11 July, 2015

Hawa ndio watatu kwenye Urais wa Tanzania waliopitishwa na CCM

WATATU CCM 

 Updates kutoka Dodoma July 11 2015 ziko kila wakati, na zinazonifikia tu  na mimi nazisogeza kwako ili usipitwe, tuliifahamu TOP 5 ya Wagombea Urais wa CCM, tatu bora je?
Mitandaoni hii ina uzito tayari, majina matatu yaliyopitishwa na CCM kwenye wagombea Urais majina ni haya >>> John Pombe Magufuli, Asha-Rose Migiro na Amina Salum Ali.



MAYWEATHER KURUDI TENA ULINGONI

Floyd Mayweather Jr. reacts after defeating Robert Guerrero by unanimous decision during a WBC welterweight title fight, Saturday, May 4, 2013, in Las Vegas. (AP Photo/Isaac Brekken)
Baada ya kumbwaga Mphilopino Many Pacquiao, bondia ambaye hajaonja ladha ya kipigo katika mchezo wa masumbwi, Floyd Mayweather Jr amethibitisha kupanda tena ulingoni Septemba 12 mwaka huu katika pambano linalotaraji kufanyika mjini Las Vegas Marekani.
Mayweather ambaye ameshinda mapambano 48 aliyopanda ulingoni bila sare wala kupoteza akishinda mapambano 26 kwa ‘knockout’, anashikilia mataji ya WBC na WBA katika uzito wa ‘welter’ aliudhihirishia ulimwengu ubora wake kwa kumtwanga kwa wingi wa alama mpinzani wake Many Pacquiao katika pambao lililovunja rekodi ya mapato katika mchezo wa ngumi ulimwenguni.
Mmarekani huyo aliyepokonywa mkanda wa WBO baada ya kukiuka masharti mapema wiki hii, ametuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii ukiashiria kurudi kwake ulingoni kabla ya kuisha kwa mwaka huu.
“Kwa mashabiki wangu. Uaminifu wenu na sapoti yenu vimenipa miaka 20 bora ambayo ningeiomba. Na nikiwa juu, napanga kwenda juu. Tukutane tena ulingoni Septemba 12,” ulisomeka ujumbe wa Mayweather.
Taarifa hizo zinaweza kuibua fununu nyingi juu ya nani atavaana na bondia huyo katika pambano hilo kwani mabondia kadhaa wameshatajwa kupanda naye ulingoni akiwemo Andre Berto aliyeshinda mapambano 30 na 23 kwa ‘knockout’ pamoja na Karim Mayfield aliyeshinda mapambano 19 huku  11 kati ya hayo akimaliza kwa ‘knockout.’
Mwingine anayevumishwa kupanda ulingoni na bingwa huyo ni bingwa wa zamani wa dunia Amir Khan ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akisaka nafasi ya kuzichapa na Mayweather bila mafanikio lakini itawabidi wapenzi wa ndondi kusubiri mpaka itakapotangzwa rasmi ni bondia gani atakwenda kuendeleza au kuvunja rekodi ya nguli huyo wa mchezo wa masumbwi ulimwenguni kwa sasa.

Bastian Schwesteiger athibitishwa kwenda Man United – awek rekodi hii

Klabu ya Manchester United imekubaliana kimsingi na mabingwa wa Bayern Munich juu ya usajili wa kiungo wa timu ya taifa ya Ujerumani Bastian Schweinsteiger.
  Bastian, mwenye umri wa miaka 30, aliomba mwenyewe klabu ya Bayern Munich kutompa mkataba mpya na angependa kwenda sehemu nyingine.
Mkurugenzi mkuu wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge ameongea na waandishi wa habari muda mfupi uliopita na kusema: “Marafiki zangu wa pale Manchester United tumekuwa na mawasiliano kwa muda kidogo. Tumefikia makubaliano juu ya uhamisho wa Bastian.
Schweinsteiger ameshaichezea Bayern Munich mechi 536 tangu alipovaa jezi ya timu hiyo kwa mara ya kwanza mwaka 2002.
 
Inamaanika kwamba Bastian amevutiwa kujiunga na Manchester United kutokana na kuwa na mahusiano mazuri na kocha Louis van Gaal ambaye alimfundisha soka wakati alipokuwa kocha wa Bayern Munich.
Ada ya uhamisho iliyolipwa kumsajili Schwesteiger inaaminika kuwa karibia kiasi cha £8m na mshahara wake utakuwa kiasi cha £7m kwa mwaka.

10 July, 2015

IKER CASILLAS AMEKATAA KUAGAWA UWANJANI NA REAL MADRID

CASI
Iker Casillas inaonekana hajapenda jinsi Real Madrid inavyomuuza kwenda Porto ikiwa yeye ndoto yake kubwa ilikua ni kumaliza soka lake ndani ya Real Madrid.
Ilibidi Casillas aagwe kwenye mechi na mashabiki wa Real Madrid lakini ripoti zinasema kwamba mchezaji huyo hajapenda jinsi anavyomalizana club hiyo iliyomlea toka utotoni.
David De Gea ndio kipa pekee anayetegemwa kuchukua mikoba ya kipa huyo japokua bado De Gea yupo Manchester united

Kama uliikosa hotuba nzima ya Rais Kikwete July 9 2015.

20101207 - Brussels , Belgium - European Development Days - The Energy Evolution - Mobilising Energy for Sustainable Development - H. E. Jakaya Mrisho Kikwete , President of the United Republic of Tanzania © European Union
Kama ulikosa time ya kumtazama au kumsikiliza Rais Kikwete kwenye hotuba yake akilivunja Bunge Dodoma June 9 2015 unaweza kuutumia muda wako kumsikiliza hapa chini.
Amezungumzia ishu nyingi sana ikiwemo Wasanii na alivyowasaidia, soka, miaka yake kumi ya uongozi na aliyoyafanya pamoja na mambo mengine

Hii ndio sababu ya Eddy Kenzo wa Uganda kupewa tuzo yake kwenye redcarpet ya BET Music Awards 2015.

 Eddy-kenzo

Msanii kutoka Uganda Eddy Kenzo ametoa sababu za kupokea tuzo yake kwenye redcarpet ya Bet badala ya kwenye jukwa la show ya BET Music Awards 2015.
Eddy Kenzo amesema “Waandaji wa tuzo za Bet walimfahamisha kuwa tuzo ya kila kipengele ilikuwa na mdhamini na kampuni iliyodhamini tuzo ya kipengele cha Viewers Choice ; Best International Artist haikulipiwa muda wa jukwaani na ndio sababu ya kukabidhiwa kwenye redcarpet”
Eddy amesema ukiacha kupewa tuzo kwenye redcarpet ,alithaminiwa vizuri na kulazwa kwenye hotel moja na mastaa kama Nicki Minaj, Drake na Tyga.


TOA MAONI YAKO

(OFFICIAL VIDEO) TAMAR BRAXTON- IF I DON’T HAVE YOU

Staa wa Rnb Tamar Braxton anatafuta mapenzi ya ukweli kwenye video ya wimbo wake mpya “If I Don’t Have You.
  TOA MAONI YAKO

(OFFICIAL VIDEO) YEMI ALADE- POSE


Msanii kutoka kwenye lebo ya Effyzzie Music, Yemi Alade amedondosha video ya pili ya wimbo wa Pose ndani ameshirikishwa Mugeez msanii kutoka Nigeria. Producer aliesimamia video hii anaitwa Paul Gambit. Hii ni version ya pili ya wimbo huu na kama wewe ni mpenzi wa kujifunza zile steps za kucheza ngoma za Kinigeria, Yemi Alade amekuraisishia kazi ndani ya hii video.

TOA MAONI YAKO

Beki wa kulia wa Barcelona Dani Alves, ametanabaisha kuwa Lionel Messi ni bora zaidi ya Cristiano Ronaldo

Ronaldo vs Messi 
Beki wa kulia wa Barcelona Dani Alves, ametanabaisha kuwa Lionel Messi ni bora zaidi ya Cristiano Ronaldo kwa sababu ya hamasa yake kubwa katika timu.  Alves amesema hayo kutokana na mjadala mkubwa uliopo ulimwenguni kwa sasa kuwa nani kati ya wawili hao ni bora zaidi ya mwenzake. 
Hata hivyo, Alves amesema kuwa Messi ana ushawishi mkubwa hasa katika kuichezesha timu kuliko ambavyo Ronaldo hufanya akiwa Real Madrid, huku akidai kuwa Mreno huyo huwa hafanyi chochote kingine uwanjani zaidi ya kufunga magoli tu.  “Messi ni bora zaidi ya Cristiano Ronaldo,” aliliambia Bola da Vez. “Messi ana ushawishi mkubwa uwanjani kitu ambacho Cristiano hana. Hebu angalia kama utaona ana kitu kingine zaidi ya kufunga na kujitokeza katika baadhi ya matukio tu”.
“Messi ana hamasa kubwa, anafunga na kutoa pasi za magoli. Messi ni kipaji kutoka kwa Mungu. Christiano anafanya mazoezi mno. Tuna mapambano yetu binafsi lakini mimi huwa namkubali sana. Ni mtu ambaye hujitolea lakini anayependa ushindani pia”.
“Ronaldo ana vitu ambavyo binafsi sivikubali kwa sababu mimi napenda kucheza kitimu. Nadhani timu ni muhimu zaidi yangu. Nadhani kwa kiasi kidogo sana yeye huweka timu mbele, baadhi ya watu walitukosoa sisi kusherehekea ubingwa wetu wakati Ronaldo alikuwa akishagilia kuwa mfungaji bora”, alimaliza Alves.

Klabu ya Sonderjyske inayoshiriki ligi kuu ya Denmark (ALKA Superliga) imemsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Simba SC, Emmanuel Okwi

IMG-20150710-WA0017

Klabu ya Sonderjyske inayoshiriki ligi kuu ya Denmark (ALKA Superliga) imemsajili aliyekuwa mshambuliaji wa Simba SC, Emmanuel Okwi kwa mkataba wa kudumu wa miaka minne na ametambulishwa rasmi. Okwi, raia wa Uganda  amepewa jezi namba 25 ambayo alikuwa anaivaa akikipiga Simba . Okwi hajafanya majaribio katika klabu hiyo kama walivyodai Simba bali amesaini moja kwa moja na siku chache zijazo ataanza kucheza mechi za ligi kuu.
Capture1Capture2
Mtandao rasmi wa klabu ya Okwi umethibitisha kumsajili
MAELEZO MAFUPI YA TIMU MPYA YA OKWI
SønderjyskE ni shirika la michezo la Denmark linalomiliki timu ya mpira wa miguu inayoitwa SønderjyskE Fodbold, yenye makazi yake mjini Haderslev.
Pia linamiliki timu mbili za mpira wa mikono, SønderjyskE Håndbold, moja ya wanaume yenye masikani yake mjini Sønderborg, moja ya wanawake inayokaa mjini Aabenraa.
Pia lina timu ya ice hockey ijulikanayo kwa jina la SønderjyskE Ishockey, yenye makazi yake mjini Vojens.
Timu zote hizi zinacheza ligi za kaskazini mwa Jutland inayojulikana kwa jina la Sønderjysk Elitesport (Kwa kiingereza: Southern Jutlandic Elite Sport).
SønderjyskE ni timu iliyoundwa kwa ajili ya Jimbo zima la Jutland kaskazini kwa lengo la kuleta ushindani katika ligi za juu za Denmark na timu hii iliweka maskani yake  mjini Haderslev ikiitwa Haderslev FK.
Mwaka 2004, timu zote, yaani ya  mpira wa miguu, ice hockey na handball chini ya Shirika hilo la SønderjyskE, zilianza kuwakilisha ukanda mzima wa Jutland Kaskazini na sio mji mmoja tena. Zilivuta hisia za watu, wadhamini, mashabiki na vyombo vya habari kutokana na kuchukua vijana wengi wenye vipaji .
Kwasasa timu 5 zinacheza katika ligi bora za Denmark, huku timu ya mpira wa miguu ikiwa tishio katika ligi kuu ya Denmark.
Capture3Capture4
 Hizi ndizo timu zinazoshiriki ligi kuu ya Denmark kwa msimu wa 2015/2016
Capture5
Matokeo ya mechi za karibuni za timu ya Okwi na ratiba ijayo…

Hatimaye klabu ya Liverpool ya Uingereza imemtangaza kiungo wake Jordan Henderson, kuwa nahodha mpya wa klabu hiyo

vvvvvvvvvvv
Hatimaye klabu ya Liverpool ya Uingereza imemtangaza kiungo wake Jordan Henderson, kuwa nahodha mpya wa klabu hiyo yenye maskani yake Merseyside. Henderson ambaye alikua nahodha msaidizi wa ‘Captain Fantastic’ Steven Gerrard msimu uliopita alitarajiwa kuchukua nafasi hiyo mara baada ya Steven Gerrard kutangaza kuihama klabu hiyo ambapo amejiunga na LA Galaxy ya MLS Marekani.
Ujio wa mchezaji James Milner katika kikosi hicho msimu huu kulitia shaka nafasi ya Henderson kumrithi Gerrard kutokana na uzoefu wa Milner mwenye miaka 29.
Hata hivyo wakiwa katika maandalizi ya msimu mpya, kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers ameona ni muhimu kumtangaza Henderson ambaye amekua ni moja ya nguzo muhimu katika kikosi cha Liverpool.
Henderson ambaye alijiunga na Liverpool akitokea Sunderland alikaribia kuondoka kikosini hapo misimu mitatu iliyopita ili ampishe Clint Dempsey wa Fulham wakati huo.
Hata hivyo nahodha huyo mpya wa Liverpool, alikataa kuondoka kikosini hapo huku akiomba apewe nafasi, aoneshe uwezo wake.
Unahodha huo wa Liverpool umekuja wakati muhimu, wakati ambao Steven Gerrard amekaririwa hivi karibuni akimpigia chapuo Henderson kurithi mikoba yake.

09 July, 2015

Hotuba ya Rais kikwete leo july 9

.Mh Dr Jakaya Kikwete ambaye ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania amemaliza kulihutubia Bunge la kwa mara ya mwisho kwenye muhula wake wa urais muda mfupi uliopita.









Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Diamond Platnumz Kaguswa na hotuba ya Rais Kikwete

ddd
Baada  ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kulianga rasmi bunge mjini Dodoma msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz ameguswa na hotuba hiyo.
Diamond Platnumz ameamplify leo kwenye AMPLIFAYA na kusema’Kipindi ambacho nimebahatika kumuona Mheshimiwa madaraka na vitu ambacho amevifanya kiukweli ni vitu ambavyo vinagusa sana hususa katika tasnia ya kwetu ya muziki unajua hatujawahi kupata mheshimiwa ambaye akawa anatizama suala la muziki na kulithamini kama la kwake kabisa sio tu suala la muziki na vitu vingi sana mimi sio mtu wa kusikiliza masuala ya siasa wala kuangalia masuala ya kisiasa‘ – Diamond Platnumz
.
.
‘Leo kwa Mara ya kwanza nilikuwa naendesha gari huku nasikiliza vitu mwanzo mpaka mwisho kuna vitu ambacho alikuwa anazungumza vinagusa moyoni kabisa kuna vitu alikuwa anaongea vya kuchekesha lakini kuna time nilikuwa nafikiri Je rais atakaekuja atakuaje atakuwa kweli anakumbuka jamii yake ukizungumzia kama wasanii na watu wengine kama alivyokuwa anafanya yeye kwasababu sio kila mtu anachukulia suala la sanaa kama serious mwingine anaweza akaona vijana hawa wanaimba imba tu lakini wengine ndio ajira yetu tunafamilia wazazi wetu ndugu marafiki na tumeajiriana wenye wenye’ – Diamond Platnumz
deee
.
‘Nikajikuta ghafla daah Je Rais atakayekuja ikiwa Je anapenda uvuvi akiwa anapenda vitu vingine labda muziki akaudharua itabidi tukashika nyavu tukavue na suala la muziki linaishia hapo hapo hakuna masuala ya Channel O au MTV nikajikuta nawaza nikajikuta naandika kutoka moyoni hakika katutoa kule anatuacha hapa ambako pako juu zaidi kama kauli yake mwenye alivyosema inagusa moyoni yaani unatamani kama inawezekana wala apewa muhula mwingine aendele tena lakini ndio haiwezekani kisheria lakini ndo hivyo namshukuru sana nampongeza kwa kipindi ambacho akiwa akilihutubia taifa la Tanzania’ – Diamond Platnumz

Magari 10 ya gharama ya mastaa wa soka Ulaya 2015

kitu
Moja ya starehe za mastaa wengi wa soka duniani ni pamoja na kutembela magari ya kifahari..ukiachilia utajiri wa magari ya kifahari anayomiliki bondia mwenye utajiri mkubwa Floyd Mayweather..wapo mastaa wa soka ambao nao wameingia kwenye list ya kutembelea magari ya kifahari zaidi.
Hawa ni mastaa 10 wa soka Ulaya ambao mbali ya kuingiza mkwanja mrefu kupitia kazi yao ya soka pia wanatembelea magari ya kifahari….
ron cars
Gari aina ya Buggati Veyron anayomiliki staa wa soka duniani Christiano Ronaldo..gharama yake ni dola 1,7000,000
dinho car
Ronaldinho anamiliki gari aina ya Buggati Veyron yenye thamani ya dola 1,800,000
etoo car
Eto’o ni mpenzi wa magari na amekua akimiliki magari mengi ya kifahari.. naye pia ni mmoja wa mastaa wanaomiliki gari aina ya Buggati Veyron
zlatan car
Zlatan Ibrahimovic anamiliki gari aina ya Porsche ambayo ina thamani ya €768,000
neymar aud
Neymar Dos Santos ndiye mchezaji ghali zaidi Brazil: anamiliki gari aina ya Audi R8 GT lenye thamani ya paundi 246,000
ozil car
Mesut Özil anamiliki gari aina ya Ferrari 458 yenye thamani ya paundi 169,000
lampard car
Frank Lampard anamiliki Ferrari Scaglietti 612 yenye thamani ya paundi 200,000
lake roon
Wayne Rooney anamiliki Aston Martin Vanquish S, thamani yake ni 150,000
mesii audi
Lionel Messi anamiliki Audi R8 Spyder lenye thamani ya paundi 102,385
bale audi car
Gareth Bale anamiliki Audi R8 GT, thamani yake ni paundi 246,000

Baba yangu alinipa pesa ya kusokota dreads na kutoboa masikio – Sheria Ngowi

 

Mbunifu wa mavazi nchini, Sheria Ngowi amesema mafanikio aliyoyapata yametokana baba yake mzazi aliyemuunga mkono kwenye kila japo analolifanya.
“Baba yangu alikuwa ananipa uhuru wa kufanya kila kitu nilichokuwa nataka kufanya,” Ngowi ameuambia mtandao wa Dar City Center.
“Hata nilipotaka kuwa mbunifu wa mavazi alinipa support, pesa ya kusokota dreads na kutoboa masikio alinipa yeye.”



DODOMA: CCM KUTOA TANO BORA LEO

Kisu kikali cha Kamati Kuu ya CCM (CC) leo kitaondoka na vichwa 33 kati ya 38 vya walioomba kuteuliwa kupeperusha bendera ya chama hicho kumrithi Rais Jakaya Kikwete anayemaliza ngwe yake.

Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndugu Philip Mangula.
Kikao hicho ni hatua ya pili baada ya kukamilika kwa kikao cha Kamati ya Maadili kilichokutana jana usiku chini ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete huku kikitawaliwa na usiri mkubwa, kuhama ukumbi na kila dalili za kubadili ratiba iliyopangwa awali ili kuvuruga mipango ya kambi za wagombea.
Habari zilizolifikia gazeti hili zilisema kulikuwa na uwezekano wa kubadili ratiba ili vikao vya Kamati ya Maadili na CC ama vifuatane au vifanyike usiku ili kuyanyima makundi nafasi ya kujipanga.

Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete.
Alipoulizwa jana kuhusu vikao hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alidai kuwa hata yeye hakuwa na uhakika wa lini na muda gani hasa kikao cha Kamati ya Maadili kingefanyika.
Awali, vifaa vya ukaguzi wa wajumbe vilikuwa vimewekwa katika Makao Makuu ya CCM, White House lakini baadaye jioni viliondolewa na hapakuwa na taarifa zozote zilizotolewa.
Habari zilizopatikana baadaye zilidai kuwa kikao hicho cha Maadili kilitarajiwa kufanyika Ikulu ya Dodoma kuanzia saa nne usiku wa jana.
Haya yanajitokeza wakati macho na masikio ya Watanzania yakiwa hapa Dodoma kusikiliza namna kazi ya kuchuja wagombea itakavyofanyika na kujua ni watu gani 33 watakaoanza kulambwa na kisu cha CC, hasa kwa majina makubwa yanayotazamwa na wengi, mara tu baada ya kujadiliwa na Kamati ya Maadili.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Kazi za Kamati Kuu leo
Kikao cha CC kina majukumu matatu leo ambayo ni kufikiria na kutoa mapendekezo kwa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), majina yasiyozidi matatu ya walioona kuwania urais wa Zanzibar ambayo imeombwa na Rais wa sasa, Dk Ali Mohamed Shein pekee, kufikiria na kutoa mapendekezo kwa NEC majina yasiyozidi matano ya walioomba kuwania urais wa Muungano na kuandaa mkutano wa NEC.
Vigezo vya maadili
Kulingana na kanuni za Uongozi na Maadili, toleo la 2012 kifungu cha 4(ii), kuhusu taratibu za kuomba uongozi, wanachama wanaogombea uongozi ambao uteuzi wao hufanywa na vikao vya kitaifa, watachunguzwa kwanza uadilifu wao na chombo cha maadili cha CCM kwa ushirikiano na vyanzo vingine.
Kanuni hizo zinasema mwanachama wa CCM anapoomba uongozi katika ngazi yoyote, itikadi na mwenendo wake vitachunguzwa kwanza na Kamati ya Usalama na Maadili inayohusika, ndipo maombi hayo yaliyoambatanishwa na mapendekezo ya kamati hiyo yatakapofikishwa mbele ya kikao chenye madaraka ya kutoa uamuzi.
Ikiwa mwanachama hakupendekezwa kwa sababu ya kukiuka Katiba ya CCM, Kanuni za CCM na sheria ya nchi, hatakuwa na haki ya kukata rufaa kwa mtu yeyote au kikao chochote. Lakini ikiwa mwanachama atakataliwa kugombea kwa sababu ya madhambi yake katika chama, basi ni wajibu wa Kamati ya Usalama na Maadili kumjulisha makosa yaliyomnyima haki ya kugombea, naye anaweza kukata rufaa kwa mujibu wa haki zake kikatiba.
Mtu yeyote anayetuhumiwa mbele ya Kamati ya Usalama na Maadili ya ngazi yoyote, kwa kosa lolote linalohusiana na maadili au nidhamu ya chama atasomewa na kutakiwa kuzijibu tuhuma hizo mbele ya wajumbe wa kamati hiyo ama kwa kauli yake mwenyewe au kwa maandishi, lakini hataambiwa nani aliyezileta tuhuma hizo, isipokuwa kama imekwishajulikana mapema kutokana na mijadala ya vikao, vyombo vya sheria au vyombo vya habari.
Kanuni ya maadili inaendelea kusema kuwa uchambuzi wa tuhuma hizo utafanywa kwa kutumia njia mbalimbali pamoja na mashahidi watakaopatikana.
Uchunguzi utakapokamilika na endapo itadhihirika kwamba tuhuma zina uzito, mtuhumiwa ataitwa mbele ya kikao cha Kamati ya Usalama na Maadili ya ngazi inayohusika, kama ni lazima, ili apate kuhojiwa ana kwa ana.
Pia, kanuni inasema Kamati ya Usalama na Maadili ya ngazi inayohusika itatoa mapendekezo yake kuhusu suala hilo kwenye kikao cha uamuzi kinachohusika. Mtuhumiwa atapewa nakala ya uamuzi kwa maandishi.
Wagombea wanne kukosa CC
Katika kikao cha CC kinachofanyika leo, wajumbe wanne ambao ni miongoni mwa majina 38 yatakayojadiliwa katika mchujo huo watalazimika kukaa kando ili kukwepa mgongano wa masilahi.
Wajumbe hao ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Asha-Rose Migiro, Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal na Waziri wa Kilimo na Chakula, Stephen Wasira.
Kwa mujibu wa Kanuni za Uteuzi wa Wagombea wa CCM katika Vyombo vya Dola, Toleo la Pili – Februari, 2005, ukurasa wa 25, kifungu cha 21 (3); wajumbe wa vikao vya uchujaji na uteuzi wa wagombea kwa ngazi inayohusika hawaruhusiwi kuendelea na kazi ya uchujaji na uteuzi iwapo wao ni wagombea katika ngazi hiyo.
Kanuni hiyo pia imetoa miiko ya shughuli za uchujaji na uteuzi wa wagombea na wajumbe wote wanatakiwa na kanuni kuzingatia maadili na nidhamu ya chama katika kusimamia na kutekeleza shughuli za uteuzi.
Kanuni hizo zinasema ni mwiko kwa kiongozi yeyote kwa maneno au vitendo kumpendelea au kumsaidia kupata kura nyingi mwombaji mmoja dhidi ya mwingine, kutumia au kuhusisha ukabila, dini, rushwa, rangi, hila na eneo analoishi au anakotoka katika shughuli yoyote ya uchaguzi.
Pia, ni mwiko kwa kiongozi yeyote au mwombaji yeyote wa nafasi ya uongozi au mwanachama yeyote aliyekabidhiwa dhamana ya usimamizi au uangalizi au uratibu wa kura za maoni, uchujaji na uteuzi, kufanya vitendo vya ukiukwaji wa kanuni.
Kuhusu misaada, kifungu cha tano (a) kinasema ni marufuku kwa mgombea yeyote mtarajiwa au wakala wake, kufanya vitendo vyovyote vinavyoonekana dhahiri kuwa ni sehemu ya kampeni za kuwania nafasi anayoitafuta kabla ya muda rasmi wa uongozi unaohusika haujamalizika.
Kanuni imetoa adhabu kwa watakaovunja miiko hiyo na kwa kiongozi atakayethibitika kuivunja atavuliwa uongozi na kwa mwanachama anayeomba kugombea nafasi yoyote atakayethibitika kuivunja hiyo hatateuliwa kugombea nafasi anayowania.

Chanzo: Mwananchi

Robin van Persie anajiandaa kufanya vipimo vya afya leo katika klabu ya Fenerbahce.

download
Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika, Robin van Persie anajiandaa kufanya vipimo vya afya leo katika klabu ya  Fenerbahce.
Van Persie anatimka Manchester United majira haya ya kiangazi na kwenda kujiunga na miamba hiyo ya Uturuki.
Mshambuliaji huyo wa Uholanzi anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na atapima afya leo mjini London.

Mchezaji raia wa Ureno, Luis Almeida da Cunha ‘Nani’ ametuma ujumbe mzito wa kuiaga klabu yake ya zamani Manchester United.

nani

Luis Nani ambaye alikua kwa mkopo wa msimu mzima nyumbani kwao na klabu ya Sporting Lisbon, amekamilisha uhamisho wa pauni 3.5m kujiunga na Fernabache ya Uturuki.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Luis Nani ameandika maneno ya moyoni kuhusu maisha yake ya soka hususani na klabu ya Manchester United na ujumbe huo ni mahususi usomwe na mashabiki wa Manchester united.
Pamoja na kuwashukuru mashabiki, wachezaji wenzake, benchi la ufundi pamoja na wote waliomsaidia kufika hapo alipo, lakini Nani ametoa salamu za pekee za shukrani kwa aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Sir Alex Ferguson.
Alex Ferguson ambaye alimsajili Nani kwa pauni 17m alistaafu kufundisha soka mwaka 2013 na kuacha maisha ya Luis Nani utatani.
Akiwa United, Luis Nani ameshinda makombe 4 ya ligi kuu, kombe la ligi yaani Capital One Cup, klabu bingwa Ulaya pamoja klabu bingwa ya dunia.
Winga huyo pia katika michezo 230 aliyoichezea klabu ya Manchester United, alifanikiwa kufunga magoli 40.
Pamoja na kutokuwa na fomu nzuri chini ya kocha David Moyes, lakini hali ilikua ni mbaya zaidi baada ya ujio wa kocha Louis Van Gaal ambaye alipofika tu aliamua kumtoa kwa mkopo wa mwaka mzima nchini Ureno (Sporting Lisbon) kabla ya kumuuza wiki hii katika klabu ya Fernabache.
nani
nani2
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Kilichojadiliwa kwenye Kikao cha CCM Dodoma, Waziri Mkuu, Urais, Makundi.. Maneno ya Rais JK

Rais JK
Stori kuhusu Siasa zinapewa nafasi kubwa sana sasa hivi, Tanzania inaingia kwenye Uchaguzi Mkuu Mwezi October 2015… Tayari wapo waliotangaza Kugombea nafasi mbalimbali lakini macho ya wengi yako kwenye nafasi ya Urais, mpaka sasa kuna majina zaidi ya 35 ya watu waliotangaza Kugombea nafasi ya Urais kupitia CCM.



 Hii ni Tweet ya Rais JK aliyoweka muda mfupi uliopita


Rais Kikwete yuko Dodoma, imenifikia hii Ripoti ya kilichoendelea jana wakati wa Kikao cha Kamati ya Usalama na Maadili cha CCM

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

08 July, 2015

Ali Kiba na Diamond Platnumz kwa midomo yao wenyewe wanakiri hawa beef.

wpid-diamond

Kwenye interview tofauti walizofanyiwa watu hawa maarufu wa muziki wa bongo fleva wote wamekiri kuwa hawana tatizo kati yao yani kwa maneno mengine hawana BEEF.
Hii ni tofauti na inavyochukuliwa na mashabiki zao ambao wamefikia kiwango cha kufanya kampeni ya kushusha wasanii hawa ilitu kuwashindanisha.
Ali kiba akiwa kwenye kituo cha Citizen alisema ” Mimi na Diamond hatujawahi kukutana sehemu tukagombana
Kiba aliendelea kusema “Hapendi kufananishwa na Diamond sababu kila mtu ana muziki na talent yake
 Kwenye Interview na Xxl wiki hii Diamond amedai kwamba ajawahi kuwa na beef nae hata siku moja… na kuhusu Team za Mitandaoni Diamond amesema “Sioni kama kuna ubaya wowote, kila mtu ana maamuzi kumchagua mtu anayemtaka yeye kumshabikia, huwezi kumlazimisha mtu”
Wawachukue msanii fulani na msanii fulani wawashindanishe na wasanii wa nje, ukiwashindanisha wasanii wa Tanzania haiwezi kusaidia Industry yetu.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Yote unayotakiwa kujua kuhusu simu mpya za iphone 6 na iphone 6 plus

Apple wamevunja ukimya wa muda mrefu baada ya kuzindua simu  aina mbili na sio moja ya iphone 6. Tofauti ya iphone hizi mbili ni ukubwa ikiwa zote zina size kubwa kuliko models za zamani. Models hizi mbili ni iphone 6 na iphone 6 plus . iphone 6 ina screen yenye ukubwa wa inch 4.7 ambayo ni kbwa kuliko ukubwa wa iphone 5s yenye inch 4 inch. iphone 6 plus yenyewe ina screen yenye ukubwa wa 5.5 na kuwa miongoni mwa aina mpya za simu wanazoziita “phablet”.iwatch
Je, lini simu hizi zinaingia sokoni ? iphone 6 na iphone 6 plus zinaingia sokoti tarehe 19 mwezi huu ambapo zitauzwa kwenye nchi 10 ambazo ni US, Australia, Canada, France, Germany, Hong Kong, Japan, Puerto Rico, Singapore na UK. Je, vipi kuhusu kukaa na chaji ? ukubwa wa simu hizi umechangiwa na kuongezeka kwa ukubwa wa betri ambapo kwa iphone 6 inaweza kukaa hadi masaa 11 ukiitumia muda wote ambapo iphone 6 plus inakaa hadi masaa 12.
Vipi , je Apple wamezindua kitu kingine ? Yes , ukiachana na iphone 6 na iphone 6 plus , Apple wamezindua kwa mara ya kwanza Apple Watches , saa za mkononi za Apple tunazoziita smartwatches ambapo itasaidia mawasiliano ya haraka kwa kutumia saa na pia kutumia Apps nyingine kirahisi kama maps na siri. Pia Apple Watch inaweza ikatumika kama kifaa cha mazoezi ambapo inaweza ku-track mazoezi yako.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Klabu ya Mnchester United inakaribia kukamilisha dili la kumsajili beki wa kulia Matteo Darmian

Darmian MatteoKlabu ya Mnchester United inakaribia kukamilisha dili la kumsajili beki wa kulia Matteo Darmian baada ya majadiliano kati ya United na klabu ya Torino ya Italia kufikia hatua nzuri.
United wanahitaji mchezaji ambaye anaweza akacheza kama mlinzi wa kulia baada ya kocha wa kikosi hicho Louis van Gaal kusema kwamba, mbrazil Rafae ameshindwa kuimudu nafasi hiyo.
Ieleweke kwamba, Man United imekuwa kwenye mazungumzo na Darmian, 25, na wanamatumaini ya kufikia makubaliano ya kumsajili nyota huyo kwa kiasi cha pauni milioni 11.
Darmian ni mchezaji wa kimataifa wa Italia ambaye ameshaitumikia timu yake ya taifa kwa michezo 13 na michezo sita akicheza muda wote (full time), Van Gaal anaamini mchezaji huyo atamsaidia kwenye nafasi ya ulinzi wa kulia.
Darmian Matteo 1Pia Van Gaal anatarajia kumuachia Rafael aondoke kabla ya kuanza kwa msimu mpya lakini atasikiliza ofa pia juu ya mlinzi wa kati John Evans ambaye mpaka sasa bado hajapewa mkataba mpya.
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

DIAMOND NA PRODUCER MANECKY WAMALIZA TOFAUTI ZAO

diamond p 
Producer Manecky na msanii wa Bongo Fleva waliowahi kuropotiwa kuwa na tofauti baada ya Diamond Platnumz kuacha kurekodi kwenye studio za Am Reocrds na Producer Maneck alipoanza kuvujisha nyimbo zake wamemaliza tofauti zao.


Manecky aliweka picha yao wakiwa pamoja kwenye studio yake ya Am na ujumbe wa kusamehana, kwa mujibu wa post yake imeonekana ni meneja wa Diamond Platnumz ndiye alimaliza matatizo yao. Hii ndio post yake “Kwa Mara nyingine Tena”In life tujifunze kusamehe na kusahau hakuna ajuae Kesho#aboutLast9te#Ramadankareem #AmRecordsHoMeGoodMusicUNAJUA VILE TUNAFANYAGA WHEN MOND meets NeCk..I missed workin with him Sasaaa Basii… @babutale ubarikiwe Boss ”

Screenshot_2015-07-08-10-32-26Screenshot_2015-07-08-10-32-58
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

‘Nitavumilia’ (Audio) Barakah Da Prince amemshirikisha Ruby

unnamed

Mwaka 2015 jina la Barakah Da Prince, mkali wa Bongo Fleva ambae anaiwakilisha Rock City Mwanza limepaa kwa nguvu kubwa sana, hits zake zimegusa kila kona.. Watu wakaweka kura nyingi kwenye KTMA 2015 category ya Msanii Bora Chipukizi, na Tuzo ikaenda kwake pia.
Hajatulia kusubiri mambo yapoe, katoa ngoma nyingine mpyampya na imenifikia tayari.. Kapewa collabo mrembo ambaye na yeye ana hit ambayo inafanya poa sana, SuperNyota Diva wa 2014, Ruby.
Barakah Da Prince Feat. Ruby– ‘Nivumilie’, unaweza kuisikiliza hapa mapema kabisa mtu wangu.. ruksa pia kushare na mtu wako wa nguvu isimpite.
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

07 July, 2015

Mario Baloteli amekumbwa na matatizo ya kufiwa na baba yake wa kufikia ‘adaptive father’ wikend iliyopita.

balo
Mshambuliaji wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Italia, Mario Baloteli amekumbwa na matatizo ya kufiwa na baba yake wa kufikia ‘adaptive father’ wikend iliyopita. Baloteli mwenye asili ya Ghana alilelewa na mzazi huyo aliye mu-adapt tangu Mario akiwa na umri wa miaka 3 tu.
Wazazi hao waitaliano walio mlea mchezaji huyu waliishi nae huko kaskazini mwa Italia na kumlea kama mwanao wa damu. Tukio hilo la kupoteza mzazi wake limesababisha Baloteli akose kuhudhuria mazoezi ya klabu yake ya Liverpool katika hatua hizi za awali.
Liverpool walimuongezea likizo mshambuliaji huyo mkorofi ndani na nje ya uwanja ili apate utulivu zaidi katika kipindi hiki kigumu cha maombolezi.
Hata hivyo Liverpool wanaamini Baloteli atajiunga nao hivi karibuni ili waendelee na maandalizi yao ya msimu ujao wa 2015/16.
Wakati hup huo mchezaji Raheem Sterling wa klabu hiyo ya Liverpool ameendelea na mazoezi ya msimu mpya na klabu yake pamoja na kuwepo sintofahamu ya hatima yake.
Liverpool walikataa ofa mara mbili kutoka kwa Manchester City waliokuja na dau la pauni 40m za Uingereza lakini inaelezwa kuwa Liverpool wanamthaminisha mchezaji huyo kwa dau lisilopungua pauni 50m.

Jina la mchezaji David Beckham, pengine ndio maarufu zaidi katika sio tu soka bali michezo kwa ujumla

beckmam
Jina la mchezaji David Beckham, pengine ndio maarufu zaidi katika sio tu soka bali michezo kwa ujumla. Becham ambaye hajawahi kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya wala dunia, lakini ndiye mchezaji ambaye amekua tajiri na maarufu zaidi kushinda hao waliwahi kushinda tuzo hizo. Na hilo linaitimiliza kauli isemayo ’mpira ni zaidi ya kuucheza’. David Robert Joseph Beckham alizaliwa mei2, 1975 huko Leytonstone, London. Beckham ni mtoto wa msusi wa nywele bi Sandra Georgina na bwana David Edward Alan Beckham. Wazazi wake Beckham walikua ni mashabiki wa kutupwa wa mashetani wekundu, Manchester United. Huku wakiwa wanaishi London walikua mara kwa mara wakisafiri hadi Old Trafford kuishuhudia Manchester United ikicheza. Maji hufuata mkondo, Beckham naye akarithi upenzi huo wa Manchester kwa wazazi wake.
MAISHA YAKE YA SOKA
Manchester United;
Alijiunga Manchester United baada ya kufanya vizuri katika majaribio kwenye mazoezi ya timu hiyo julai8, 1991 na kuwa sehemu ya vijana wenzake akina Paul Scholes, Ryan Giggs na Gary Neville chini ya kocha Eric Harrison na kuisaidia klabu kushinda kombe la vijana la chama cha soka cha England, FA mnamo mei 1992. Alifanya vizuri katika timu ya vijana hadi kupelekea kuingizwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo septemba 1992, huku akisajiliwa kama mchezaji wa kulipwa mwaka 1993. Alipelekwa kwa mkopo Preston North End msimu wa 1994/95 ili akapate uzoefu wa kucheza kikosi cha kwanza. Akiwa Preston alifunga mara mbili katika michezo mitano aliyocheza, huku akifunga moja kwa moja kwa mpira wa kona. Mwisho wa msimu alirudi tena Manchester na juhudi zake uwanjani zilimfanya awe moja kati ya figa muhimu katika kikosi cha Sir Alex Ferguson akicheza kama kiungo wa kulia. Alifanikiwa kucheza kwa mafanikio zaidi huku akiwa na wenzake akina Nick Butt, Neville brothers, Ryan Giggs, Paul Scholes walishinda kikombe cha ligi pamoja na Fa Cup mara mbili na kufanikiwa kuitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza kwenye michuano ya Euro 1996.

“Ilibadilisha maisha yangu, mpira ulionekana kama unaenda juu, lakini ukatulia na ukazama nyavuni. Nilijihisi niko juu mawinguni, na kutamani kumshika mkono kila mtu pale uwanjani” Becham akielezea goli lake mwaka huo huo wa 1996 alilolifunga dhidi ya Wimbledon nyuma ya mstari wa katikati, goli lililofanya awe Beckham huyu kila mtu anamjua.  Msimu wa 1996/97 David alikabidhiwa jezi namba 10 aliyokuwa akiivaa Mark Hughes lakini baadae mwaka 1997 Eric Cantona alistafu soka na kuiacha jezi maarufu Old Trafford, jezi namba7 na kumfanya Beckham amuachie jezi namba 10 Teddy Sheringham  aliyesajiliwa kutokea Tottenham Hotspurs na kisha yeye kuvaa namba 7.
Msimu wa 1998/99 Beckham alikua miongoni mwa wachezaji muhimu walioshinda mataji matatu ‘treble’ baada ya kushinda Fa cup, ligi kuu na klabu bingwa ulaya. Katika fainali ya Uefa dhidi ya Bayern Munich Beckham alicheza kama kiungo wa kati baada ya nahodha Roy Keane na Paul Scholes kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano. Katika usiku usiosahaulika mjini Barcellona katika dimba la Camp Nou, ikiwa imefungwa goli moja kwa bila hadi dakika ya tisini, kona mbili zilizopigwa na kijana huyo baba wa watoto wanne hadi sasa ndio zilizaa mabao kupitia kwa Teddy Sherigham na Ole gunna Solkjear.  Huku akiwa nyuma ya Rivaldo katika tuzo ya mchezaji bora wa dunia na Ulaya msimu huo wa 1999.
Agombana na kocha Ferguson
Kuanzia miaka ya 2000 uhusiano kati ya Beckham na kocha wake Sir Alex Ferguson ulianza kupungua. Hilo lilitokana na Beckham kuchagua umaarufu zaidi ya mpira amekaririwa Sir Alex akiyasema hayo katika kitabu chake cha hivi karibuni. Kwani mwaka huo wa 2000 Beckham aliruhusiwa kutofanya mazoezi ili akamuone mwanae Brooklyn aliyekua anaumwa, lakini Ferguson alikasirika baada ya kuona picha za Victoria Beckham ‘Posh’ mke wake Beckham akifanya manunuzi ‘shopping’ usiku huo huo Beckham alioruhusiwa. Fergie alimkata mshahara wa wiki mbili Beckham kama faini kwa madai kua Posh angeweza kuwa na mtoto na yeye kuzingatia mazoezi. “hakua ni tatizo, ila hadi alipofunga ndoa. Alikua akifanya mazoezi kwa bidii na makocha wa academy hapa. Alikua ni kijana mzuri sana. Kuoa kulikua ni kitu kigumu sana kuanzia wakati huo. Hakua Beckham tuliye mfahamu. Alikua ni staa mkubwa, na kufanya mpira sehemu ndogo ya maisha yake” Ferguson akizungumzia ugomvi wake na Beckham mwaka 2007. Pamoja na kufanya vizuri uwanjani na kuipa mafanikio timu yake lakin hali bado ilikua tete kati yake na kocha Ferguson. Uhusiano wao ulipotea kabisa mapema mwaka 2003 katika chumba cha kubadilishia nguo baada ya kufungwa goli mbili na Arsenal katika mchezo wa FA cup na kusababisha Ferguson ampige na kiatu chake katika paji la uso kwa hasira na kumuumiza vibaya jichoni. Hali hiyo ilipelekea kuondoka kwa Beckham na kuuzwa Real Madrid.
Atua Real Madrid, Hispania
“Ni mchezaji mkubwa ambaye ataingia katika historia ya klabu na kufanya vizuri. Ni mchezaji mwenye njaa ya mafanikio na kipaji cha ajabu, ni moja kati ya wachezaji bora kabisa wa kiingereza wa muda wote.” Alikaririwa raisi wa Real Madrid Florentino Perez katika utambulisho wa Beckham. Julai1 mwaka 2003 Beckham akatua Madrid kwa uhamisho wa dola za kimarekani 35m. kutokana na nahodha Raul kuvaa jezi namba7, Beckham alichagua jezi namba 23 akionesha kumkubali mkongwe wa mpira wa kikapu Michael Jordan. Akiwa sambamba na nyota kibao wakati huo kama Zinedine Zidane, Raul, Iker Casilus, Carlos, Figo na wengine walitwaa vikombe muhimu kama Spanish super Cup  dhidi ya Mallorca mwishoni mwa 2003 kwa ushindi wa 3-0 Beckham akifunga goli la tatu. Akiwa Hispania Beckham alioneshwa kadi nyekundu mara3 kwa kipindi cha miaka4. Real Madrid hawakufanikiwa kufanya vizuri katika michuano ya klabu bingwa Ulaya kwani mara nyingi walitolewa hatua ya robo fainali. Beckham alifanikiwa kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Hispania katika msimu wake wa mwisho na Real Madrid, 2007 chini ya kocha Fabio Capello. Kutokana na kuwekwa benchi muda mwingi na muitaliano Fabio Capello, Beckham alijiunga na ligi kuu ya soka ya Marekani. Mwezi mmoja baada ya Beckham kumaliza maisha yake ya soka na Madrid, gazeti la Fobres liliripoti kwamba Beckham alikua ni mchango mkubwa sana kibiashara Real Madrid kwa kuisaidia kuongeza mapato hadi kufikia dola 600m kwa kipindi cha miaka minne aliyokaa na Madrid.
LA Galaxy, Marekani
“siji huko kuwa supa staa, siji huko kuigiza filamu, nakuja huko kuwa sehemu ya timu, kufanya kazi kwa bidii na ikiwezekana kushinda mataji. Kwangu mimi soka ndio kipau mbele. Nakuja kuonesha tofauti, nakuja kucheza mpira. Sisemi ujio wangu huko utafanya soka kuwa mchezo maarufu zaidi huko, ni kitu kigumu. Kikapu na michezo mingine ipo huko kwa muda sasa.” Maneno ya Beckham katika safari yake ya kwenda Marekani. Taarifa za kujiunga na LA Galaxy zilianza tangu akiwa na Real Madrid, January 2007. Utambulisho wa Beckham Marekani ulikuwa ni wa kihistoria baada ya kutikisa vyombo vyote vya habari duniani. Mkataba wa Beckham LA Galaxy uliineemesha LA Galaxy kwa kuingiza pesa nyingi kutokana na makampuni kibao kufanya nayo biashara kutokana na uwepo wa Beckham. Mkewe Victoria, Posh alinunua nyumba ya gharama ya thamani ya dola 18.2m ili aishi na familia yake. Beckham akasaini mkataba mnono wa miaka 5 wenye thamani ya us$32.5m sambamba na mikataba yake binafsi iliyokuwa inamuingizia pesa kote duniani. Akiwa nchini Marekani alichezea kwa mkopo mara mbili Ac Milan katika miezi ambayo ligi ilikua imesimama. Na hatimaye akaisaidia LA Galaxy kumaliza katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu ya Marekani, MLS. Katika msimu wake wa mwisho na LA Galaxy aliisaidia kushinda taji la ligi, MLS Cup huku akifanyiwa mabadiliko katika dakika ya 89 kwenye mechi ya mwisho dhidi ya Houston na kushinda 3-1 huku akitokwa machozi baada ya uwanja mzima kusimama na kumshangilia. Mwaka huo huo 2012 yeye na timu yake ya LA Galaxy walialikwa ikulu ya White house na rais Barack Obama.
Paris Saint Germain na kustaafu soka
January 31, 2013 mwisho wa siku ya usajili Beckham aliripotiwa kufanya vipimo vya afya na kujiunga na Paris Saint Germain ya Ufaransa kwa mkataba wa miezi mitano huku akikataa kuchukua mshahara wake hata kidogo na kuchangia katika mfuko wa watoto yatima na wasiojiweza. Alicheza mechi yake ya kwanza na Paris dhidi ya Olympique Marseille akiingia kutokea benchi dakika ya 76 ya mchezo. Alifanikiwa kucheza michezo mingi na timu yake hiyo chini ya kocha Carlo Ancelloti dhidi ya Barcellona katika michuano ya klabu bingwa ulaya. Hatimaye akawa muingereza wa kwanza kushinda vikombe katika ligi nne tofauti baada ya mei12, 2013 kushinda taji la ligi kuu ya Ufaransa katika ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya Lyon. Akatangaza kustaafu soka meiu 16, 2013 na PSG wakamtengenezea viatu vya aina yake avae katika mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Brest. Alivaa kitambaa cha unahodha katika ushindi wa 3-1 na kufanyiwa mabadiliko dakika ya 80 ya mchezo na kuagwa na mashabiki wote uwanjani huku akibubujikwa na machozi kwa hisia.
Anunua timu, Miami nchini Marekani
Tarehe 5 February 2014, ligi kuu soka Marekani ilitangaza kwamba David Beckham amenunua timu kwa dau la dola 25m za marekani ikiwa ni sehemu ya mkataba aliosaini akiwa na LA Galaxy 2007. Timu hiyo itakua mjini Miami na itaanza 2016 au 2017 kutokana nan kukamilika kwa ujenzi wa uwanja.
Umaarufu wa Beckham
Umaarufu wa Beckham nje ya uwanja ulikuwa kama moto wa shamba. Mikataba mikubwa na Coca_Cola company na IBM ndiyo sababu nyingine kubwa ya umarufu wake na utajiri. Ndoa yake na Victoria mwanamitindo mwenye pesa nyingi pia kumekua ni sababu ya yeye kuwa imara kiuchumi na umaarufu. Beckham amekua katika mitindo kwa uda huku akifanya matangazo lukuki. Beckham amekua akihusudiwa sio tu nchini China ambako watu walimtengenezea sanamu, bali dunianin kote.

Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

Sababu sita usizotaka kuzijua kwanini bado upo single….

Sio kila mtu anataka kua katika mahusiano kitu ambacho ni sawa kwa asilimia 100.Lakini kuna watu ambao kila saa wanalalamika kwa kua wapo single japokua hawajahi kujaribu kutatua naweza kusema tatizo hili. Kuna watu inawezekana ni kweli hawajakutana na watu sahihi wa kuwa nao lakini kunawengine huamua kuwa wa kweli kueleza ni sababu gani wapo single.
1 . Unajibana mwenyewe na vigezo na viwango fulani
Utasikia jamaa anasema mimi nataka demu mwenye umbo zuri kama Kim Kardashian , sasa jiulize hawa watu wako wangapi na hata kama wapo wengi hua wana wanaume kibao wanawafukuzia. Au kwa upande wa wadada utasikia nataka mtu mwenye gari , awe na nyumba , awe msomi , analipwa mshahara wa kutosha kunitoa kila weekend. Watu wanaweza kukushangaza   lakini hawawezi kama utawageuzia migongo na kutowapa nafasi. Haya ni mahesabu tu, kama ukiweka vigezo na viwango kibao vya jinsi unavyotaka  mpenzi wako aweje utabakia na watu 10 tu duniani wanaoweza kua hivyo na wewe utakua ni mpumbavu sababu umejitengenezea mtu wa kusadikika na unastahili kuwa single.kubali kwamba hauelewi chochote kinachoendelea baina yako na mtu fulani na vingine vitakuja kawaida tu. Zingatia kukutana na watu halisi , jifunze na upate kuwajua , na upime kama unaendana nao kama watu halisi na sio watu wa kufikirika ambao hata kama wapo inawezekana wasikutake wala kukupenda. Inauma lakini ndio ukweli halisi.
Relationship-Wamegombana-hawa
2. Kama unataka bora  inabidi na wewe uwe bora
Watu wanajipenda ambacho ni kitu cha kawaida kabisa na wanafikiria kwamba wanaitaji mtu bora katika maisha yao lakini jiulize ili upate mtu aliye bora haufikiri kwamba inabidi uweze kukidhi ubora wa mtu huyu unayemtaka ? Unaposema nataka mtu mrefu , anayelipwa mshahara wa mamilioni,anayependa watu, mwenye nyumba nzuri na gari zuri , anayeweza kulea watoto , je ni kitu gani ambacho na wewe utakiongeza kwenye uhusiano wako na mtu huyu? Uhusiano sio “One-way Street” kawa watasha wanavyosemaga.Si maanishi kwamba inabidi uwe bora kabisa , hapana sema ni muhimu kujitathmini mwenyewe na kuangalia ni kitu gani unaweza kuchangia kama ukimpata mtu fulani. Wakati upo single una muda mwingi wa kujifunza kuhusu wewe , sio lazima uwe bora lakini unaweza kufanya vitu vidogovidogo  kama kua msikilizaji mzuri wa maongezi , kujifunza mambo unayopenda kufanya na kadhalika.
Relationship-wapenzi-wanachuniana-kitandani
3. Unajipenda Sana
Ushawahi kuona watu wanaojiona kama Dhahabu , watu kama hawa hata siku moja hawawezi kukubali kama wamekosea sehemu au wamefanya kitu kibaya kwasababu wanajipenda sana na kujiona kwamba wao ndio bora kuliko wengine. Kuna mda inabidi uamke usingizini na ujitambue kwamba wewe sio bora na kwamba inabidi utoe ili upokee.  kwa mfano kama wewe demu unajijali sana na unategemea mwanaume akufukuzie , akutafute kila saa , aonyeshe dalili zote kwamba anakupenda wakati wewe unamwangalia tu labda utakua hauko tayari kupenda na kujali kama watu wafanyavyo kwenye mwanzo wa mahusiano.Sio kila saa ni kuhusu unachotaka kwani ni wakati muafaka wa kuanza kujali na kusikiliza upande wa pili unataka nini.Watu hua wanajua kama mtu anajisikia , kama mtu anategemea kuabudiwa na ni kitu ambacho hakivutii kabisa.
Relationship-woman-at-bar
4. Unajifungia ndani
Kuna watu wanajifungia ndani alafu wanapigia watu makelele kwamba wapo single,sijui wanataka story kama ya cinderella. Kwa watu hawa inabidi waamke. Kama unataka kuwa na mtu usitegemee atadondoka tu kutoka popote.Yes, unaweza hotea lakini ukweli ni kwamba upo katika hatihati ya kuishi peke yako maisha yako yote.Najua kutoka na kujichanganya ni vigumu hasa kwa wale watu ambao hawapo “Comfortable”  jinsi walivyo.Kutoswa inaogopesha na inauma.Lakini unajua kitu gani hakiumi? ni kujua kwamba umejaribu na umeweka juhudi zako zote . Kuamini kitu unachotaka ni muhimu na  kukitafuta pia.Toka nje, kutana na watu , sio tu bar bali hata kwenye vitu mbalimbali  kama movies hivi au swimming kutokana na “hobby” yako. Kama vyote umeshindwa na bado unataka kujifungia ndani basi fanya hata “online dating” , siku hizi kuna app ya simu inaitwa tinder ina watoto kibao wazuri wa kibongo.
Relationship-Amelala
5. Haujielewi unataka nini
Hii ni muhimu sana , kama upo tayari kuwa serious katika mahusiano basi uwe tayari kuwa serious. Kama ukikutana na mtu akaanza kusema maneno kaka ” Sitafuti kitu serious kwa muda huu” au “Sijielewi bado ninataka nini”  basi usijidanganye na kusema ” Sawa tu , ngoja tuone mambo yataendaje” kwani utaishia pabaya na mwisho wake kutofanikisha malengo yako.
Relationship-wapenzi-wanagombana-beach
6. Sio mvumilivu na unakata tamaa kirahisi
labda ushajiweka mara kibao kwa wadau au umekuwa na dates mbaya nyingi au haujajibiwa message zako. Kwa sababu fulani fulani watu wengine hnyoosha mikono juu na kusema “Yamenishinda, hamna haja” , lakini ukweli ni kwamba sio kila mtu utakayekutana naye inabidi awe bora tena ni jambo la kheri umefikiria hivyo. kwahiyo fanya kila majaribio kama sehemu ya kupata ujuzi zaidi.Relationship-Giving-Up

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...