28 July, 2015

MOURINHO: HAZARD NI BORA KULIKO RONALDO

Eden Hazard
Winga wa Chelsea Eden Hazard ni lazima azingatiwe kuwa miongini mwa wachezaji watatu bora wa dunia- yaani juu ya Cristiano Ronaldo kwa sasa, hayo ni maneno ya kocha Jose Mourinho .
Ronaldo na Lionel Messi wamekuwa wakipokezana tuzo ya mchezaji bora wa dunia (Ballon d’Or), kwa miaka ya hivi karibuni, huku wakiwa wanafunga mamia ya magoli huko ligi kuu nchini Uhispania, lakini bosi huyo wa ‘The Blues’ amesema kitendo cha Ronaldo kukosa kombe lolote msimu uliopita ndio sababu ya kuwa nyuma ya Hazard.
Hazard alichukua tuzo ya mchezaji bora wa ligi ya Uingereza msimu wa 2014-15 huku Chelsea wakitwaa ndoo hiyo, hivyo Mourinho anasema hii ndio sababu ya winga wake kupewa mazingatio makubwa katika hili.
“Ni dhahiri inategemeana na msimu walionao”, aliwaambia waandishi. “Wanatakiwa kushinda makombe tu, au sio? Mpira bila ya makombe ni sawa na hamna kitu”.
“Messi alishinda makombe matatu. Ameshinda michuano mitatu mwaka jana, vile vile amefika fainali ya Copa America. Alikuwa na msimu bora kabisa na kwa timu yake pia. Sipendi wachezaji au mameneja wanajishindia tuzo binafsi bila ya timu.
“Msimu uliopita, ndio”, Mourinho aliendelea wakati alipoulizwa kama Hazard alikuwa na msimu bora kuliko Ronaldo”, bila kujali kwamba Ronaldo alikuwa yuko vizuri. Alikuwa yuko vizurri sana. Alifunga idadi ya magoli ya kutosha tu.
“Sina shaka kwamba ni mchezaji wa kiwango cha juu. Ninachosema ni kwamba, kwa mtazamo wangu, kila mcheza soka duniani lazima aelewe kwamba timu lazima iwe mbele ya makombe (timu kwanza, mchezaji baadaye)
“Eden anakuja kwa kasi sana sasa na alipaswa kuwa moja ya wachezaji bora Ulaya mwaka uliopita. Lakini kwa mtazamo wangu ni kwamba anatakiwa kuwa kwenye tatu bora na sio kumi bora.
“Nadhani Eden ni mchezaji bora wa nchi yetu. Mchezaji bora wa Uingereza. [Chama cha Waandishi wa Habari za Soka] walimpigia kura pia, mchezaji bora wa EPL.Kama ilivyo ada EPL ni ligi bora duniani, Nadhani ni miongoni mwa wachezaji wa kiwango cha juu duniani”.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...