05 March, 2016

Sipendi kuisikia ‘DSM Stand Up’ – Chid Benz

Msanii Chid Benz amesema huwa hapendi kuisikiliza nyimbo yake ya Dar es salaam Stand Up na kwamba hata anapo ‘perform’ jukwaani hujisikia vibaya.
chid
Chid Benz ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema ukubwa wa wimbo huo unamuumiza hisia zake, hivyo hujisikia vibaya kila anapousikiliza.
“Hii nyimbo sipendi kuisikiliza kwa sababu inaniumiza ni ngoma kubwa flan kubwa sana, hata nikiwa na perform ile watu wanashangilia , kelele nini ndiyo inanipa ushindi ila inanipa hisia tofauti”, alisema Chid Benz.
Chid Benzi amesema ngoma hiyo aliiachia kwa baraka za mama yake, baada ya kumuambia aitoe kwani ndiyo ilikuwa ngoma bora kati ya nyimbo 80 alizokuwa amerekodi kabla haijatoka.
“Dar es slaam stand up ilikuwa ndani ya nyimbo hizo 80 nilizorekodi, siku moja mama yangu akaniambia ule wimbo unaoanza unalia tttt uko wapi? nikamwambia, ngoja nikutafutie, akaniambia hii itoe, nzuri hii nikaichukua nikaipeleka kwa Duly nikamkuta Pancho, nikamuita Ditto akaja kuweka sauti na tukaifanyia kazi”, alisimulia Chid Benz.

Magazeti ya Leo Jumamosi March 4, 2016


New Music: Ochu Sheggy – Shemeji Yako

maxresdefault
Nyimbo mpya ya Ochu Sheggy inaitwa Shemeji Yako, wimbo huu umetengenezwa ndani ya studio za Flava Production chini ya producer Cristone ambaye pia alitengeneza Dumange.
Unaweza usikiliza na kupakua hapa chini.
Bofy HAPA kuudownlod

Arsenal watamkosa mlinda lango wao Petr Cech kwa wiki tatu hadi wiki nne kutokana na jeraha

CechArsenal watamkosa mlinda lango wao Petr Cech kwa wiki tatu hadi wiki nne kutokana na jeraha, meneja wa klabu hiyo Arsene Wenger amesema.
Kipa huyo wa umri wa miaka 33 atakosa mechi tatu za Ligi ya Premia, pamoja na mechi muhimu ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya ugenini dhidi ya Barcelona.
Aidha, atakosa mechi ya marudiano Kombe la FA dhidi ya Hull.
Aliumia mguuni alipokimbia kurejea kwenye ngome yake baada ya kuruka juu kudaka mpira wa kona wakati wa mechi ya Jumatano ambayo walichapwa 2-1 na Swansea nyumbani.
The Gunners wamo nambari tatu ligini, alama sita nyuma ya viongozi Leicester, na alama tatu nyuma ya Tottenham walio nambari mbili.
Arsenal, wanaojaribu kushinda taji la Ligi ya Premia mara ya kwanza tangu 2004, watakuwa ugenini dhidi ya Spurs Jumamosi.

Tarehe Wapinzani Michuano
Jumamosi, 5 Machi Tottenham (Ugenini) Ligi ya Premia
Jumanne, 8 Machi Hull (Ugenini) Marudiano (Kombe la FA)
Jumamosi, 12 Machi West Brom (Nyumbani) Ligi ya Premia
Jumatano, 16 Machi Barcelona (Ugenini) Champions League last 16
Jumamosi, 19 Machi Everton (Ugenini) Ligi ya Premia
Jumamosi, 2 Aprili Watford (Nyumbani) Ligi ya Premia

Saa zinazoweza kutumiwa kuiba mitihani

saa
Saa za kisasa ambazo zimetengenezwa mahususi kutumiwa kudanganya wakati wa mtihani zimekuwa zikiwakosesha usingizi walimu na wasimamizi wa mitihani.
Saa hizo zina uwezo wa kuweka akiba data na maelezo ambayo yanaweza kusomeka mtu anapofanya mtihani.
Aidha, zina kitufe cha dharura ambacho kinaweza kubadili uso wa saa hizo haraka sana na badala ya kuonesha habari ziwe zinaonesha uso wa kawaida wa saa.
Saa hizo zinatangazwa katika soko la kuuza bidhaa mtandaoni la Amazon.
Mojawapo ya aina ya saa hizo ina uwezo wa kuweka akiba data ya 4GB. Nyingine, ambayo itaanza kuuzwa baadaye mwaka huu, itakuwa na uwezo wa 8GB na inaweza kuhifadhi hata video.
Baadhi ya saa hizo, zina kifaa kidogo sana cha kusikizia ambacho hakitumii nyaya, jambo linalowezesha mtu kusikiliza kilichohifadhiwa kwenye saa hiyo bila kuonekana.
Tangazo moja katika mtandao wa Amazon linasema mtu anaweza kununua saa ya aina hiyo kwa $61 (£43).
Kuna pia matangazo ya saa hizo eBay.
Naibu mwalimu mkuu wa shule moja kutoka Bath, Uingereza anasema saa hizo zinaweza zikawashawishi wanafunzi kuhadaa katika mtihani.
Bw Joe Sidders wa shule ya Monkton Combe Senior School amesema ingawa saa hizo zinaweza kudhibitiwa kwa kutumia sheria zinazoharamisha simu na kompyuta kutoka vyumba vya mitihani, ni changamoto kubwa sana kwa watu wanaosimamia mitihani.
Amesema uuzaji wa saa hizo unafaa kudhibitiwa.
Kuna pia “kalamu za kuiba mtihani” ambazo zinaweza kuhifadhi habari na maelezo.
Ongezeko la matumizi ya saa kuiba yamefanya baadhi ya mashirika kupiga marufuku saa katika vyumba vya mitihani Uingereza.

04 March, 2016

Movie: London Has Fallen

Storylines  After the British Prime Minister passes away, his funeral becomes a target of a terrorist organization to destroy some of the world’s most powerful leaders, devastate the British capital, and unleash a terrifying vision of the future. The only hope of stopping it rests on the shoulders of the President of the United States (Aaron Eckhart) and his formidable Secret Service head (Gerard Butler), and an English MI-6 agent (Charlotte Riley) who rightly trusts no one. Morgan Freeman also stars as the Vice President of the United States.

click for larger (if applicable)                  Watch The Trailar

Hii hapa ndiyo orodha ya Fifa ya mataifa bora Afrika Machi:

Cape
Cape Verde wametua kileleni mwa orodha ya Fifa ya uchezaji kandanda barani Afrika ya mwezi Machi.
Huo ni ufanisi mkubwa kwa taifa hilo linalojumuisha visiwa kadha vidogo kaskazini magharibi mwa Afrika.
Wamefanikiwa kuwapita mabingwa wa Afrika wa mwaka 2015 Ivory Coast ambao wameshuka hadi nambari mbili.
Cameroon pia wameimarika, na kuingia katika orodha ya 10 bora na kuwaondoa Guinea.
Licha ya kushinda Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wameshuka nafasi moja hadi nambari 58.
Miongoni mwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uganda inaongoza ikiwa nambari 67, ikifuatiwa na Rwanda (85), Kenya (103), Tanzania (125), Burundi (129) na Sudan Kusini (140).
Mataifa yanayoshika mkia Afrika n Somalia, Eritrea na Djibouti, yote yakiwa nambari 204.
Duniani, Ubelgiji wanaongoza wakifuatwa na Argentina.

Hii hapa ndiyo orodha ya Fifa ya mataifa bora Afrika Machi:

  1. Visiwa vya Cape Verde
  2. Ivory Coast
  3. Algeria
  4. Ghana
  5. Tunisia
  6. Senegal
  7. Misri
  8. DR Congo
  9. Congo
  10. Cameroon

Orodha ya 10 bora duniani

  1. Ubelgiji
  2. Argentina
  3. Uhispania
  4. Ujerumani
  5. Chile
  6. Brazil
  7. Ureno
  8. Colombia
  9. England
  10. Austria

Magazetini Leo ijumaa march 4,2016

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...