20 August, 2015

HII NDIO SABABU KUBWA YA KASEJA KUCHAGUA KUJIUNGA NA MBEYA CITY…

kaseja

Bada ya mlinda mlango wa zamani wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ Juma Kaseja kusaini mkataba wa miezi sita kujiunga na timu ya Mbeya City ya mkoani Mbeya, kipa huyo mkongwe ameweka wazi ni kwanini amejiunga na timu hiyo ya wagonga nyungo wa jiji la Mbeya wakati kulikuwa na vilabu vingi vikiiwinda saini yake.
Kaseja amesema, kikubwa alichoangalia kabla ya kuamua kusaini mkataba wa kuitumikia klabu ya Mbeya City ni ushindani wa klabu atakayokwenda kucheza kwenye ligi kuu Tanzania bara na baadae kuamua kujiunga na Mbeya City.
“Kwanza nachoweza kusema ni kwamba, naviheshimu vilabu vyote, naiheshimu Coast, African Sports, Ndanda, Mwadui na timu zote zinazocheza ligi kuu ni timu kubwa kwahiyo zote naziheshimu. Nilijaribu kuwa mtulivu kwa kipindi chote hiki kuangalia ni timu ipi nitaenda kucheza ambayo itakuwa na ushindani mkubwa”, amesema Kaseja.
Kaseja anaesubiri kujumuishwa kwenye kikosi cha Mbeya City amewaomba wachezaji wenzake wa kikosi hicho pamoja na mashabiki wa timu hiyo kuwa na muungano, umoja na amani ili kuifikisha timu yao pale ambapo kila mwana Mbeya City anataka timu hiyo ifike.
Hapa chini nimekuwekea stori nzima ya Kaseja wakati akifanya mahojiano na Shaffih Dauda, bofya hapo kusikila kila kitu….

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...