04 December, 2015

Filamu ya uchumba wa Obama kutolewa 2016

Obama
Filamu ya ucheshi kuhusu mkutano wa kwanza wa kuchumbiana kati ya Barack Obama na Michelle ni miongoni mwa filamu ambazo zitaonyeshwa kwenye maonyesho ya filamu ya Sundance 2016.
Filamu hiyo kwa jina Southside With You inaigiza yaliyojiri adhuhuri moja majira ya joto 1989 pale Obama alipomchumbia mkewe wa baadaye Michelle Robinson, mjini Chicago.
Filamu nyingine zitakazoonyeshwa ni Swiss Army Man, ambapo mwigizaji mashuhuri Daniel Radcliffe anaigiza kama maiti.
Makala ya 2016 ya maonyesho ya Sundance yatafanyika 21 hadi 31 Januari katika Park City, Utah.
Maonyesho hayo yaliasisiwa na mwigizaji Robert Redford.
Tika Sumpter anaigiza Michelle naye Parker Sawyers Bw Obama.

Uchina kutoa dola bilioni 60 kwa Afrika

Uwekezaji wa Uchina Afrika
Rais wa Uchina Xi Jinping amesema taifa lake litatoa ufadhili wa dola bilioni 60 kwa nchi za Afrika.
Tangazo hilo amelitoa kwenye mkutano mkuu wa ushirikiano kati ya Uchina na nchi za bara Afrika, ambao umeanza leo jijini Johannesburg. Viongozi kadha wa mataifa ya Afrika wanahudhuria.
Tangazo la fedha hizo za mabilioni ya dola ambazo zitatolewa kupitia ruzuku, mikopo na ufadhili wa miradi ya maendeleo lilisubiriwa, lakini kiasi cha fedha kilichoahidiwa kimezidi matarajio, mwandishi wa BBC aliyeko Afrika Kusini Karen Allen anasema.
Sehemu kubwa ya usaidizi huu wa kifedha sana utatolewa kupitia miradi ya miundo mbinu, kusaidia kusisimua ukuaji wa kiuchumi, lakini maelezo zaidi hayajatolewa.
Kiongozi mwenza wa mkutano huo Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amesifu ushirikiano kati ya Uchina na nchi za Afrika.
Amesema watu wanaoishi Uchina na Afrika ni theluthi moja ya watu wote duniani, na kwamba hilo ni soko kubwa la bidhaa.
Uchina, nchi yenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani, imetoa msururu wa mikopo kwa nchi za Afrika, ambazo nazo huuzia taifa hilo mafuta na bidhaa nyingine muhimu.
Hata hivyo, idadi ya bidhaa ambazo mataifa hayo huuzia Uchina imekuwa ikipungua.Xi na Zuma
Uwekezaji wa Uchina Afrika ulishuka asilimia 40 nusu ya kwanza ya mwaka huu, kwa mujibu wa wizara ya uchumi ya Uchina.
Ziara ya Bw Xi barani Afrika imetazamwa na wengi kama hatua ya kuyahakikishia mataifa ya Afrika kwamba Uchina itaendelea kuwekeza katika bara hilo licha ya kupungua kasi kwa ukuaji wa uchumi wa Uchina.
Mapema wiki hii Uchina na Afrika Kusini zilitia saini mikataba na mikopo ya thamani ya $6.5bn (£4.3bn), inayoangazia zaidi miundo mbinu.
Jumla ya mikataba 26 ilitiwa saini Jumatano, $2.5bn zikienda kwa shirika la reli la serikali.Kabla ya kutua Afrika Kusini, Bw Xi alizuru Zimbabwe Jumanne, ambako pia aliahidi taifa hilo mikopo ya kusaidia kuinua uchumi wake uliodorora.

Kasi ya Rais Magufuli Haiko Kwenye Makontena Bandarini tu, imepita na TFF Ambapo TRA Imesitisha Safari Ya Timu Ya Taifa Ya Vijana


Ikiwa bado siku moja Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli atimize mwezi mmoja toka aapishwe kuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, tumeshuhudia mengi yakitokea katika suala zima la upambanaji na watu wanaokwepa kodi sambamba na kusimamishwa kazi kwa viongozi kadhaa wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) waliopo Bandarini.

December 4 kasi ya Rais John Pombe Magufuli inaonekana kuwashitua viongozi wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), kwani wameanza harakati za kuwaadhibu watu wanaodaiwa kodi.

Juma lililopita Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liliaga timu ya Taifa ya Vijana Chini ya umri wa miaka 15 (U15) ikianza ziara yake ya Afrika Mashariki kuanza kucheza na Burundi mjini Kigoma na baadaye Kigali, Rwanda, Kampala, Uganda na mwisho Nairobi Kenya.

Bahati mbaya ziara hiyo itaishia Mwanza na Kigoma kufuatia Mamlaka ya Mapato Tanzani (TRA) kuizuia account ya shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) kwa kushindwa kulipa kodi ya Tsh bilioni  1,637,334,000 (bilioni 1.6 tshs) ikiwa ni kodi kwa kipindi cha 2010 – 2013

Sehemu kubwa ya kodi hiyo ni makato kwenye mishahara (PAYE) ya walimu wa kigeni, Jan Poulsen, Kim Poulsen na Jacob Michelsen na vilevile kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye mchezo wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) dhidi ya Brazili uliofanyika mwaka 2010.

Walimu wa Timu za Taifa wamekuwa wakilipiwa mishahara na Serikali na hivyo TFF haikuwajibika kuwakata kodi. Aidha, mchezo kati ya Tanzania na Brazil ulisimamiwa na kamati maalum ya Serikali na fedha zake hazikuingizwa katika akaunti za TFF.

Kutokana na hatua hii ya TRA shughuli nyingine za mpira zitakazohathirika  ni:

1. Kulipia madeni ya usafiri, chakula na posho za Timu za Taifa zilizoshiriki mtoano wa kombe la Dunia na mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (Challenge Cup)

2. Program za mpira wa Wanawake na vijana zitalazimika kusimama.

3. Mashindano ya kombe la Shirikisho raundi ya pili iko kwenye hatihati kwani hakuna fedha za kugharimia michezo hiyo.

4. Mashindano ya Ligi Daraja la Pili (SDL) inayoendelea yatalazimika kusimama vilevile. Mashindano haya TFF imekuwa ikiyaendesha bila mdhamini.

5. Vifaa vya michezo (Mipira) kwa ajili ya shule za msingi na vituo vya maendeleo (Regional Football Development Centres) vinatarajiwa kuwasili nchini wakati wowote na TFF haitakuwa na uwezo wa kulipia usafirishaji na ushuru wake.

6. Malipo ya gharama za kambi na karo kwa ajili ya vijana wa timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 13 walioko shule ya Alliance Academy ya jijini Mwanza.

7. Huduma za kiutawala ikiwa ni pamoja na utunzaji viwanja na majengo, maji, umeme, ulinzi pamoja na mishahara na stahiki nyingine za wafanyakazi

8. Mwelekeo na mwitikio mzuri wa wadhamini uko kwenye hatari ya kupotea pindi mashindano na shughuli wanazozidhamini zitakapofubaa au kusimama kabisa.

9. Mkutano Mkuu wa kawaida wa Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) wa Mwaka 2015 uliopangwa kufanyika Tanga 19-20 Desemba 2015 sasa una hatihati ya kuweza kufanyika.

Hata hivyo, kwa kutambua umuhimu wa ulipaji kodi na wajibu wa Mamlaka ya Mapato katika kuhakikisha kodi inakusanywa kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya Taifa,TFF ipo katika mawasiliano na TRA katika kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa suala hili ikiwa ni pamoja na kupitia upya mahesabu ili kujua wajibu halisi (net liability) wa TFF na namna ya kulipa au kulipwa kutegemea ulali wa mahesabu.

Kwa taarifa hii TFF inaomba utulivu kwa wanamichezo wote pamoja na ushirikiano wa karibu kutoka katika vyombo vyote husika ikiwemo TRA na wadau wengine ili jambo hili lipate ufumbuzi wa kudumu utakaoleta tija kwa serikali ya awamu ya tano ikiwa ni pamoja na kuongeza uwekezaji katika maendeleo ya mpira wa miguu na michezo kwa ujumla wake.

Rick Ross asema afurahishwi na mambo ambayo Birdman anamfanyia Lil wayne


Rick Ross ni mmoja ya watu ambao hawafurahishwi na mambo anayokumbana nayo Lil wayne chini ya uongozi wake wa Cash Money.

Akifanya mahojiano na kipindi cha The Breakfast Club, Rick Ross amefunguka kuhusiana na wimbo wake wa ‘Colour Money’ ambao unamashairi ambayo yametafsiliwa kama diss ambayo inaweza kuwa imekwenda kwa Lil wayne au Birdman ,  mashairi hayo yanayosema
“So run Forest got some shooters and they dying too / I got more money than that pussy that you’re signed to,”
Alipoulizwa kuhusiana na mistari hiyo iwapo aliirenga kwa Lil wayne au Birdaman, Rick Ross alisema Lil wayne ni rafiki yake na alikuwa nae siku chache zilizopita hivyo kuonesha moja moja kuwa maneno hayo yalimrenga Birdman
“Weezy my homie. I was just with Weezy the other night in the club, he was just on the remix with me. J Prince that’s my big homie.” Alisema Rick Ross
Pia aliongeza kuwa hana uhusiano wowote Birdman na hafurahishwi na vitendo anamvyomfanyia Lil wayne
“Right now, really me just seeing what Wayne going through as an artist, me idolizing Birdman at a time, me looking up to Lil Wayne, Wayne being the first artist making to make so many feats not just as an artist but an artist coming through the South, that’s something I took personal. For me to see the way things are transpiring, I can’t respect that, and I don’t respect that.” Alifunguka Rick Ross aka Young Renzel
Miezi michache Lil wayne alijitokeza na kufunguka kuwa uongozi wake ulikua haumtendei haki na alionesha nia ya kuondoka kwenye label hiyo ambayo ipo chini ya Birdman.

Polisi wa Nigeria wampa shavu la ubalozi Korede Bello wa Godwin.

korede bello Godwin7
Msanii wa Mavin Records “Korede Bello” ametajwa kuwa msanii wa kwanza nchini Nigeria kuwa balozi wa kwanza wa vijana kwa Polisi.
Mwaswali mengi yameibuka kuhusu yeye kuchaguliwa kupewa nafasi hio na kazi ambayo atakuwa akifanya, Kuna uvumi kuwa atakuwa akisambaza ujumbe wa amani na utulivu kwa vijana, kupunguza uhalifu na vibaka mtaani.
Korede Bello amehit hivi karibuni na wimbo wake wa Godwin na anamiaka miwili kwenye sanaa Nigeria.
 Korede-Bello 2 Korede-Bello

Bobby Shmurda akosa dhamana ikiwa ni jaribio la sita toka ameingia jela December mwaka jana.

schmurda
Rapa Bobby Shmurda amekosa dhamana tena ikiwa ni jaribio la sita toka ameingia jela December mwaka jana.
Mwanzoni mwa wiki hii palikuwa na taarifa kuwa mawakili wa Bobby walitayarisha sababu “bulletproof” zakumpa dhamana rapa huyu ambaye dhamana yake ni dola milioni 2.
Bobby Shmurda alikuwa jela toka december mwaka jana akikabiliwa na kesi ya kukutwa na silaha kinyume cha sheria, kupanga mauwaji na kukamatwa na dawa za kuleya.
Bobby Shmurda atakuwa mahakamani tena Jan 11 2016

Mwanamke aliyekataa matibabu ya figo kuokoa maisha yake akidai amepoteza mng’ao afariki

post-feature-imageMwanamke aliyekataa matibabu ya figo kuokoa maisha yake nchini Uingereza, akisema ameshapoteza mng’ao, amefariki. Mwanamke huyo wa umri wa miaka 50 aliyetambuliwa tu kama C, aligonga vichwa vya habari baada ya jaji kuamua kwamba ana haki ya kukataa kupokea matibabu ya kusafisha damu.

Figo za C ziliharibika baada yake kunywa dawa kupita kiasi akitaka kujiua. Mahakama iliambia kwamba katika maisha yake, C aliangazia zaidi "sura yake, wanaume na vitu vya thamani.”

Mmoja wa bindi zake aliambia mahakama: “Kupona kwake si kwamba figo zake zianze kufanya kazi tena pekee, bali atahitaji kupata ‘mng’ao’, jambo ambalo anaamini hawezi kuapata tena kutokana na umri wake.”

Mwaka uliopita, C alikuwa amepatikana na saratani ya matiti lakini akakataa matibabu akisema matibabu hayo yangemfanya kuwa mnene.

Baada ya kupata matatizo ya figo, wakfu wa Huduma ya Taifa ya Afya Uingereza katika hospitali ya King’s College ulitaka alazimishwe kupokea matibabu. Lakini Jaji MacDonald, kwenye uamuzi alioutoa Novemba 13, alisema C ana uhuru wa kufanya uamuzi.
House of Entertainment, News, Gossip, Music and Videos!

YANGA YAANZA KUPIGA CHINI WACHEZAJI WAKE, TAYARI MMOJA ATOSWA KIPINDI HIKI CHA DIRISHA DOGO…JE, KUNA WENGINE YATAWAKUTA?

Yanga-Kikosi
Mlinda mlango wa mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara klabu ya Yanga amejikuta hayupo kwenye hesabu za benchi la ufundi kwa ajili ya wachezaji ambao wanahitajika kukitumikia kikosi hicho cha Jangwani.
Mudathir Khamis ametupiwa virago vyake kutoka klabu ya Yanga na tayari amesharejea Zenj kama mchezaji huru na anaweza kujiunga na timu yoyote.
Baada ya kuzagaa taarifa hizo kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii kuwa mlinda mlango wa Yanga Mudathir Khamis ameachwa, mtandao huu leo umemtafuta mchezaji huyo na kusema kuwa amependelea aongee na kocha wake wa zamani wa KMKM Ali Bushir na kumpa taarifa hizo ambapo tayari amemuonesha barua yake.
Tukamtafuta kocha Ali Bushir na kuthibitisha kuwa kweli Muda ameachwa na kikosi cha Yanga.
“Nikweli Mudathir ameachwa na Yanga na mimi leo asubuhi kaniletea barua hiyo ambayo kasaini katibu wa Yanga, nimeipitia barua hiyo ya kusitisha rasmi mkataba na Yanga na kumuwachia awe huru kwenda klabu yoyote, barua hiyo imeandikwa tarehe 21 November ikisema kuwa Mudathir si mchezaji tena wa Yanga”, amesema kocha Bushir.
Aidha kocha Bushir amesema wachezaji lazima wawe makini pale wanaposaini mikataba na timu akiwataka kutafuta wanasheria ambao watawasimamia ili wasije kukosa haki zao za msingi pindi yanapotokea matatizo mengine ya kusitishwa mikataba yao kiholela.
Yanga imeamua kusitisha mkataba na mchezaji huyo mkataba ambao ulikuwa unamalizika mwezi Mei, 2018.

KIBIBI KIZEE CHA TURIN KITAFANIKIWA KUMKAMATA TAI WA ROMA?

lazio vs JuventusHii leo SSC Lazio  watacheza na klabu ya Juventus  katika raundi ya 15 ya Serie A ya msimu wa huu wa 2015/16.Ni mchezo wenye maswali mengi sana kwa kuangalia hali ya timu zote mbili kwa sasa.
Je,Lazio watafuta uteja wa kutoifunga Juventus katika Serie A kwa miaka 12?
Lazio hawafanyi vizuri katika Ligi ya Italia kwa msimu huu kwani wanashika nafasi ya 10 katika Ligi wakiwa na pointi 19 katika michezo 14 waliyocheza mpaka sasa.
Kocha wa Lazio Stefano Pioli yupo katika wakati mgumu sana na inawezekana kufungwa na Juventus  hii leo ikawa mechi yake ya mwisho kuiongoza Lazio msimu huu.
Juventus wanarudi katika mji wa Roma kwa mara ya pili kwani tayari wamekwishacheza katika mji huo dhidi ya AS Roma na Juventus kufungwa magoli 2-0 katika uwanja wa Olimpico.
Safari hii Juventus wataendaje katika mji wa Roma?
Mpaka sasa klabu ya Lazio imepoteza michezo saba ya Ligi kwa msimu huu ambayo ni mingi tofauti na msimu uliopita ambapo timu hiyo ilipoteza michezo 11 tu katika michezo 38 ya Ligi ya Italia.
Kukosekana kwa beki wake wa kati Stefan De Vrij kumeonekana kuwa pengo kwa Lazio kwani mabeki wawili wa kati wa sasa Santiago Gentiletti na Mauricio hawajaweza kutengeneza ushirikiano mzuri ’chemistry’ nzuri baina yao na hivyo  Lazio kuruhusu magoli 22 katika michezo 14 mpaka sasa.
Ubora wa kiungo Lucas Biglia unaweza kuwa chachu ya Lazio kupata matokeo hii leo kwani anaonekana anaweza kupambana na wachezaji wa kariba ya Claudio Marchisio,Stefano Sturaro na Mario Lemina.
biglia 1Biglia ni mfungaji bora namba mbili kwa upande wa Lazio akiwa na magoli matatu huku Felipe Anderson akishika nafasi ya kwanza kwa kufunga magoli manne.
Lakini pia Biglia ndiye mchezaji aliyepiga pasi nyingi sahihi ‘complete pass’ kwa Lazio kutoka eneo moja la uwanja kwenda eneo lingine la uwanja akiwa na asilimia 81.6 ya kupia pasi sahihi.
Silaha nyingine ya Lazio itakuwa kwa mshambuliaji raia wa Brazil  Felipe Anderson ambaye ameonekana kuwa muhimili kwa Lazio hasa katika ushambuliaji.
Felipe Anderson ana magoli 4 mpaka sasa katika Serie A ingawa tatizo lake kubwa ni kuwa hana muendelezo mzuri wa uchezaji wake na hii imekuwa ikiwapa Lazio wakati mgumu sana kupata matokeo kutokana na ubutu wa safu yao ya ushambuliaji.
Miloslav Klose hayupo katika fomu yake lakini pia nyota wengine wa  Lazio kama Eddy Onazi ,Stefano Mauri na Senad Lulic wataendelea kukosekana hii leo kwa sababu ni majeruhi.
Jambo la kusikitisha kwa upande wa klabu ya Lazio ni kuwa klabu hiyo imepata ushindi wa Serie A mara ya mwisho tarehe 25/10/2015 katika mchezo dhidi ya Torino kwa  ushindi wa magoli 3-0.
Baada ya hapo Lazio haijashinda mchezo wowote wa Ligi Kuu ya soka nchini Italia mpaka sasa.
Kwa upande wa Juventus hakuna shaka kuwa fomu ya Paulo Dybala mwenye magoli 6 na asisti 3 imeifanya safu ya ushambuliaji ya Juve kuwa na makali kwa siku za hivi karibuni.
Kwani Juventus imeshinda michezo minne iliyopita ya Ligi ya Italia ikifunga magoli 9 na kufungwa magoli 2 tu.
Hapo kabla kocha wa Juventus Allegri hakuonekana kumpa nafasi Dybala huku akijitetea kuwa mchezaji huyo bado hajakomaa kuweza kuanza kikosi cha kwanza.
paulo dybala 1Lakini hali imekuwa tofauti kwani Dybala amekuwa msaada mkubwa kwa Juventus kwa sasa na anamuweka benchi hata mshambuliaji bora wa Juventus kwa msimu uliopita Alvaro Morata.
Kutokuwepo kwa Paul Pogba katika mchezo wa kesho kunaweza kumpa nafasi  kiungo Stefano Sturaro kucheza sambamba na Claudio Marchisio na Mario Lemina.
Kiungo Sami Khedira hajasafiri na timu na badala yake kiungo wa timu ya taifa ya Ghana Kwawdo Asamoah amejumuishwa katika kikosi kilichosafiri kwenda kucheza na Lazio leo.
Msimu uliopita Juventus walipata ushindi wa magoli 3-0 mbele ya Lazio katika uwanja wa Olimpico.Mara ya mwisho kwa Lazio kushinda mchezo wa Ligi kuu ya Italia dhidi ya Juventus ilikuwa tarehe 6 Desemba mwaka 2003 waliposhinda kwa magoli 2-0.
Magoli ya Lazio ya wakati huo yalifungwa na Bernardo Corradi na Stefano Fiore.
Naamini mashabiki wa soka wana kila sababu ya kuutazama mchezo huu na kujua kama Juventus imerudi katika makali yake au itakuwa ndio mwisho wa kocha wa Lazio Stefano Pioli.

Benitez hali tete – Madrid waondolewa Copa Del Rey kwa uzembe wake

Wakati kukiwa na presha ya kuhakikisha timu yake inapata matokeo chanya, baada ya mfululizo wa matokeo mabaya katika La Liga, Hali inazidi kuwa tete kwa kocha Rafael Benitez baada ya maamuzi yake katika upangaji wa kikosi kuiponza Madrid kuondolewa katika michuano ya Copa Del Rey.
  Kwa mujibu wa taarifa kutoka gazeti la AS, miamba hiyo ya La Liga, imeondolewa kwenye Copa Del Rey baada ya kumchezesha mchezaji aliyefungiwa Dennis Cheryshev katika mechi ya michuano hiyo dhidi ya timu ya daraja la pili Cadiz, jumatano iliyopita.
  Cheryshev alifunga goli la kwanza katika mechi ya ushindi vs Cadiz kabla ya kutolewa baada ya Madrid kuwaambiwa walikuwa wamecheza ‘blunder’ kumchezesha Cheryshev ambaye alikuwa na kadi – ambazo alipata wakati akiwa kwa mkopo Villareal, hata hivyo Madrid wamejitetea kwamba hawakuwa wamepewa taarifa juu ya zuio hilo kwa mchezaji wao – lakini Fransico Rubio, mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya soka Hispania amegoma kusikiliza utetezi huo wa Madrid.
Madrid pia wanaamini kwamba mchezaji husika ilibidi ataarifiwe juu ya kufungiwa kwake kabla ya mchezo na sasa inaonekana wazi klabu hiyo itakata rufaa juu ya uamuzi huo baada ya Raisi wa klabu hiyo Florentino PĂ©rez alisema jana kwamba wanaangalia uwezekano wowote wa kisheria ili kesi hiyo washinde.
Uamuzi huu wa kamati ya mashindano umezidi kumeongezea presha kocha Rafael Benitez ambaye wadau wengi wamekuwa wakimlaumu kwa uamuzi wa kunchezesha Cheryshev bila kuangalia kama hakuwa na shida yoyote.

LA LIGA KUTANGAZWA KWA KUTUMIA LUGHA YA KISWAHILI

la ligaDstv Tanzania inaendelea kuleta huduma mpya kwa wateja wake kama ilivyo kawaida yake. Hivi sasa wameanzisha huduma mpya ambapo mechi za La Liga zitaonyeshwa Live na watangazaji watakua wanatangaza kwa kutumia lugha ya kiswahili.
Kama lugha ilikua tatizo wakati una enjoy mechi basi usiwe na wasiwasi tena kwasababu Dstv wameshamaliza hilo swala. Lugha ya taifa sasa itatumika kutangaza mechi za La Liga.
Hizi hapa ni baadhi ya mechi ambazo zitaanza kutangazwa kwa lugha ya kiswahili kuanzia kesho Jumamosi tarehe 5/12/2015
Saturday 05/11
Real Madrid vs Getafe
Ch – SS7
On Air – 16:55
Kick off – 17:00 sast
Valencia vs Barcelona
Channels – SS5A
On air time – 21:15 sast
Kick off – 21:30 sast
Sunday 06/11
Villareal vs Rayo Valleccano
Channels – SS5A
On air time – 16:55 sast
Kick off – 17:00 sast

HIVI NDIVYO SIMON MSUMVA ALIVYOSHEREKEA BIRTHDAY YAKE

msuvaBaada ya kuona picha sasa ni zamu yako kuona video jinsi Simon Msumva alivyosherekea birthday yake pamoja na marafiki zake.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...