01 August, 2015

KUELEKEA MCHEZO WA NGAO YA JAMII MOURINHO AMPA TANO TERRY

John TerryKocha wa Chelsea Jose Mourinho amemsifia beki wake John Terry kuwa ni beki bora wakati wa maandalizi kuelekea mchezo wa ngao ya jamii uatakaopigwa kesho.
Terry (34) alikuwa ni nguzo imara ya Chelsea wakati wa msimu uliomalizika akikiongoza kikosi hicho kutwaa ubingwa wa ligi ya England (EPL) kwa mara ya kwanza tangu walipofanya hivyo kwa mara ya mwisho mwaka 2010.
Ubora aliouonesha Terry ulimfanya atajwe kuwa kwenye kikosi cha PFA kwa msimu uliopita ikiwa ni mara ya kwanza tangu alipotajwa kwenye kikosi hicho kwa mara ya mwisho msimu wa 2005-06.
“Nilipokuja, nilikuja na swali: Nitamkuta John wa aina gani? Atafanya nini? Ataimarika? Atamkaribia John yule ninaemfahamu mimi?” Mourinho aliuambia mtandao wa ESPN.
Kabla ya ujio wa Mourinho 2013, hatma ya Terry ilikuwa mashakani ndani ya Stamford Bridge na alikuwa na wakati mgumu wakati wa utawala wa Rafa Benitez.
Mchezaji huyo wa zamani wa kikosi cha England alianza kwenye mechi 24 kati ya 69 ambazo Chelsea ilicheza kwenye mashindano yote kwa msimu wa 2012-13. Mourinho akaongeza kuwa hakujua kuwa, ubora wa beki huyo ulikuwa uko mikononi mwake.
“Hususan kabla sijaja wakati wa kipindi cha Rafael Benitez nilidhani huyu mtu amekwisha kwasababu alikuwa hachezi mechi kubwa nikafikiri atakuwa kwenye matatizo”.
Chelsea wanaanza mapambano ya msimu mpya mwishoni mwa juma hili kwenye dimba la Wembley, wakati watakapopambana na Arsenal kuwania taji la kwanza la ngao ya jamii.
Chelsea imepata nafasi hiyo ya kucheza mchezo wa ngao ya jamii baada ya kushinda taji la ligi kuu ya England wakai Arsenal wao walishinda kombe la FA.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...