30 July, 2015

KALI: “ANGEL DI MARIA AMEPOTEA, ATAYEMPATA KUZAWADIWA £30

angel-di-maria
Nyota aliyevunja rekodi ya usajili ya Manchester United, Angel Di Maria anaonekana kukaribia kujiunga na PSG.
Winga huyo wa Argentina mwenye umri wa miaka 27 hakuwepo katika kikosi cha Man United kilichofanya ziara ya maandalizi ya msimu mpya nchini Marekani, huku Louis van Gaal akidai kwamba hajui lolote kuhusu alipo Di Maria.
Van Gaal alizungumza hayo na waandishi wa habari baada ya United kufungwa 2-0 na PSG alfajiri ya leo.
Mwandishi wa talkSPORT,  Alan Brazil ameleta kali baada ya ku-post tangazo huko Manchester akitangaza kumtafuta Di Maria akitania kwamba amepotea.
Jamaa huyo amesema atakayemuona Di Maria popote pale alipo ampigie simu Van Gaal kwa namba inayoonekana pichani chini na atapewa zawadi ya paundi milioni 30.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...