06 February, 2016

Guardiola:Kazi ya Man City haitaniathiri


Mkufunzi wa timu ya Bayern Pep Guardiola amesema hatua yake ya kuelekea katika kilabu ya Manchester City haitaathiri kazi yake katika kilabu ya Bayern Munich msimu huu.
Guardiola mwenye umri wa miaka 45,amekubali mkataba wa miaka mitatu wa kuchukua mahala pake Manuel Pellegrini mwishoni mwa msimu huu.
Katika misimu misita ,kocha huyo wa zamani wa Barcelona ameshinda mataji 19 ikiwemo vikombe sita vya ligi na viwili vya bara Ulaya.
''Kwa nini vigumu?Mimi ni kama mwanamke,naweza kufanya kazi mbili mara moja na kudhibiti hali zote mbili.Nina talanta kubwa katika hili,''alisema Guardiola.
Guardiola ameripotiwa kukataa kandarasi mpya na kilabu hiyo ya Bundesliga mwaka uliopita na kutangaza mwezi Disemba kwamba ataondoka.

Magari 2 yakamatwa yakihusishwa na wizi ofisi ya Kamishna Mkuu TRA

Sirro
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Naibu Kamishna Simon Sirro.
Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kukamata magari mawili yakihusishwa na wizi katika ofisi ya kamshina mkuu wa TRA huku yakiwa na vifaa vilivyoibiwa katika ofisi hiyo vikiwa ni pamoja na komputa, na TV.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kamanda Simon Sirro amesema kutokana na oparasheni kali iliyokuwa ikiendeshwa na jeshi ilifanikiwa kuwatia nguvuni watuhumiwa wanne wakiwa na vifaa vilivyoibiwa.
Aidha kamanda huyo wa kanda maalum ya Dar es Salaam amesema katika oparesheni hiyo pia jeshi la polisi lilifanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi milioni 150 mali ya Bw Ahmed Huwel mkazi wa Msasani.
Katika hatua nyingine Kamanda Sirro ametangaza kusitishwa kwa muda kwa shughuli za ulinzi shirikishi katika vituo vya polisi kutokana na vikundi hivyo kualamikiwa na wananchi kwa kutokuwa na tija katika jamii.

Habari Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi Ya Februari 6

05 February, 2016

Hii ndio Club ambayo Ander Herrera atakwenda pindi atakapo ihama United

ander Herrera
Ander Herrera ameweka wazi kuwa siku moja angependa kuja kuichezea klabu ya Boca Juniors wakati atakapoachana na klabu ya Manchester United.
Herrera ameongeza kuwa kabla ya kwenda Argentina, angependelea kurudi kunako klabu yake ya zamani ya Real Zaragoza kabla ya umri wake kumtupa mkono.
“Kama siku moja napata fursa ya kucheza Amerika ya Kusini, basi ningependelea zaidi kucheza katika klabu ya Boca.
“Uwepo wa Marcos Rojo pia hunifanya kuwa na shauku zaidi ya kwenda kucheza huko.”

Official AUDIO | Alikiba - LUPELA | Download


Click HAPA

VIDEO: Daniel Sturridge is ready to quit Liverpool this summer

Daniel Sturridge is ready to quit Liverpool this summer over his fury at criticism questioning his desire to play for the club.
Manager Jurgen Klopp has spoken publicly of his frustrations over Sturridge’s fitness and several former Anfield stars have intimated it is time for the club to sign a replacement.
Sturridge is fed up at a growing perception that he lacks the hunger to fulfil his potential and believes a clean break is required this summer. Daniel Sturridge is ready to quit Liverpool this summer over fury at criticism of his injury recordSturridge has not featured for Liverpool since coming off the bench against Newcastle in early December

England striker Sturridge's Liverpool career has been plagued by a number of serious injuries

Ubelgiji imeendelea kukaa katika nafasi ya kwanza kwenye viwango vya ubora vya FIFA


Ubelgiji imeendelea kukaa katika nafasi ya kwanza kwenye viwango vya ubora vya FIFA kwa muhjibu wa viwango viliyotolewa Alhamisi.
Katika kumi Bora imebaki vile vile bila mabadiliko huku Mabingwa wa Dunia, Germany, wakiwa Nafasi ya 4.
Ivory Coast imeporomoka hadi Nafasi ya 9 kwa bara la afrika na sasa ipo Nafasi ya 28 Duniani ikifuatiwa na Cape Verde ambayo ipo Nafasi ya 33 baada ya kupanda Nafasi huku Algeria ikiwa Nafasi ya 36 baada ya kushuka Nafasi 8.
Timu nyingine katika ishirini bora ni Ubeligiji, Argentina, Uhispania, Ujerumani na Chile.
20 bora katika viwango vya Fifa.
1 Ubelgiji
2 Argentina
3 Uhispania
4 Ujerumani
5 Chile
6 Brazil
7 Portugal
8 Colombia
9 England
10 Austria
11 Uruguay
12 Switzerland
13 Ecuador
14 Uholanzi
15 Italy
16 Romania
17 Wales
18 Croatia
19 Hungary
20 Uturuki

MICHEZO: Ligi kuu England kuendelea jumamosi


Ligi kuu ya soka ya England inatarajiwa kuendelea tena umamosi kwa michezo mbalimbali katika viwanja tofauti, Manchester City watakuwa wenyeji wa Leicester, Aston Villa watamenyana na Norwich city, Liverpool watawaalika Sunderland, Newcastle united dhidi ya West Brom, Stoke watakuwa wenyeji wa Everton,Swansea watawakabili Crystal Palace, Watford watakuwa wageni wa Tottenham, na Southampton watakuwa nyumbani dhidi ya West Ham.

Kakatika kwa umeme mara kwa mara ni kutokana na uchakavu wa miundo mbinu


Serikali  imesema tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara nchini linatokana na uchakavu na kuzidiwa kwa vituo vya kupoza umeme na miundombinu ya usafirishaji na usambazaji nishati hiyo.
Katika kukabiliana na tatizo hilo Tanesco inachukua hatua za kujenga mifumo ya njia kubwa za umeme wa msongo wa kilovoti 400 (Iringa- Dodoma-Singida-Shinyanga), gridi ya Kaskazini Mashariki (Dar es Salaam, Chalinze,Tanga –Arusha), ya Kaskazini Magharibi (Geita- Kagera –Katavi- Kigoma- Rukwa na Mbeya) na Makambako- Songea wa kilovoti 220.
Kauli hiyo ilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani wakati akijibu swali la Mbunge wa Magu, Boniventure Kiswaga (CCM). 
Kiswaga alitaka kufahamu serikali imejipangaje kukabiliana na tatizo la kukatika katika kwa umeme.
Pia mbunge huyo alitaka kufahamu, Je serikali itakamilisha lini kupeleka umeme katika vijiji vya jimbo hilo ikizingatiwa mpaka sasa ni asilimia 20 tu ya vijiji ndiyo vina umeme. 
Kalemani akijibu swali hilo, alisema tatizo la kukatika kwa umeme linatokana na uchakavu na kuzidiwa kwa miundombinu ya kupoza umeme pamoja na matukio ya kulipuka kwa transfoma yanayosababishwa na radi hasa kipindi cha mvua pamoja na wizi wa mafuta ya transfoma unaofanywa na wananchi wasio waaminifu.
Alisema Tanesco inakamilisha upanuzi wa usambazaji wa umeme katika majiji makubwa ya Arusha, Dar es Salaam, na Mwanza ambapo kazi hizo zitahusisha ujenzi wa njia mpya za umeme na kupanua vituo vya kupoza umeme.

“Kukamilika kwa kituo cha kupoza umeme cha KIA mkoani Kilimanjaro kumeimarisha upatikanaji wa umeme maeneo ya Mirerani na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA),” alisema Kalemani.

Pia vituo vya kupoza umeme katika jiji la Dar es Salaam vya Gongo la Mboto, Kipawa, Mbagala, na Kurasini vitaunganishwa kwa njia ya sakiti mzunguko kutoka Ubungo na Kinyerezi kuanzia Machi mwaka huu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa Ya Februari 5

04 February, 2016

Jose Chameleone kanunua viatu pair mbili kwa thamani ya Tsh 20mliion?

Jose Chameleone ambaye ni miongoni mwa mastaa wa muziki Afrika Mashariki na Afrika wenye pesa nyingi zaidi amenunua pea mbili ya viatu aina ya Nike Air Mag venye thamani ya dola 9000 mpaka 12500 za Kimarekani ambazo ni zaidi ya milioni 20 za Tanzania.
chameleone 2
Picha hii iliambatana na ujumbe huu kuhusu viatu hivi.
Thanks DHL fast delivery!! . Back to the future #NIKEAIRMAG Limited Edition These God Damn Shows R Correct>>>>>> you can get one too from this Nike Store https://m.fancy.com/things/261000449/Nike-Air-Mag-Back-to-The-Future
cham 2

Jamhuri ya Demokrasia ya Congo imefuzu kwa fainali ya mchuano wa CHAN


Jamhuri ya Demokrasia ya Congo ilijikatia tikiti ya fainali baada ya kuilaza Guinea mabao 5-4 kwa mikwaju ya penalti.
Mechi hiyo ilikuwa imeishia sare ya moja kwa moja katika muda waziada baada ya Ibrahim Sankhon kuisawazishia Guinea kunako dakika ya mwisho ya kipindi cha pili cha muda wa ziada.
Lakini dalili za kufuzu zilionekana mapema,Ibrahim Bangoura alipokosa penalti ya kwanza ya Guinea.
Kimwaki,Mika,Jonathan Bolingi,Gikanji,Mechak Elia walifungia Leopards ya DRC huku
Ibrahim Sankhon,Leo Camara,Kile Bangoura,Daouda Camara wakiifungia Guinea.
Hata hivyo Kipa nambari moja wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo Vumi Ley Matampi aliokoa mkwaju wa penalti uliopigwa na Youla na kuipa DRC ushindi wa mabao 5-4 Guinea
Timu hizo zilitoshana nguvu muda wa kawaida na mechi ikaingia muda wa ziada uwanjani Amahoro, Rwanda.
Ni katika muda wa ziada ambapo Jonathan Bolingi Mpangi kunako dakika ya 101 alifanikiwa kutikisa wavu wa Guinea.
Mapema kwenye mechi, mchezaji wa DR Congo Padou Bompunga alipewa kadi ya njano dakika ya 38. Hili lina maana kwamba hataweza kucheza fainali iwapo timu yake itafuzu.

Makamanda wa juu wa wanamgambo wa Islamic State wameingia nchini Libya


Makamanda wa juu wa wanamgambo wa Islamic State wameingia nchini Libya miezi ya karibuni wakitokea Iraq na Syria,Afisa wa maswala ya intelijensia nchini Libya ameeleza.
Afisa huyo ameliambia Shirika la utangazaji la uingereza  BBC kuwa wapiganaji wa kigeni wameingia mjini Sirte.
Wawakilishi kutoka nchi 23,wakiwemo wa kutoka Marekani na Uingereza wamekutana Rome siku ya jumanne kujadili tishio la wanamgambo wa IS nchini Libya.
Hali ya kutokubaliana kwa serikali hasimu nchini humo imesababisha jitihada za kupambana na IS kugonga mwamba.
IS iliudhibiti mji wa Sirte mwaka jana.mji huo ulikuwa makazi ya aliyekuwa Kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Kundi la IS linaaminika kuungwa mkono na wale waliokuwa watawala wa utawala uliopita.
Lakini Ismail Shukri, mkuu wa idara ya intelijensia mjini Misrata, ameiambia BBC kumekuwa na wapiganaji wengi wa kigeni miezi ya karibuni.
Wengi wa wapiganaji wa IS ni wageni kwa asilimia 70. Wengi wao ni raia wa Tunisia,wakifuatiwa na Misri, raia wa Sudan na wachache kutoka Algeria.
Pia Raia wa Iraq na Syria, raia wengi wa Iraq wanatoka kwenye jeshi la Saddam Hussein.
Shukri amesema makamanda wa IS wamekimbilia Libya,kutokana na matukio ya mashambulizi ya anga nchini Iraq na Syria.
Mamlaka mjini Misrata zimesema zinajiandaa kupambana na IS mjini Sirte.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...