11 July, 2015

MAYWEATHER KURUDI TENA ULINGONI

Floyd Mayweather Jr. reacts after defeating Robert Guerrero by unanimous decision during a WBC welterweight title fight, Saturday, May 4, 2013, in Las Vegas. (AP Photo/Isaac Brekken)
Baada ya kumbwaga Mphilopino Many Pacquiao, bondia ambaye hajaonja ladha ya kipigo katika mchezo wa masumbwi, Floyd Mayweather Jr amethibitisha kupanda tena ulingoni Septemba 12 mwaka huu katika pambano linalotaraji kufanyika mjini Las Vegas Marekani.
Mayweather ambaye ameshinda mapambano 48 aliyopanda ulingoni bila sare wala kupoteza akishinda mapambano 26 kwa ‘knockout’, anashikilia mataji ya WBC na WBA katika uzito wa ‘welter’ aliudhihirishia ulimwengu ubora wake kwa kumtwanga kwa wingi wa alama mpinzani wake Many Pacquiao katika pambao lililovunja rekodi ya mapato katika mchezo wa ngumi ulimwenguni.
Mmarekani huyo aliyepokonywa mkanda wa WBO baada ya kukiuka masharti mapema wiki hii, ametuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii ukiashiria kurudi kwake ulingoni kabla ya kuisha kwa mwaka huu.
“Kwa mashabiki wangu. Uaminifu wenu na sapoti yenu vimenipa miaka 20 bora ambayo ningeiomba. Na nikiwa juu, napanga kwenda juu. Tukutane tena ulingoni Septemba 12,” ulisomeka ujumbe wa Mayweather.
Taarifa hizo zinaweza kuibua fununu nyingi juu ya nani atavaana na bondia huyo katika pambano hilo kwani mabondia kadhaa wameshatajwa kupanda naye ulingoni akiwemo Andre Berto aliyeshinda mapambano 30 na 23 kwa ‘knockout’ pamoja na Karim Mayfield aliyeshinda mapambano 19 huku  11 kati ya hayo akimaliza kwa ‘knockout.’
Mwingine anayevumishwa kupanda ulingoni na bingwa huyo ni bingwa wa zamani wa dunia Amir Khan ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa akisaka nafasi ya kuzichapa na Mayweather bila mafanikio lakini itawabidi wapenzi wa ndondi kusubiri mpaka itakapotangzwa rasmi ni bondia gani atakwenda kuendeleza au kuvunja rekodi ya nguli huyo wa mchezo wa masumbwi ulimwenguni kwa sasa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...