06 August, 2015

Sudan Kusini:Mazungumzo ya amani yaanza


Mazungumzo mapya yanayolenga kumaliza mgogoro wa vita vya wenyewe kwa wenyewe wa miezi 19 Sudan Kusini yameanza katika mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Wapatanishi kutoka shirika la IGAD wanajaribu kuwarai rais Salva Kiir na kiongozi wa waasi Riek Machar kutia sahihi mkataba wa amani kufikia mwezi Agosti.
Bwana Machar amesema kuwa makataa yaliowekwa ni vigumu kuyaafikia.
Baraza la makanisa lenye ushawishi mkubwa nchini humo limewataka viongozi hao wawili kusitisha vita hivyo mara moja ,likisema haikubaliki kwamba watu wanaendelea kufariki huku wao wakizozania mamlaka.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...