Watu watatu wamepelekwa hospitali 
kaskazini mwa Siera leone wakiwa na majeraha yaliyotokana na kupigwa 
risasi baada ya kulumbana na askari juu ya mambo gani wanapaswa 
kuzingatia ili kuepukana na Ebola.
Polisi wamesema walirusha 
mabomu ya machozi baada ya vijana hao kuvamia kituo chao huko mjini 
Barmoi,eneo ambalo mtu mmoja alikufa kutokana na Ebola wiki iliyopita.la
 Nchi ya Siera leone ilitangaza kuwa iko huru na ugonjwa huo kabla ya 
kifo hicho kutokea.Vijana walikuwa na hasira juu ya kufungwa kwa soko katika mji mmoja nchini humo lakini utawala ulitanabahisha kwamba ulisimamisha shughuli hizo za kibiashara kuendelea sokoni ili waweze kubaini watu watatu walipotea huku wakiwa wameathirika na ugonjwa huo.
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment