12 December, 2015

Tanzania misses the chance in Top 30 of Miss World

Only 5 African countries have made it to the Top 30 list of Miss World,for the Top Model challenge. These are Cameroon, Cote d'Voire, Ethiopia, South Africa and South Sudan


Sadly,Tanzania made it to the Top 50 and that was it...

We still have other chances to raise the flag high, let's use the social media chance to vote our Miss Tanzania into the Top list...

Sababu 5 Kwanini Neymar Atakuwa Mwanasoka Bora Wa Dunia Miezi Kadhaa Ijayo

Kwa mara ya kwanza jukwaa la Ballon D’or litapata ugeni mpya wakati mshambuliaji wa kibrazil Neymar Dos Santos atakapoungana na wafalme wawili wa tuzo hizo ambao wameitawala tuzo hiyo zaidi ya miaka 8 – Cristiano Ronaldo na Lionel Messi – itakapofika January 2016. Kama isingekuwa siasa za soka basi mbrazil huyo angeweza kushika nafasi ya pili nyuma Lionel Messi. Lakini hii ni ‘era’ mpya ya soka.
IMG_1225.JPGKatika miaka 8 iliyopita Ballon D’or imekuwa inatawalia na Messi dhidi ya Ronaldo, lakini kadri siku zinavyozidi kwenda inaonekana mtu wa kupambana na Messi si Ronaldo tena ambaye umri unamtupa – anakaribia kutimiza miaka 31, Ni Neymar ambaye nyota yake inazidi kung’aa kila kukicha.
Pamoja na kufanya kazi kwa kushirikiana vizuri na washambuliaji wengine wa Barca, pia Neymar ameonyesha anaweza ku-control mechi kama ilivyo kwa Messi, tofauti na Ronaldo.
Wadau na wachambuzi wengi wa michezo duniani wanaamini katika kipindi kifupi kijacho Neymar atakuja kuwa mwanasoka bora zaidi duniani, mimi nikiwepo kwenye kundi hilo na hizi ndio sababu zangu.
  1. Kupafomu vyema Anapokosekana Messi 
281D9A4600000578-3060793-image-a-29_1430309883032Unapocheza pembeni ya Lionel Messi, vitu huenda kiurahisi zaidi. Wakati Messi alipoumia hivi karibuni kwa zaidi ya mwezi mmoja, wachambuzi wengi walikuwa na mashaka na uwezo wa Neymar kuziba pengo na kuisadia Barcelona kama ilivyokuwa kwa Messi. Lakini matokeo yake, Neymar akafanya vizuri zaidi katika kuisadia Barcelona kushinda kila mara na sasa wapo juu ya kilele cha msimamo wa ligi na wamefuzu raundi ya 16 bora wa UEFA Champions League. Kuziba pengo la mmoja wa wanasoka bora zaidi kuwahi kuugusa mpira sio jambo rahisi kabisa lakini kwa namna Neymar alivyohimili presha na kuifanya kazi, inaonyesha wazi dalili za world class player mwenye uwezekano wa kutwaa  Ballon d’Or hivi karibuni.
  1. Uwezo Binafsi
150606223921-neymar-champions-league-final-super-169Yes, ni kweli hivi sasa Neymar amekuwa mchezaji anayecheza kitimu zaidi kuliko ilivyokuwa zamani. Hata kuna wakati timu ikiwa inacheza vibaya, Neymar amekuwa akijitokeza na kuchukua majukumu ya timu kutumia uwezo binafsi kuiletea timu matokeo chanya. Anaweza kuchukua ‘vijiji’  kiurahisi na kuiletea madhara makubwa ngome ya timu pinzani, si rahisi kutabiri nini atafanya wakati mwingine. Ni mchezaji ambaye ni vigumu kumkaba na mbinu zake kali alizonazo miguuni na kadri anavyoendelea kucheza na kupata uzoefu, Neymar yupo njiani kuwa mwanasoka bora zaidi duniani.
3. Uwezo wa Kuwachezesha Wenzie
neymarhighs_sf6ly9x16vcg10w421p262n2m-1425743415Baadhi ya wachezaji  bora duniani wamekuwa bora kutokana na ukweli kwamba wana uwezo wa kuwachezsha wachezaji wenzao. Mchezo wa Neymar huko nyuma ulikuwa umeegemea katika uwezo wake binafsi zaidi na kuna muda alifanya iwe rahisi kwa wapinzani kuzuia dhidi ya timu yao. Lakini kadri siku zinavyozidi kwenda amekuwa sehemu muhimu ya timu, Neymar ameuelewa zaidi mfumo na sasa anawachezsha mpaka wachezaji wenzie. Takwimu zinaonyesha hivi sasa anapiga sana pasi kuliko ilivyokuwa zamani, hili la kupiga pasi limeongeza kutokutabirika kwa mchezo wake na kuzidi kuwapa wakati mgumu wanaomzuia kumkaba. Hili limeleta mabadiliko makubwa katika staili ya uchezaji wa Neymar – pia limemletea mafanikio kuliko mwanzoni.
  1. Influence in the International side :
Neymar of Brazil celebrates his second goal against Turkey during their international friendly soccer match at Sukru Saracoglu stadium in Istanbul November 12, 2014. REUTERS/Murad Sezer (TURKEY  - Tags: SOCCER SPORT)Wanaompinga Neymar wana utetezi wao kwamba mchezaji huyo anafanya vizuri Barcelona kutokana na sapoti ya Messi na Suarez lakini kiwango cha Neymar kinapoangaliwa kwenye level ya timu ya taifa – ushahidi unaonyesha Neymar ndio msingi mkuu wa mashambulizi ya timu ya Selecao. Nahodha huyo wa Brazil ameitawala safu ya ushambuliaji ya timu hiyo na ameiongoza kimafanikio mpaka sasa akiwa na miaka 23 tu. Bado ana safari ndefu kuendelea kuwa na kiwango kikubwa alichonacho. Ameyabeba majukumu ya unahodha vizuri sana na anaamini hivi karibuni ataipa mafanikio Brazil.
5. Kawaacha Mbali Waliokuwa Wanashindanishwa Nae

5Mbrazil huyu amekuwa kiwango cha juu sana msimu uliopita na zaidi msimu huu. Unapojaribu kumlinganisha na wachezaji wa kizazi chake kama Eden Hazard, Antoine Griezmann, Gareth Bale utofauti wa uelewa wa mchezo na kukua kwa Neymar. Anausoma mchezo vyema zaidi kuliko alivyokuwa Santos, anajua wapi anatakiwa kukimbia na mpira na wapi kwa kupasia na hazidishi manjonjo kama ilivyokuwa mwanzoni. Uhamisho wake kwenda Barcelona umemsaidia katika kukua kiuchezaji na kuboreka zaidi katika mchezaji hatari zaidi, hizi ni ishara halisi za mchezaji mwenye ubora wa kuwa bora duniani.

MAJWEGA, KIONGERA, NJE SIMBA VS AZAM LEO

Kiungo wa Simba aliyesajiliwa kutoka Azam FC Brian Majwega
Wakati klabu ya Simba ikiwa imefanya usajili katika kipindi cha dirisha dogo kuhakikisha inakiongezea nguvu kikosi chake, taarifa zinadai kwamba, wachezaji hao waliosajiliwa katika kipindi cha dirisha dogo hawataruhusiwa kucheza kwenye mchezo dhidi ya Azam FC unaosukumwa jioni ya leo kwenye uwanja wa taifa .
Wachezaji hao hawatacheza kwasababu bado hawajathibitishwa na kamati ya sheria na hadhi za wachezaji ya TFF ili waanze kuitumikia klabu hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa inamatarajio ya kuwatumia wakali hao kutaka kuangamiza Azam.Mshambuliaji wa Simba Paul Kiongera
Mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Boniface Wambura amesema kamati ya sheria na hadhi za wachezaji hukutana mara baada ya dirisha la usajili kufungwa kwa ajili ya kuidhinisha usajili wa wachezaji wa vilabu ikiwa ni pamoja na kupitia pingamizi zilizowekwa kwa wachezaji mbalimbali.
“Kanuni za usajili au kanuni za ligi zinasema klabu au timu inamuombea usajili mchezaji kwa TFF kwahiyo TFF ndiyo inaidhinisha usajili kwahiyo baada ya TFF kuidhinisha ndipo mchezaji anapata license au mchezaji anaweza akawa ameidhinishwa lakini hata hati ya uhamisho wa kimataifa lakini itakapofika tu acheze”, amesema Wambura.
“Lakini mpaka sasahivi kamati ya sheria na hadhi za wachezaji ambayo ndiyo inathibitisha usajili haijakutana kwahiyo ikikutana watu wakapata license wanaweza wakacheza lakini kama hawajapata license ni wazi hawawezi kucheza mpaka kamati itakapokuwa imekaa”.
Lakini kamati mpaka sasa bado haijakutana kwahiyo wachezaji wote wa vilabu vyote (vinavyoshiriki ligi kuu pamoja na ligi daraja la kwanza) waliosajiliwa katika dirisha dogo hawatakuwa na uhalali wa kucheza katika michezo ya ligi kuu Tanzania bara itakayopigwa leo na kesho.
Kwahiyo wachezaji kama Brian Majwega, Paul Kiongera na Dany Lyanga hawata nafasi ya kucheza kwani hadi sasa kamati ya sheria na hadhi za wachezaji bado haijakutana kuidhinisha uhalali wa wachezaji wote waliosajiliwa kwenye dirisha dogo na mara nyingi kamati hukuta mara baada ya dirisha la usajili kufungwa.

VAN PLUIJM AWATOA HOFU YANGA

Hans van der Pluijm, kocha mkuu wa club ya Yanga SC
Kocha mkuu wa mabingwa wa kikosi cha Yanga mholanzi Hans van Pluijm amewatoa hofu mashabiki na wachama wa Yanga juu ya wachezaji ambao ni majeruhi na kuwaahidi ushindi kutoka kwa kikosi ambacho kitacheza mchezo dhidi ya Mgambo JKT  kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo jioni.
Yanga itawakosa wachezaji wake muhimu kama nahodha wake Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Salum Telela na mshambuliaji Donald Ngoma ambao wote ni majeruhi huku Haruna Niyonzima akiwa bado hajajiunga na kikosi hicho tangu aende kwao kukitumia kikosi cha timu ya taifa ya Rwanda kwenye michuano ya CECAFA Challenge Cup.
“Kila kocha kocha ukimuuliza kuhusu mchezo ulioko mbele yake atakwambia anahitaji pointi tatu, tutafanya kila tunachoweza ili kuzipata pointi hizo, kwa bahati mbaya kikosi chetu kina majeruhi lakini tunakikosi cha wachezaji 24 kwahiyo wapo wengine wataochukua nafasi za hao ambao ni majeruhi”, hayo ni maneno ya kocha wa Yanga ‘kibabu’ Hans van Pluijm.
Nimeshawahi kuwanona wapinzani wetu Mgambo wakicheza mara kadhaa na ninafahamu jinsi wanavyocheza, wanacheza kwa kutumia sana nguvu lakini sisi pia tuna aina yetu ya uchezaji na tuko tayari kuwakabili.
Mgambo JKT wanatambulika kuwa ni wagumu hasa wanapocheza kwenye uwanja wao wa nyumbani na wamekuwa wakifanya mazoezi magumu kwa takribani mwezi mzima chini ya kocha wao ‘Mchawi Mweusi’ Bakari Shime wataingia uwanjali wakiwa full hawana mchezaji majeruhi hata mmoja huku kiungo wao Ali Nassoro Fudu akirejea uwanjani baada ya kuwa nje kwa majeruri ya muda mrefu.

Polisi Tanzania wasaka mshukiwa wa sakata bandarini

Kontena
Polisi nchini Tanzania wameahidi zawadi kwa atakayesaidia kukamatwa kwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni moja anayetuhumiwa kuhusika katika kupitisha makontena bandarini bila kulipiwa kodi.
Kamanda kamishna wa polisi Suleiman Kova amesema wanamtafuta Abdulkadir Kassim Abdi, 38, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Regional Cargo Services LTD.
Anashukiwa kuhusika katika kutoa makontena 329 kwenye bandari kavu ya Azam (Azam ICD) bila kulipia kodi.
Abdulkadir ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni zilitumiwa kutoa makontena hayo bandarini, kwa mujibu wa serikali.
Polisi imetangaza zawadi nono ya takribani dola elfu 10 kwa atakayesaidia kupatikana kwa mtuhumiwa.
Makontena hayo 329 yaligundulika kukosekana kwenye ICD ya Azam kuanzia mwezi Julai hadi Novemba 2015.
Uchunguzi wa awali ulikuwa umeonyesha makontena 2489 yalitolewa Bandari ya Dar es Salaam kati ya Machi na Septemba 2014 kinyume cha taratibu kwa lengo la kukwepa kodi na ushuru.

Marekani yazitaka pande husika kuinusuru Burundi

Burundi
Mjumbe maalum wa Marekani katika eneo la maziwa makuu amezitaka pande husika nchini Burundi kuafikiana ili kulinusuru taifa hilo ambalo linaelekea kuangamia na vita.
Thomas Perrielo alikuwa akizungumza na BBC baada ya wapiganaji kuvamia kambi moja ya kijeshi katika mji mkuu wa Bujumbura.
Amesema kuwa Burundi inaelekea kuwa taifa lililofeli .Amesema kuwa Marekani inaunga mkono vikosi vya kuleta amani kutoka mataifa jirani badala ya wanajeshi wa Umoja wa Mataifa.
Serikali imesema kuwa jeshi limewauwa wapiganaji 12 ambao walivamia kambi hiyo.Milio ya risasi pamoja na milipuko imekuwa ikisikika katika mji huo kwa saa kadhaa.
Wakati huohuo mashirika ya ndege ya Kenya Airways na RwandAir yamesitisha safari zake za kuelekea mji mkuu wa Burundi, Bujumbura, kufuatia makabiliano ya risasi mjini humo.
Kwa mujibu wa afisa mkuu wa mawasiliano wa shirika la ndege la Kenya, KQ, Wanjiku Mugo, safari hizo zimesitishwa kutokana na ukosefu wa wafanyakazi katika uwanja wa ndege wa Bujumbura.
Serikali ya Burundi imesema uwanja huo haujafungwa ila tu shughuli zimetatizika kwa sababu wafanyakazi hawakuweza kufika katika uwanja huo, kutokana na makabiliano makali ya risasi kati ya wapinzani wa serikali walioakuwa wamejaribu kuvamia kambi kadhaa za kijeshi mjini humo.
Shirika la kimataifa ya Msalaba mwekundu ICRC nalo kwenye Twitter limesema kuwa halikufanikiwa kuingia katikati mwa mji mkuu Bujumbura kutokana na vizuizi vilivyowekwa na maafisa wa jeshi ambao wanaendelea na msako dhidi ya watu wanaomiliki silaha.
Ripoti zinasema kuwa watu wanane wameuawa kwenye makabiliano hayo huku wengine wengi nao wakiwa wamejeruhiwa.
Mitaa ya Mutakula na Musaga ndiyo iliyoathirika zaidi huku wakaazi wa mitaa hiyo wakirpoti milio ya risasi kuanzia saa kumi alfajiri.
Huku hayo yakijiri Rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza ameongoza mkutano wa baraza lake la mawaziriMsemaji wa rais Willy Nyamitwe amesema lengo la mkutano huo limekuwa kujadili bajeti ya serikali ya mwaka ujao.
Kuhusu makabiliano ya asubuhi, Bw Nyamitwe amesema kuwa watu wenye silaha walijaribu kuvamia kambi kadhaa za kijeshi, katika kile alichokitaja kama jaribio la kutaka kuwaachilia huru wafungwa.
Nyamitwe amesema kuwa juhudi hizo zimezimwa na Jeshi na kuwa hali ya utulivu imeanza kurejea.
Machafuko yalianza nchini Burundi Aprili mwaka huu, wakati rais Nkurunziza alipotangaza kuwa atawania muhula wa tatu kinyume na mkataba wa Arusha uliosainiwa zaidi ya muongo mmoja uliopita.
Umoja wa Mataifa umesema kuwa zaidi ya watu 200 wameuawa tangu machafuko hayo kuanza huku maelfu ya wengine nao wakikimbia nchi jirani.

Victoria: Sina mpango na wanaume wa Kenya

post-feature-imageMSANII wa muziki nchini Kenya, Victoria Kimani, amesema hana mpango wa kuolewa na wanaume wa nchini Kenya kwa kuwa hawajui kukaa na wapenzi wao.

Mrembo huyo amesema wanaume wengi wa nchini humo wamekuwa tofauti na wale wa nchini Nigeria, hivyo ni bora aelekee huko kwa ajili ya kupata mwanaume bora ambaye atadumu naye.

Msanii huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri katika muziki mara baada ya kusaini mkataba mpya katika kampuni ya kusimamia kazi zake ijulikanayo kwa jina la Chocolate City Music Label, amesisitiza kwamba lengo lake kubwa ni kuolewa na mtu kutoka Nigeria.

“Wanaume wa Nigeria wanajua jinsi ya kuishi na mwanamke, wanaonyesha heshima ya hali ya juu na hivyo ndivyo ninavyotaka katika maisha yangu,” alisema Victoria.

Tanzania yapata maabara ya kipekee ya aina hiyo kwa Afrika kusini mwa jangwa la Sahara

post-feature-imageTanzania ni moja kati ya nchi zilizofanikiwa duniani kuratibu maabara inayohamishika kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ebola na magonjwa mengineyo ya mlipuko.

Maabara hii inaweza kusafirishwa mpaka kwenye maeneo yaliyoathirika, ikiwa ndani ya masanduku yaliyofungwa vyema badala ya kusafirisha sampuli kwa ajili ya vipimo kutoka eneo moja kwenda jingine na kuwa katika hatari ya kuathiriwa na vijidudu vingine.

Tanzania na Nigeria ndizo nchi pekee kusini mwa Jangwa la Sahara zenye maabara ya aina hii ambayo itakuwa msaada mkubwa pia kwa nchi za jirani za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya taifa ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, NIMR Dokta Mwele Malecela, amesema maabara hii ina umuhimu kwa kuwa itawezesha kufanyika kwa uchunguzi kwa urahisi na haraka zaidi, hata katika maeneo yaliyo na ugumu kufikiwa.

Changamoto ambayo ilionekana wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa Ebola Afrika Magharibi ni wahudumu kutofika kwa urahisi kwenye maabara kwa ajili ya uchunguzi wa haraka kutokana na umbali na miundo mbinu mibovu.

Adele ametawala tuzo za pili za BBC baada ya kushinda tuzo ya msanii bora Uingereza

post-feature-imageNyota wa muziki wa Pop Adele ametawala tuzo za pili za BBC baada ya kushinda tuzo ya msanii bora Uingereza na maonyesho bora ya moja kwa moja. Mwanamuziki huyo hakuweza kuhudhuria sherehe hiyo,lakini alituma ujumbe unaosema nimefurahi sana, nilitoa muziki wangu mpya hivi karibuni.

Mwanamuziki wa Ireland Hozier alishinda tuzo ya wimbo bora wa mwaka 'Take me to Church'.
Taylor Swift pia alishinda tuzo ya msanii bora wa kimataifa huku akikubali tuzo hiyo kupitia video akiwa nchini Australia. ''Mungu wangu tuzo hii ni nzito sana.nafurahi sana kwa kunitumia kwa sababu lazima imewagharimu''.

Vijembe kati ya 50 CENT na Rick Ross vyazidi kuchkua sura mpya

091113-music-career-defining
Rapa 50 Centhajakubali kuizika beef yake na Rick Ross na sasa ameanza kumtania kuhusu mauzo mabaya ya album mpya ya Ric Ross ‘Black Market’ .
50 Cent ambaye hivi karibuni ametoa mixtape ya The Kanan Tape amemtania Rozay kwa kusema album yake yake ya Black Market imeuza kopi 34,388 tu na kwama 15000 zimenunuliwa na Rick Ross mwenyewe.

jarida la Fader lasema Ojuelegba ni wimbo No12 bora zaidi duniani 2015,haikuhitaji sauti ya Drake

IMG_5365
Wimbo wa WizKid ‘Ojuelegba Remix’ watajwa kuwa No 12 kwneye nyimbo bora za 2015 na jarida la Fader kwenye orodha ya nyimbo 107 bora za mwaka 2015.
Wimbo huu wa ‘Ojuelegba Remix’ unasauti ya rapa Drake kutoka Marekani na  Skepta kutoka Uingereza.
Jarida la Fader limeandika haya kuhusu wimbo huu.
“Drake ameingia kwenye wimbo wa huyu msanii kutoka Nigeria na kuupa umaarufu zaidi Marekani, vesi ya Drake na Skepta zimeipendezesha zaidi “Ojuelegba” lakini ukweli ni kuwa wimbo huu tayari ulikuwa mkubwa sana Marekani na nchi zingine, wimbo unaujumbe mzuri wa shukurani na matumaini kuhusu nyumbani kwao”.

11 December, 2015

eyooo VIDEO MPYA YA DIAMOND "Utanipenda"

Mkali wa Bongo fleva ambaye amezoeleka kuchukua headlines na video zake kali kila siku Diamond Platnumz, jioni ya December 11 aliachia video yake mpya inakwenda kwa jina la Utanipenda?

Itazame hapaaa

Mbwa wa Benjamin Netanyahu huuma wageni

Kerry
Mbwa ambaye anayefugwa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliwauma wageni wawili, akiwemo mbunge, katika hafla ya kidini.
Kisa hicho kilitokea katika hafla ya kuwasha michumaa kuadhimisha sikukuu ya Kiyahudi ya Hannukah nyumbani kwa Bw Netanyahu.
Mbunge huyo Sharren Haskel na mume wa Tzipi Hotovely, naibu waziri wa mashauri ya kigeni, hawakuumia sana.
Bw Netanyahu alimchukua mbwa huyo kwa jina Kaiya kutoka kwa kituo cha kuwaokoa wanyama waliotelekezwa mapema mwaka huu.
Waziri mkuu huyo alipakia kwenye Twitter picha yake akiwa na mbwa huyo wa umri wa miaka 10 mwezi Agosti.
"Ukitaka mbwa, tafuta mbwa aliyekomaa kutoka kituo cha kuwaokoa wanyama. Hutajuta,” aliandika.
Kaiya amekutana na wageni mashuhuri akiwemo Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani John Kerry.

Trump aahirisha ziara yake ya Israel

Trump
Mgombea urais wa chama cha Republican Donald Trump amesema ameahirisha ziara yake aliyopangiwa kuifanya nchini Israel.
Mfanyabiashara huyo tajiri ameandika kwenye Twitter kwamba atafanya ziara hiyo “baadaye baada yangu kuwa Rais wa Marekani”.
Mapema wiki hii, Bw Trump alipendekeza Waislamu wazuiwe kwa muda kuingia Marekani.
Tamko lake lilishutumiwa vikali na viongozi duniani, akiwemo Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.
Matamshi hayo ya Trump lingetia utata kwenye ziara hiyo upande wa kiongozi huyo wa Israel, ambaye hangetaka kuwaudhi Waislamu.
“[Bw Netanyahu] alisema tutakuwa na mkutano na anasubiri kwa hamu mkutano huo na mengine mengi. Lakini sikutana kumuwekea shinikizo,” Bw Trump aliambia Fox News mnamo Alhamisi.
Pendekezo lake alilitoa baada ya shambulio lililoua watu 14 mji wa San Bernardino, jimbo la California, ambalo lilitekelezwa na wanandoa Waislamu waliokuwa na itikadi kali.

Label ya Cash Money Records ndio sababu ya kwanini ‘Hotline bling’ ya Drake haijaingia kwenye Tuzo za Grammy 2016

Wimbo wa Drake ‘Hotline bling’ mbali ya kuwa moja ya nyimbo zilizohit zaidi lakini haujawanominated kwenye tuzo za Grammy 2016.
Mtandao wa  Hits Daily Double umedai sababu kubwa ya wimbo huo kutoingia kwenye Tuzo hizo ni kwasababu label inayosimamia kazi za Drake, Cash Money Records ilichelewa kutuma wimbo huo kwa ajili ya mchakato wa nomination.
Hata hivyo Drake ameingia kwenye vipengele  5

10 December, 2015

video mpya ya Jux ‘One More Night’ itazame hapa.

juxvideo mpya ya Rnb super staa Jux inaitwa ‘One More Night’. Audio imetayarishwa na Nahreel

HOFU YATANDA WACHEZAJI MAN UTD, NI KUHUSU ‘NOTE BOOK’ YA VAN GAAL

Van Gaal 3
Gazeti la daily mail la nchini England limeripoti kuwa wachezaji wa klabu ya Manchester United hata kabla ya mchezo wa juzi wa klabu bingwa Ulaya wamekua wakikabiriwa na hofu kubwa kuhofia kuingia katika kitabu cha kocha wao Louis Van Gaal.
Habari zinasema kuwa kocha Louis Van Gaal huandika kola kosa linalofanywa na wachezaji wake wakati wa mechi na mazoezi ya timu hiyo, jambo ambalo linawafanya wachezaji wasijiamini kuhofia kuandikwa katika kitabu hicho ambacho kimejaa makosa ya wachezaji hao.
Man U
Mapema mwezi September mwaka huu, nahodha Wayne Rooney na Michael Carrick walifika ofisini kwa kocha wao na kumuonya kuhusu utaratibu wake wa udhibiti wa wachezaji kwamba sio wa afya kutokana na ukweli kwamba kocha huyo huwabana wachezaji kila sekunde, vikao mara kwa mara, ratiba za chakula na video za makosa ya wachezaji.
Inaelezwa kuwa utaratibu huo huwakera na kuwachosha wachezaji ambao hukosa kujiamini. Angel Di maria anatajwa kuwa miongoni mwa sababu zilizomuondoa klabuni hapo ni udikteta wa kocha Louis Van Gaal, huku Memphis Depay nae akionywa.
Matatizo haya ya kocha Louis Van Gaal yameigharimu klabu hiyo na sasa wametolewa nje ya michuano ya klabu bingwa Ulaya katika hatua ya makundi huku wakiwa hali ya kuchechemea katika ligi kuu soka nchini England.

TIMU YAKABIDHI WACHEZAJI WAKE BODABODA

URA
Taasisi ya mapato nchini Uganda (URA) kupitia timu yake ya URA FC imewapa wachezaji wake zawadi ya pikipiki maarufu kama ‘bodaboda’ kwa ajili ya kuongeza vipato vyao mbali na mshara wanaoupata kila mwezi kutoka kwenye klabu yao.
URA imewasaidi wachezaji wake kwa kuwapa pikipiki hizo za biashara ‘bodaboda’ ambazo zimesambaa nchini Uganda na Afrika Mashariki kwa ujumla kwa ajili ya kusafirisha abiria pamoja na mizigo.
Kutokana na hali ya maisha kupanda kwenye mji kuu wa Uganda Kampala, mwenyekiti wa klabu hiyo Ali Ssekatawa amesema kwamba, hawataki wachezaji wao wategemee mishahara pekee hivyo wakaona ni vyema kuwatafutia vyanzo vingine vya kupata pesa vitakavyowasaidia kujipatia kipato mbali na kazi yao ya kucheza mpira.
“Tunaangalia mfumo wa kuwafanya waweze kujitegemea wenyewe na tukifanikiwa katika hilo basi wachezaji wetu watacheza vizuri”, amesema Ssekatawa.
URA ni moja kati ya vilabu maarufu kwenye ligi ya Uganda (Uganda Premier League) na wamekuwa wakiwakilisha ukanda wa Afrika Mashariki kwenye michuano ya CAF Champions League pamoja na ile ya Confederation Cup ambayo kwa pamoja ni michuano mikuwa barani Afrika kwa ngazi ya vilabu.
Mapema mwaka huu commissioner wa URA FC Doris Akol aliahidi watawasaidia wachezaji kujipatia kipato cha ziada na mwenyekiti wa klabu Ssekatawa amekabidhi bodaboda 17 kwa wachezaji kwenye uwanja wa mazoezi.
Mchezaji liyedumu kwenye kikosi hicho kwa muda mrefu na kuwahi kuitumikia timu ya taifa ya Uganda Simeon Masaba amesema amefurahishwa na hatua hiyo na itawasaidia wachezaji kupata kipato cha ziada kwa ajili ya familia zao.
Beki huyo aliongeza kuwa, japo biashara ya bodaboda ni hatari pamoja na wezi pia kuwaandama waendesha bodaboda, anaamini kama zitatunzwa na kutumiwa vizuri zitawasaidia wachezaji wa URA kama sehemu ndogo ya bishara yao.
Kocha wa timu hiyo Kefa Kisaala pia amepokea moja ya bodaboda hizo na kusema amefurahishwa na zoezi hilo.
Kwa upande wake kiungo wa timu hiyo Saidi Kyeyune yeye amesema, hakubaliani na mpango huo kwasababu anafikiri itakuwa ni vigumu ku-manage.

MSIKIE JULIO ANAVYOSEMA KUHUSU SHINYANGA DERBY

IMG-20150825-WA0015
Wakati macho na masikio ya wengi yakiwa yameelekezwa kwenye mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Simba SC utakaochezwa December 12 kwenye uwanja wa taifa, kule mkoani Shinyanga kutakuwa na bonge la derby kati ya Stand Unted ‘chama la wana’ dhidi ya Mwadui FC chini ya Super Coach Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ katika mwendelezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.
Kocha wa Mwadui FC Jamhuri Kihwelo amesema timu yake ipo katika maandalizi mazuri kuelekea mchezo huo huku akikiri kuwa mchezo huo utakuwa mgumu na lolote linaweza kutokea japo ametamba kikosi chake kimejipanga kwa ajili ya kuibuka na ushindi kwenye mchezo huo.
“Sisi tutacheza mchezo wa Shinyanga derby dhidi ya Stand United timu ambayo ilianza kupanda daraja kabla yetu sisi na mwaka unaofuatia sisi tukapanda. Ni watu wa mkoa mmoja lakini watu wenye upinzni na ushindani wa kimchezo kiasi ambacho naweza kusema mechi itakuwa ngumu na lolote linaweza kuokea lakini timu yangu ipo katika maandalizi mazuri, tumejipanga vizuri kwa ajili ya ushindi wa mechi hiyo”, amesema Julio.
“Nimemsajili Gabriel Emanuel kutoka timu ya JKT Oljoro na mwingine ni Ismail Gabo mchezaji ambaye tumempata kwa mkopo kutoka Azam FC kwahiyo nafikiri kutokana na wachezaji nilionao nikiongeza na hawa wawili nitakuwa na idadi kamili ya wachezaji watakaomalizia msimu huu wa ligi ya Vodacom”.
Mchezo huo unazikutanisha timu hizo huku Stand United ikiwa nafasi ya tano kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 19 wakati Mwadui FC yenyewe ipo nafasi ya saba kwa pointi zake 15.

Kanye West asema majivuno na kujiskia kunamfanya awe na collabo chache.

kanye-west-22Rapa Kanye West ametoa sababu za kwanini anafanya collabo chache na kusema ni kutokana na majivuno na kujiskia kwake.
Kanye West anasema ” mimi najiskia sana, hilo ndio tatizo, nikiweza na kuacha kujiskia nadhani watu watapata nafasi ya kufanya kazi na mimi “.
Kanye West pia anasema mafanikio ya Drake yamefanya abadilishe mfumo wake wa kufikiria na kufanya vitu.
Kanye anasema ” kuona mafanikio na mabadiliko ya kazi za Drake kumenifanya nibadilisha ufanisi wangu wa kazi na ninavyo fikiria mambo, Drake ameweza kubadilika na kuwa tofauti na kila mtu kwa muda mfupi, amenishawishi sana “.

From the Runway to the Beach- Jokate kills it!

 


Wearing a Lavo Delamo design by an upcoming designer,Upendo,who actually won Upcomin Designer of the Year 2015 through Swahili Fashion Week,Jokate shows how to rock a day at the beach in this hot Dar es Salaam

 My ooh my! Isn't that one sexy and stylish lady! No wonder Jokate won the most Stylish Personality at the Swahili Fashion Week 2015
Photos by Albert Manifester...

Madaktari kupandikiza uume Marekani ili kumuwezesha mgonjwa kufanya tendo la ngono

post-feature-imageUpasuaji umepangwa kufanyika kwa mara ya kwanza kupandikiza uume nchini Marekani, kwa lengo la kuwasaidia mpiganaji wa zamani. Upasuaji huo wa saa 12- utahusisha ushonaji wa neva muhimu na mishipa ya damu kwa ajili ya kutunza mkojo na kumuwezesha mgonjwa kufanya tendo la ngono.

Upasuaji huu unafuatia mafanikio ya kwanza kabisa ya upandikizaji wa uume nchini Afrika kusini mwaka jana. Jopo la madaktari kutoka Hospitali ya chuo kikuu cha Hopkins (JHU) wanapanga kumfanyia upasuaji huyo mwanajeshi wa zamani mwenye umri wa miaka 60kama sehemu ya majaribio.

Hatua ya kwanza ya upasuaji huo itaanza kwa kuondoa uume kutoka kwa kijana aliefariki ambaye alijitolea kutoa uume wake kwa ruhusa ya familia yake. Kwa mujibu wa jopo la madakatari katika JHU matumaini ya mwanajeshi huyo wa zamani ni kwamba hisia za uume wake zitarejea katika muda wa miezi 12.

Uwezekano wa mgonjwa kupata watoto, utategemea kiwango cha jeraha na mafanikio ya upasuaji huo. Lakini Wanasayansi wanasema kutokana na kwamba ni upasuaji mmoja wa kupandikiza uume uliofanyika, madaktari watakua makini kuhakikisha kuna matumaini ya kweli.

Rais wa Argentina awaaga raia wake


Rais wa Argentina aliyemaliza muda wake , Cristina Fernandez de Kirchner, amewaaga maelfu ya wafuasi wake ambao walikusanyika katikati mwa mji wa Buenos Aires.
Katika hotuba yake ambayo ilijaa hisia nje ya ikulu, Fernandez alivishutumu vyombo vya habari vya nchi hiyo kwa kuipiga vita serikali yake ya mrengo wa kushoto.
Fernandez na mume wake ambae tayari ameaga dunia, Nestor Kirchner, wamekuwa madarakani kwa muda wa miaka kumi na mbili.
Ametetea hali ya uchumi, na kusema hakuna katika utawala uliopita ambao uliiacha Argentina bila madeni.
Na kuwataka raia wa Argentia kutetea haki zao na maslahi yao ambayo wameyapata.
Makundi yaliyokusanyika katika eneo hilo yalikuwa yakiimba wakati Fernandezi akipanda katika jukwaa.

Nyota wa Hollywood ‘kuhamia Afrika’ Trump akishinda

Jackson
Nyota wa Hollywood Samuel L Jackson atahamia Afrika Kusini iwapo Donald Trump atashinda uchaguzi wa urais Marekani, tovuti ya News 24 imeripoti.
Trump, mmoja wa wanaowania tiketi ya kugombea urais Marekani kupitia chama cha Republican, ameshutumiwa vikali baada ya kupendekeza Waislamu wazuiwe kuingia Marekani.
Haijabainika iwapo matamshi ya mwigizaji huyo, yaliyopeperushwa kwenye sehemu ya kipindi cha Jimmy Kimmel Live iliyorekodiwa awali Jumatatu, yalitolewa kabla au baada ya matamshi hayo ya majuzi zaidi kutoka kwa Trump.
Bw Trump, wakati mmoja amewahi kunukuliwa akikosoa kundi linalotetea haki za watu weusi Marekani la Black Lives Matter.

Rais Magufuli kaandikwa tena na tovuti ya gazeti la Uingereza, ni kuhusu Dec 9.


Sasa hivi sio habari mpya tena kuona gazeti au mtandao wa nchi flani maarufu duniani limemuandika Rais Magufuli wa Tanzania, tayari mpaka sasa tumeshaona Magazeti ya Australia, South Africa, Zimbabwe, Kenya, China, Uganda na Uingereza yamemuandika Dr. Magufuli.
December 9 2015 baada ya Rais Magufuli kuchukua headlines za yeye kufanya usafi, The Telegraph (telegraph.co.uk) wameandika mistari ambayo inaonyesha kabisa kitendo cha Dr. Magufuli kuingia mtaani kufanya usafi kimewagusa na ni tofauti na Waziri mkuu wa Uingereza ambaye sio rahisi kumuona au kufanya alichofanya Dr. Magufuli.
Kwenye sehemu ya stori yenyewe wamenukuu mistari ya Rais Magufuli kusema ni aibu kusherehekea siku ya uhuru Tanzania wakati nchi ina Wagonjwa wa kipindupindu ambapo kwenye taarifa hiyo ziliambatanishwa picha zikimuonyesha Rais JPM akifanya usafi.
magu 3
magu 2
Magu 1

09 December, 2015

FASHION TANZANIA:::WHEN DID DIAMOND PLUTNUMz WORE HIS PRINTED SHIRT BETTER?????


Diamond Plutnumz must be loving this printed tee of his.Jana alipost a pic of this t shirt which he wore with a ripped jeans shorts ,aka accessorize na sneakers nyeusi alizotinga na socks za weed na kuu akatilia silver chains na Black shades kama kawaida
dai
First time alikuwa spotted huko kwa SA kwenye Green carpet ya BET Experience and he wore the t shirt with a  black skinny jeans,same sneakers na chains zake ,this time hakuvaa miwani only his cape.
12301201_834820473282778_1164849566_n
Which look do you prefer the one with jeans shorts au hii alovaa na black jeans.

Mambo 5 ambayo unatakiwa kuyajua kuhusu Raheem Sterling baada ya kufikisha miaka 21

dfs
Jana December 8 ni siku ya kuzaliwa ya Raheem Sterling ambapo amefikisha miaka 21 na kutupia goli mbili kwenye mechi ya UEFA.
Hivi hapa ni vitu vitano ambavyo ambavyo ni vizuri ukavijua kuhusu Raheem Sterling.
1)Mwaka 2015 kwenye utafiti wa kitaalamu kwenye Soccerex ulimthaminisha Raheem Sterling kuwa ni mchezaji mwenye umri mdogo na thamani kubwa kuliko wachezaji wote Ulaya. Thamani yake ilikua ni €49 million
2)Alizaliwa kwenye jiji la Kingstone Jamaica baadae alihamia na mama yake kwenye jiji la London akiwa na miaka 7 ambapo ndio maisha yake na soka yalianza kuelekea kwenye mafanikio.
3)Baba yake aliuliwa na watu wasiojulikana huko Kingstone Jamaica akiwa wakati Raheem akiwa na miaka 9.
4)12 July 2o15 alikamilisha makubaliano na Manchester City na kwa gharama ya £44 million akitokea Liverpool na kumfanya kuwa mchezaji namba 7 kwa kuhama kwa gharama kubwa.
5)8 August 2013 Raheem aliwai kukamatwa na polisi baada girlfriend wake wa zamani kutoa mashtaka ya kudhalilishwa lakini kesi hiyo ilipotezewa baada ya kutokua na ushahidi wa kutosha
Happy Belated Birthday kwa Raheem Sterling

Mawaziri waidhinisha kura ya muda wa rais Rwanda

Kagame
Baraza la mawaziri Rwanda limeidhinisha kufanyika kwa kura ya mamuzi kuhusu marekebisho ya katiba yatakayomruhusu Rais Paul Kagame kuendelea kukaa madarakani.
Kikao cha baraza la mawaziri kimetangaza kuwa kura ya maamuzi kuhusu katiba hiyo mpya itafanyika tarehe 18 Desemba, ambayo ni Ijumaa wiki ijayo, kwa wananchi wa Rwanda na tarehe 17 kwa raia wa Rwanda wanaoishi ng’ambo.
Tangazo hilo la baraza la mawaziri limethibitisha pendekezo lililotolewa na wa mkutano mkuu wa chama tawala RFP mwishoni mwa wiki iliyopita wa kufanyika kwa kura hiyo haraka iwezekanavyo.
Marekebisho ya katiba tayari yamekwisha idhinishwa na bunge la Rwanda.
Kulingana na katiba mpya, Rais Paul Kagame baada ya kumaliza muhula wake mwaka 2017, atakuwa huru kugombea muhula wa tatu ambao utakuwa wa miaka 7 na baadaye kuruhusiwa tena kugombea mihula mingine miwili, kila mmoja ukiwa wa miaka 5.
Katiba iliyokuwepo ilikuwa inaweka ukomo wa mihula miwili pekee madarakanRFPMarekebisho ya katiba nchini Rwanda yamekwisha pingwa na baadhi ya nchi wafadhili wa taifa hilo kama vile Marekani, Uingereza na umoja wa nchi za ulaya kwa madai kuwa marekebisho hayo yanakandamiza demokrasia.
Hata hivyo, akijibu shutuma hizo, Rais Paul Kagame alisema kuwa kilichotokea nchini humo ni matakwa ya wananchi ambao bila shaka watapewa haki ya kudhihirisha hivyo kupitia kura ya maamuzi.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...