05 August, 2015

Wakimbizi wa Somalia warejesha kwao

Wakimbizi wa kwanza 100 wamerejeshwa Somalia kufuatia makubaliano kati ya Shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikia maswala ya wakimbizi,UNHCR na serikali ya Kenya na Somalia.
malia
Uhamisho huo wa kujitolea wa wakimbizi umeafikiwa baada ya Kenya kutishia kuwafurusha wakimbizi wa Somalia baada ya mashambulizi ya kigaidi yaliyotekelezwa na kundi la wapiganaji kutoka Somalia al Shaabab.Awali Kenya ilikuwa inawasafirisha wakimbizi kwa mabasi lakini kutokana na changamoto za kiusalama katika eneo la Kaskazini Mashriki mwa Kenya ,UNHCR imeanzisha safari za moja kwa moja kutoka Daadab kwenda Somalia.
ds
Kiongozi wa UNHCR bwana Raouf Mazou anasema kuwa ”huu ni mwanzo mpya””Ndege za kwanza mbili, zimeondoka Daadab kuelekea Kismaayona miji mingine midogo ya Luuq na Baidoa.”Serikali ya Kenya ilikuwa imetishia kuwafurusha wakimbizi wa Somalia kutoka kwenye kambi ya Dadaab kufuatia ripoti za kijasusi zilizoeleza kuwa njama zote za mashambulizi ya Kundi la wapiganaji wa Kiislamu kutoka Somalia,Al Shabaab yalikuwa yakipangwa na kufanikishwa kutoka Dadaab.
ds2Kenya ilitoa amri hiyo punde baada ya wanamgambo wa kiislamu wa Al Shabaab kuwaua wanafunzi wakristu takriban 150 katika chuo kikuu cha Garissa mapema mwezi Aprili.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...