15 August, 2015

Zijue Sifa 10 za mgombea urais bora wa upinzani 2015

Lengo la uchambuzi huu ni kuwafanya Watanzania waanze kuwafahamu viongozi wao wajao na hata aina ya sifa wanazoweza kuwa nazo. Inawezekana kabisa kuwa wagombea waliochambuliwa asitokee mmoja wao kugombea au la, lakini hapa ninachoangalia ni kwamba tayari wananchi watakuwa “wamesogezwa karibu na ajenda ya uchaguzi” na hata akiletwa mgombea kutoka wapi, walau wananchi watakuwa wanajua wafanye uamuzi wa namna gani.

Ni jana tu nimemaliza uchambuzi wa watu wanaotajwa au waliojitokeza kugombea urais au wale ambao hawajajitangaza na hawana nia lakini jamii ndani na nje ya vyama vyao inawataja kama watu wenye sifa, uwezo na hata vigezo vya kuiongoza nchi yetu, kutoka vyama vya upinzani.

Lengo la uchambuzi huu ni kuwafanya Watanzania waanze kuwafahamu viongozi wao wajao na hata aina ya sifa wanazoweza kuwa nazo. Inawezekana kabisa kuwa wagombea waliochambuliwa asitokee mmoja wao kugombea au la, lakini hapa ninachoangalia ni kwamba tayari wananchi watakuwa “wamesogezwa karibu na ajenda ya uchaguzi” na hata akiletwa mgombea kutoka wapi, walau wananchi watakuwa wanajua wafanye uamuzi wa namna gani.

Leo nahitimisha hoja ya wagombea wa upinzani kwa kutoa sifa 10 za mgombea urais bora kutoka upinzani ambaye anaweza kupigiwa kura nyingi na Watanzania na hatimaye kuwa rais mpya wa Tanzania:

1. Mwenye umaarufu/umashuhuri na anayekubalika

Sifa hii ni muhimu, unapokuwa nje ya dola na nje ya chama tawala siyo rahisi kukishinda chama kinachoongoza Serikali. Umaarufu, umashuhuri na kukubalika ni mambo ya lazima. Ukitizama historia ya dunia na hata Afrika, vyama vikongwe vilipoondolewa madarakani waliofanya hivyo walikuwa wapinzani mashuhuri. Umuhimu wa sifa hii ni kuwa walau mtu maarufu na mashuhuri au anayekubalika, tayari amewekeza “mbegu” kwenye mioyo ya wananchi, wanaweza kumwamini ili waondoe hatima ya nchi mikononi mwa chama kilichowaongoza kwa miaka 50 na kuiweka mikononi mwa watu wapya. Wananchi wasipomwamini kiongozi wa upinzani anayekuja kwa sababu wanamkubali, ndipo huzuka ile kasumba ya “tupige kura kwenye zimwi likujualo”.

Hatari ya sifa hii

Umaarufu, umashuhuri na kukubalika vitaweza kufanya kazi kwa upinzani ikiwa mgombea husika hatatumia mwanya wa kukubalika kwake kujenga kiburi na hatimaye kuwasaliti wananchi. Ndiyo kusema kuwa vyama vya upinzani vitapaswa kuchagua mtu bora ambaye atatimiza matakwa ya wananchi “hata kama ni maarufu kuliko jua”.

2. Atakayebeba ajenda bora na kuifafanua vizuri

Kubeba ajenda bora na kuwa na uwezo wa kuifafanua kwa lugha rahisi ni jambo la muhimu kwa mtarajiwa kutoka upinzani. Moja kati ya makosa makubwa ya vyama vya upinzani katika bara la Afrika ni kutaka kubeba ajenda nyingi na kumrundikia mgombea urais, nakubali kuwa Afrika ina matatizo katika kila sekta ya maisha ya mwanadamu, lakini lazima iwe na vipaumbele vinavyowaumiza wananchi. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa na ajenda bora kuliko ile ya CCM na atapaswa kuwa na uwezo wa kuifafanua akaeleweka na mipango ya utekelezaji wake ikawa siyo ya “kusadikika”.

Hatari ya sifa hii

Ni pale inapotokea kuwa mgombea bora wa urais kutoka upinzani anazunguka nchi na ajenda iliyo bora kabisa lakini utekelezaji wake ukifanana au kushabihiana moja kwa moja na ule wa mgombea wa CCM. Wananchi wakiona upinzani unahubiri mipango na mbinu zilezile za CCM wataamua pia kuchagua “shetani wanayemjua” ili kujiweka kwenye mazingira ya usalama zaidi. Hivyo, ajenda ya mgombea bora wa upinzani na utekelezaji wake vinapaswa kuwa “vya kipekee”.

3. Mwenye uzoefu na rekodi ya uchapakazi

Uzoefu wa uongozi na uchapakazi unaofahamika ni jambo la msingi kwa mgombea bora wa urais kutoka upinzani. Vyama vya upinzani haviwezi kushinda uchaguzi na mgombea bora vitakayekuwa naye ikiwa mtu huyo si mzoefu na mchapakazi anayefahamika, mtu mwenye kujali wengine katika kazi lakini ambaye wananchi wataamini kuwa huyu atasimama pamoja na sisi usiku na mchana kuleta mabadiliko ya nchi.

Katika siasa, wananchi hupaswa kwanza kuamini na kisha hufanya uamuzi. Ikiwa mgombea bora wa urais wa upinzani hatakuwa na rekodi za uzoefu wa utumishi (katika taasisi za dini, serikali, vyama vya siasa na nyinginezo) si rahisi kumuuza kwa wananchi. Pia, ni lazima awe ni mtu ambaye rekodi zake zinatajwa kuwahi kuleta mabadiliko makubwa mahali alipofanya kazi.

Hatari ya sifa hii

Sifa hii hupaswa kuelezewa na kufahamika kwa wananchi kutoka kwa timu za kampeni za wagombea, wakati mwingine wapambe wa wagombea huchukua muda mwingi kutaja elimu ya mgombea wakidhani wananchi wanachagua elimu, kumbe elimu ni jambo moja tu kati ya sifa 100 za kiongozi. Ikiwa sifa hii muhimu haielezwi kwa uwazi kwa wananchi na hasa kwa kutaja rekodi bora za mgombea wa upinzani, wananchi wanaweza kumpa kisogo.

4. Mwenye uadilifu usio na shaka

Mgombea bora wa upinzani katika uchaguzi, anapaswa kuwa na uadilifu uliotukuka, usio na madoa wala shaka. Hapa nina maana kuwa, awe ni mtu ambaye uadilifu wake unatambulika kwa wananchi na kwa Taifa zima. Awe na rekodi za uadilifu kumshinda mgombea wa CCM, nina maana kuwa, wananchi wakimpima huyu wa upinzani na yule wa CCM – haraka haraka wasimame na kusema, “…naam! Huyu wa upinzani ni mwadilifu zaidi”. Marais wengi walioingia madarakani hasa hapa Afrika na hata Ulaya na Marekani kwa kuviondoa vyama vilivyokuwa madarakani, walipimwa kwa sifa hii.

Hatari ya sifa hii

Kigezo hiki hupata shida kubwa katika nchi ambazo uelewa wa wananchi vijijini na hata mjini si mkubwa. Wagombea waadilifu nao huweza kuchafuliwa ndani ya siku moja tu. Katika nchi ambayo si ajabu mgombea akawa hata na uwezo wa “kuhonga” chombo cha habari ili kimchafue mwenzake, sifa za mgombea bora zinaweza kuingizwa katika tope. Vyama vya upinzani vitapaswa kuwa na mfumo sahihi wa kuhakikisha uadilifu wa mgombea wake unazungumzwa kama ulivyo na haubadilishwi na propaganda za CCM.

5. Mwenye uwezo wa kusimamia, kuinua uchumi

Moja ya matatizo ambayo hayana dawa hapa Tanzania ni usimamizi wa uchumi. Nchi yetu inayumba kila mara na tunashindwa kutekeleza mipango yetu kwa sababu ya uchumi dhaifu, unaobadilika kila dakika na ambao hauna dira. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa na uwezo wa kusimamia na kuinua uchumi wa nchi. Awe ni mtu ambaye akisimama na kuweka ajenda ya uchumi mezani, Watanzania wote wanamwelewa, kwamba “naam, huyu ana uwezo wa kusimamia uchumi na kuondoa umaskini wa nchi”.

Hatari ya sifa hii

Ni pale mgombea wa upinzani atazunguka na mipango kabambe ya uchumi lakini yenye shaka kubwa kwenye utekelezaji au kuondoa umaskini, lakini pia ni pale mipango hiyo haitakuwa ya muda mfupi. Katika nchi maskini, wananchi wanahitaji matokeo haraka, vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kuwa na mipango ya mfano ya muda mfupi ili kuwahakikishia wananchi kuwa ile ya muda mrefu pia itaweza kutekelezeka kwa wakati

6. Kuongoza mapambano dhidi ya rushwa

Rushwa ni adui wa haki na ni tatizo kubwa katika ukuaji wa uchumi wa Afrika. Mgombea bora wa urais kutoka upinzani atapaswa kuwa mtu wa kipekee ambaye moja ya sifa zake kuu ni mapambano dhidi ya rushwa, ndogo na kubwa. Awe ni Mtanzania ambaye si tu kwamba anapiga vita rushwa, bali anawachukia wala rushwa kama “kifo” na ni mtu ambaye yuko mbali kabisa na wala “rushwa”. Ndani ya CCM kwenyewe nadhani watatafuta mgombea wa namna hii ili kulinda hadhi yao, vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kutafuta mpinga rushwa mahiri kuliko yule wa CCM, kwamba ukiwaweka pamoja hawa wawili – wananchi wenyewe waseme “…naam huyu wa upinzani anaweza mapambano haya zaidi kuliko huyu wa CCM”

Hatari ya sifa hii

Ikiwa upinzani utakuwa na mtu mashuhuri katika mapambano ya rushwa lakini ukawa hauna mipango ya kuhuisha haraka mifumo inayoleta mianya ya rushwa ndani ya nchi. Ndiyo kusema kuwa moja ya mipango ya upinzani inapaswa kuwa ni pamoja na kuweka wazi mifumo mipya ya usimamizi wa mapambano dhidi ya rushwa na hata kueleza watu watakaokuwa na sifa za kufanya kazi na mifumo hiyo.

7. Asiyependa kulipiza visasi na atakayefuata sheria

Jambo hili si dogo katika siasa. Rais ajaye kutoka upinzani anapaswa kuwa na sifa hii. Kwamba afahamike na kujulikana kwa kutokuwa na tabia ya kulipiza visasi lakini ambaye atazingatia matakwa ya sheria katika utendaji na awe na rekodi hizo. Unajua, kuna mambo ya kisheria ambayo ni lazima rais yeyote yule akiingia lazima ayafuate, mfano, wizi wa pesa za umma, hata kama umefanywa mwaka 1960 na ushahidi upo, lazima watuhumiwa wachukuliwe hatua leo, “jinai haifi wala kupotea”. Lakini kuna masuala mengine mengi tu ya kawaida ambayo yalikuwa yanatendwa na uongozi uliopita kwa sababu “za kipuuzi” na zisizo na maana, hayana haja ya kuwa kichwani kwa rais anayekuja.

Hatari ya sifa hii

Wananchi wengi huhofia masuala ya usalama iwapo vyama vipya vitaingia madarakani, hasa Afrika na moja ya masuala ambayo hupoteza usalama ni “kulipiza visasi”. Ndiyo maana vyama vya upinzani vinawajibika kuwa na mgombea ambaye hatalipiza visasi kwa makosa ya nyuma ya kiutendaji, ila atafanya hivyo kwa yale yaliyokosewa kwa makusudi na kwa kutofuata sheria.

8. Uwezo wa kubadilisha mfumo wa nchi

Tangu tumepata uhuru, nchi yetu imekuwa inasifika kwa kuwa na mifumo mibovu na isiyo na tija katika kila sekta. Hili ni janga kubwa. Rais bora ajaye kutoka upinzani ana kazi kubwa ya kubadilisha mfumo wa sasa wa nchi katika kila eneo ili mifumo ifanye kazi kwa mbio na kwa tija kubwa zaidi. Leo kuna watu walishtakiwa miaka ya 1990 na bado wako gerezani bila kuhukumiwa, kuna Kiwanda cha Sukari Kilombero na huko bei ya sukari ni kubwa kuliko Dar es Salaam. Haya ni matatizo makubwa ya kimfumo. Wananchi watahitaji kuwa na kiongozi ambaye atakuja kubadilisha kabisa mifumo ya utendaji kazi katika nchi. Kwa bahati nzuri, upinzani unaweza kuwa na hoja kama hii kwani vyama hivyo havikuwahi kuongoza Serikali na vimekuwa “waathirika” wa mfumo uliopo.

Hatari ya sifa hii

Ubadilishaji wa mifumo ukifanywa haraka na kwa pupa, utaingilia na kuvunja hata mifumo ambayo ilikuwa imeanza kukua na kukomaa kwa upande chanya. Ni jukumu la mgombea bora wa upinzani na timu zake kutambua mifumo yote ya utendaji katika sekta za jamii na kubainisha tangu wakati wa kampeni, ipi itavunjwa na ipi itarekebishwa ili kutoleta hofu yoyote kwa wapiga kura.

9. Msimamo unaoeleweka juu ya Katiba

Suala la katiba mpya ni ajenda muhimu katika uchaguzi wa mwaka huu. Mgombea bora wa upinzani atapaswa, yeye mwenyewe kuwa na busara za kutosha na msimamo thabiti juu ya masuala ya kikatiba na hasa mchakato wa Katiba Mpya. Naona kuna Watanzania wengi watapiga kura katika uchaguzi wa mwaka huu kwa chama au mgombea ambaye atakuwa na misimamo ya wananchi katika suala la katiba. Hadi sasa hatuelewi kama katiba itapitishwa au la na hatuelewi kama wananchi wanaikubali au wanaikataa. Nani atatuvusha na kwa utaratibu gani? Majibu atakuwa nayo mgombea bora wa urais kutoka upinzani.

Hatari za sifa hii

Msimamo wowote ule wa mgombea urais wa upinzani katika jambo hili unaweza kuwa na athari chanya au hasi kulingana na namna wananchi wanavyolitazama suala la katiba. Kama mgombea huyu atakuwa na msimamo katika kuikataa Katiba Inayopendekezwa na kwamba ataanzisha mchakato mpya na ikiwa hayo ndiyo matakwa ya wananchi walio wengi, jambo hili peke yake litamuongezea kura za kutosha. La ikiwa kinyume chake, litakuwa na athari ya kiwango hichohicho bila kujali kama athari yenyewe ni chanya au hasi.

10. Uzoefu wa masuala ya kimataifa

Moja ya kazi kubwa za mkuu wa nchi ni kuliwakilisha Taifa katika masuala ya kimataifa. Rais bora kutoka upinzani hakwepi kuwa na rekodi imara ya masuala ya kimataifa, si kuishi Ulaya na Marekani, lakini kuwe na ushahidi wa kutosha kuwa amewahi kushiriki katika baadhi ya shughuli muhimu za kimataifa na kwamba huenda hata kimataifa yeye ni mtu bora. Nadhani CCM inaweza kuwa na mgombea mwenye sifa hii pia, ni jukumu la upinzani pia kuwa na mtu ambaye amejipanga vyema kimataifa na mambo aliyoyasimamia kimataifa pia yanajulikana, si lazima yawe ya kiserikali, yanaweza kuwa ya kijamii, ya kitaasisi au ya kitaaluma.

Hatari ya sifa hii

Sifa hii inaweza kufanywa moja ya propaganda za kuisaidia CCM, kwamba ndicho chama pekee chenye watu waliofanya kazi za kimataifa na wataifanya Tanzania ikubalike kimataifa. Vyama vya upinzani vitakuwa na jukumu la kupambana na propaganda hii kwa kuwa na mgombea ambaye tayari wananchi wanatambua kuwa ana uzoefu wa kimataifa usio na shaka ili kusiwe na tabu ya kuanza kumwelezea muda mrefu kwa wapigakura juu ya eneo hili.

HITIMISHO

Andiko hili peke yake haliwezi kujadili sifa zote muhimu za kiongozi bora kutoka vyama vya upinzani anayeweza kulivusha Taifa. Nimechokoza mjadala wa masuala muhimu tu. Tukumbuke kuwa, kazi ya kuongoza Serikali si nyepesi, inataka kujipanga kila idara na kuwathibitishia wapigakura kuwa mnaweza bila shaka. Tabia ya wapigakura huwa ni kutafuta namna gani watawaamini watu wanaowapa madaraka. Bahati nzuri vyama vya upinzani katika Taifa letu vimekwishafanya kazi ya kupigiwa mfano inayothibitisha, uzalendo, uadilifu, uzoefu uwajibikaji na utendaji kazi bora.

-Mwananchi

Lipumba Asisitiza kutokubaliana na uamuzi wa Ukawa kumsimamisha Lowassa kugombea urais

Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba alirejea nchini jana jioni akitokea Kigali, Rwanda alikokwenda mara tu baada ya kujiuzulu wadhifa huo siku nane zilizopita.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Rwanda

Profesa Lipumba aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) saa 10.10 jioni kwa ndege ya Rwanda Air.

Akihojiwa na Azam Tv kwa simu akiwa Kigali, siku tatu baada ya kuondoka nchini, Profesa Lipumba alisema alikuwa nchini humo akifanya utafiti kuona namna gani Tanzania inaweza kujifunza mambo ya kiuchumi kutokana na nchi hiyo kupiga hatua kubwa katika sekta hiyo.

Alipoulizwa jana, Profesa Lipumba alisema akiwa huko alikuwa na mazungumzo na Bodi ya Maendeleo ya Rwanda (RDB), wadau wa masuala ya rushwa, waziri wa fedha wa nchi hiyo na makamu mwenyekiti wa Bodi ya Utawala.

“Wenzetu wamepiga hatua kubwa katika kukuza uchumi ndani ya kipindi kifupi, hivyo safari yangu ilikuwa ya kujifunza mbinu walizotumia kufikia malengo yao,” alisema.

Akizungumzia hatima yake kisiasa, licha ya kusema ataendelea kuwa mwanachama wa CUF, alisema hatashiriki kufanya kampeni kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuwa umoja huo umemsimamisha mwanachana wa CCM, Edward Lowassa.

“Kisiasa hatima yangu ni kama ya Mtanzania mwingine yeyote, Ukawa tuna mgombea kutoka CCM, amehama juzi tu, pia mle ndani ya Bunge la Katiba hakuunga mkongo Rasimu ya Katiba na ndiyo maana nikasema dhamira yangu inanisuta,” alisema Profesa Lipumba.

Alisema wanachama wa CUF hawana sababu ya kuona kama amewaacha kwa kuwa bado yupo nchini.

Awali, akitangaza kujiuzulu, nguli huyo wa uchumi, alisema alifikia uamuzi huo kutokana na Ukawa kumkaribisha Lowassa kugombea urais kupitia umoja huo, hivyo dhamira yake inamsuta.

Membe afunguka kuanguka urais CCM

Tangu ashindwe kwenye kura hizo mapema mwezi uliopita, waziri huyo hakuwahi kuzungumzia kuanguka kwake, lakini jana aliweka bayana hisia zake.

Waziri wa Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amezungumzia kinyang’anyiro cha urais ndani ya CCM, akifananisha kushindwa kwake na kifo cha ghafla.

Akizungumza jana kwenye kongamano la Diaspora, Membe ambaye alivuka hatua ya awali ya mchujo akiwa mmoja wa watu watano ambao majina yao yalipelekwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM, alishika nafasi ya mwisho kwenye kura akiwa nyuma ya Dk John Magufuli, Balozi Amina Salum Ali, Dk Asha-Rose Migiro na January Makamba.

Tangu ashindwe kwenye kura hizo mapema mwezi uliopita, waziri huyo hakuwahi kuzungumzia kuanguka kwake, lakini jana aliweka bayana hisia zake.

“Kwenye mpira unaweza kupata timu nzuri sana inacheza kwenye ligi, ikafanya vizuri,” alisema.

“Lakini mwishoni inapotoka droo (sare) na timu nyingine, timu zinakwenda kwenye penalti. Sasa inaweza kutokea ikafungwa penalti zote tano na timu nyingine ambayo wewe hukutegemea ikashinda vizuri tu.

“Kwenye lugha ya kimichezo, kile kitendo cha timu iliyocheza vizuri ikashindwa kwenye penalti, maana yake inakufa kifo kinachojulikana kama sudden death (kifo cha ghafla). Inapopata sudden death, huitegemei isimame na kueleza kilichotokea.”

Membe alikuwa anaonekana kuwa mmoja wa makada waliokuwa wakipewa nafasi kubwa ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kwenye urais, lakini alianguka vibaya kwenye kura za wajumbe wa Halmashauri Kuu.

Kuhusu kongamano hilo la siku tatu alilofungua kwa niaba ya Rais Jakaya Kikwete, alisema licha ya kuwa anakaribia kuondoka madarakani atahakikisha anaendelea kupambana ili Watanzania wanaoishi nje wapate uraia wa nchi mbili.

“Ndipo tutakapopata maendeleo ya kweli ya wanadiaspora. Wanadiaspora watakuwa na kazi nzuri watakapokuwa nchi za nje na watakuwa wanaingiza mabilioni ya fedha nchini kama ilivyo kwa Kenya na Nigeria,” alisema.

Alisema hivi sasa Watanzania hao wanashindwa kusafirisha fedha zao kwa wingi nchini kwa sababu wengi wao ‘wamejilipua’ kwa hiyo wanazituma kinyemela, lakini pale watakapopata fedha wakiwa na uraia wa nchi mbili, wataweza kutuma bila kuficha.

“Natoka huku nikiendelea kuamini kwamba diaspora ya kweli ya Tanzania na isiyo na woga wowote ni pale watakapopata pesa za kufurahia uraia wa nchi mbili,” alisema.

Ikimpata straika huyu, Simba Bingwa

SimbaKOCHA wa Simba, Dylan Kerr ametamba kikosi chake kimekamilika kila idara na endapo atapata nafasi ya kumsajili straika mwenye rekodi nzuri, hakuna kitakachoizuia timu yake kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara.
Kerr raia wa Uingereza hakulificha Championi Jumamosi, kwani amesema, kila akikitazama kikosi chake anaona kimekamilika kuanzia mabeki, viungo na hata washambuliaji lakini akagutuka kitu kidogo tu.
“Timu yangu naiona imetimia kila idara, lakini kuna kitu kimoja kinaniumiza kichwa, nacho ni kusajili straika mmoja hatari mwenye uwezo wa kufunga na kutoa pasi za mwisho.
“Tena huyo mchezaji nataka awe na rekodi zilizo wazi kila mmoja ajue, siyo sifa za kuambiwa na watu! Huyo simtaki kabisa kwani hatokuwa na jipya,” alisema Kerr kwa msisitizo.
Ili kuonyesha kwamba hana utani, Kerr alisema: “Nina majina ya mastraika tisa kutoka nchi mbalimbali za Afrika, kati yao ni mmoja tu nitakayemsajili baada ya kuridhika na sifa zake.”
Mastraika hao wanatokea nchi za DR Congo, Rwanda, Nigeria, Zambia, Botswana, Msumbiji, Ghana, Namibia na Afrika Kusini.
Huku akizungumza kwa umakini, Kerr alisema: “Bado naendelea kupitia rekodi ya kila mmoja wao na kujiridhisha na uwezo wao wa kufunga mabao kupitia Mitandao ya Wikipedia na Youtube, nikiridhika nitakuambia nani namsajili.”
Alisema mbali ya uwezo wa kufunga na kutoa pasi za mwisho, straika anayemuhitaji ni mwenye umri usiozidi miaka 28 kwani atakuwa bado na uwezo wa kupambana.
“Mawakala wanaendelea kunitumia majina na video za mastraika na kazi yangu ni kutazama yupi anafanya vizuri, halafu namchagua aliye bora kati yao,” alisema Kerr.
Kwa sasa, safu ya ushambuliaji ya Simba inaundwa na Hamis Kiiza, Mussa Mgosi waliosajiliwa na hivi karibuni na Ibrahim Ajib. Katika mechi sita ilizocheza, Simba imefunga mabao 17 huku washambuliaji hao wakifunga mabao 10. Mgosi na Kiiza wamefunga matatu kila mmoja huku Ajib akifunga manne.

MAKALA : MUZIKI WA DANCE TANZANIA UNAKWENDA WAPI?

Ni jambo lakumshukuru Mwenyezi Mungu Muumba wa ulimwengu yakwamba bado ninaishi na nazidi kudunda. Kwani uliwahi kujiuliza Mungu angetudai kulipia PUMZI tunayotumia tungelipia kiasi gani cha fedha? Hakuna mtu angeweza kulipia ADA hiyo.
   Baada yakusema hayo, leo tuje kwenye MAKALA yetu na Leo nitazungumzia MUZIKI WA DANCE TANZANI. Ni wazi kwamba miaka ya nyuma MUZIKII huu ulitamba sana na kila mahali ulipokua ukikatiza basi sikio lako haikosi kusikia muziki huu ila miaka hii yakizazi kipya MUZIKI WA DANCE umeonekana ukipotea licha ya BENDI tofauti tofauti kuendelea kurudishia uhai muziki huu.
    MARA nyingi nimekuwa nikijiuliza maswali mengi yasiyo na majibu pale ninapowasikia watu ambao naamini hasa ni mashabiki wa muziki wa dansi wakilalamika juu ya kupotea kwa muziki huo, licha ya kuwepo kwa bendi ambazo zinajinadi kupiga aina hiyo ya muziki hivi sasa.

   Pengine wafuatialiji hasa wa muziki huu wanaweza kutambua ukweli wa jambo hili hasa kwa kulinganisha zama hizi na zile za Dar International, Moro Jazz, Cuban Marimba Bend ,Kimulimuli JKT, Tabora Jazz, Nyanyembe Jazz na nyingine nyingi ambapo wanamuziki mahiri kama Marijani Rajabu, Mbaraka Mwinshehe, Juma Ubao,Salum Abdalah, walitamba na kuufanya muziki wa Tanzania kujulikana kimataifa.
   Jambo la kujiuliza hapa ni kwa nini muziki wetu wakati huo ulikuwa unakubalika na jamii yote licha ya kuwa kulikuwa na upinzani mkali kutoka kwa muziki wa Zaire (sasa DRC Congo) ambayo nayo wakati huo ilikuwa na wanamuziki vigogo kama Tabu Ley, Luambo Lwanzo Makiadi (Franco) , Abeti Maskini, Mbilia Mbel, Mpongo Love, n.k.

Ukweli wa hili utaujua ukigundua kuwa wanamuziki wa Tanzania kipindi hicho walikuwa hawapendi kuiga kutoka kwa wageni badala yake walisimama imara kupiga na kuulinda muziki wao, ndiyo maana ilikuwa vigumu kutekwa kimuziki na wageni.

Ukirudi nyuma kidogo miaka ya 80 na 90 kulikuwa na msururu wa bendi za muziki huo hapa nchini ambapo licha ya wingi wake, zilisimama imara na kuendelea kutangaza muziki huu kimataifa zaidi ya ilivyokuwa mwanzo.
   Hakuna asiyefahamu ubora wa Bendi za Vijana Jazz wakati huo ikiwa na Hemed Maneti , Super Matimila chini ya gwiji la muziki Dk Remmy Ongara, DDC Mlimani Park ya Cosmas Chidumule, Juwata Jazz ya TX Moshi William, Tancut Almasi ya Kasaloo Kyanga na Kyanga Songa, Bima Lee ya kina Jerry Nashon ‘Dudumizi’ n.k, bendi ambazo kila moja ilipiga muziki wa dansi wa Tanzania kwa mtindo wa wake lakini bado ukawa juu kuliko ule wa kutoka nje.

Lengo letu hapa si kuzitaja bendi hizo lakini kiukweli nyingi kati ya hizo zilikuwa hazifanyi hata matangazo ya barabarani, lakini wapenzi wake walikuwa wanajua mahali ambapo zilikuwa zinafanya maonyesho na kwenda kufurahia burudani ya muziki halisi wa dansi ambao leo haupo tena.

Iko wapi leo Njata Njata , au ni wapi iliko Mwenge Jazz ‘Paselepaa’, Bantu Group ‘Kasimbagu’, Tancut Almas ‘Kinyekinye kisonzo’ ni wazi ukikumbuka haya kama ulikuwa mpenzi wa kweli wa burudani wakati huo lazima chozi litakutoka hasa ukiiona Sikinde ya sasa iliyobaki jina tu, huku ikishuhudiwa muziki wake kumezwa na aina ya muziki kutoka Congo DRC.

Kwa sasa asilimia kubwa muziki wa Tanzania imemezwa na muziki wa Kikongo, kwani kila bendi hivi sasa baada ya wimbo kuisha kinachofuata ni rap ambazo zinachukua nafasi kubwa huku zikiwa hazina ujumbe wowote zaidi ya kusifia watu

Hii ni tofauti na siku za nyuma ambapo mbali na kupata wimbo wenye mashairi mazuri yenye mafunzo kilichokuwa kinafuta baada ya wimbo kumalizika ni kuachia ufundi wa wapiga vyombo kumalizia burudani na kuwafanya mashabiki walioshiba ujumbe vichwani mwao kujimwaga ukumbini kuserebuka.

Hakika hii ilikuwa maana halisi ya dansi. Hebu tuambizane ukweli ni nani ama ni bendi ipi leo inafanya haya niende ukumbi gani ambapo sitakutana na makelele ya rapu za kumsifia mfanyabiashara fulani wa magari ambaye hana anachokijua katika muziki zaidi ya kumwaga hela ukumbini ah ah! Kazi kwenu mnaojiita vijana!

Hakika miaka hiyo ilikuwa ya ukweli kwa dansi la Tanzania kwani mbali na ubora wa bendi na wanamuziki waliokuwa hodari wa utunzi na upigaji vyombo wakati huo pia kulikuwa na Mashindano ya kutafuta bendi bora Tanzania yaliyojulikana kama (MASHIBBOTA), mashindano ambayo kwa kiasi fulani yalikuwa nguzo ya muziki huo ambayo kwa sasa yamebaki historia.

 
Wako wapi waimbaji wa kike muziki wa dansi nchini?

14 August, 2015

Mrema asema UKAWA umepoteza mwelekeo

Mwenyekiti wa taifa wa TLP Augustine Mrema amewatahadharisha watanzania kuwa macho juu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ambao umepoteza mwelekeo na kuyumba kisiasa na kudai kuwa hawafai kuingia ikulu na kuongoza nchi.
Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha TLP , Augustino Lyatonga Mrema
Mrema ametoa tahadhari katika eneo la njiapanda baada ya kurejea ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Moshi kuchukua fomu za kugombea ubunge katika jimbo la Vunjo huku akisindikizwa na wafuasi wake.
Amesema, kitendo cha ukawa kumkashifu hadharani waziri aliyestaafu Mh
Edward Lowasa kuwa ni fisadi na baadaye kumpokea na kumteua kuwa mgombea wa urais ukawa imeonyesha udhaifu mkubwa na kwamba watanzania wa sasa si wakuburuzwa.
Mh. Mrema amesema kuwa haiwezekani mtu alieachwa na chama na kuonekana hafai kutokana na tuhuma za ufisadi kicha CHADEMA ndio wakaona anafaa kuwa mgombea huko ni kuonyesha kutokuwa na msimamo ndani ya hivyo ni vigumu kuwapa uongozi wa nchi.

Amisom waliwaua 6 harusini Somalia


Amisom waliwaua wageni harusini Somalia.
Shirika la kupigania haki za binadamu lenye makao yake makuu huko Washington Marekani,Human Rights Watch (HRW), limesema kuwa majeshi ya mataifa ya muungano wa Afrika Amison yaliwashambulia wageni katika harusi moja iliyokuwa imeandaliwa huko Merka Somalia mwezi uliopita.
Katika ripoti yake mpya shirika hilo la kupigania haki za kibinadamu mpya Human Rights Watch,linasema kuwa wanajeshi wa Uganda walivamia kijiji kimoja ambako kulikuwa na halaiki ya watu harusini.
Waliingia chumbani na kuwatenganisha wanaume na wanawake.
'Katika chumba kimoja kilichokuwa na wageni, wanaume 6 walitenganishwa na wanawake na kisha wakawapiga risasi na kuwaua papo hapo.'
'Kati ya wanaume hao sita, wanaume wanne walikuwa ni ndugu baba yao mzazi na ami wao.'
'Wanne walikufa papo hapo kisha mmoja wa ndugu hao aliyejificha chini ya kitanda akawachwa hapo akavuja damu hadi akafa.'
'Walioshuhudia wanasema kuwa wanajeshi hao walikataa kata kata jamaa zao wasiwapeleke hospitalini'' Ripoti hiyo inaeleza.
Kulingana na HRW tukio hilo lilitokea tarehe 31 Julai.
Umoja wa Afrika haujajibu shtuma hizo za HRW.
Shirika hilo la HRW linapendekeza uchunguzi wa kina ufanyike.
'Kuwaua watu bila makosa ili kulipiza kisasi cha mashambulizi dhidi yenu sio jambo jema na hilo litahakikisha kuwa hali itakuwa mbaya zaidi katika siku za usoni ripoti hiyo inasema.
HRW lingali linachunguza ripoti kuhusu mauaji ya raia huko Marka mapema mwezi huu.

Ubalozi wa marekani wafunguliwa Cuba

Sherehe za ufunguzi wa ubalozi wa Marekani huko Cuba zimefanyika mjini Havana.
Hii ndio mara ya kwanza kwa ubalozi huo na haswa bendera ya Marekani kupepea tena nchini humo tangu mwaka wa 1961.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, aliyeko Havana ndiye aliyekuwa mgeni mheshimiwa katika dhifa hiyo ya kufungua upya ubalozi wa nchi yake nchini Cuba

Katika sherehe zilizofanyika Havana, Kerry aliandamana na wanajeshi watatu wa zamani ambao waliishusha bendera ya Marekani katika jengo la ubalozi huo mnamo 1961.
Rais Obama na mwenzake wa Cuba Raul Castro walikubaliana mnamo December mwaka jana kuurudisha uhusiano wa kidiplomasia.
Marekani imelegeza baadhi ya vikwazo vya biashara na usafiri, hatahivyo bado vingine vingi vingalipo.

EPL LEO NI ASTON VILLA vs MAN UNITED, NIMEKUWEKEA VIKOSI NA MSIMAMO

2B336FAF00000578-3193460-image-a-14_1439287505311
Ligi kuu England inaendelea leo kwa mechi moja kati ya Aston Villa na Manchester United.
Mchezo huu utaanza saa 3:45 usiku kwa saa za Afrika mashariki.
VIKOSI VINAVYOTARAJIWA
MSIMAMO MPAKA SASA EPL

Jux: Video ya ‘Looking for you’ imegharimu Million 31 za Kitanzania

ux amefunguka kuwa video yake ‘Looking for you’ imegharimu Kiasi cha dolla 15,000 ambayo ni sawa na Pesa za kitanzania Million 31.jumaJux amesema hayo muda mchache uliopita wakati akiachia rasmi Audio ya track hiyo aliyomshirikisha Joh makini.
Kama Bado hujaiona, Itazame hapa chini

Azam TV Yazindua Huduma Yake Ya “Azam Sports HD”


Azam Media leo imezindua rasmi chaneli yake mpya yenye ubora wa juu kabisa iitwayo “Azam Sports HD”, tangu kuanza kwa huduma za Azam TV, wateja wamekuwa wakijiuliza hasa ni kipi wanachopata kutokana na alama ya HD iliyo mbele ya kisimbuzi, kuanzia sasa watafahamu.
Baada ya miezi 18 ya mipango na uwekezaji, leo umeshuhudiwa uzinduzi wa channel ya kwanza itakayowezesha wateja kufaidi picha na sauti za ubora wa juu kabisa “HD” kutokana na teknolojia ya kiwango cha juu.
Wateja wa kifurushi chenye channel mpya ya “Azam Sports” wataweza kuona timu zao wazipendazo katikaVPL katika picha ang’avu zaidi ambazo hazijawahi kuonekana, zaidi, kampuni pia imetangaza rasmi ujio wa ligi kuu ya Uhispania maarufu la liga ambayo wateja wataipata katika ubora wa HD kupitia chaneli mpya.
Mchezo wa kwanza kuoneshwa katika msimu mpya wa la liga 2015/16, ni Malaga dhidi ya Seville wa Ijumaa 21 Agosti 2015 na timu zote vigogo zitakuwa zikicheza na kuonyeshwa Live mwisho wa juma lijalo, na kila mzunguko wa msimu mzima katika ubora wa HD.
Kifurushi kinachojumuisha chaneli ya Azam Sports HD kitaonekana kwa watazamaji wa Azam TV wa Tanzania pekee ambao wanalipa kifurushi chochote kati ya vitatu vya sasa, Pure, Plus au Play na nyongeza ya shilingi 15,000 kwa mwezi, ikijumuisha VAT. Pamoja na chaneli mpya ya Azam Sports HD, malipo hayo yatajumuisha chaneli za klabu za Manchester United, Liverpool na Real Madrid ambazo kwa sasa ni sehemu ya kifurushi cha Azam Play. Kadhalika malipo ya mwezi kwa kifurushi cha Play kitapunguzwa hadi 25,000 kuanzia sasa.

Kwa wale wasiokuwa na luninga zenye uwezo wa kuona picha za HD au waya maalum wa HD (HDMI), watapata chaneli mpya na kufuatilia La Liga na mengineyo – japo si kwa ubora wa HD. Pia kwa wateja wasiohitaji kujiunga na kifurushi kipya hawapaswi kuwa na wasiwasi wa kutoona michezo ya VPL kwani itaendelea kuonyeshwa kupitia Azam One na Azam Two kama ilivyokuwa kabla , jambo lililotofauti ni kuwa mchezo yenye mvuto zaidi itaonyeshwa pia kwenye Azam Sports HD.

Zaidi ya La Liga na VPL , Azam Sports HD, itakuwa na vitu mbalimbali vya kimichezo vitakavyojumuisha michezoya Ligi za soka za Uganda, Kenya na Burundi itakayoanza hivi hivi karibuni.
Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi, Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington amesema “Uzinduzi wa Azam Sports HD ni hatua kubwa katika maendeleo ya Azam TV. Hata kabla ya ya kuanza mwaka 2013 tulijipanga kukidhi mahitaji ya kiteknolojia kwa ajili ya kutoa picha za ubora wa HD ili kutuwezesha baadaye kumpatia mtazamaji picha bora zaidi bila kulazimika kununua vifaa kwa kuonyesha moja kwa moja soka la Liga! Ambalo ni bora zaidi barani Ulaya”.

Uwezo wa kuona moja kwa moja na katika HD timu mzipendazo huko Hispania na kwa VPL , pamoja na vipindi vingine vya michezo kutoka sehemu mbalimbali duniani, unatoa chaguo muhimu na ambalo wateja wetu wanalimudu, huu ni mwanzo tu – jiandae kwa makubwa zaidi”.
DSCN5578
Meneja wa mauzo na masoko Mgope Kiwanga
DSCN5591
Mtendaji Mkuu Uhai Productions/Azam TV Dunstan Tido Mhando
DSCN5632 DSCN5596 DSCN5597 DSCN5598 DSCN5599 DSCN5601 DSCN5602 DSCN5603 DSCN5604 DSCN5605 DSCN5606 DSCN5607 DSCN5608 DSCN5609 DSCN5611 DSCN5612 DSCN5613 DSCN5615 DSCN5616 DSCN5617 DSCN5618 DSCN5619 DSCN5620 DSCN5624 DSCN5625 DSCN5626 DSCN5627

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...