08 July, 2015

Klabu ya Mnchester United inakaribia kukamilisha dili la kumsajili beki wa kulia Matteo Darmian

Darmian MatteoKlabu ya Mnchester United inakaribia kukamilisha dili la kumsajili beki wa kulia Matteo Darmian baada ya majadiliano kati ya United na klabu ya Torino ya Italia kufikia hatua nzuri.
United wanahitaji mchezaji ambaye anaweza akacheza kama mlinzi wa kulia baada ya kocha wa kikosi hicho Louis van Gaal kusema kwamba, mbrazil Rafae ameshindwa kuimudu nafasi hiyo.
Ieleweke kwamba, Man United imekuwa kwenye mazungumzo na Darmian, 25, na wanamatumaini ya kufikia makubaliano ya kumsajili nyota huyo kwa kiasi cha pauni milioni 11.
Darmian ni mchezaji wa kimataifa wa Italia ambaye ameshaitumikia timu yake ya taifa kwa michezo 13 na michezo sita akicheza muda wote (full time), Van Gaal anaamini mchezaji huyo atamsaidia kwenye nafasi ya ulinzi wa kulia.
Darmian Matteo 1Pia Van Gaal anatarajia kumuachia Rafael aondoke kabla ya kuanza kwa msimu mpya lakini atasikiliza ofa pia juu ya mlinzi wa kati John Evans ambaye mpaka sasa bado hajapewa mkataba mpya.
Usisumbuke Mawerenewz.blogspot.com ndio mtandao wako wakipekee unaokupa habari za BURUDANI,MICHEZO, SIASA, na HABARI MBALIMBALI ZA KIMATAIFA pamoja na KITAIFA Endelea kutembelea MTOKA MBALI pia nifuate twitter>>>@mawere3, facebook>>>Mawere Mtoka Mbali, Instagram>>>mawere_mtoka_mbali,

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...