10 December, 2015

Rais wa Argentina awaaga raia wake


Rais wa Argentina aliyemaliza muda wake , Cristina Fernandez de Kirchner, amewaaga maelfu ya wafuasi wake ambao walikusanyika katikati mwa mji wa Buenos Aires.
Katika hotuba yake ambayo ilijaa hisia nje ya ikulu, Fernandez alivishutumu vyombo vya habari vya nchi hiyo kwa kuipiga vita serikali yake ya mrengo wa kushoto.
Fernandez na mume wake ambae tayari ameaga dunia, Nestor Kirchner, wamekuwa madarakani kwa muda wa miaka kumi na mbili.
Ametetea hali ya uchumi, na kusema hakuna katika utawala uliopita ambao uliiacha Argentina bila madeni.
Na kuwataka raia wa Argentia kutetea haki zao na maslahi yao ambayo wameyapata.
Makundi yaliyokusanyika katika eneo hilo yalikuwa yakiimba wakati Fernandezi akipanda katika jukwaa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...