingi 515,000/=…. Kaa tayari mtu wa nguvu, mzigo unaweza kugusa sokoni Afrika pia.
Unaweza kuiangalia simu yenyewe hapa, kama huna imani na vitu vya kichina cheki na hiki

12 December, 2015

Tanzania yapata maabara ya kipekee ya aina hiyo kwa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara

post-feature-imageTanzania ni moja kati ya nchi zilizofanikiwa duniani kuratibu maabara inayohamishika kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ebola na magonjwa mengineyo ya mlipuko.

Maabara hii inaweza kusafirishwa mpaka kwenye maeneo yaliyoathirika, ikiwa ndani ya masanduku yaliyofungwa vyema badala ya kusafirisha sampuli kwa ajili ya vipimo kutoka eneo moja kwenda jingine na kuwa katika hatari ya kuathiriwa na vijidudu vingine.

Tanzania na Nigeria ndizo nchi pekee kusini mwa Jangwa la Sahara zenye maabara ya aina hii ambayo itakuwa msaada mkubwa pia kwa nchi za jirani za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, NIMR Dokta Mwele Malecela, amesema maabara hii ina umuhimu kwa kuwa itawezesha kufanyika kwa uchunguzi kwa urahisi na haraka zaidi, hata katika maeneo yaliyo na ugumu kufikiwa.

Changamoto ambayo ilionekana wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi ni wahudumu kutofika kwa urahisi kwenye maabara kwa ajili ya uchunguzi wa haraka kutokana na umbali na miundo mbinu mibovu.

23 August, 2015

KAMPUNI YA APPLE YAZINDUA APP MPYA YA MUZIKI

Kampuni ya Apple imetangaza kubuni programu tumizi mpya inayojumuisha maktaba ya kupeperusha muziki moja kwa moja kwenye internet, programu ya kusikiliza redio kwenye internet na njia maalum ambayo wasanii wataweza kubadilishana vibao vya miziki ambayo bado haijachapishwa rasmi.
App hiyo mpya inajumuisha mfumo wa kubashiri na kupendekeza utakaotumia mwelekezo wa binadamu kuchagua pamoja na sheria ya hisabati ya kutegua kitendawili kwa mifumo au algorithms.
150608221644_2
App hiyo mpya inalenga kuzipa upinzani Spotify, Tidal na app nyinginezo za muziki.
Kadhalika Apple imefichua kwamba Uingereza ndiyo itakayokuwa nchi ya kwanza kupata huduma ya kulipia ya Apple Pay nje ya Marekani. Watumiaji wa simu pamoja na vifaa vingine vya apple kupaa njia mpya ya kusikiliza muziki pamoja na redio.
” Watu wengi katika sekta hii wanachukulia kuzinduliwa kwa huduma hii ya muziki kama jambo kubwa, na matumaini yao ni kwamba hii itasaidia kubadili upokeaji wa huduma kwa usajili wa malipo kuwa bure,” amesema Chris Cooke, kutoka tovuti ya maswala ya muziki Complete Music Update.
“Lakini Spotify ina mbinu yenye matangazo ya kibiashara inayotolewa bure kuisadia kutangaza bidhaa zake jambo ambalo Apple haina.”
Huduma hii mpya ya Apple inazindua kituo cha radio cha Beats 1, mtangazaji katika kituo hicho ni aliyekuwa DJ wa BBC Zane Lowe miongoni mwa watangazaji wengine mashuhuri.
150608203311_apple_music_640x360_apple.com_nocredit
App hiyo vile vile ina uwezo wa kufanya kazi pamoja na programu tumizi ya Siri inayotoa msaada wa maelekezo kwa sauti na kuwawezesha watumiaji kuiamuru icheze wimbo kutoka sauti ya filamu au mwaka bila kuhitaji kujua jina la wimbo huo.

13 August, 2015

Meet Sundar Pichai,the new Google CEO

Google is now part of a company called ALPHABET...No,it has not been sold to another company, but rather the owner and former CEO Larry Page decided to start a new company that will be a mother-company to brands like Google and others he acquired and continue to add on...

Thus, Larry Page is now the CEO of ALPHABET while Sundar Pichai who was Senior Vice President of Products,becomes the CEO of Google. Sundar is a Stanford dropout, being a very technical guy who studied in India before moving to the US.

What Mr Page is trying to do is concentrating in expanding beyond Google's core work and he can only do that by owning a mother company...a rather smart move.

Question is, will Google strip down some of its current products and switch gears? Will Blogspot survive this new change?

10 August, 2015

Apple to launch Apple TV on September

September is set to be full of surprises from Apple...New Iphone,new ipad and now,rumor of an Apple TV can not be ignored. No,am not talking about an actual TV set but rather the baby below...

 It is rumored that Apple will launch this baby on September,bringing all the fun at home..whereby movies,music,games etc are all a click away


From their website,i got this description..."Apple TV gives you access to tons of great HD content in a tiny package. Enjoy blockbuster movies, TV shows, live sports and news, your music, photos, and more — right on your high-definition TV. You can even play content from your iOS devices or Mac on your TV using AirPlay. Best of all, Apple TV is just $69."..
I can't imagine where tech will take us next....

Are you excited about this new Apple product?

17 July, 2015

Samsung yazindua simu nyembamba zaidi

Kampuni ya Samsung imezindua simu yake nyembamba zaidi aina ya smartphone kufikia sasa.
Simu hiyo kwa jina Galaxy A8 ina upana wa milimita 5.9 ikiwa ni wembamba wa asilimia 85 ikilinganishwa na simu ya Galaxy S6 Edge.
Licha ya wembamba huo waandisi wameweza kuiweka betri pamoja na kamera yenye uwezo wa mega pikseli 16.null
Mmoja ya wataalam aliuliza swali la muhimu wa kutengeza simu nyembamba.
Kwa sasa Samsung imetangaza kwamba simu hiyo itauzwa nchini Uchina na Singapore.
''Galaxy A8 haitauzwa nchini Uingereza'' alisema msemaji wake.
Ijapokuwa itakuwa simu nyembamba zaidi kutoka kwa mojwapo ya kampuni kubwa ,kampuni nyengine za Uchina tayari zimeanza kuuza simu kama hizo.

16 July, 2015

IJUE VIZURI SIMU YA HUAWEI P8 KABLA HAUJAINUNUA

PPP
Jana kwenye hoteli ya Hyatt Regency kampuni ya Huawei inayouza na kuzalisha “simu zenye akili”a.k.a SmartPhone ilizindua toleo jipya la simu zake kwenye P Series. Baada ya watu mbalimbali kufurahia P7, hivi sasa ni wakati wa kutumia P8. Hizi hapa ni sababu za kutosha kabisa zitakazo kufanya uimiliki  simu hii ya Huawei P8.
Battery:
Ukizungumzia matatizo ya Smartphone hili ni moja wapo, huwezi kuniambia niache kusikiliza music na kuchat kwa pamoja kisa battery. Kila mtu anaitaji kufanya vitu mbalimbali kwa wakati mmoja kwenye smartphone yake. Director of Sales and Marketing Samson Majwala amesema kwamba battery ya Huawei P8 inauwezo wa kukuwezesha kufanya yote na kukaa kwa siku nzima na chaji. Battery lake halitoki kwenye simu na lina uwezi mkubwa wa Li-Po 2680 mAh
p5
Camera:
Smartphone bila camera kali bado haijawa smart, Huawei P8 inakuja na camera yenye mega pixel 13 (4160 x 3120 pixels) zaidi ya hapo camera hiyo ina uwezo wa Autofocus, optical image stabilization, dual-LED (dual tone) flash. Haijaishia hapo, bali ukiwa unapiga picha uweza kufanya Geo-tagging, touch focus, face/smile detection, panorama na HDR.
Vipi camera ya selfie, hapo unakutana na camera yenye uwezo wa 8 mega pixel na 1080p. So Huawei P8 inakupa uwezo wa kurekodi video ya High Definition ya 1080p@30fps.
p17
Umbo:
Samson Majwala anaendelea kusema kwamba mara nyingi tuvaa nguo ambayo imetu-fit vizuri na hatutaki mizigo mingi kwenye mifuko yetu. Ukiizungumzia Huawei P8 ni nyembamba na bado ni ngumu hata ukiiweka mfukoni sio rahisi kukusumbua. Ina vipimo vya 144.9 x 72.1 x 6.4 mm. Uzito wake ni 144 g (5.08 oz) na nyembamba kwa 6.4mm
Sim Card
Huawei inakupa machaguo mawili kwenye swala la simcard. Zipo Huawei P8 zenye line moja na nyingine zina line mbili.
Operating System
Kama kawaida Huawei huwa inatumia O.S ya Android, lakini Huawei P8 sio tu kutumia Android bali inatumia Android mpya kabisa ambayo ni version 5.0.2 (Lollipop).
p2
Speed
Hakuna anetaka kufungua camera na kuisubili sana kufunguka au kufanya kitu chochote kwenye simu yako na ikawa slow. Huawei P8 imezingatia hilo kwa kuipa uwezo wa Quad-core 2 GHz Cortex-A53 & quad-core 1.5 GHz Cortex-A53. Pia Ram ya Huawei P8 ni 3GB ambayo ni RAM inayozidi hata baadhi ya laptop.
Memory
Mfano kama picha inapigwa na camera ya 13 mega pixel basi lazima inahitajika memory ya kutosha kuhifadhia picha,video na mafaili mengine. Huawei P8 inaweza kuwa na memory ya 16GB au 64GB na pia kwa speed yake unaweza kuongeza memory card hadi yenye 128GB na simu ikabaki kwenye ubora wake.
20150715152416
Mr Samson Majwala (Huawei Director of Sales & Marketing) na Peter Zhang Huawei Country Manager
Network
Huawei P8 imepewa uwezo mkubwa wa kudaka network ya mtandao wako wa simu. Mr Majwala anasema kuna wakati simu inavyobadilisha mnara, inawezekana kuwepo na delay kidogo. Lakini simu hii inauwezo wa kudaka haraka network na sio rahisi kupiga simu na isiunganishwe na mtandao. Pia inawezo wa haraka wa kudaka WiFi. Smartphone hii a.k.a simu yenye akili inauwezo wa kuchagua WiFi ambayo ina nguvu sana kwa wakati huo.
Ziada
Vitu vya ziada ni kwamba ukiwa unataka ku-screenshot kwenye Huawei P8 basi kazi ni rahisi sana. Una doubletap screen na utakua umesha screenshot.
p1
Director’s mode : Kwenye Huawei P8 unaweza kurekodi video kwenye angle 3 na ukawa una mix hizo video wakati unarekodi kama dirrector na mwisho siku ukapata video iliyokua mixed vizuri kama na director.
Huawei P8 ni ngumu imetengenzwa kwa design nzuri ya kuvuti ikiwa na cover la chuma ngumu kulinda simu yako vizuri.
Unaipataje?
Huawei P8 lazima itakua kwenye maduka muhimu ya kuuzia simu. Ukitaka yenye line mbili ni Tsh 1,200,000 na ukitaka yenye line moja ni Tsh 1,100,000

08 July, 2015

Yote unayotakiwa kujua kuhusu simu mpya za iphone 6 na iphone 6 plus

Apple wamevunja ukimya wa muda mrefu baada ya kuzindua simu  aina mbili na sio moja ya iphone 6. Tofauti ya iphone hizi mbili ni ukubwa ikiwa zote zina size kubwa kuliko models za zamani. Models hizi mbili ni iphone 6 na iphone 6 plus . iphone 6 ina screen yenye ukubwa wa inch 4.7 ambayo ni kbwa kuliko ukubwa wa iphone 5s yenye inch 4 inch. iphone 6 plus yenyewe ina screen yenye ukubwa wa 5.5 na kuwa miongoni mwa aina mpya za simu wanazoziita “phablet”.iwatch
Je, lini simu hizi zinaingia sokoni ? iphone 6 na iphone 6 plus zinaingia sokoti tarehe 19 mwezi huu ambapo zitauzwa kwenye nchi 10 ambazo ni US, Australia, Canada, France, Germany, Hong Kong, Japan, Puerto Rico, Singapore na UK. Je, vipi kuhusu kukaa na chaji ? ukubwa wa simu hizi umechangiwa na kuongezeka kwa ukubwa wa betri ambapo kwa iphone 6 inaweza kukaa hadi masaa 11 ukiitumia muda wote ambapo iphone 6 plus inakaa hadi masaa 12.
Vipi , je Apple wamezindua kitu kingine ? Yes , ukiachana na iphone 6 na iphone 6 plus , Apple wamezindua kwa mara ya kwanza Apple Watches , saa za mkononi za Apple tunazoziita smartwatches ambapo itasaidia mawasiliano ya haraka kwa kutumia saa na pia kutumia Apps nyingine kirahisi kama maps na siri. Pia Apple Watch inaweza ikatumika kama kifaa cha mazoezi ambapo inaweza ku-track mazoezi yako.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...