20 February, 2016

Marekani yashambulia kambi ya IS Libya

Maafisa wa Marekani wamethibitisha kuwa ni ndege za Marekani zilizofanya mashambulio huko Libya wakiwalenga wanamgambo wa IS. Hata hivyo shambulio hilo la karibu na mji wa Sabratha,lililonuiwa kumlenga hasa mpiganaji mmoja wa Tunisia limeripotiwa kuwauwa watu 30 .
Mpiganaji huyo wa Tunisia anasemekana ndiye aliyefanya shambulio la mwaka jana katika kumbukumbu za Bardo na hoteli ya ufuoni mwa bahari ya Sousse huko Tunisia ambako watu zaidi ya 10 waliuawa.
Mashambulio hayo yalilenga kambi moja ya wapiganaji wa Islamic State na kumuua kiongozi mmoja mwenye itikadi kali ,maafisa wa Marekani wamesema. Noureddine Chouchane anahusishwa na mashambulio mawili nchini Tunisia mwaka uliopita ,ikiwemo shambulio lililowaua raia 30 wa Uingereza.
Kundi la IS limekuwa likifanya oparesheni zake nchini Libya kwa kipindi cha mwaka mmoja na Marekani inakadiria kwamba lina hadi wapiganaji 6,000 nchini humo.Libya inasalia katika machafuko ya wenyewe kwa wenyewe miaka minne baada ya kupinduliwa kwa aliyekuwa kiongozi wake Muammar Gaddafi,na inapiganiwa na makundi tofauti ikiwemo kundi la IS.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...