02 January, 2016

Ratiba ligi kuu Uingereza leo january 2,2016

 
 Leo EPL inaendelea na kutakua na mechi zifuatazo

Saturday 02 January

West Ham 12:45 Liverpool

Arsenal 15:00 Newcastle

Leicester 15:00 Bournemouth

Manchester United 15:00 Swansea

Norwich 15:00 Southampton

Sunderland 15:00 Aston Villa

West Bromwich 15:00 Stoke

Watford 17:30 Manchester City

KLABU ZIKIZUILIWA CAF, WAKULAUMIWA NI TFF

Jamal Malinzi, Rais wa TFF
Jamal Malinzi, Rais wa TFF

Kwanza nikutakie heri ya mwaka mpya 2016 wewe msomaji wa safu hii ya kujuzana mambo mbalimbali yanayotokea katika michezo hasa soka. Mengi yamepita katika mwaka 2015, tumshukuru Mungu kuiona 2016.
Bila kuchelewa leo mada yangu inahusu kauli ya Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi kwamba, klabu zisiilaumu TFF endapo watapata matatizo ya kutopata leseni kutoka Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kwa kutokidhi vigenzo vya kushiriki michuano yake.
Baadhi ya vitu ambavyo klabu inatakiwa kuwa navyo ili kupata leseni hiyo ni kuwa na uwanja binafsi wa mazoezi na angalau kuwa na timu moja ya vijana inayoeleweka.
Tunapozungumzia uwanja wa mazoezi ni ule ambao timu inaweza kufanya mazoezi yake muda wowote bila kuingiliana na klabu nyingine na uwe upo kisheria kabisa siyo ubabaishaji.
Malinzi siku chache zilizopita katika mkutano wake na waandishi wa habari alisisitiza kwamba, TFF isilaumiwe endapo klabu yoyote itaondolewa katika michuano inayosimamiwa na CAF  kutokana na kutokidhi vigezo vya kupata leseni.
Nionavyo ni kwamba, Malinzi anakimbia jukumu lake kwani klabu zinazoshiriki michuano ya CAF kutoka Tanzania Bara ni mbili tu Yanga na Azam FC. Yanga inashiriki Ligi ya Mabingwa na Azam itacheza Kombe la Shirikisho.
Kwa nini Malinzi asizikomalie klabu kuhusu kutimiza masharti ya kupata leseni mapema mpaka anapoibuka hivi sasa na kutoa onyo hilo? Kuna kitu amekiona mbele na hivyo anaanza kujihami mapema asionekana mbaya.
Ukitazama kanuni za Ligi Kuu Bara, kuna sehemu ya klabu kupatiwa leseni na ili upate leseni ni lazima uwe na vitu nilivyotaja hapo juu yaani uwanja wa mazoezi na timu ya vijana inayoeleweka.
Sasa kwa nini TFF inaziruhusu timu kucheza ligi kuu huku zikiwa hazijatimiza masharti ya leseni? Upuuzaji wa vigezo vya leseni ulianza kwa TFF kwa kuziogopa timu vigogo hasa Simba na Yanga na kuziacha ziendelee kucheza ligi bila ya kutimiza masharti hayo.
Naamini kama TFF ingekuwa makini na kuzikomalia Yanga na Simba kutimiza masharti hayo ya kupata leseni leo hii Yanga ingekuwa imetengeneza pale Kaunda na Simba ingekuwa tayari ipo Bunju.
Tatizo lililopo ni TFF kuruhusu mambo kufanyika kienyeji bila kufuata kanuni zinasemaje, leo hii kuna michuano ya Kombe la Shirikisho (Kombe la FA), hapo timu za Ligi Daraja la Pili, la Kwanza na Ligi Kuu zinachuana kupata timu moja itakayocheza Kombe la Shirikisho Afrika mwaka 2018, lakini bado hakuna kinachoeleweka kuhusu ishu ya leseni au kukidhi mahitaji ya CAF.
Chukulia mfano, timu ya daraja la pili inachukua ubingwa na kupata nafasi hiyo ya CAF, je, itakuaje linapokuja jambo la kukidhi mahitaji ya CAF? TFF itatoa tena tamko la kutohusika endapo timu itazuiwa kushiriki michuano hiyo.
Kwa kutoa kauli kwamba wasilaumiwe endapo klabu itaondolewa katika michuano ya CAF ni sawa na kukimbia lawama, kwani kabla ya CAF ni TFF iliyokuwa na mamlaka ya kuzizuia klabu hata kucheza ligi kuu kwa kutokidhi mahitaji ya kupatiwa leseni.
Maofisa wa CAF siyo wanaokuja kuzikagua klabu, bali ni TFF yenye wajibu huo hivyo kabla ya CAF kufikia uamuzi wowote TFF ilipaswa kuwa ya kwanza kuzifungia klabu kutocheza ligi kuu kwa kutokidhi vigezo.
Lakini kutokana na soka letu kuendeshwa kisiasa zaidi, TFF inashindwa kuthubutu kutoa adhabu kwa klabu za ligi kuu tena bila sababu ya msingi na sasa wanaibuka na kauli za kujihami.
Malinzi na timu yake asikimbie majukmu yake kwani alipaswa kulitazama mapema ili jambo na kuzipa onyo klabu na ikiwezekana kuzizuia kucheza ligi hadi zitimize masharti hayo.
Kwa jinsi mambo yanavyoenda, adhabu ya CAF inaweza kutua Yanga kwani Azam tayari ina viwanja vyake vya mazoezi hadi mechi ndiyo maana Malinzi anaanza mapema kujivua ili asionekane mbaya.
Hapa Malinzi hawezi kuepuka lawama kwani aliacha mwenyewe timu ikacheza hadi ligi kuu bila ya kukidhi mahitaji ya leseni na sasa anaona CAF ipo makini ndiyo anataka kukwepa lawama.
Tuwe wakweli tu kwamba, klabu ikizuiwa kucheza mechi za CAF, itakayolaumiwa ni TFF na siyo mtu mwingine.

Magufuli Awakuna Wananchi Wenye Ulemavu, wamshukuru kwa kutimiza ahadi ya kuwakumbuka katika uongozi wake

lianza na Dkt. Abdallah Possi, wakafuata Profesa James Epiphan Mdoe na Mhe. Amon Anastaz Mpanju na kusababisha mshangao wa furaha miongoni mwa wananchi wenye ulemavu kwa kile wanachokitaja kama kukumbukwa katika uongozi wa Serikali ya awamu ya Tano ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. 
 
Rais alipomteua Dkt. Abdallah Possi kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, kazi, Ajira, Bunge, Vijana na walemavu wengi walifurahi kuona Mtanzania wa kwanza mwenye ualbino anaingia katika Baraza la Mawaziri 
 
Furaha hiyo ilizidi alipowateua Mhe. Amon Anastaz Mpanju mlemavu wa kuona kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria na Profesa James James Epiphan Mdoe kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, ambaye ni mlemavu wa miguu.
 
 Mhe Mpanju, ambaye kitaaluma ni mwanasheria na ambaye pia alikuwa mmoja wa wajumbe wa Bunge la Katiba, alishangaza kila mtu wakati alipokula kiapo mbele ya Rais bila kusoma mahali kama ilivyo desturi. 
 
“Huyu bwana pamoja na ulemavu wake hakika ni mtu wa kazi” alisikika mmoja wa wageni waliohudhuria hafla ya kuapishwa Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu wakuu Ikulu siku ya Mwaka mpya. 
 
Akiwa amesindikizwa na mke wake, Mhe. Mpanju alipokea Biblia Takatifu na kuinyanyua juu na kuanza kula kiapo, ingawa mkewe alikuwa ameshika karatasi ya maandiko ya vitone ambayo ilikuwa aitumie. Hata Rais alitabasamu kwa hilo. 
 
Huko mitaani, ambako tukio hilo la kuapishwa Makatibu wakuu lilikuwa likirushwa ‘live’ na vituo kadhaa vya TV na Redio na mitandao, wengi walishikwa na butwaa, huku wakimsifia Rais Magufuli kwa kuwakumbuka watu wenye ulemavu. 
 
Waliendelea kufurahi walipomuona Profesa James James Epiphan Mdoe, ambaye ni msomi aliyebobea katika Kemia,  akisogea mbele kwa mikongojo miwili na kula kiapo cha kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini. 
 

 Dkt. Abdallah Possi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, kazi, Ajira, Bunge, Vijana na walemavu - siku alipoapishwa rasmi Ikulu jijini Dar es salaam Desemba 13, 2015


 Profesa James James Epiphan Mdoe akila kiapo kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini mbele ya Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam jana January 1, 2016


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Amon Anastaz Mpanju akiongozwa na msaidizi wake kujiunga na viongozi wenzie ili kutia saini Ahadi ya Uadilifu kwa Viongozi wa Umma  mbele ya Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli Ikulu jijini Dar es salaam  jana January 1, 2016

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Jaruari 2, 2016

01 January, 2016

JITIHADA ZA GENK ZAMVUTIA SAMATTA KUTUA UBELGIJI

 


Leo Mbwana Samatta amemalizia simulizi yake ya siku tatu ya ‘Safari ya Samatta kutoka Mbagala kwenda Ulaya’. Leo ameeleza namna ambavyo timu ya Genk ilivyokuwa serious kumtaka akaitumikie ukilinganisha na timu nyingine za Ulaya ambazo zilikuwa zinamuhitaji.
Samatta pia ametaja sababu ambazo zimemfanya akubali kujiunga na timu hiyo na kuzikacha offer za timu nyingine ambazo zilikuwa zikimuwania.
Option zilikuwepo lakini timu nyingi walikuwa wanatumia zaidi mitandao yani walikuwa wananitafuta kupitia mitandao, lakini Genk wameonesha interest ya moja kwa moja, walisafirisha mtu kutoka Belgium hadi Dar es Salaam kuja kufatilia masuala yangu ya mkataba, mkataba wangu upoje ili wanapoanza process za kunisajili kusiwe na matatizo kwenye masuala yanaohusu mikataba.
Wakatoka Dar wakaja hadi Japan kuja kuonana na mimi mwenyewe moja kwa moja kipindi hicho tulikuwa kwenye mashindano ya klabu bingwa dunia. Wakaja kuniambia wameweka kitu hiki na kile kwa ajili yangu. Ni timu ambayo ilinifanya nijisikie kwamba kweli wananihitaji ukilinganisha na timu nyingine.
Halafu timu ambayo inakuhitaji moja kwa moja inakuwa inakuhitaji ili ikakupe nafasi tofauti na timu nyingine ambazo labda zinawachezaji wake lakini labda kuna mapungufu labda mchezaji ameumia au ametoka kwahiyo wanakuhitaji kwa ajili ya kuziba pengo tofauti na timu ambayo inakuhitaji moja kwa moja na lengo langu mimi ni kupata nafasi kwsababu bila kupata nafasi kwa asilimia zaidi ya 70 ni ngumu kuonesha kiwango changu na ni ngumu kupata opportunity nyingine.

Wiz Khalifa anatoka na huyu Porn Star?

wizkhalifa1Wiz Khalifa amekua akijulikana kama mtoto wa nyikani ambae ana namna yake yakula bata amekua akihusishwa kwenye mahusiano na wanawake kadhaa akiwemo Amber Rose, Rita Ora na sasa ameonekana akidate na porn star Jada Stevens A video surfaced of the two smoking together. Could this be Wiz’s new lady, just a friend, or just a good smoke session?

Kundi la YMCMB limerudi tena kama Zamani?

drake lil wayne baby birdman instagramkwa inavyo onekana ni kwamba Crew imerudi tena pamoja! Drake, Wayne, Baby pamoja na wana wengine wamepiga picha wakiwa pamoja kwenye party ya kuukaribisha mwaka mpya. Katika akaunti ya Instagram anayomiliki Drake aliweka picha ifuatayo hapo chini drake lil wayne baby birdman cash money young money - drake instagram
NIO BEEF LIMEKATA

Mambo ni rahisi zaidi.. utaweza kupima chakula kwa simu yako kabla ya kula, hapo vipi?.. (+Video)


Tunasema asante kwa teknolojia kila siku kwa sababu ya vitu vizuri ambavyo tunakutana navyo vikikufikia na kurahisisha mambo mengi kwa sababu tu wataalam wamekaa na wamebuni kitu kizuri !!
Unaambiwa ni suala la kukaa tayari wakati wowote kuanzia sasa tutakuwa na simu zenye uwezo wa kufanya scanning chakula na kutoa majibu kwamba kwenye chakula kuna nini na nini…
scio_results_2-100264526-orig
Kwa sasa kuna kifaa kinaitwa SCiO scanner ambacho ni kidogo tu hivi na kina uwezo wa kufanya scanning kugundua vitu vingi kama kiasi cha sukari kwenye chakula, au mafuta, chumvi, kemikali na vitu vingine… hiki kifaa kimeingizwa kwenye list ya ugunduzi mkubwa uliofanywa kwa mwaka 2015.
Ukiwa na SCiO scanner kama ni mtu mwenye tatizo la kisukari au presha inaweza kumsaidia pia kwa ajili ya kuweza kudhibiti kula vyakula ambavyo havitakiwi kwa wakati akiwa kwenye hali ya kuumwa.

Video ya kifaa chenyewe hii hapa.


Profesa Ndalichako Atoa Siku 30 Kwa Katibu Mtendaji NACTE Kuvichunguza Vyuo Vyote Nchini Kujua Ubora Wake


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ametoa siku 30 kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (Nacte), Dk Primus Nkwera kufanya ukaguzi wa vyuo vyote na kumkabidhi ripoti ili kujiridhisha na ubora wa elimu inayotolewa.

Pia, amewataka watendaji wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) kuandaa mitalaa yenye matokeo ya kujenga wanafunzi watakaozalisha kwenye jamii.

Waziri huyo ambaye amewahi kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), alitoa maagizo hayo jana wakati wa ziara yake katika ofisi hizo ikiwa ni siku tano baada ya kuapishwa kuiongoza wizara hiyo.

Alisema anawafahamu vyema watendaji wote wa taasisi hizo na hatavumilia kuona ubora wa elimu ukiendelea kuporomoka nchini.

Aliitaka TET kuhakikisha mtalaa wa KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu) kwa darasa la kwanza na la pili unapelekwa shuleni kabla ya Januari 13.

“Lakini pili, ningependa muanze kutumia walimu wastaafu kwenye uandaaji mitalaa hiyo na ukaguzi uimarike kwa wanafunzi, mnaweza kuwa na mitalaa mizuri lakini ufuatiliaji ukikosekana haitasaidia,” alisema.

Kuhusu ubora wa elimu alisema: “Ningependa uonekane kwa matokeo baada ya kumaliza shule, sihitaji kusikia amefaulu kwa alama ngapi ila amejengewa uwezo gani kichwani,” alisema.

Alisema kasi ya uwajibikaji TET imekuwa ndogo kwani kitabu cha kurasa 16 kinatengenezwa kwa mwaka mmoja. 

“Ninaweza kuja hapa mnipatie nafasi halafu tujipime na nyie tuone, naomba mbadilike nimeona mko nyuma sana ya kasi yangu,” alisema.

Mbali na maagizo hayo, Profesa Ndalichako aliiagiza Nacte kufanya usajili wa vyuo kwa kuzingatia mahitaji ya soko badala ya kusajili holela bila ufuatiliaji kwa kuwa baadhi vinajiendesha kwa ujanja ujanja.

Alisema suala la ubora wa elimu linamkosesha usingizi. Alilitaka baraza hilo kungeongeza kasi ya ushawishi katika uwekezaji wa shule za ufundi badala ya kujikita kwenye upandishaji wa hadhi ya vyuo na kuondoa dhana ya biashara katika sekta ya elimu.

“Lakini pia ningependa wafanyakazi wote mbadilike, tuache kufanya kazi kwa mazoea. Katika upandishaji hadhi ya vyuo, lazima tujiridhishe na mahitaji ya Taifa, pia kwa suala la udahili wa wanafunzi, ningependa vyuo ambavyo havijatambuliwa kwenye mfumo wa Necta viingizwe ili kuondoa udanganyifu wa vyeti wa usajili,” alisema.    

Taarifa Muhimu Kutoka Baraza La Mitihani Kuhusu Viwango Vya Ufaulu (Grade Ranges)


Baraza la Mitihani la Tanzania limekuwa likipigiwa simu na watu mbalimbali wakiomba ufafanuzi kuhusu taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa limebadilisha Viwango vya Ufaulu (Grade Ranges).

Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwajulisha watahiniwa na umma kwa ujumla kuwa taarifa hizo ni za UONGO na zinalenga kupotosha umma na kuleta taharuki. 

Hivyo, Baraza linaomba umma kuzipuuza taarifa hizo kwa kuwa Baraza halijafanya mabadiliko yoyote kuhusu Viwango vya Ufaulu vinavyotumika sasa. 

Imetolewa na,
AFISA HABARI NA UHUSIANO

Sasa wezi wa simu wapatikana, wataanza kujiibia wenyewe bila kujijua.


WEZI wa simu nchini watakuwa na wakati mgumu baada ya programu maalumu kubuniwa. Programu hiyo inaweza kulinda taarifa zote za simu ya mteja pamoja na simu yenyewe pindi ikiibwa, ambapo mwizi ataweza hadi kupigwa picha bila mwenyewe kutambua. 
Programu hiyo iliyobuniwa na Mtafiti wa kitanzania, Godfrey Magila kupitia Kampuni yake ya Magila Technologies, itakuwa ikitumiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo Tanzania. “Programu hii ni maalumu kwa wateja wa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo na inajulikana kama ‘Tigo backup’. 
Imeshaanza kutumiwa na wateja wa kampuni hiyo,” alisema Magila. Magila alisema kuwa wateja wa Tigo, wanaweza kujiunga na programu hiyo ya ulinzi wa taarifa zao zote za simu, ikiwa ni pamoja na simu yenyewe, ambapo simu ikiibwa pia inaweza kupatikana kwa haraka. 
Alisema mara nyingi watu wamekuwa wakipoteza simu zao na taarifa zote katika simu hizo, ikiwa ni pamoja na namba za simu, picha zao za kumbukumbu na vitu vingine muhimu na simu zenyewe, hivyo alibuni kwa lengo la kuwasaidia watanzania kulinda simu zao. 
Kupitia programu hiyo ya ‘Tigo Backup’, mtu anaweza kupata taarifa zake na simu ikipotea, unaweza kutumiwa taarifa zote mahali ilipo simu yako na picha ya mtu anayeitumia simu hiyo pasipo mwizi kujijua. 
Akizungumzia programu hiyo, Meneja Biashara na Maendeleo wa Dar Development Bussiness Incubator (DTBI), Collin Gumbu alisema ubunifu wa programu hiyo ni wa hali ya juu na una uwezo mkubwa huku akizitaka kampuni za mawasiliano nchini kuwaunga mkono vijana wa Tanzania wanaobuni programu za aina hiyo. 
“Vijana wamekuwa wakifanya utafiti na ubunifu wa programu za aina mbalimbali za simu, ambazo kama kampuni za simu nchini zingeweza kuzinunua zingewasaidia sana vijana wetu na kuweza kujiajiri huku wakiitangaza Tanzania kimataifa katika sekta ya sayansi na teknolojia,” alisema Gumbu. 
Gumbu aliipongeza kampuni ya simu ya Tigo kwa kuchukua programu hiyo na kuomba kampuni nyingine nchini kuiga mfano huo. Akiwasiliasha mada katika se mina ya siku moja, iliyoandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, Gumbu alisema vikwazo vilivyopo katika baadhi ya kampuni, huwarudisha nyuma vijana walio na nia ya ubunifu. 
Alitaja baadhi ya bidhaa ambazo zilibuniwa na watanzania na sasa zinafanya kazi vizuri na kutoa ajira mbalimbali kwa watanzania kuwa ni pamoja na MaxMalipo. Mbali na programu hiyo ya simu za mkononi, pia Magila amebuni programu ambayo inawawezesha watu wenye ulemavu kushiriki katika upigaji kura. 
Pia programu ya simu ambayo inawawezesha wananchi kusikiliza bunge na kushiriki katika mijadala ya Bunge moja kwa moja na kutoa maoni yao wakati bunge likiendelea.

MAN UNITED 'WAENDEA MBIO' SAINI YA KIUNGO MBRAZIL WA LAZIO MAN UNITED 'WAENDEA MBIO' SAINI YA KIUNGO MBRAZIL WA LAZIO

KLABU ya Manchester United ipo kwenye mazungumzo ya kumsajili kiungo Lazio, Felipe Anderson katika jitihada zake za kusaka kiungo mbunifu.
Mbrazil huyo mwenye umri wa miaka 22 alitakiwa na kocha Louis van Gaal tangu mwanzoni mwa msimu na wasaka vipaji wa Old Trafford wameendelea kufuatilia maendeleo yake mjini Rome, huku Lazio ikimthaminisha kwa Pauni Milioni 35.
United bado inafanya mpango wa kumsajili Sadio Mane - ambao ulikwama Agosti - na Southampton haiko tayari kumuuza mmoja wa wachezaji wake tegemeo Januari.

Manchester United inataka saini ya kiungo wa Lazio, Felipe Anderson ifikapo Januari PICHA ZAIDI GONGA HAPA

Anderson, ambaye amefunga mabao matano msimu huu kutoka eneo la kiungo, amezivutia klabu nyingine kadhaa kubwa Ulaya.
United imejikuta katika wakati mgumu msimu huu kutokana na kukosa kiungo wa maana na inajipanga kuimarisha kikosi chake kabla ya kuanza mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya England.

HILI NDIYO JINA JIPYA LA WEMA SEPETU,AANZA NALO MWAKA


FARID MUSSA AENDA HISPANIA KUFANYA MAJARIBIO YA KUCHEZA SOKA YA KULIPWA

WINGA machachari chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Farid Mussa Malik anayechezea klabu ya Azam FC, anatarajiwa kwenda Hispania kufanya majaribio ya kucheza soka ya kulipwa.
Farid ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE kwamba ataondoka mapema wiki ijayo kwenda katika klabu ya bingwa ya Slovenia, FC Olimpija Ljubljana ambako amepewa siku 10 za majaribio.
"Kwa mujibu wa ratiba niliyopewa, mimi nitakwenda kuungana na hiyo timu Hispania kwa ajili ya majaribio hayo, naomba Watanzania wenzangu waniombee dua ili nifanikiwe tuongeze idadi ya wachezaji wanaocheza Ulaya,"amesema Farid.Maana yake, sasa Farid hatacheza michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza Jumapili visiwani Zanzibar. 
Na huyo atakuwa mchezaji wa pili wa kikosi cha kwanza cha Azam FC kukosekana katika Kombe la Mapinduzi, baada ya beki wa kati, Aggrey Morris, ambaye anatarajiwa kwenda Afrika Kusini kufanyiwa upasuaji wa goti.

Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, wanatarajiwa kuondoka leo jioni mjini Dar es Salaam kwa usafiri wa boti kuelekea visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi.
Azam FC imepania kulitwaa tena taji hilo ambalo ilibeba mara ya mwisho mwaka 2012 wakiifunga Tusker FC ya Kenya katika fainali mabao 2-1 Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Azam FC itatupa kete yake ya kwanza Jumapili kwa kumenyana na mabingwa wengine wa zamani wa Kombe hilo, Mtibwa Sugar usiku, mchezio utatanguliwa na mchezo mwingine wa Kundi B kati ya mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga SC dhidi ya wenyeji, Mafunzo ya Zanzibar.

Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya Tarehe 1 Januari 2016

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...