Mpiganaji huyo wa Tunisia anasemekana ndiye aliyefanya shambulio la mwaka jana katika kumbukumbu za Bardo na hoteli ya ufuoni mwa bahari ya Sousse huko Tunisia ambako watu zaidi ya 10 waliuawa.
Mashambulio hayo yalilenga kambi moja ya wapiganaji wa Islamic State na kumuua kiongozi mmoja mwenye itikadi kali ,maafisa wa Marekani wamesema. Noureddine Chouchane anahusishwa na mashambulio mawili nchini Tunisia mwaka uliopita ,ikiwemo shambulio lililowaua raia 30 wa Uingereza.
Kundi la IS limekuwa likifanya oparesheni zake nchini Libya kwa kipindi cha mwaka mmoja na Marekani inakadiria kwamba lina hadi wapiganaji 6,000 nchini humo.
No comments:
Post a Comment