09 July, 2015

Diamond Platnumz Kaguswa na hotuba ya Rais Kikwete

ddd
Baada  ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete kulianga rasmi bunge mjini Dodoma msanii wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz ameguswa na hotuba hiyo.
Diamond Platnumz ameamplify leo kwenye AMPLIFAYA na kusema’Kipindi ambacho nimebahatika kumuona Mheshimiwa madaraka na vitu ambacho amevifanya kiukweli ni vitu ambavyo vinagusa sana hususa katika tasnia ya kwetu ya muziki unajua hatujawahi kupata mheshimiwa ambaye akawa anatizama suala la muziki na kulithamini kama la kwake kabisa sio tu suala la muziki na vitu vingi sana mimi sio mtu wa kusikiliza masuala ya siasa wala kuangalia masuala ya kisiasa‘ – Diamond Platnumz
.
.
‘Leo kwa Mara ya kwanza nilikuwa naendesha gari huku nasikiliza vitu mwanzo mpaka mwisho kuna vitu ambacho alikuwa anazungumza vinagusa moyoni kabisa kuna vitu alikuwa anaongea vya kuchekesha lakini kuna time nilikuwa nafikiri Je rais atakaekuja atakuaje atakuwa kweli anakumbuka jamii yake ukizungumzia kama wasanii na watu wengine kama alivyokuwa anafanya yeye kwasababu sio kila mtu anachukulia suala la sanaa kama serious mwingine anaweza akaona vijana hawa wanaimba imba tu lakini wengine ndio ajira yetu tunafamilia wazazi wetu ndugu marafiki na tumeajiriana wenye wenye’ – Diamond Platnumz
deee
.
‘Nikajikuta ghafla daah Je Rais atakayekuja ikiwa Je anapenda uvuvi akiwa anapenda vitu vingine labda muziki akaudharua itabidi tukashika nyavu tukavue na suala la muziki linaishia hapo hapo hakuna masuala ya Channel O au MTV nikajikuta nawaza nikajikuta naandika kutoka moyoni hakika katutoa kule anatuacha hapa ambako pako juu zaidi kama kauli yake mwenye alivyosema inagusa moyoni yaani unatamani kama inawezekana wala apewa muhula mwingine aendele tena lakini ndio haiwezekani kisheria lakini ndo hivyo namshukuru sana nampongeza kwa kipindi ambacho akiwa akilihutubia taifa la Tanzania’ – Diamond Platnumz

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...