Everton imemsajili mchezaji wa
kimataifa Yannick Bolasie raia wa Dr Congo anayechezea timu ya Crystal
Palace kwa gharama ya paund milioni 25, kwa mkataba wa miaka 5.Bolasie,
mwenye umri wa miaka 27, alitumia misimu minne akiwa na timu ya Palace
baada ya kujiunga na timu ya Bristol City ya mjini London mwaka 2012.
Amesukuma
gozi mara 143 akiwa na timu ya Palacena kufanikiwa kufunga magoli
kumi na tatu , na baadaye akabadilika na kuwa kiungo mbadala katika
mechi ya mwishoni mwa wiki iliyopita pale timu yake ilipofungwa na West
Brom bao moja kwa nunge.
Meneja wa timu ya Palace Alan Pardew
alisema baada ya kufungwa bao moja kwa yai tulitambua kuwa moyo na
nafsi yake ziko viko mahali kwingine
Bolasie anasema kwamba
uamuzi wa kuhamia upande wa Mersey haukuwa wa busara na kuongeza kwamba
lakini sasa nimeibukia Everton, kazi haijafanyika bado .Napaswa kufanya
kazi kwa juhudi na maarifa na kujisikia nimo ndani yake.Niko tayari
kukabiliana na changamoto zilizoko mbele yangu.sio suala la pesa kwa
upande wangu ,suala ni kutimiza malengo ya baadaye ya klabu na kule
ambako wanatarajia kuifikisha, napenda tu kucheza mpira.
Naye
meneja wa timu ya Everton Ronald Koeman anasema kwamba mchezaji huyo
Yannick ni mchezaji aliyekuwa anamnyemelea muda mrefu ulio pita
kwasababu ni aina ya winga anaye mpenda ,kwanza ana kasi,ana nguvu, na
anao uwezo mkubwa wa kucheza katika nafasi mbali mbali hasa mstari wa
mbele.
Bolasie ni mchezaji wa nne kusajiliwa na Everton katika majira haya .
Moja
ya majembe hayo yaliyosajiliwa ni pamoja na mlinda mlango Maarten
Stekelenburg anatokea timu ya Fulham, Idrissa Gueye kutoka Aston Villa,
wakati kiongozi wa timu ya Wales Ashley Williams aliungana na timu
hiyo tarehe kumi ya mwezi huu akitokea Swansea kwa ada isiyojulikana,
huku ikidhaniwa kuwa ni paundi milioni kumi na mbili.
Everton,ilitoka
sare ya goli 1-1 mwishoni mwa juma lililopita na timu ya Tottenham ,
wako kwenye mazungumzo ya kumsajili beki wa Sunderland Lamine Kone huku
nia ikiwa wazi ya kusalia na mshambuliaji Romelu Lukaku.
Mfanya
biashara mkuwa kutoka nchini Irani Farhad Moshiri amenunua hisa
asilimia 49.9 % katika timu ya Everton mapema mwaka huu mnamo mwezi wa
pili , na kuhitimisha ukame wa muongo mzima wa kusaka uwekezaji mpya.
CHANZO: BBC