15 December, 2015

Ijue smartphone inayokaa chaji siku 15.. (+Video)


Mawasiliano muhimu sana mtu wangu, ndio maana watu wengi wanaona umuhimu wa kuwa na smartphone ili mawasiliano ya njia nyingi yaweze kumfikia.
Wataalam wa mambo wakaingia kazini na kubuni kitu kinaitwa powerbank… ambayo kama smartphone yako ikiisha chaji basi hiyo inakusaidia uendelee kubaki hewani, lakini simu+powerbank ni sawa na mizigo miwili ya kubeba mkononi, usijali… Wachina wanajali mahitaji yako.
CHINA
Kwa sababu unahitaji kitu nafuu, usipitwe na stori kwamba Wachina wameingia chimbo na kuja na mzigo wa smartphone ambazo zinaweza kukaa chaji kwa siku 15, hesabu hiyo kwa lugha nyingine ni kwamba inakaa na chaji kwa wiki mbili kamili !!
Simu yenyewe inaitwa Oukitel K10000 ambayo Wachina wenyewe wamesogezewa tayari sokoni ndani ya nchi yao na pia inapatikana Marekani kwa bei ya kama dola 239 ambazo kwa TZ inasomeka kwa shilingi 515,000/=…. Kaa tayari mtu wa nguvu, mzigo unaweza kugusa sokoni Afrika pia.
Unaweza kuiangalia simu yenyewe hapa, kama huna imani na vitu vya kichina cheki na hiki

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...