Showing posts with label ENTERTEINMENT. Show all posts
Showing posts with label ENTERTEINMENT. Show all posts
03 January, 2016
Rucky Baby kaja na video ya wimbo ‘Give me some’, kama ilikupita unaweza kuicheki hapa…
14 October, 2015
Hii ndio orodha kamili ya washindi wa Tuzo za BET HipHop 2015
Tuzo za BET Hiphop 2015 zimeoneshwa rasmi usiku wa jana, Big sean na Kendrick Lamar wametawala tuzo hizo kwa kushinda tuzo 3 kila mmoja, wakifuatiwa na Drake aliyeshinda Tuzo mbili ikiwa ni pamoja na ‘MVP of the Year’ na Fetty wap aliyeshinda tuzo ya “track of the year” na tuzo ya “who blew up”
Hii ndio orodha kamili ya washindi
Best Hip Hop Video: Kendrick Lamar “Alright”
Best Collabo, Duo or Group: Big Sean feat. Drake and Kanye West – “Blessings”
Best Live Performer: J. Cole
Lyricist of the Year: Kendrick Lamar
Video Director of the Year: Benny Boom
DJ of the Year: DJ Mustard
Producer of the Year: DJ Mustard
MVP of the Year: Drake
T rack of the Year: “Trap Queen” – Produced by Tony Fadd (Fetty Wap)
Album of the Year: J. Cole “2014 Forest Hills Drive”
Who Blew Up Award: Fetty Wap
Hustler of the Year: Dr. Dre
Made-You-Look Award (Best Hip-Hop Style): DeJ Loaf
Best Club Banger: Big Sean feat. E-40 – “IDFWU”
Best Mixtape: Future – 56 Nights
Sweet 16: Best Featured Verse: Drake – “My Way (Remix)” (Fetty Wap feat. Drake)
Impact Track: Kendrick Lamar – “Alright”
People’s Champ Award: Big Sean feat. Drake and Kanye West – “Blessings
17 August, 2015
Blogs za Nigeria zimekamata comment ya instagram ya msanii Wiz Kid akimkaribisha rapa Dej Loaf wa Marekani akae karibu yake kwenye shughuli waliyo hudhuria.
Fahamu kuwa WizKid anampenzi wake anayefahamika kama Tania Omotayo na ameonekana kwenye video mpya ya ‘Sade’.
Wiz Kid aliandika kwenye picha ya Dej Loaf “U need to come sit on this ting baby gyal“. Oooh! .
Hakuna ushahidi kuwa Dejloaf aliona comment hio na hata kuja kukaa karibu na Wiz Kid.
16 August, 2015
Alikiba na Diamond, Davido na Wizkid kuwania ‘Msanii Bora’ na ‘Wimbo Bora wa Mwaka’ tuzo za AFRIMA 2015
Orodha ya wasanii wanaowania tuzo za All Africa Music Awards (AFRIMA)
2015 za Nigeria yametangazwa. Tanzania inawakilishwa na Diamond, Alikiba
na upande wa wasanii wa kike ni Linah.Wasanii wenye ushindani mkubwa Afrika Mashariki, Diamond na Alikiba pamoja na wasanii wenye ushindani mkubwa Afrika Magharibi, Davido na Wizkid wote kwa pamoja wamekutana katika vipengele muhimu vya ‘Wimbo Bora wa Mwaka’ na ‘Msanii Bora wa Mwaka’.
Alikiba na Diamond pia wanawania kipengele cha ‘Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki’, na Wizkid na Davido wanashindania ‘Msanii Bora Wa Kiume Afrika Magharibi’. Mwingine kutoka Afrika mashariki katika kipengele hiki ni Jose Chameleone wa Uganda.
Linah anawania kipengele cha ‘Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki’.
Upigaji wa kura umeanza August 14, na tuzo zitatolewa November 15, 2015 jijini Lagos, Nigeria.
Hii ni orodha ya Nominees.
11 August, 2015
Kilicho mkuta WEMA Instagram baada ya kuwakataza wanao tumia jina lake kumpost Lowasa au kumuunga mkono
Wema Sepetu avamiwa kwenye account yake ya Instagram baada ya kuwataka wanao jiita Team Wema au kama kuma kuna mtu anatumia jina lake kwenye account yake kuwa wasimuunge mkono Lowasa wala hata ku post picha yake.Wema ameandika haya "Wamoja havai Mbili...... Alafu nina msg
to Team Wema ... Please my darlings... kama kuna mtu anatumia account
yenye jina langu naomba msimpost Lowassa tafadhal... Kama unashindwa
then badili tu jina... Dont use my name kumpost Lowassa .... Jamani Iam
Not Team Lowassa.... Thank u... CCM tu hapa... TeamMagufuli to death ...
Nilishasema mi ni CCM Damu Kabisa... Sidanganyiki... UKAWA mtaenda
msojielewa...."Hizi ni baadhi ya comment ambazo wamempinga Wema.
sam.kiriahapo umebugi mamaaa nshaku unfollow kwa uswechu wako mchoma sindano za matako we
nassy_junior6_chotta Nlikuheshim now mejua Y watu wengi hawakupend licha ya mazur ulofanya !!! Kumbe huna tofaut sana na wale wanaokuchukia bila sababu. Umesoma hujaelimika .... Pumbaaaaa kabisa wee sio wakuandika huu utumbooo ungekaa kimya tyuuu watu wakaelewa
newahosimkoko @wemasepetu Kioo cha jamii anatakiwa kuwa na busara na hekima, nikweli unapenda ccm but tumia busara kwenye matamshi na ukiwazacho, usitukane mamba kabla ujavuka mto, mbona Tanzania wasanii ni wengi, mbona wazuri na wajulikana sana na wanapendwa, najiuliza mbona wao wapo kimya, kila siku wema kwanini usi focus kwenye vitu vya msingi na kunyamaza watu waone matendo na si maneno, jua we ni mama wa baadae, je utawafundisha nini watoto wako ukiwa ufanyi busara kwenye kila utendalo
A photo posted by 👄wemasepetu👄 (@wemasepetu) on
Tazama kihonjo cha video mpya ya Jux akimshirikisha Joh Makini – Looking for You
10 August, 2015
Hemed Kumshirikisha Christian Bella kwenye Rmx ya ngoma yake “Imebaki Story”
Msanii wa Bongo Fleva na Filamu, Hemed Suleiman au Hemed Phd amefunguka kuwa atamshirikisha mkali wa masauti Christian bella kwenye Rmx ya track yake “Imebaki story” ambayo inafanya vizuri kwasasa.
Hemed amefunguka kuwa idea ya ngoma hiyo ni kuwa yeye ataimba kikongo na Christian bella ataimba kiswahili. Icheck original video ya hiyo ngoma
Huyu ndio mtanzania aliyefanya Cover ya track ya dr.dre ‘Talking to my diary’ Isikilize hapa
06 August, 2015
Kwamujibu wa Forbes, Hawa ndio waigizaji 10 wanaolipwa mkwanja mrefu zaidi duniani
Usanii wa uigizaji katika filamu hutuacha na hisia tofuati tunapowatazama hasusan waigizaji nguli.Lakini je, unafahamu kiasi cha fedha wanazolipwa kwa uigizaji wao ?
Jarida la Forbes limezindua orodha ya waigizaji bora na wanaolipwa mshahara wa juu zaidi duniani.
Jarida hilo limeangazia faida wanazopata baada ya kulipa gharama kama vile kodi na ada ya wasimmamizi wao. Kwa mwaka wa tatu mfululizo, muigizaji wa filamu ya Iron Man, Robert Downey Jr anaongoza orodha hiyo.
Downey Jr alitia kibindoni dola milioni $80m . Downey ameshiriki katika filamu za 'Avengers' na 'Age of Ultron'. Na kwa mara ya kwanza, orodha hiyo imewashirikisha waigizaji wanaoigiza nje ya Hollywood.
Hii inamaanisha kuwa wasanii watajika katika filamu nje ya Marekani kama vile Bollywood ya India na wasanii wa Asia pia wamejumuishwa katika orodha hiyo. Muigizaji nyota kutoka Uingereza Daniel Craig aliorodheshwa katika nafasi ya 15 sawa na Chris Hemsworth kutoka Australia.
Wawili hao walizoa takriban dola milioni $27m kwa mujibu wa Forbes. Msanii Jackie Chan wa filamu ya Karate Kid miongoni mwa nyingine nyingi tu, ameorodheshwa katika nafasi ya pili.
Chan alipokea dola milioni 50 mwaka uliopita kwa kazi yake.
Tazama Orodha kamili hapa
Hawa ndio wasanii wanaolipwa vyema kulingana na Forbes.
- Robert Downey Jr - $80m
- Jackie Chan - $50m
- Vin Diesel - $47m
- Bradley Cooper - $41.5m
- Adam Sandler - $41m
- Tom Cruise - $40m
- Amitabh Bachchan - $33.5m
- Salman Khan - $33.5m
- Akshay Kumar - $32.5m
- Mark Wahlberg - $32m
05 August, 2015
Mastaa wa soka na vioja vyao Uwanjani
Wachezaji mpira ni miongoni mwa watu
maarufu sana kutokana na kazi yao kupendwa au kuwa na mashabiki wengi
kutoka sehemu mbalimbali, miongoni mwa vitu ambavyo huwezi kuvidhania
kama unaweza kuviona kwa mastaa wako wa soka ambao umezoea kuwaona
wakiwa katika muonekano uliozoeleka kuonekana labda wakiwa katika mechi
au matukio ya kawaida.
Katika pitapita zangu mtandaoni nimekutana na hii list ya mastaa wa soka waivyoamua kujiachia kwa vioja kabisa.
Dani Alves
Dani Alves aliwahi kuvaa wigi wakati akisherehekea ushindi wa Timu yake ya Taifa
Ni
mchezaji wa zamani wa Arsenal anatajwa kuwa sio miongoni mwa watu
wanaouchukulia mchezo wa mpira wa miguu serious.. Ndani ya Uwanja akaona
afanye kioja kupindisha uso wake.
Chochote anachokifanya Balotelli huwa hakiko mbali na headlines za Waandishi wa Habari.
Antonio Cassano akishangilia ushindi wa goli 2-0 Italy ilivyoifunga Ufaransa katika michuano ya Euro 2008.
Zlatan Ibrahimovic wakati alipovua nguo Uwanjani bila hofu kabisa.
Kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester City Stephen akishangilia goli kwa staili ya kuvua bukta
David Luiz beki ghali wa klabu ya PSG ya Ufaransa akishangilia goli
04 August, 2015
NEW: PINK FT. YOUNG DEE – USIOGOPE (OFFICIAL VIDEO)
Timaya wa Nigeria akutana na Rihanna, Riri aupenda wimbo wa Bum Bum.
Msanii kutoka Nigeria Timaya ameonekana kwenye visiwa vya Barbados
kwenye tamasha la muziki akiwa na Bad girl Riri aka Rihanna. Timaya na
Rihanna walipiga picha pamoja na baadae Riri alionekana akicheza wibo wa
Ti,aya ‘Bum Bum’. Inasemekana kuna collabo inakuja na itafanywa na Don
Jazzy.
03 August, 2015
EW MUSIC: CHUSE BOY FT. MAKAMUA & COUNTRY BOY – TUNA HUSTLE
VIDEO – MIRROR NA PETIT MAN HAWAPO TENA ENDLESS FAME?
Diamond Platnumz ameshinda tuzo zingine mbili.
Msanii wa bongo fleva Diamond Platnumz ameshinda tuzo zingine kubwa Afrika, kupitia kurasa yake ya instagram ametufahamisha kuhusu ushindi huu na tuzo.
“ Thanks alot to my all Fans around the World, for your unconditional love and Support that you been Giving me… i can’t even explain how grateful i am… two awards on NollyWood & African People Choice Awards @Africannafca
FAVOURITE SONG OF THE YEAR (Nana)
FAVOURITE ARTIST OF THE YEAR
thanks alot @Africannafca
(Naomba nitumie Muda huu kuwashkuru Mashabiki zangu wote kwa Mapenzi na Sapoti yenu ya Dhati mnayoendelea kunipa…ningependa niwataarifu kuwa kijana wenu mmeniwezesha kushinda tunzo mbili ambazo ni MSANII ANAEPENDWA AFRICA na NYIMBO INAYOPENDWA AFRICA (#NaNa ) kwenye Tunzo za NollyWood & African people Choice Awards @Africannafca zitazotolewa tareh 12 /09 /2015
Nuh Mziwanda naye afunguka haya baada ya BASATA kumfugia Shilole kazi za sanaa kwa Mwaka moja
Issue ya kufungiwa kazi za sanaa na BASATA kwa msanii Shilole kumeshtua wengi wasanii maana haijawahi kutokea kuona msanii akafungiwa kazi za sanaa. Wengi wamekuwa wakilalamika kuwa BASATA huwa
wanasikika pale tu msanii anapo cheza au kuonekana nusu uchi jukwaani,
Kufungia video yenye kuonyesha uchi au kinyume na maadili ya Kitanzania.Baadhi ya wasanii na wadau wa sanaa wamesema BASATA huwa haionekani kusemea suala la hati miliki ya kazi za wasanii au kusimamia maslahi ya wasanii bali imeishia kwenye nidhamu tu.
Nuhu Mziwanda ambaye ni msanii wa muziki wa Bongo Flava na pia ni mpenzi wa Shilole naye ameamua kuandika yake baada ya mpenzi wake kufungiwa kazi za sanaa kwa mwaka mzima.
Haya ndiyo aliyo aandika Instagram.
"Hili si swala la kuchekelea au kumkejeli mtu au kueka chuki'sisi sote binadamu tunapita katika hii dunia na kila mtu ana kazi anayofanya 'tunalalamikaga kazi zetu zinaibiwa lakini hakuna hatua yoyote inayochukuliwa 'tuuze madawa ya kulevya ili tuuwawe nchi za watu,au mnataka ajiuze barabarani? na si kila afanyae kazi anapatia'kuna mda ajali zinatokea popote hata uwe unauza vitumbua vinaweza vikaungua jikoni'sisi ni Watanzania na inabidi tulichanganue hili swala ili kukuza mziki wetu mana ni tatizo kubwa sana na ni msanii mkubwa mwenye mashabiki wengi sana Africa'naomba tuungane kueka jambo sawa'Basata ni wazazi wetu na wanaelewa tunategemea sanaa kula ugali na kuendesha familia'hili swala lifikiliwe mara ya pili" Ameandika Nuhu Mziwanda.
02 August, 2015
NI NUHU NA WEMA
Tazama video, Chris Brown aeleza hisia zake kwa Rihanna asema anamuheshimu na ana mapenzi juu yake
Ambapo Breezy aliongelea ukweli wa ku-perform BBHMM wimbo wa Rihanna wakati wa concert kwakusema wimbo huo wa Rihanna ni mzuri, Anamuheshimu Rihanna kama msanii. Prezzy akasema kuwa anauhakika pia hata Rihanna anasikiliza muziki wake.“That song is hot. I respect her as a artist you know. I’m pretty sure she plays my music.”
Chris Brown alieleza kuwa Rihanna ni rafiki yake kwakuwa wanajuana kwanzia akiwa na umri wa miaka 14 na hawatakuwa na tofauti. Pia anamapenzi na heshima juu yake.
“She is my friend. We’ve known each other since we were 14. We always gonna be cool. I got a lot of love and respect for her.”
Alikiba amesema tayari ameshafanya kolabo na msanii wa Congo DRC, Fally Ipupa Tazama video Hii
Mkali wa Bongo Fleva Alikiba amesema tayari ameshafanya kolabo na msanii wa Congo DRC, Fally Ipupa na kwamba ukifika wakati itatoka.Alikiba ambaye yupo kwenye mikakati ya kufanya kolabo na Davido, ameiambia Clouds TV kuwa ikifika wakati ataiachia kolabo hiyo ambayo amedai ipo tayari. Tazama video hii akielezea jambo hilo“Mwana ilikuwa ni nyimbo ambayo nifanye na Fally Ipupa, beat imetengenezwa na Man Walter. Lakini kitu ambacho kilikwenda kutokea wakati nakwenda studio kufanya nyimbo nyingine kabisa, nikakuta Man Walter ameniandalia beat, ‘ile nyimbo yako unataka kufanya na Fally Ipupa hii hapa.’ Akaweka beat nikaanza ku-flow pale, nikaimbaimba nikapata melody. Kesho yake nikarudi nikafanya demo, kufanya demo nikarudi nyumbani nikakaa kama wiki, baada ya wiki moja nikaenda nikaimaliza yote,” alisema Kiba.
“Lakini sasa tukakaa na Man Walter nikasema Fally Ipupa anaimbaje hapa? Akasema kwa kweli umeperfome vizuri sana, mimi naona ume-perfome vizuri sana. Tukapanga tufanye nyimbo nyingine. Basi akasema poa lakini Mwana ilikuwa Fally Ipupa aimbe. Kolabo na Fally Ipupa ipo, lakini kama ilivyo kawaida yangu napendaga kuwa-surprise watu kwa sababu watu wanakuwa hawajui Ali anafanya kitu gani muda wowote. Lakini ngoma ya Fally na mimi ipo na siwezi sema ni nyimbo gani lakini nyimbo ni nzuri sana na imesharekodiwa,” alisema Alikiba.
Pia Alikiba amesema kolabo yake na Davido ipo kwenye hatua nzuri na muda ukifika mashabiki wa muziki wake watajua lini itatoka.
01 August, 2015
“Kuacha Aina Ya Muziki Uliokutambulisha Unakuwa Haupo Loyal Kwa Mashabiki Wako” – Mansuli
Msanii wa hip hop, “Kina kirefu” rapper Mansuli amefunguka na kusema
kwamba msanii kuacha aina ya muziki uliokutambulisha wakati unaanza
kufanya unakuwa haupo loyal kwa mashabiki wako unakuwa hauwatendei haki
watu wako, ingawa kila mtu anakuwa na uhuru wa kufanya kitu ambacho
anakipenda.
Mansu,I ni moja ya wasanii wanaofanya hip hop halisi, ameendelea kufanya hivyo toka alipoingia kwenye game, toka ngoma ya “Kina kirefu” ilipomtambulisha katika gemu, ameendelea kupewa heshima ndani ya gemu la hip hop.
Kwa sasa Mansulii amerudi rasmi baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu kutokana na masomo, leo Jumamosi ameachia ngoma mpya inayokwenda kwa jina la “Usiku Mmoja” feat Maulo, ngoma ambayo imefanywa na producer Pala kutoka Tatoo Records Masaki Dar es salaam.
Anafanya mipango ya kufanya video ya ngoma na mkali Director Hanscana, akiamini kwamba directors 1a Tanzania pia wao wanaweza, akiongelea kuhusu video kupigwa Tv za kimataifa kwa nyimbo za Kibongo amesema ni kitu kizuri.
Mansu,I ni moja ya wasanii wanaofanya hip hop halisi, ameendelea kufanya hivyo toka alipoingia kwenye game, toka ngoma ya “Kina kirefu” ilipomtambulisha katika gemu, ameendelea kupewa heshima ndani ya gemu la hip hop.
Kwa sasa Mansulii amerudi rasmi baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu kutokana na masomo, leo Jumamosi ameachia ngoma mpya inayokwenda kwa jina la “Usiku Mmoja” feat Maulo, ngoma ambayo imefanywa na producer Pala kutoka Tatoo Records Masaki Dar es salaam.
Anafanya mipango ya kufanya video ya ngoma na mkali Director Hanscana, akiamini kwamba directors 1a Tanzania pia wao wanaweza, akiongelea kuhusu video kupigwa Tv za kimataifa kwa nyimbo za Kibongo amesema ni kitu kizuri.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...
-
Mpenzi msomaji wa safu hii ni siku nyingine tunakutana katika kujuzana,kukumbushana, na kuelimishana mila na desturi za makabila mbalimbal...
-
This is a song sang by a very gifted woman Adele, I sang it to show world that everyone appreciate and love to enjoy good music! Asa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...













