Showing posts with label Entertainment. Show all posts
Showing posts with label Entertainment. Show all posts

25 October, 2016

Sipendi 'bifu' na msanii yeyote - Joh Makini

Msanii wa miondoko ya Hip Hop nchini Joh Makini amesema katika vitu ambavyo hapendi kwenye kazi zake za kisanii ni kuwa na 'bifu' na msanii mwenzake katika tasnia ya sanaa nchini.
Makini ameyasema hayo alipokuwa akijibu maswali ya wapenzi wa muziki wa Bongo Fleva waliokusanyika kushuhudia program maalumu ya Kamatia Kitaa katika  kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio.
“Sipendi kuwa na bifu na msanii yeyote , mimi naamini katika muziki wangu na kuheshimu kila mmoja katika kazi yake” Amesema Makini
Aidha Makini ameongeza kuwa katika mambo ambayo humuumiza sana ni kuona kazi za wasanii zikiwa zimezagaa mtaani na kuuzwa bila wasanii kunufaika na chochote.
“Jambo hili inabidi serikali iingilie kati kwa sababu ugumu wa maisha mtaani umefanya vijana kuanza  kudurufu kazi zetu na kuziuza bila sisi kunufaika na chochote na jambo hili linatokana na jamii kutokuwa na elimu ya kutosha “ Amesema Joh Makini.

Pamoja na hayo Makini amewataka mashabiki kuendelea kuwaunga mkono kwani kundi la weusi limejipanga vyema katika kutoa burudani ya uhakika kwa mashabiki.

CHANZO: eatv.tv

Kelele zamuondoa Justin Bieber jukwaani kwa hasira

Justin Bieber aliondoka katika jukwaa la tamasha yake mjini Manchester baada ya kuwataka mashabiki kutopiga kelele wakati anapoimba.

Wakati wa tamasha zake tatu zilizopita katika mji huo ikiwa miongoni mwa ziara yake ya dunia nzima mwanamuziki huyo alisema : Nathamini msaada ninaopata, nathamini mapenzi munayonipa na nathamini ukarimu wenu.Lakini kelele munazopiga wakati ninapoimba lazima zisitishwe.Tafadhali na ahsanteni.Sidhani ni muhimu ninapojaribu kusema kitu na nyinyi munapiga kelele.

Na mashabiki hao walipokataa kusitisha kelele zao aliangusha kipaza sauti na kuondoka katika jukwaa,huku baadhi ya mashabiki wakimzoma.
Baadaye kijana huyo wa miaka 22 alirudi kuendelea na tamasha yake na kuelezea kwa nini aliondoka kwa hasira.

''Nahisi kwamba nataka wasiliana nanyi.Lengo hapa ni ninapowaangalia katika macho ,munajua kwamba tuko katika wakati muhimu na kwamba tunawasiliana''.

22 October, 2016

Jay Mo amwagia misifa Juma Nature

Msanii Jay Mo amesema ukongwe wa Juma Nature kwenye game ya bongo fleva ni kitu cha kuthaminiwa sana kwani ameleta mchango mkubwa kwenye muziki huo mpaka kufikia hapa ulipo.
Akizungumza kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Jay Mo amesema wataendelea kumheshimu Juma Nature kwani vitu ambavyo amevifanya, ndivyo vimesababisha wasanii kama kina Diamond kujulikana kimataifa.
“Tutamkumbuka kwa kufanya vitu ambavyo vimewafanya mpaka kina Diamond wakajulikana, muziki anaoimba Juma Nature ni ule muziki wa watu wa chini, amegusa maisha ya watanzania halisi, unajua sisi hata kama tulikuwa tunafanya muziki lakini haikuwa kama ya Juma Nature, kipindi hicho unaenda kweny show ya Juma Nature unakuta watu wanapanga foleni ndefu kukata tiketi, alikuwa anaweka kiingilio cha chini ili kila mtu aweze kuingia, hajajichukulia mi super star na kuvaa ukinondoni au u ilala, muziki wake ulikuwa umelalia maisha ya mtaa na watu wengi, alikuwa mjanja kutarget hawa watu wenye uwezo wa chini kimaisha”, alisema Jay Mo.

Jay Mo amesema kutokana na aina hiyo ya muziki wa Juma Nature, ndiyo ume'inspire' vijana wengi na kufuata nyayo zake, ikiwemo yeye mwenyewe na kuandika mistari ya wimbo wa stori 3 na Jua na mvua.

CHANZO: eatv.tv

Collabo yangu na Jay Dee inakuja - Diamond

Baada ya kilio cha muda mrefu kutoka kwa mashabiki waliotamani kuona Diamond Platnumz na mwanadada Lady Jay Dee wakifanya kazi pamoja, wakali hao wa bongo fleva huenda wakaja na 'collabo' ya hatari, siku chache zijazo.
Hatua hiyo inatokana na msanii Diamond kufunguka kuwa hakuna sababu yoyote inayowakwamisha kufanya kazi ya pamoja, isipokuwa muda na ratiba zao kubana.

Dangote ametoa kauli hiyo hivi karibuni alipotembelea ofisi za Kituo cha runinga EATV, na kukutana na maswali mbalimbali ikiwemo sababu za wao kutofanya kazi ya pamoja licha ya mashabiki kuitamani  'collabo yao.

"Siku si nyingi tutafanya kazi pamoja na Jay Dee, kilichotukwamisha ni ratiba zetu, lakini pia nilikuwa sijafikiria hilo, ila sasa kwa kuwa mashabiki wamekuwa wakiomba kila mara, nitawasiliana naye, na tutafanya kazi ya pamoja muda mfupi ujao, hakuna sababu nyingine tofauti na kubanwa na kazi nyingi, pamoja na ratiba zetu kutoendana"

Kuhusu ni lini mashabiki wategemee kazi hiyo, Dangote alisema kuwa hawezi kuahidi tarehe, lakini ana uhakika  'collabo' hiyo inakuja.

CHANZO:eatv.tv

21 October, 2016

IZZO B -Bado tunawekana sawa na YCEE, ngoma inakuja

Mkali wa Rap kutoka Mbeya City IZZO B amesema wimbo wao wa The Amaizing walioimba na YCEE utatoka bila ya msanii YCEE kusikika na baadaye watafanya Remix ya wimbo huo ambayo YCEE atasikika.
Izzo
Amesema kuwa hiyo ni kutokana na kutoafikiana na kutokubaliana kibiashara baina ya wasanii hawa.

Akipiga story ndani ya kipindi cha eNewz Izzo amesema "Kuna sababu za kibiashara ambapo bado kuna vitu tunaweka sawa kwa kuwa hatutaki kukaa kimya kwa muda mrefu tutatoa wimbo halisi na baadaye tutakuja tena na marudio ya wimbo huo (remix)".

Pia Izzo alisema kuwa kutokana na muda kuwa mrefu na kuna vitu ambavyo bado wanaviweka sawa juu ya makubaliano ya kibiashara na kwamba wimbo huo ni wa siku nyingi zaidi hivyo wameona watoe wimbo halisi kwanza kwa kuwa wanavyozidi kukaa muda utakuwa mrefu zaidi.

CHANZO: eatv.tv

20 October, 2016

Maua Sama: Nipo tayari kufanya kazi na label yenye mafanikio

Muimbaji wa Mahaba Niue, Maua Sama amedai kuwa anaweza kufanya kazi na label yoyote ile inayofanya vizuri na yenye mafanikio yanayoonekana.
Hata hivyo ameongeza kuwa kwa sasa yupo chini ya usimamizi wa THT na kwamba si rahisi kuhama, bali inawezekana kushirikiana na msanii yeyote nje ya uongozi wake.

Akiongea na kituo kimoja cha redio nchini, Maua amesema so far THT imemfikisha sehemu nzuri na haoni mapungufu yoyote kwenye muziki wake.
Kwa upande mwingine Maua amedai kuwa mashabiki wake watarajie kazi nzuri na mpya kutoka kwake.

18 October, 2016

Napenda kufanya kazi na undergrounds - Manecky

Mtayarishaji wa muziki kutoka katika studio za 'AM Records' Manecky amefunguka na kusema kuwa yeye anapenda sana kufanya kazi na wasanii chipukizi au wasanii ambao tayari walikwisha potea kwenye muziki.

Amesema kupitia wasanii hao yeye kama producer anaweza kuonesha uwezo wake katika kufanya muziki tofauti na kufanya kazi na wasanii ambao tayari ni wakubwa au ambao wapo kwenye soko kwa wakati huo.

Manecky alipokuwa akizungumza na shirika la habari la taifa alidai kuwa yeye kama mtayarishaji anaweza kuonesha uwezo wake pindi anapofanya kazi na wasanii wachanga na wasanii ambao wamepotea kwenye 'game'.

"Mimi huwa napenda kufanya kazi na 'undergrounds' kwa sababu kupitia hao wasanii naweza kuonesha uwezo wangu kama producer hawa wasanii wakubwa wanaweza kukubana kuonesha uwezo wako, lakini leo hii ukifanya na mwanamuziki mkubwa ni kweli utafahamika na utakuwa unasikika mara kwa mara lakini siku akiacha kufanya kazi na wewe ndiyo na wewe umeshapotea kwenye ramani, lakini ukiweza kumtoa msanii mchanga na kuwa mkubwa ina maana utakuwa na uwezo wa kumtoa mwingine na kuwa mkubwa pia, hivyo utaendelea kuwepo kwenye tasnia siku zote" alisema Manecky

17 October, 2016

New Music: Raymond ft Ney Lee – Rudi

Kutoka WCB ni ngoma baada ya ngoma, na hii ni ya Raymond-Rayvan akimshirikisha mwanadada Ney Lee wimbo umepewa jina la RUDI, mkono wa producer Zest kutoka moja moja Rec. Enjoy

16 October, 2016

Wasanii hawa walitamani jukwaa la EATV AWARDS

Tuzo kubwa za muziki na filamu zinazotarajiwa kufanyika kwa mara ya kwanza tar 10 Desemba 2016 jijini Dar es salaam Tanzania, zimeleta hamasa kubwa wasanii wa nchi za Afrika Mashariki wakisema ni neema kwao, huku wengine wakilitamani jukwaa lake.
Wakizungumza na East Africa Tv na East Africa Radio kwa nyakati tofauti tofauti, baadhi ya wasanii wamesema wapo tayari kutoa burudani siku ya kutolewa kwa tuzo hizo, burudani ambayo itaandikwa kwenye historia ya EATV AWARDS.

Kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, msanii Peter Msechu alisikika akisema iwapo hatakuwa nominated kwenye tuzo hizo, anatamani apewe fursa ya kutoa burudani ambayo itaacha historia kwake na kwa mashabiki.

"Yani acha niseme tu kwa kweli, hata nisipokuwa nominated au kushinda hizo tuzo, basi naomba nipewe fursa ya kuperfom kwenye EATV AWARDS, na siku hiyo nawaambia nitatoa burudani ya kufa mtu, kwa mara ya kwanza nitaperfom tumbo wazi, nitavua shati ili watu wote waone litumbo langu siku hiyo, naitamani hiyo siku kama nini", alisema Peter Msechu.
Naye msanii mkongwe wa rap hapa bongo ambaye alikaa kimya kwa muda mrefu na kurudi kwa kishindo, King Crazy GK, amesema anatamani angeperfom kwenye sherehe za utoaji wa tuzo hizo, kwani itakuwa ni furaha kubwa kwake.

"EATV AWARDS tunaisubiria kwa hamu, na natamani yani natamani sana, achana na kupata tuzo, japo hata kuperfom katika tukio kama hilo", alisema King Crazy GK.

EATV AWARDS ndio tuzo kuwa za kwanza kuanzishwa na media Afrika Mashariki, ambazo zitahusisha wasanii wa filamu na muziki wa nchi za Afrika Mashariki moja kwa moja.

CHANZO: EATV

10 October, 2016

50 Cent kuachia Mix-tape yake mpya Hivi karibuni.

Mashabiki wa 50 Cent wamekua wakiuliza maswali mengii ambayo yanatokana na Kimya cha huyu jamaa katika social media tofauti tofauti. Kuna kila dalili kwamba Mashabiki wa 50 watapata kitu roho inapenda hivi karibuni maana DJ Whoo Kid yupo studio akifanya mixing ya ngoma za Mixtape ya nne ya 50 Cent.

Mix-tape hii itahusisha ngoma zote za 50 ambazo bado hazijatoka kama vile Young Buck, Lloyd Banks, Tony Yayo na Kidd Kidd.

08 October, 2016

Video: Snura – Chura

Msanii Snura hatimaye ameachia video yake mpya ya wimbo wa “Chura”, baada ya kufunguliwa kwa wimbo huo.

30 September, 2016

All the way Up Rmx- Diamond Plutnum Part 2


Diamond ameachia verse nyingine ya Remix yake ya ‘All the way Up’ , amejibu tetesi za kuchepuka, jina la Simba na mpinzani wake, Alikiba.
Kulikuwa na tetesi kuwa muimbaji huyo wa ‘Salome’ amerudiana na Wema sepetu kimyakimya, pia kuna tetesi kuwa amechepuka na Hamisa mobetto ambaye pia ametokea kwenye video yake mpya, Jibu ndio hili


“Mara nakula hamisa mobetto, ati Sepenga kaja magetho, ilimradi Zari apate mchecheto, Tale waambie waache unambinambi hata nikila wote dini yangu sio dhambi” 
Diamond na Alikiba ni washindani wakubwa kimuziki na maneno ya hapa na pale hayakosekani, Huku Diamond akiwa amesaini dili kubwa zaidi la kuwa balozi wa Vodacom, Alikiba na yeye alipata dili la kuwa Balozi wa Wild Aid, inayopinga mauaji ya tembo. Diamond nalo kaliongelea


“Siachi pengo hadi waombe poo, wao wakipost tembo si tunapost show”
Kama unajiuliza Tilalila ni nani, basi jua kuwa ni Mr.Blu jina limetokana na wimbo wake wa ‘Tilalila’ wa muda kidogo, Mr. Blu na Diamond waliwahi kuingia kwenye mgogoro wa jina la ‘Simba’, Chibude nalo hajaliacha lipite,
Mwambie na tilalila, kamwe kanzu haifanani na dera”
Enjo All the Way Up rmx

28 September, 2016

List ya wasanii wa Hip-Hop watakao wania Tuzo za BET

Hii ndiyo list kamili ya wasanii na DJs watakao wania Tuzo za BET 2016. Sherehe za utoaji tuzo hizi zitafanyika kwenye ukumbi wa Cobb Energy Performing Arts Centre jijini Atlanta, Georgia, na zitaoneshwa na kituo cha BET (DStv channel 129) Alhamisi ya October 6, 2016.


Best Hip-Hop Video
2 Chainz – Watch Out
Desiigner – Panda
DJ Khaled F/ Jay Z & Future – I Got the Keys
Drake – Hotline Bling
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
Kanye West F/ Rihanna – Famous
 
Best Collabo, Duo or Group
DJ Khaled F/ Drake – For Free
DJ Khaled F/ Jay Z & Future – I Got the Keys
Drake & Future – Jumpman
Drake F/ Wizkid & Kyla – One Dance
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
 
Best Live Performer
Drake
Future
Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Lyricist of the Year
Chance the Rapper
Drake
Cole
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Video Director of the Year
Benny Boom
Colin Tilley
Director X
Hype Williams
Kanye West
 
DJ of the Year
DJ Drama
DJ Envy
DJ Esco
DJ Khaled
DJ Mustard
 
Producer of the Year
DJ Mustard
Dr. Dre
Metro Boomin
Mike WiLL Made-It
Pharrell Williams
 
MVP of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Kanye West
Kendrick Lamar
 
Track of the Year
All the Way Up – Produced By Cool & Dre and Edsclusive (Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared)
Controlla – Produced By BOI-1DA (Drake)
Hotline Bling – Produced By Nineteen85 (Drake)
I Got the Keys – Produced By Southside (DJ Khaled F/ Jay Z & Future)
Panda – Produced By Menace (Desiigner)
Album of the Year
DJ Khaled – I Changed A Lot
Dr. Dre – Compton
Drake – Views
Fetty Wap – Fetty Wap
Future -DS2
Kanye West – The Life of Pablo
 
Best New Hip-Hop Artist
Anderson .Paak
Bryson Tiller
Chance the Rapper
Desiigner
Tory Lanez
 
Hustler of the Year
DJ Khaled
Drake
Future
Jay Z
Kanye West
 
Made-You-Look Award (Best Hip Hop Style)
A$AP Rocky
Drake
Future
Kanye West
Nicki Minaj
 
Best Hip Hop Online Site/App
Allhiphop.Com
Complex.Com
Hotnewhiphop.Com
Worldstarhiphop.Com
XXLMag.Com
Best Mixtape
Chance the Rapper – Coloring Book
French Montana – Wave Gods (Hosted By Max B)
Future – Purple Reign
Lil Uzi Vert – Lil Uzi Vert VS. The World
Young Thug – Slime Season 3
 
Sweet 16: Best Featured Verse
2 Chainz – No Problem (Chance the Rapper F/ Lil Wayne & 2 Chainz)
Drake – Work (Rihanna F/ Drake)
Kendrick Lamar – Freedom (Beyoncé F/ Kendrick Lamar)
Kodak Black – Lockjaw (French Montana F/ Kodak Black)
Nicki Minaj – Down In the DM – Remix (Yo Gotti F/ Nicki Minaj)
 
Impact Track
Cole – Love Yourz
Jay Z – Spiritual
Jidenna – Long Live The Chief
Raury F/ Key – Trap Tears
Sir The Baptist F/ ChuchPeople – Raise Hell
 
People’s Champ Award
Desiigner – Panda
DJ Khaled F/ Drake – For Free
Fat Joe & Remy Ma F/ French Montana & Infared – All the Way Up
O.T. Genasis F/ Young Dolph – Cut It
Travis Scott – Antidote
Young Thug – Best Friend

Video: Feza Kessy – Walete (Official Video)

Ni mwezi mmoja umepita tangu mwanadada Feza Kessy aiachie audio ya ngoma yake mpya inayoitwa “Walete” katika media tofautitofauti. 
Na huu ameona ndio wakati mzuri wa kuiachia video ya ngoma hiyo. Itazame hapa chini

22 September, 2016

Diamond Platnumz achaguliwa kuwania uzo za Ghana Music Awards UK

Habari ni kwamba Diamond Platnumz amepata nafasi nyingine kubwa ya kuiwakilisha Tanzania kwenye tuzo za Ghana Music Awards UK zinazoandaliwa kwa ushirikiano wa kampuni mbili za Alordia Promotion & West Coast UK Entertainment za nchini Ghana na Uingereza.
 
Diamond Platnumz anawania tuzo hii kupitia kipengele cha AFRICAN ARTIST OF THE YEAR akichuana na mastaa wengine akiwemo Patoranking, Fally Ipupa, Davido, AKA, Wizkid, Olamide na Tekno Milles.

Sherehe za utoaji wa tuzo hizi zimepangwa kufanyika jijini London, Uingereza mnano November 5th, 2016, kwenye ukumbi wa Gaumont Palace zamani ulikuwa ukiitwa Dominion Centre, huko 9 The Broadway Wood Green London N22 6DS

Hii ni List nzima ya wasanii waliotajwa kuwania tuzo hizo kwenye vipengele 26.
AFRICAN ARTISTE OF THE YEAR
Patoranking
Fally Ipupa
Davido
AKA
Wizkid
Diamond Platnumz
Olamide
Tekno

BEST CLUB DJ OF THE YEAR
DJ Bibi
DJ Fiifi
DJ Invisible
DJ Sawa
DJ Billy
DJ Chris Vibez

GOSPEL SONG OF THE YEAR
Hour by Hour – SP Kofi Sarpong ft. Joyce Blessing
M’asem (Yoboyo) – Kofi Gyan
Wowo Nkwa Wo Wo Ade3 – Mary Owusu
Hyebre Sesafo – Obaapa Christy
Wafom Kwan – Patience Nyarko
Aporsor – Nicholas Omane Acheampong

GOSPEL ARTISTE OF THE YEAR
Obaapa Christy
Nicholas Omane Acheampong
Joe Mettle
SP Kofi Sarpong
Patience Nyarko
Preachers

NEW ARTISTE OF THE YEAR
Nero X
Kofi Kinaata
Wisa
Atom
Mr. Eazi
Nii Funny

MUSIC PRODUCER OF THE YEAR
Mobeatz – Skolom
Bisa Kdei – Brother Brother
Kaywa – Mansa
Beatz Dakay – Mightylele
Dr. Ray – Yewo Krom
Kin Dee – Susuka
The Maker – Chop Kiss

BEST MUSIC VIDEO OF THE YEAR
MzVee – Hold Me Now
Joey B – U And Me
Obrafour – Nkontompo
YaaYaa – Dumb Drum
Edem – Girlfriend
Teephlow ft. Sarkodie – The Warning
Mr Eazi ft. Sarkodie – Anointing
Becca ft. Bisa Kdei – Hwe
VVIP ft. Samini – Dogo Yaro

BEST GROUP OF THE YEAR
VVIP
R2Bees
Keche
4×4

BEST RAPPER OF THE YEAR
EL
Guru
Yaa Pono
M.anifest
Pappy Kojo
Flowking Stone
Obrafour
Edem
Sarkodie
Omar Sterling

HIPLIFE SONG OF THE YEAR
Atom – Yewo krom
EL – Koko
Wisa – Ekikimi ft. Luther
VVIP – Skolom ft. Sena Dagadu
Guru – Pooley Swag
Mr. Eazi – Hollup

HIGHLIFE SONG OF THE YEAR
Bisa Kdei – Mansa
R2Bees – Makoma
Bisa Kdei – Brother Brother
Kofi Kinaata – Susuka
Ofori Amponsah – Alewa ft Sarkodie
Kwabena Kwabena – Tua Mu Daa

HIGHLIFE ARTISTE OF THE YEAR
Bisa Kdei
Afriyie
Ofori Amponsah
Nero X
Kwabena Kwabena

MOST POPULAR SONG OF THE YEAR
Mansa – Bisa Kdei
Brother Brother – Bisa Kdei
Go Higher – Stonebwoy
Ekikimi – Wisa ft. Luther
Baby (Chop Kiss) – Shatta Wale
Yewo Krom – Atom ft. Jhunea
Susuka – Kofi Kinaata
Kakai – Shatta Wale

REGGAE / DANCEHALL SONG OF THE YEAR
Go Higher – Stonebwoy
Enemies – Jupitar ft Sarkodie
Mightylele – Stonebwoy
Kakai – Shatta wale
Hold it – Shatta Wale
Pumpum – Rudebwoy Ranking ft Episode

REGGAE / DANCEHALL ARTISTE OF THE YEAR
Stonebwoy
Jupitar
Samini
Episode
Mzvee
Shatta wale

AFROBEATS ARTISTE OF THE YEAR
Mr. Eazi
D-Cryme
Pappy Kojo
Kofi Kinaata
R2Bees
Wisa

BEST COLLABORATION OF THE YEAR
Mr. Eazi ft. Efya – Skin Tight
VVIP ft. Sena Dagadu – Skolom
Sarkodie ft. Akwaboah – Mewu
Pappy Kojo ft. Sarkodie – Aye Late
Wisa ft. Luther – Ekikimi
D-Cryme ft. Sarkodie – Koko Sakora
Mr Eazi ft. Eugy – Dance For Me
Jupitar ft. Sarkodie – Enemies
Becca ft. Bisa Kdei – Hwe

ALBUM OF THE YEAR
Mary – Sarkodie
Elom – EL
Breakthrough – Bisa Kdei
I Believe – SP Kofi Sarpong
After The Storm – Shatta Wale
Necessary Evil – Stonebwoy
Breaking News – Samini

ARTISTE OF THE YEAR
Shatta Wale
Nero X
Sarkodie
Stonebwoy
Bisa Kdei
SP Kofi Sarpong
EL
Mr. Eazi

BEST UK BASED GROUP
Kwamz & Flava
Vibez Squad
NSG
Kraze
CXCV
IRAY MVNT

BEST UK BASED AFROBEATS ARTISTE
Jaij Hollands
Mista Silva
K Weezy
Scob Original
Charsey
Kwamz & Flava

BEST UK BASED AFRO-POP ARTISTE
Zafi B
Eugy
Areatha Anderson
Tinchy Stryder
Prince Rapid
Fuse ODG
Stormzy
NSG

BEST UK GOSPEL SONG
Amazing God – Sonnie Badu
We Love You – Louisa Annan
Yebe Duru – Nhyira Hemaa
Jesus the Reason for the Season – Kwame Amponsah
Bisa Awurade – Betty Acheampong
Work In Progress – Diana Antwi Hamilton

BEST UK BASED GOSPEL ARTISTE
Sonnie Badu
Mama Fausty
Ohemaa Jackie
Antwi Diana Hamilton
Louisa Annan
Nhyira Hemaa
Osei Kofi
Kwame Amponsah
Betty Acheampong
Ohene Darko

BEST UK BASED MUSIC VIDEO
Tina – Fuse ODG ft. Angel
New Girl – Reggie N Bollie
Pinga – Jaij Hollands ft NSG
B.A.D (Best Achieving Don) – Mr Silva
Watch Nobody – Atumpan ft. Paigey Cakey

UK BASED GHANAIAN INTERNATIONAL ARTISTE
Fuse ODG
Tinchy Stryder
Sonnie Badu
Reggie N Bollie
Lethal Bizzle
Stormzy

20 September, 2016

Ndoto Yangu Kushinda Grammy- Vanessa Mdee

Mwanamuziki wa kike anayesumbua ndani na nje ya Bongo, Vanessa Mdee ‘Vee Money’ amesema ana ndoto kubwa.

Ndoto yake siku moja, kuwa msanii kutoka Tanzania atakayeshinda tuzo za heshima, Grammy.Anaamini kuwa, mwanzo wa kukaribia kuiishi ndoto hiyo umewadia.

Vee Money ni mmoja wa wasanii wa Afrika, waliochaguliwa kurekodi wimbo na mshindi wa Grammy na nyota wa RnB nchini Marekani, Trey Songz.
Shukrani kwa kipindi cha Coke Studio Africa (International Week) msimu wa 4, kinachomdondosha staa huyo.

Akiwa pia anawania tuzo ya Loeries za Afrika Kusini kwa kazi yake ya video bora, Niroge.

“Katika harakati zangu za kutafuta ushindi wa Grammy katika career yangu ya muziki, inanipa nguvu kufanya kazi kwa ukaribu na Trey Songz, ambaye alishawahi kushinda tuzo hiyo.” amesema Vanessa.
Msimu mpya wa Coke Studio utaanza mwezi ujao.

19 September, 2016

Game of Thrones yatawala tena tuzo za Emmy


Filamu ya televisheni ya Game of Thrones kwa mara nyingine imezoa tuzo nyingi katika tuzo kuu za vipindi vya televisheni Marekani, Emmy.

Washindi wa tuzo hizo wametangazwa katika hafla iliyofanyika mjini Los Angeles.
Mwendelezo huo wa filamu umeshinda tuzo kumi na mbili za Emmys, zikiwemo tuzo za uelekezi bora na utunzi bora wa hadithi.

Mshindi mwingine mkuu amekuwa kipindi cha ucheshi wa siasa 'Veep,' huku Julia Louis-Dreyfus akishinda tuzo yake ya tano mtawalia ya Emmy kwa uigizaji wake kama makamu wa rais wa Marekani.

Game of Thrones
Filamu ya The People versus OJ Simpson inayoangazia uhalifu nayo imeshinda tuzo tisa za Emmy.
Filamu hiyo huangazia kesi mbili za mauaji pamoja na kuondolewa makosa kwa nyota wa zamani wa soka Marekani Orenthal James "O. J." Simpson.

12 September, 2016

VIDEO: Barnaba ‘Lover Boy’

Tizama Video mpya ya Barnaba inayokwenda kwa jina la  ‘Lover Boy’ Pia unaweza Kudownload Audio yake kwa kubonyeza DOWNLOAD hapo chini.

SHILOLE: Jina langu ni Fursa ya mafanikio.

 
Mwanamuziki na Muigizaji Zuenna Muhamed maarufu kama Shilole "SHISHI BABY" amesema Usanii ni mlango wakupitia ili kufuata mafanikio yalipo, huku akiahidi kuifanyia kazi kila nafasi itakayo katiza mbele yake. Akizungumza hivi karibuni, Shilole alisema ukiwa msanii unafahamiana na watu wengi wanao fanya mambo mbali mbali, hivyo ni nafasi yakufahamu mambo mengi pia.

 Shilole alisema tangu muziki hajawahi kukatishwa tamaa wala kufikiria kufanya hivyo licha yakua na mashabiki wa aina mbali mbali wanao kubali kazi zake. Alisema 
" Watu wengi wanatafuta nafasi yakufahamiana na watu wengi ili wapanue uwigo wa uelewa kati yaon na kufanikisha ndoto zao, sasa kwa nini mimi nimepata nafasi hiyo bado mimi nishangae, naifanyia kazi kila Fursa nitakayoiona mbele yangu"
Shilole aliwataka wasanii wakike na wakiume kuwekeza kipindi ambacho wana nguvu ili iwe msaada Baadae. 
"Wasanii hatuna kiinua mgongozaidi yakukikuza kile kidogo tunacho pata, hakuna njia nyingine zaidi ya Biashara, wasichana tupunguze mashindano ya mavazi tandae kiinua mgongo, Vivyo hivyo wavulana wapunguze Bata wajiandalie kiinua mgongo"

09 September, 2016

Video: TID ft Joh Makini – Confidance

Video mpya kutoka kwa msanii TID ya wimbo “Confidance”, amemshirikisha Joh Makini. Video imeongozwa na kampuni ya Kwetu Studios. Downlaod Audio hapo chini

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...