22 August, 2015

MAKALA: WAKO WAPI MAN DOJO NA DOMOKAYA?

Awali ya yote nipende Kutoa Shukrani zangu za kipekee kwa mwenyezi Mungu kwa kunilinda wiki nzima hata nmepata nafaSi yakuwepo tena leo hii hapa mtoka mbali. Pia nichukue nafaSi hii kuku Shukuru we kamanda kwa kutembelea makala zetu na kuziSoma pia.
   
     Katika makala yetu leo tuna angaza jicho kwa wakali hawa wa bongo fleva ambao miaka ya nyuma waliweza kuzikonga nyoyo za maShapiki  wao vilivyo, na hawa si wengine ni MAN DOJO NA DOMO KAYA. Naweza sema kwamba vijana hawa sii wageni kuwaskia maskioni mwako kwani waliweza kuziteka media tofauti tofauti zenye ukubwa hapa Tanzania na hata nchi za njee kwa vibao vyao vilivyo kua vimejaa ujumbe tele kwa jamii mfano DINGI, BARUA, na NIKUPE NINI. Hivyo ni baadhi ya vibao walivyopata kutesa navyo kipindi cha miaka ya mwanzoni mwa 2000.
    Jambo lakujiuliza ni je wakali hawa wamepotelea wapi?
Ni wazi kwamba leo hii ukipata nafasi yaku onana nao, swali utakalo wauliza ni mbona siku hizi hatuwasikii? Hicho ndicho kilichomo katika fikra za mashabiki wa hawa wakali au ukipenda waite manguli wa bongo fleva. Yawezekana kabisa kwamba hawa jamaa wanatamani kurudi katika game ya muziki nakuwika tena kama ilivyokua mwanzini laki inakua ni vigumu kwani muziki wa bongo fleva unazidi kukua siku baada ya siku na kwa vile ukimya wao kwa muda mrefu bila kusikika, imefanya hata mashabiki wao kuwasahau kabisa. Lakini tukumbuke yakua wahenga walisema "hakuna marefu yasiyo na ncha" yawezekana katika game hii ya muziki wakizazi kipya imekua ngumu na wala sii rahisi kama ilivyokua kipindi cha nyuma ambapo muziki huu haukua na soko ki vile, na kwakusema hivyo ni dhahiri yakua wakali hawa wamepotea kabisa.
 Waliweza kutengeneza vibao vingi ambavyo nimeweza kuvitaja baadhi hapo juu na vingine ni kama vile HISTORIA, WANA KNOCK KNOCK, NIZIKWE HAI, na TASWIRA. Kama kweli wewe ni mpenzi wa muziki wa bongo ni wazi kua vibao hivi vilikukonga moyo ipasavyo na hadi leo unawakumbuka hawa jamaa vilivyo.
      Siwezi sema yakwamba hawa jamaa hawawezi kurudi katika umahiri wao kama mwamzo ila jitihada na juhudi zao ndizo zitawaleta tena kwatika game ya muziki na kuwika tena mbele ya wadogo zao katika muziki huu wa bongo fleva.
  Ni malizie kwa kusema, "Yatupasa kuwakumbuka vijana kama hawa ambao mchano wao katika jamii ni mkubwa mno, tuwape shime pale wanapo anguka ili waweze rudi katika hai zao za kawaida masha kusonga mbele"

 Nipende kukushukuru wewe ulichukua muda wako adhimu na wenye dhamani kwa kukaa kitako nakusoma makala zetu. Endelea kutembelea MTOKA MBALI ili uweze kupata kile unachokitaka.

MAKALA hii imeandikwa na Francis Mawere kwa hisani ya MAWERE MEDIA GROUP Ltd
TUTUMIE email yako kupitia mtokambali2015@gmail.com au piga simu namba 0767322193

21 August, 2015

Kikwete azijibu hoja za Ukawa

Tanzania's President KikweteRAIS Jakaya Kikwete, amesema Serikali yake iko imara ikijivunia utekelezwaji wa Ilani ya CCM kwa vitendo na wote wanaosema nchi imemshinda, wanajidanganya kwa kufurahisha nafsi zao.

Alisema miezi michache kabla ya kumaliza muda wake, kumekuwa na uhuru mkubwa kwa watu kutoa maoni yao na wengine kupitiliza, lakini Serikali haipo tayari kuona mtu anatumia vibaya uhuru huo, kuleta machafuko na kuvuruga amani iliyopo nchini.

Hivi karibuni, baadhi ya viongozi wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), walimtuhumu Rais Kikwete na kudai nchi imemshinda kutokana na umaskini mkubwa wa Watanzania.

Rais Kikwete aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na wafanyakazi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora akitumia fursa hiyo kuwaaga na kusisitiza kuwa, haki za binadamu na utawala bora vikiheshimiwa, vitasaidia kulinda amani na utulivu wa nchi.

"Maneno ya wapinzani wetu kisiasa hayanisumbui, anayesema nchi imenishinda mpuuzeni, haijanishinda na wanajidanganya wenyewe, mimi sina wasiwasi na hilo lakini hatutakubali kuona mtu anatumia uhuru huo kuleta migogoro ya kidini au ukabila," alisema Rais Kikwete.

Aliongeza kuwa, hata wale wanaosema nchi za Ulaya zina demokrasia ikiwemo Marekani, wajue hata huko sheria zao haziruhusu maandamano ya watu karibu na Ikulu, lakini hapa kwetu Tanzania, wanasiasa wanataka kuandamana Kariakoo wakiamini wana kundi kubwa la watu kumbe wengi wao ni vibaka wanaoiba bidhaa za wafanyabiashara.

"Ukitaka kuandamana, nenda Jangwani na ukiheshimu sheria ndio haki za binadamu zinapoheshimiwa, hata kama unayo haki lakini timiza wajibu upate haki," alifafanua Rais Kikwete.

Alisema katika utawala wowote, lazima kuwepo na uhuru na hilo kama halipo, watu wataidai kwa njia mbalimbali ili wapate haki yao, wakishindwa wanaweza kutumia bunduki kudai uhuru huo kwa kuwa msingi mkubwa wa amani ni haki.

Rais Kikwete alisema baadhi ya nchi zenye migogoro, chanzo kikubwa ni ukosefu wa haki; hivyo watu wanaweza kudai kwa mazingira ya kawaida na baadaye kupitia wanaharakati, nchi yoyote isiyo na haki za binadamu na utawala bora, si nchi tena bali ni msitu kwa sababu watu wanaweza kufanya lolote kwa wengine wasio na nguvu.

Migogoro ya ardhi

Akizungumzia migogoro ya ardhi, Rais Kikwete alisema lazima kuwepo mpango wa kutenga maeneo ya wakulima na wafugaji ambao wanapaswa kupunguza mifugo yao.

Alisema migogoro mingi ya ardhi inachangiwa na baadhi ya viongozi ambao si waaminifu kwa kuuza kiwanja kimoja kwa watu wawili au watatu huku wananchi wakiwa hawana elimu ya kutosha juu ya masuala ya ardhi hali inayowafanya wenye uwezo kutumia fursa hiyo kuchukua ardhi yao.

"Tumeshughulikia migogoro mingi ya ardhi, jambo hili hatuwezi kuliacha kwani kuna viongozi ambao ndio chanzo, tangu niingie madarakani kila anayetaka ardhi kubwa lazima niidhinishe.

"Maombi yote yaliyofika kwangu, niliagiza lazima Mkuu wa Wilaya katika eneo husika, aitishe mkutano na wananchi ili awaambie na wakikubali nami ndio naidhinisha kwa kutia saini," alisema.

Mauaji ya albino

Rais Kikwete alionesha masikitiko yake juu ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kutokana na ukatili wanaofanyiwa ukiwemo wa kukata viungo vyao kwa ajili ya imani za kishirikina.

"Inauma sana, wakati mwingine unachukia hadi unaamua kulala lakini tangu niingine madarakani, sijawahi kutoa idhini ya kunyonga zaidi ya kufungwa maisha, jambo hili kwa nchi yetu bado hivyo ni kazi yenu
tume kutoa elimu juu ya masuala haya," alisema Rais Kikwete.

Aliishukuru tume hiyo kwa kufanya kazi nzuri ya kutoa elimu inayohusu masuala mbalimbali yakiwemo mauaji ya albino kwani huwezi kuwatenga kwa kuwapa majengo yao, barabara zao hivyo lazima nao waishi kama wengine ndio maana wanachanganywa hata shuleni.

Mwenyekiti wa tume

Mwenyekiti wa tume hiyo, Bahame Nyanduga, alisema kipindi cha miaka 10, imepokea malalamiko 26,818 ya uvunjaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.

Alisema malalamiko 19,508 yalitolewa uamuzi na 7,310 yapo katika hatua za kupatiwa ufumbuzi ambapo hadi sasa kuna kesi 14 zilizopo mahakamani na tume inaendelea kufanya tafiti  mbalimbali katika
baadhi ya mikoa, kutembelea magerezani, kuangalia haki za wafungwa.

"Tunakushukuru sana Rais Kikwete, tunaviomba vyama vya siasa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Jeshi la Polisi nchini watende haki ili kulinda haki za binadamu, utawala bora, kuendeleza amani iliyopo," alisema.

Mwanzilishi wa Chama Ufaransa atimuliwa

Waanzilishi wa Chama cha national front chenye mrengo wa kushoto kimemfukuza mwanzilishi wa chama hicho bwana Jean-Marie Le Pen.
Kuondolewa huko katika nafasi hiyo kubwa kulitokana na ugomvi wake mkubwa na wa waziwazi na mwanae wa kike marine ambae alikichukua chama hicho kutoka kwake miaka minee iliyopita.
Binti yake huyo amekuwa akifanya jitihada za kukinusuru chama hicho kutoka kwenye sura ya ubaguzi wa kirangi na wa dini.
Lakini baba yake alisisitiza chama hicho kiendeleze itikadi zake za awali na kuenzi jadi za chama hicho na kutoa wito hivi karibuni kwa ufaransa kui unga mkono urusi kwa kile walicho kiita kuisaidia dunia ya weupe .
Aliwahi kufanikiwa katika kuweka vizingiti vya kisheria hapo awali vyakumsimamisha kiongozi wa chama hicho.
Na wiki iliyopita bwana le alisema hato mpa kura yake mwanae ifikapo mwaka 2017 katika kugombea nafasi ya uraisi huko nchini ufaransa na kwamba anasikia aibu kutumia jina moja la uko.

Muhubiri wa Kenya aachiliwa kwa dhamana


Muhubiri mwenye utata James Ng'ang'a ameachiliwa kwa dhama ya 500,000.
Amekuwa chini ya kizuizi cha polisi kwa siku mbili na ameshtakiwa na shtaka la kusababisha kifo kupitia uendeshaji gari mbaya.Shtaka ambalo amekanusha.
Muhubiri huyo pia amekana madai kwamba alijaribu kuficha kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa dereva wakati gari hilo lilipogongana ana kwa ana na gari jingine na kumuua mwanamke mnamo mwezi Julai.
Kampeni katika mtandao wa twitter iliwashinikiza maafisa wa polisi kuchunguza ajali hiyo na kwa sasa jina lake linaendelea kusambaa katika mitndao ya kijamii.
Washtakiwa wenzake wakiwemo maafisa wawili wa polisi na mtu aliyejitokeza na kusema yeye ndiye aliyeendesha gari hilo pia waliwachiliwa kwa dhamana na mahakama hiyo ya Limuru.
Magazeti ya Kenya pia yameripoti kwamba nyumba ya muhubiri huyo iliopo katika mji wa Nairobi huko Karen imevamiwa na kulingana na gazeti la Standard , wezi walitoweka na vifaa vya kielektroniki na mali nyengine isiojulikana thamani yake.

Nahreel kufungua chuo cha kufundisha vijana muziki.

nahreelProducer na Msanii toka kundi la NavyKenzo Nahreal, anatarajia kufungua chuo cha muziki kitakachokuwa chini ya Studio yake ya The Industry. Chuo hiko kitatoa mafunzo ya utengenezaji wa midundo (beat) kufanya mixing, kuimba na kurap!

Picha: Beyoncé, Nicki Minaj, Rihanna wakiwa ndani ya vazi la kuogelea, Yupi anapendeza zaidi?

Nikawaida kwa masataa kutupia vazi la kuogelea pale wanapokuwa kwenye mapumziko yao baada ya shughuli za kuwaburudisha mashabiki na kuchukua mwanja wao.

Hizi ni picha za baadhi ya mastaa wakiwa kwenye vazi la kuogelea, Tizama alafu niachie comment hapo chini unadhani nani kapendeza kuliko wote?

Beyoncé.




Nicki Minaj.




Rihanna.



Diamond Platnumz afanya ngoma na msanii Ne-Yo, Hii hapa picha wakiwa studio

Wengi tulijua ya kuwa Ali Kiba ndiye msanii pekee wa Tanzania ambaye atafanya ngoma na Ne-Yo msanii wa Rn'B kutoka Marekani ambaye yupo Kenya kwenye Coke-Studio Afrika.

Lakini usiku wa kuamkia leo, Diamond Platnumz ameweka picha hii inayo muonyesha yeye mwenyewe akiwa studio na Ne-Yo ambapo ameweka caption yenye shukrani kwa msanii huyo kwa kukubali kufanya ngoma pamoja ambayo inawezekana kupitia kwenye mikono ya Sheddy Clever.

Diamond Platnumz ameandika haya "Thanks alot my Brother @neyo and the Whole Compound Crew had a great Session, and it was realy nice working with you...can't wait for the World to hear this Hit Song!! @Diamondplatnumz ft @neyo ..... Cc @sheddyclever @Compoundu @thecorpshow @Jullianl #AfricaTotheWorld"

20 August, 2015

SIRI YAFICHUKA: DAKTARI WA CHELSEA ALILALA NA MCHEZAJI.

DRDR

Baada ya wiki ngumu Stamford Bridge, Chelsea wakianza vibaya huku pia Jose Mourinho akimuondoa katika benchi, daktari Eva Carneiro kwa madai ya kupoteza muda kwa kumtibia Eden Hazard, sasa Ex-boyfriend wa daktari huyo amefunguka na kusema yaliyojiri.
Mpenzi huyo wa zamani wa Eva, aitwaye Rupert Patterson-ward amesema aliachana na Eva kwa sababu alimwambia alikua akitembea na mchezaji mmoja klabuni hapo.
Rupert aliyekutana na Eva 2011 kabla hawaja achana 2013 anasema kwamba Eva ni mtu wa mapenzi sana na kwamba anapenda zaidi ngono.
Rupert anadai walitaka kufanya familia na kuoana lakini Eva alimfukuza na kumwambia kuwa alilala na mchezaji mmoja kikosini hapo.
Hata hivyo habari hizi hazina mahusiano ya moja kwa moja na kitendo cha Mourinho kumfukuza katika benchi mwanadada huyo.
Gazeti la Manchester Evening wiki hii liliripoti kuwa huenda Ivanovic akawekwa benchi kutokana na kuchukizwa na maamuzi ya Mourinho kumfukuza daktari huyo mrembo.
Hata hivyo wakitoa maoni wasomaji wa gazeti hilo, wamesema kila mtu ana haki ya kufanya mapenzi huku wakiamini inaweza pia kuwa mbinu za kumchafua Eva zinazofanywa na mpenzi wake huyo wa zamani.

HII NDIO SABABU KUBWA YA KASEJA KUCHAGUA KUJIUNGA NA MBEYA CITY…

kaseja

Bada ya mlinda mlango wa zamani wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Juma Kaseja kusaini mkataba wa miezi sita kujiunga na timu ya Mbeya City ya mkoani Mbeya, kipa huyo mkongwe ameweka wazi ni kwanini amejiunga na timu hiyo ya wagonga nyungo wa jiji la Mbeya wakati kulikuwa na vilabu vingi vikiiwinda saini yake.
Kaseja amesema, kikubwa alichoangalia kabla ya kuamua kusaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Mbeya City ni ushindani wa klabu atakayokwenda kucheza kwenye ligi kuu Tanzania bara na baadae kuamua kujiunga na Mbeya City.
“Kwanza nachoweza kusema ni kwamba, naviheshimu vilabu vyote, naiheshimu Coast, African Sports, Ndanda, Mwadui na timu zote zinazocheza ligi kuu ni timu kubwa kwahiyo zote naziheshimu. Nilijaribu kuwa mtulivu kwa kipindi chote hiki kuangalia ni timu ipi nitaenda kucheza ambayo itakuwa na ushindani mkubwa”, amesema Kaseja.
Kaseja anaesubiri kujumuishwa kwenye kikosi cha Mbeya City amewaomba wachezaji wenzake wa kikosi hicho pamoja na mashabiki wa timu hiyo kuwa na muungano, umoja na amani ili kuifikisha timu yao pale ambapo kila mwana Mbeya City anataka timu hiyo ifike.
Hapa chini nimekuwekea stori nzima ya Kaseja wakati akifanya mahojiano na Shaffih Dauda, bofya hapo kusikila kila kitu….

Ben Pol akiri alipitia kwenye wakati mgumu baada ya kutoka MLAB

Muimbaji wa Sophia, Benard Paul aka Ben Pol amedai kuwa baada ya kuisha mkataba na kampuni ya MLAB iliyomweka kwenye ramani, alipitia wakati mgumu hadi kuweza kusimama mwenyewe.

Akiongea hivi karibuni kwenye kipindi cha Chill na Sky, Ben Pol alisema changamoto kubwa iliyomkabili baada ya kuchana na MLAB ni njia za kusambaza kazi zake.

Anasema wimbo wake Number One Fan ulipotoka alijikuta akiwapa watu wachache tu kwakuwa hakuwa akijuana na watu wengi tofauti na mwanzo ambapo MLAB ilikuwa ikifanya kazi hiyo yenyewe.

“Lakini ule wimbo ulienda wenyewe hadi mpaka next year ukapata nomination ya Best RnB song,” alisema msanii huyo.

Wimbo huo ulishinda tuzo hizo za KTMA mwaka 2012 bila kutarajia.

Joketi Mwegelo ‘Kidoti’ awataka wasanii wakike wanunue bidhaa zake badala ya maneno matupu tu!

MWANAMITINDO, Joketi Mwegelo ‘Kidoti’, amewataka wasanii wenzake hasa wa kike wamtie nguvu kwa kununua bidhaa zake badala ya maneno matupu.

Mrembo huyo ambaye ni Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006, alifafanua kwamba wasanii wengi wa kike wamekuwa wakisifia bidhaa zake kwa maneno lakini hawamuungi mkono kwa kuzinunua.

Jokate ambaye pia ni mwanamuziki na mwigizaji, alisema wasanii hao wakitumia bidhaa zake zitamuongezea kipato na kumtangaza yeye pamoja na taifa kwa ujumla kwa kuwa wasanii hao wana majina makubwa ndani na nje ya nchi.

“Wapo wasanii wanaonunua kazi zangu kwa wingi lakini wengine wanaahidi tu hawanunui, nawaomba wanunue ili tusaidiane kuzitangaza na pia tutangaze taifa letu kwa ujumla kutokana na nafasi na majina yetu yalivyo makubwa ndani na nje ya nchi,’’ alisema.

Video ya Mayunga ‘Nice Couple’, itazame hapa.

Mayunga+Nice+Couple+SleeveHii video ya mshindi wa Trace Star Afrika kutoka Tanzania, Mayunga Narimi, Video ya wimbo wake wa ‘Nice Couple’ na kazi yake inasimamiwa na Universal Music (Pty) Ltd South Africa.

video mpya ya Sauti Sol ‘Shake Yo Bam Bam’ itazame hapa

bambam

Baada ya video yao ya ‘Nerea’ kufanya vizuri nje na ndani ya Afrika Mashariki, Sauti Sol wametoa video mpya ya wimbo wao mpya ‘Shake Yo Bam Bam’.
Video imefanyika jijini  Nairobi na Director  kutoka Nigeria Clerence Peters

19 August, 2015

KOCHA MSAIDIZI AZAM AKUBALI YAISHE…

NsimbeAliyekuwa kocha msaidizi wa Azam FC George Nsimbe Best ametimka kunako klabu hiyo baada ya makubaliano ya pande hizo mbili kuafikia muafaka wa kufanya hivyo ambapon tayari kocha huyo wa zamani wa klabu ya KCCA FC ya Uganda amesharejea nyumbani kwao Uganda.
Afisa habari wa Azam FC Jafar Idd Maganga amehibitisha kuondoka kwa Nsimbe ndani ya Azam na kusema nafasi yake imechukuliwa na Romano ambaye atakuwa akimsaidia kocha mkuu wa timu hiyo Stewart Hall.
“Ni kweli mwalimu George Best hatuko naye, alikuwa ni mwalimu msaidizi kwenye timu yetu lakini mchezo wa mpira una kuingia na kutoka, amekaa na uongozi wamezungmza na wamekubaliana hatimaye George Best merejea Uganda na Romano ndiye amechua nafasi ya ukocha msaidizi kumsaidia Stewart Hall kwa kipindi hiki”amesema Maganga.
Nsimbe alipewa majukumu ya kuinoa Azam kwa muda mara baada ya aliyekuwa kocha mkuu wa kipindi hicho, Joseph Omog kutimuliwa kwenye nafasi hiyo mwezi Februari mwaka huu kufuatia kuondoshwa kwa timu hiyo kwenye michuanon ya vilabu bingwa barani Afrika na timu ya Al Merreikh ya Sudan.
Kocha huyo alikisaidia kikosi cha Azam kumaliza kikiwa nafasi ya pili nafasi ambayo ilikuwa ikigombewa pia na ‘Wekundu wa Msimbazi’ Simba.
Baada ya Azam kuamua kumrejesha kocha wao wa zama Stewart Hall, Nsimbe alirudishwa chini na kuwa kocha msaidizi wa kikosi hicho chini ya Muingereza Hall ambaye ndiye aliyekabidhiwa mikoba ya ukocha mkuu wa matajiri hao wa jiji la Dar es Salaam.

BAADA YA USAJILI MPYA….KIKOSI CHA CHELSEA KINAWEZA KUWA HIVI

1358693-29167764-1600-900
Mourinho aliwai kusema kwamba yeye kwa msimu huu hatasajili kwa fujo anaamini kikosi chake kipo vizuri lakini mambo yanaonekana kuwa sio mambo kwake baada ya kuanza na dalili mbaya za kutetea ubingwa.
Sasa Chelsea wanafanya usajili wa haraka na kutumia pesa kadri iwezekanavyo ili wawe ndani ya muda na kuziba mapengo ya kikosi chao.
Chelsea imeshamsajili Baba Rahman ambae anategemewa kuwa pamoja Branislav Ivanovic kwenye defence ya Chelsea. Pedro anategemewa kuja kum-replace Oscar kwenye kikosi kitakachoanza akiwa pamoja Willian.
2B78503700000578-0-image-a-14_1439987020410
Baada ya kukatiliwa ofa yao kutaka kusajili John Stones, Chelsea bado haijakata tamaa na wanajiandaa kuweka mzigo mpya ili kumpata mchezaji huyu ambae anategemewa kujifunza mambo mengi kutoka kwa John Terry.
2B64EFF700000578-0-image-a-11_1439986534296
Wachambuzi wengi wanakipiga chapua kuwa hiki ndicho kikosi kinachoweza kuisaidia Chelsea kurudi kwenye harkati za kutete taji lake na sio kama walivyoanza.
2B7E700400000578-3203451-image-a-25_1439991734076

SCHWEINSTEIGER ALIPIGA PASI NYINGI KWENYE DAKIKA 45 ZAIDI YA MCHEZAJI YOYOTE WA BRUGES NA WAYNE ROONEY

2B78D91E00000578-0-image-a-1_1439986410756
Memphis Depay amechukua headline ya mechi ya jana lakini pia kwenye takwimu mkongwe Bastian amefanya kazi kubwa licha ya kuingia kipindi cha pili.
Katika dakika 45 alizocheza Bastian amepiga pasi nyingi zaidi ya mchezaji yoyote wa Club Bruges ambae amecheza dakika zote 90.
Pia amewatia aibu wachezaji wenzake ambao walikua wanacheza tangu mwanzo wa mechi kwa kupiga pasi nyingi zaidi yao. Mfano Wayne Rooney,Memphis Depay na Adnan Januzaj. Bastian amepiga jumla ya 54 ndani ya dakika 45 alizocheza.
Wastani ni kwamba kila dakika ya mchezo alikua anapiga pasi kwenda kwa mchezaji mwenzake ili waende kutupia nyavuni. Hii inaonyesha jinsi gani alikua busy uwanjani na kuchangia ushindi wa 3 – 1.

CHELSEA YAIPIGA TOBO MANCHESTER…PEDRO KUSAINI NA CHELSEA MUDA WOWOTE

2B46703200000578-3203285-image-a-11_1439982383807
Katika kile kilichotafsiriwa kama ni Van Gaal kupigwa tobo na Jose Mourihno katika harakati za kumsajili Pedro, imekua ni habari ya kushtukiza sana kwa mashabiki wa Manchester tofauti na walivyotegemea. Hadi mara ya mwisho kila mtu alikua anajua kwamba Pedro atacheza kwenye kikosi cha Manchester United, lakini mambo yanaenda kombo.
Licha ya kumtuka vice chairman wao Ed Woodward mtu maarufu kabisa kwa kufanya madili yanayoipa faida Manchester, lakini muda huu anaonekana kuwa amechemsha. Habari ni kwamba pesa kiasi cha pound milion 21.1 zimetumika kusamjili Pedro kujiunga na Chelsea ikichangiwa na ushawishi mkubwa wa mmiliki wa Chelsea Abramovich.
Pedro alionekana kutokulidhishwa na Manchester baada ya Chelsea kumpa dili la £19m wakati United walitoa £17m.Siku ya leo ndio inategemewa Pedro atadondoka wino na kuwa Team Blue rasmi. Chelsea wanaonekana kutumia kwa nguvu sana muda huu uliobaki kusajili wachezaji kutokana na kuanza vibaya na kusitasita kwenye harakati za kutetea ubingwa wao.

Mfahamu mpenzi wa Ommy Dimpoza ambaye yeye humfananisha na Beyoncé

Mara kadhaa hivi nimekuwa nikipita kwenye account ya msanii Ommy Dimpoz na kukuta picha zake binafsi, Lakini ni mara chache huwa anweka picha ya msrembo huyu anaye onekana kufanana na mwanamuziki wa Marekani na mke wa rapper Jay Z. Okay hapa ninamzungumzia Zerthun mwenye muonekano wa Beyoncé.

Ambapo anaonekana kuwa ni mpenzi wa msanii Ommy Dimpoz kutokana na picha wanazo share kwenye account zao za Instagram. Mfano kwa Ommy nimekuta alishare maneno haya yakiambatana na picha ya mrembo huyu "�� #MrsPKP������❤️❤️" jana na siku za nyuma aliweka haya "Keep Calm I'm on FaceTime with Bae (beyonce)#WCE" hayo niya Ommy Dimpoz. Naye Zerthun aliweka picha ya Ommy nakuandika "Just way too fly! ❤️".

Hizi hapa chini ni picha za mrembo huyo, Zitazame kisha tupia maoni yako hapo chini kama ni kweli anafanana na Beyoncé.








Amber Rose ahusishwa kwenye skendo ya kuwashawishi 'models' kwenye vitendo vya ukahaba

Akitumia njia za zamani za Amber Rose kama account yake ya Ustream na kampuni feki akiwashawishi models na kuwaambia kuwa anatafuta models chipukizi na kuwasaidia pia. Utaalamu wake umepitiliza hadi kutumia video za zamani za Amber kushawishi wadau kumfuata mawazo yake.

Mara tu watakapo kubaliana na kazi yake, basi atawaunganisha kwa matajiri kuwa na mahusiano nao ya kimapenzi na kuwaambia kuwa hiyo itawasaidia kukuza kipaji chapo na kufanikisha ndoto zao katika fani yao ya model.

Hataivyo mmoja wa models hao alitoa taarifa kwa shirika la polisi la Los Angeles LAPD kuhusiana na suala hilo.
Amber Rose hajaliongelea suala hilo hadi sasa.

Picha: Rapper Wiz Khalifa anamahusiano na msanii Rita Ora!

Mahusiano mapya. Wiz Khalifa ambaye bado hajawa wazi kwenye mahusiano ambayo anaweza kuwa kwa sasa kwanzia aachane na mke wake Amber Rose, Inawezekana akawa kwenye mahusiano mapya ya kimapenzi na Rita Ora.
Wiz Khalifa na kipenzi hicho Rita walianza kuonekana mara tu kwenye Teen Choice Awards ambazo zilifanyika jumapili iliyopita. Wawili hao walikuwa huru sana haswa wakati wakichukuliwa picha ya pamoja nyuma ya jukwaa.

Kwamujibu wa TMZ, wawili hao walionekana kutoka kama wapenzi na kwenda dinner usiku wa jumatatu nabaada ya hapo walitembelea studio ya muziki.








Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...