30 July, 2015

UZI MPYA WA SIMBA SC WATOKA KWA KASI….

simba-sports-club-231-768x403
Jezi za Simba zimeanza kuuzwa rasmi leo tarehe 30 – 7 – 2015 kwa mashabiki na wapenzi wa klabu ya hiyo na wapenda mpira wa soka wote Tanzania.
Kama walivyoahidi simbasports.co.tz imewapatia zawadi mashabiki wa Simba wawili wa kwanza kununua jezi hizo, ambapo washindi ni Fabiani Mayenga na Amina Hussein.
Simbasports.co.tz ilifanya mahojiano na mmoja wa washindi, Fabiani Mayenga na kusema “najisikia vizuri sana kwa kuwa ndani ya klabu inayonijali sana, leo hapa nimekuja kununua uzi mpya wa Simba na kupewa zawadi hakika nimefurahi sana na ninaishukuru klabu yangu kwa kutujali wapenzi wake “.
Mayenga pia amewataka wapenzi na mashabiki wa Simba kujitokeza mapema kununua jezi kwa TSH 15,000 ili nao waweze kuichangia klabu yao kwani kununua jezi hizo na kuongeza mapato kwa klabu tofauti na awali ambapo klabu ilikuwa haifaidiki na jezi feki.
Kwa wakazi wa Dar es Salaam wanaweza kupata jezi hizi makao makuu ya Simba pamoja na kwenye maduka ya Uhl Sports yaliopo mtaa wa Sinza na Jamhuri, kwa wakazi wa mikoani kwa sasa wanaweza kupata jezi hizi kupitia kwenye duka mtandao la Jumia www.jumia.co.tz .
Simbasports.co.tz itaendelea kutoa Jezi pamoja au tiketi ya VIP bure kwa wateja wawili wa kwanza kwenda kushuhudia mechi zitakazochezwa siku ya Simba Day tarehe 8 – 8 – 2015.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...