Showing posts with label Habari Kimataifa. Show all posts
Showing posts with label Habari Kimataifa. Show all posts

26 October, 2016

Gambia kujiondoa katika mahakama ya uhalifu ICC

Serikali ya Gambia imesema kuwa itajiondoa kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC mara moja.
Hatua hiyo imekuja kutokana na madai kuwa ICC hushughulika na Waafrika pekee.


Maamuzi ya kujitoa katika mahakama hiyo yanafuatia baada ya Burundi na Afrika ya Kusini kutangaza kujiondoa
Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh amekua madarakani tangu mapinduzi nchini humo mwaka 1994.

Uchaguzi ujao unatarajiwa kufanyika desemba lakini mapema mwaka huu viongozi nane wa upinzani walikamatwa na kuhumiwa miaka mitatu jela kwa kuhusika katika maandamano ambayo hayakua na kibali.
Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty limesema kuwa maamuzi hayo ni sehemu ya muendelezo wa ukandamizaji wa haki za binadamu nchini Gambia.

25 October, 2016

Mmiliki wa Mtandao wa Wikileaks afariki Dunia

Mwanzilishi wa mtandao maarufu wa Wikileaks, Gavin MacFadyen (76) amekutwa amefariki Jumamosi ambapo  chanzo cha kifo chake bado hakijajulikana.

Mtandao wa Wikileaks umekuwa ukiibua mambo mbalimbali ya siri ya mgombea  urais wa Marekani, Hillary Clinton. 

Wengi hawajayaamini kifo chake ambacho kimewastua na kuumiza mioyo ya watu wengi hasa pale wanapomkumbuka marehemu kama mwanzilishi wa kituo cha habari za uchunguzi (Centre for Investigative Journalism) mwaka  2003 ambapo wanahabari wengi wakubwa duniani wamejifunza hapo.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...