22 August, 2015

MAKALA: WAKO WAPI MAN DOJO NA DOMOKAYA?

Awali ya yote nipende Kutoa Shukrani zangu za kipekee kwa mwenyezi Mungu kwa kunilinda wiki nzima hata nmepata nafaSi yakuwepo tena leo hii hapa mtoka mbali. Pia nichukue nafaSi hii kuku Shukuru we kamanda kwa kutembelea makala zetu na kuziSoma pia.
   
     Katika makala yetu leo tuna angaza jicho kwa wakali hawa wa bongo fleva ambao miaka ya nyuma waliweza kuzikonga nyoyo za maShapiki  wao vilivyo, na hawa si wengine ni MAN DOJO NA DOMO KAYA. Naweza sema kwamba vijana hawa sii wageni kuwaskia maskioni mwako kwani waliweza kuziteka media tofauti tofauti zenye ukubwa hapa Tanzania na hata nchi za njee kwa vibao vyao vilivyo kua vimejaa ujumbe tele kwa jamii mfano DINGI, BARUA, na NIKUPE NINI. Hivyo ni baadhi ya vibao walivyopata kutesa navyo kipindi cha miaka ya mwanzoni mwa 2000.
    Jambo lakujiuliza ni je wakali hawa wamepotelea wapi?
Ni wazi kwamba leo hii ukipata nafasi yaku onana nao, swali utakalo wauliza ni mbona siku hizi hatuwasikii? Hicho ndicho kilichomo katika fikra za mashabiki wa hawa wakali au ukipenda waite manguli wa bongo fleva. Yawezekana kabisa kwamba hawa jamaa wanatamani kurudi katika game ya muziki nakuwika tena kama ilivyokua mwanzini laki inakua ni vigumu kwani muziki wa bongo fleva unazidi kukua siku baada ya siku na kwa vile ukimya wao kwa muda mrefu bila kusikika, imefanya hata mashabiki wao kuwasahau kabisa. Lakini tukumbuke yakua wahenga walisema "hakuna marefu yasiyo na ncha" yawezekana katika game hii ya muziki wakizazi kipya imekua ngumu na wala sii rahisi kama ilivyokua kipindi cha nyuma ambapo muziki huu haukua na soko ki vile, na kwakusema hivyo ni dhahiri yakua wakali hawa wamepotea kabisa.
 Waliweza kutengeneza vibao vingi ambavyo nimeweza kuvitaja baadhi hapo juu na vingine ni kama vile HISTORIA, WANA KNOCK KNOCK, NIZIKWE HAI, na TASWIRA. Kama kweli wewe ni mpenzi wa muziki wa bongo ni wazi kua vibao hivi vilikukonga moyo ipasavyo na hadi leo unawakumbuka hawa jamaa vilivyo.
      Siwezi sema yakwamba hawa jamaa hawawezi kurudi katika umahiri wao kama mwamzo ila jitihada na juhudi zao ndizo zitawaleta tena kwatika game ya muziki na kuwika tena mbele ya wadogo zao katika muziki huu wa bongo fleva.
  Ni malizie kwa kusema, "Yatupasa kuwakumbuka vijana kama hawa ambao mchano wao katika jamii ni mkubwa mno, tuwape shime pale wanapo anguka ili waweze rudi katika hai zao za kawaida masha kusonga mbele"

 Nipende kukushukuru wewe ulichukua muda wako adhimu na wenye dhamani kwa kukaa kitako nakusoma makala zetu. Endelea kutembelea MTOKA MBALI ili uweze kupata kile unachokitaka.

MAKALA hii imeandikwa na Francis Mawere kwa hisani ya MAWERE MEDIA GROUP Ltd
TUTUMIE email yako kupitia mtokambali2015@gmail.com au piga simu namba 0767322193

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...