05 August, 2015

Albamu Ya Dr.Dre Ya “Compton” Itatoka Kwa Mara Ya Kwanza Mtandaoni

Albamu ya “The Chronic” rapper Dr. Dre itatoka kwenye mtandao lakini haitakuwa halisi yenyewe lakini kupitia kwenye mitandao ndio itakuwa sehemu ya kwanza kusikiliza mzigo huo.

Albamu hiyo inayokuja ya “Compton” itapatikana kupitia Apple Music kuanzia saa 6pm-9pm PST siku ya Alhamisi Agosti 6, taarifa kupitia Beats 1 radio zimetengazwa na mtangazaji Zane Lowe.

“Listen to the premiere of @drdre new album, Compton,” (August 4). “Uncensored & exclusively on @AppleMusic.” Aliandika Lowe

Dr. Dre alitangaza albamu hiyo siku ya Jumamosi Agosti 1, kupitia kipindi chake cha “The Pharmacy” kupitia radio ya Beats 1, kwenye albamu hiyo ameshirikishwa Eminem, The Game, Kendrick Lamar, Jon Connor, Snoop Dogg, King Mez na wengine, albamu hiyo imepangwa kutoka Jumamosi Agosti 8.

Mwanzilishi huyo wa Aftermath alisema alivutiwa na filamu inayokuja ya N.W.A movie, Staright Outta Compton ndo maana akaamua atengeneza albamu yake ya kwanza baada ya zaidi ya miaka 10, filamu inatarajiwa kutoka Agosti 14.

Wapenda hip hop, movies get ready to hit the bottons na theaters….compton1

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...