12 May, 2016

New Video: Ben-Pol "moyo mashine"

Kwa muda mrefu sasa Ben-Pol amekuwa akizidi kutamba katika game la Muziki wa r&b hapa nyumbani na Africa mashariki kwa ujumla wake, na leo katuletea Video mpya inayo kwenda kwa jina la Moyo Mashine aloifanya huko Bondeni kwa Mzee Mandela.

Download Music: Alikiba Ft. M.I - Aje

 
 Alikikiba leo katuletea single yake mpya inayokwenda kwa jina la "AJE" akimshirikisha vyema Rapper M.I kutika kule Nigeria.

11 May, 2016

Acha kuogopa maisha, Thubutu kufanya...

“Kuzaliwa Masikini Sio Kosa Lako, ila Kufa Masikini ni Kosa Lako Kubwa Sana”Msingi wa kufanikiwa ni kuthubutu kufanya jambo fulani kwa mfano kufungua miradi, kufanya biashara, kusoma kwa bidii na mambo mengine kibao.


Ngoja nikuulize tena, maana najua utakua ushaulizwa hili swali mara nying, Hivii unatamani kuishi au uwe kama nani ? wengi wetu mtasema natamani kuishi maisha mazuri na bora.


Hii iko hivi unapozungumza na watu wote duniani kila mtu atakwambia kuwa anataka kuwa na maisha mazuri ,huenda na ni vigumu kwa mtu wa kawaida kusema anataka maisha yake yawe ya shida kila siku. Huyo atakua ana lake.Wewe una stashahada una shahada na elimu nyingine nyingi, sijui umeahudhulia workshop kama ishirini, ila ndugu yangu bado utaendelea kuchapwa bakora na maisha kama hautakuwa makini na kuthubutu kufanya mambo unayotamani kufanya.


 Kusoma sana ama kidogo kuwa na marafiki waliofanikiwa ama wasiofanikiwa,kwenda nje ya nchi ama au kuzaliwa katika familia masikini au tajiri bado sio tiketi ya kukufanya uwe na maisha bora .


Kuna watu kwa mfano unaweza kuona anakata tamaa eti kisa amezaliwa katika familia maskini kitu ambacho sio sahihi.Bill Gates alisema “Kuzaliwa Masikini Sio Kosa Lako, ila Kufa Masikini ni Kosa Lako Kubwa Sana”


Yaani anamaanisha duniani kuna fursa nyingi sana ambazo unaweza kuzitumia na kuwa na maisha unayoyataka.


Kuwa na maisha bora ni kufanya kazi kwa bidii na  kwa malengo zaidi usiishi tuu ilimradi siku zinaenda mbele. Kwa chochote unachokifanya kifanye kwa kutafakari na kuangalia faida na hasara yake.

Yapo mambo mengi ambayo yameweza kuzungumzwa ambayo yanaweza kukusababishia wewe kusonga mbele kimaisha lakini hata ukisoma mambo mengi yanayohusu mambo ya kimaisha bila kuthubutu kufanya kitu unachotaka kufanya ni kazi bure.


 Inabidi kuwatathimini watu ambao wanakuzunguka, kuanzia marafiki, majirani, na hata baadhi ya ndugu.Kuna wengine hata ukimwangalia sura yake tu anaonekana wazi kuwa hana furaha unapomwambia kuwa mambo yako yanakwenda vizuri kwa sababu watu wengi wanapenda kusikia kuwa unaishi maisha ya shida ndio wengi walivyo na wakijua hivyo ndio unaongeza uoga wa kuthubutu kufanya kazi. Sijui kwa nini hii inatokea, lakini achana na hao wewe kazana kubuni miradi mingi ili uwe na maendeleo bora maana wao kukasirika haikuzuii kufanya mambo yako.


Mafanikio yako yanatokana na akili yako ulionayo maana wengine wamekuwa wakisema kuwa ugumu wa maisha ndio kipimo chako cha akili yako.


Katika jamii tunakoishi utakua ushasikia watu wanalalamika kuwa maisha ni magumu,na hawajui wafanyaje lakini nikwambie kuwa kipimo cha maisha unacho hapo wewe mwenyewe na akili yako. Kama unajua kusoma na kuandika ni tosha kabisa kwa wewe kujiendeleza.


Kwaiyo jamani ni vizuri ukakaa na kutathimini unatamani maisha yako yaweje au unataka kuishi vipi  au maisha yako yakae katika level gani ya kimaisha hapa duniani? Kipimo cha maisha ambayo unataka  kuishi unacho wewe mwenyewe pia uoga wako ndo umaskini wako yawezekana hapo ulipo kaa una wasiwasi ,una uoga ,unawaza una tathimini wakati nguvu unazo, sababu unazo, elimu unayo vifaa pia unavyo. Ila… kwa kumalizia Kitu kimoja tu unahitaji ndugu yangu. “JITUME”.


Ukitaka kuelewa hii angalia wiki nzima iliyopita kama umefanya kitu ambacho kinaendana na mambo ambayo unataka kufaninikiwa maishani mwako. Kama kipo Good… kama hakipo, basi anza kujituma leo… yaani leo namaanisha anza kupanga mikakati, kama serikali inavyoweka mipango na mikakati ya miradi yake kwa wananchi na wewe kaa chini tengeneza mikakati ya maisha yako.


Kumbuka Unapanga mikakati ya maisha YAKO! Sio ya jirani yako ambae anakusema sema kila siku au mlie kosana nae juzi.


PITIA NA HIZI PIA

   >>> Tuzungumze yanayo tusibu na Kupata suluhisho.

  >>>  Viashiria 6 ni kwa nini unatakiwa kubadili Maisha yako Leo.  

 >>>    Furaha ya kweli inaletwa na wewe mwenyewe.


09 May, 2016

Josee Chemelion ni nani?


Who Is Dr Jose Chameleone Moja kati ya Wana muziki nguli katika ulimwengu  wa Burudani ya Muziki kwa upande wa Africa mashariki na Africa kwa Ujumla ni Josee Chemelion.

Jina lake kamili anajulikana kama Joseph Mayanja na alizaliwa mnamo mwaka 1979 Huko nchini Uganda. Josee Chamelion alianza kazi za sanaa mnamo mika ya 1990 nakuendelea wakati akiwa sekondary na alianza kama Mc na Dj kwenye Night clubs..

Baadae alijiunga na Ogopa Djs nchini kenya na Ngoma yake ya kwanza kufanya ilikuwa ikijulikana kama "BAGEYA" mabayo alimsha Mkali mwingine kutoka kenye anaekwenda kwa jina la Red-son.
Aina ya muziki anayoimba Josee ni muunganiko wa ladha za muziki aina zouk, Rumba, na ragga na muziki kidogo kutoka pale Uganda kidogo.

Mpaka ilipo fika mwaka 2013 Chamelion alikuwa teyari ana album zipatazo 12 na album hizo ni Bageya-2000, “Mama Mia” - 2001, “Njo Karibu”- 2002, “The Golden Voice”- 2003, “Mambo Bado”-2004  “Kipepo” - 2005, "shida za dunia"-2006, "sivyo ndivyo"-2007, "Bayunga"-2009, "Vumilia"-2010, "Valu valu"-2012, Badilisha-2013.

Ni Raisi wa Ugandan Music label inayojulikana kwa jina la "Leone Island" ambayo ndani yake kuna wasanii kama Mosses Radio, Wheezle, AK 47 na wakali wengine wengi.

Ni member katika kundi la wasanii nchini Uganda ambalo wasanii hao hutumia majina yao na umaarufu wako kupinga na kupambana na umasikini pamoja na HIV/AIDS,

Tuzo alizo wahi kutwaa ni kama ifuatavyo:-

  • Beffta Awards UK – Best International Act
  • 2003 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year, Best Male Artist, Best Contemporary Artist & Song of the Year ("Mama Mia")
  • 2004 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year & Song of the Year ("Jamila")
  • 2005 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group & Best Afro Beat Single ("Kipepeo")
  • 2004 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Bei Kali")
  • 2005 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Jamila")
  • 2006 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group
  • 2006 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Mama Rhoda) & Best Ugandan Music Video (Mama Rhoda)
  • 2007 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Sivyo Ndiviyo with Professor Jay)
  • 2011 Ugandan Radio Dotcom Music Awards – Artiste of The Year
  • 2013 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Valu Valu"
  • 2014 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Tubonge"
  • 2014 HiPipo Music Awards – Song of the Year "Badilisha"
  • 2014 HiPipo Music Awards – Best Male ZOUK Song "Badilisha"
  • 2015 AFRIMA Awards - Africa Song Writer of the year 2015

Enjoy video mpya kutoka kwa  Josee Chemelion inayokwenda kwa jina la Agatako.

Hayo ni machache tuu kuhusu nguli huyu wa muziki Africa, Je una maoni gani kuhusu Blog hii? tafadhali nitumie maoni yao katika cooment box na mimi nitayafanyia kazi.

Maajabu ya khanga!

  Na The Bitoz

 Hakuna mwanamke ambaye hajawahi kuvaa khanga, vilevile hakuna mwanaume ambaye hajawahi kufunikwa na khanga (utotoni si ulibebwa )....Yafuatayo ni maajabu ya khanga


1/Historia

Asili ya vazi hili ni pwani ya Afrika Mashariki kama sehemu za Mombasa nchini Kenya na visiwani Zanziba. Ndio walikuwa watu wa kwanza kulivaa vazi hili na kuliheshimu.Haijajulikana ilikuwa ni miaka gani. Kwahiyo historia inaonyesha vazi la khanga limeasisiwa na watu wa pwani ya Afrika Mashariki


2/Fahari ya Mwafrika

Khanga ni fahari kwa wanawake wa kiafrika , Ni vazi ambalo limetumiwa miaka kwa miaka, kizazi kwa kizazi.....ni utambulisho wa waafrika na halichuji !!


3/Linapendwa na rika zote

Khanga ndio vazi linalopendwa na wanawake wa aina zote, vijana kwa wazee, mjini kwa vijijini ....ni mwendo wa kutupia khanga !!


4/Matumizi kibao

Khanga ni vazi lenye matumizi mengi pengine kuliko yote, linatumika kubebea watoto, kufungia ngata,kama kamba.taulo n.k


5/Khanga moko ni shida

Wanawake wakitupia khanga moko mwanaume lazima utoe jicho , khanga moko uswahilini ni balaa hadi kwenye vigodoro....mwanamke khanga!!!


6/Vazi linalosema

Khanga huwakilisha hisia za mvaaji kupitia maneno yaliyoandikwa, kuna vijembe, busara,matusi, hekima n.k

 [​IMG]

Jionee mwenyewe maajabu haya .....

[​IMG]

Mwanamke khanga Babu weeee...


[​IMG] 

Tuzungumze yanayo tusibu na Kupata suluhisho.


Mtu mmoja alipata kusema "Hasara roho, pesa makaratasi" na mimi nasema ni kweli kabisa.
Je una Amani ya moyo mwako? Je uhuru ulio nao unautumiaje? Je ukitazama ndani ya Fikra zako unaona Mafanikio yeyote? Je una imani juu ya ndoto zako? Je una mpango wowote juu ya Kuthubutu kuishi ndani ya Ndoto zako?.....

     Leo nimepanda hapa MTOKAMBALI nikiuliza maswali hayo nikiwa na maana ya kwamba maswali hayo Yamekuwa chachu ya Mafanikio ya mtu yeyote hapa Ulimwenguni,,, Huwezi niambia ya kwamba utaweza kufanikiwa katika mambo yako angali Huna Amani Moyoni mwako wala kufanikiwa wakati umeshindwa kuutumia vyema Uhuru ulio nao ama Kufanikiwa angali hujawahi kuthubutu kufanya chochote juu ya ndoto zako...

Licha ya kuishi katika nchi yenye Uhuru lakini bado kuna vijana wenzangu hawana UHURU katika maisha yao. Wamekuwa wakiishi kama watumwa, wamekuwa wakipoteza hata matumaini yakuishi.. Hii yote inasababishwa na KIFUNGO CHA FIKRA.

Acha nikuambie rafiki yangu,
Hakuna jambo la muhimu na lenye nguvu katika maisha ya mwanadamu awaye yeyote hapa ulimwenguni litakalo weza kuishinda nguvu ya Fikra.(Weka kumbu-kumbu juu ya mstari huu tafadhali).

Kile ambacho unafikiri kwa Muda mrefu ndicho kitakachotokea katika maisha yako. Fikra zako zina nguvu ya uumbaji.. na zaidi ya yote fikra zako ndizo zitakazo kupatia Uhuru wa kweli katika maisha yako na mafanikio tele utayaona. Ila pale unapokuwa mtumwa wa fikra zako, hakika utatamani kuiona Ardhi inapasuka kisha Uingie ndani yake na kupotea katika ulimwengu huuu wenye dhiki tele.

Leo nitakupatia njia ambazo zitakufanya uondokane na Utumwa wa fikra zako na kisha kupata uhuru wa Fikra zako na kufanikiwa kuishi katika baadhi ya ndoto zako. Tambua yakwamba njia hizi nitakazo kupatia, ni njia ambazo nilizitumia mimi kipindi nikiwa Utumwani na hadi Leo nathubutu kusema "NIKO HURU".

Je uko teyari? lets move-on...

       1. Jiamini unaweza
Katika maisha ya mwanadamu ni lazima kila mmoja ajiamini kwamba anaweza. Mwana harakati mmoja aliwahi kusema "Uoga wako ndio umasikini wako". Njia ya kwanza ya kutoka katika kifungo cha fikra zako ni kuamini kwamba unaweza kuleta mabadiliko yeyote katika maisha yako licha ya hali uliyo nayo. Amini kwamba utaweza kuboresha maisha yako yakawa bora zaidi kama tuu utaongeza bidii katika hilo.

       2.Ondoa Mawazo hasi katika maisha yako.
Moja ya maadui wakubwa wa Uhuru wa fikra za mwanadamu na Maisha kwa ujumla ni Fikra hasi(potofu). Fikra hasi huwa na hulka ya kukua kidogo kidogo katika maisha ya mwanadamu awaye yote yule na mwishoni huleta maafa makubwa mno na majuto yale ya mjukuu. Ili kuepuka hali hii unapaswa kuchukulia mambo kwa upande wa chanya zaidi kuliko upande wa hasi... hii itakusaidia sana katika kufikiri kwenda mbele ya mafanikio yako. Fikra hasi hupoteza matumaini siku zote hivyo yakubidi kuziepuka.

      3.Epuka kuchukulia mambo kwa ujumla 
Kuna vijana wengi huchukulia mambo kirahisi kama yalivyo na mwisho wa siku wanajikuta katika hali ngumu mno katika maisha yao. Embu jaribu kuchambua jambo moja moja kwa kina kisha ainisha ni lipi jema na ni lipi baya katika huo ujumla ulio nayo. Kumbuka unapokuwa ukichukulia mambo kwa ujumla, hutopata changamoto yeyote ile ambayo itakufanya Kufikiri kwa kina.

       4.Thubutu kufanya.
Njia nyingine ya kutoka katika utumwa na kuupata uhuru wako ni kuthubutu kufanya kile ulicho nacho katika fikra zako juu ya maendeleo yako. Natambua kila mmoja wetu hapa ana ndoto fulani kubwa katika maisha yake na kama( huna ndoto yeyote katika maisha yako jua una hali mbaya kupindukia..). Je uliwahi kujaribu kuifika hata nusu ya ndoto zako? kama jibu ni ndio basi endelea na safari maana bado kidogo utafika mpendwa na kama bado hujathubutu basi kwa nzia sasa thubutu.

     5.Acha kufanya mambo mengi kwa mawazo yako.
Mwanadamu hajakamilika siku zote na kila mwanadamu ana mapungufu yake , hivyo mapungufu yako wenda ikawa mwenzako anaweza kuyatua na wewe pia unaweza kuyatatua, hivyo utaona ni kwa namna gani utakapo kuwa ukishirikiana na wenzako katika kutimiza mambo yako utafanikiwa zaidi kuliko kufanya peke yako..
       6.Jali muda wako.
Nafahamu kwamba kwa asilimia kubwa mno vijana wengi wamekuwa wakipoteza muda wao katika mambo yasiyo na msingi na mwisho wa siku wanajikuta hawajafanya mambo yaliyo wapasa kufanya kwa wakati ule na kuanza kujuta ni kwa nini..... Embu kabla ya kupata majuto, jaribu kufanya mambo katika muda husika bila hata kupoteza sekunde moja katika Muda wako. "Majuto ni mjukuu"

Kwa kusema hayo, nammba nikwamie hapo na ni matumaini yangu kwamba nimekupatia kile unachokihitaji. Nimejfunza mengi mno katika maisha haya licha ya Umri wangu mdogo nilio nao. Likini kwa kuwa naamini katika ndoto zangu, sioni kama naumia bali nayaona maisha yangu katika Ulimwengu wa mafanikio.

Je umependa somo langu? Tafadhali niachie maoni yako hapo chini.


NINEPENDA PIA UPITIE NA HIZI:-
>>>> Viashiria 6 ni kwa nini unatakiwa kubadili Maisha yako Leo

>>>> Furaha ya kweli inaletwa na wewe mwenyewe.

>>>>  Amani ya Moyoni mwako ndio Kunawiri kwa Uso wako.


08 May, 2016

Video: Shetta - Namjua

Tizama Video mpya ya Shetta inayokwenda kwa jina la Namjua. Mi wimbo wa kwanza wa Shetta alio fanya akiwa mwenyewe baada ya kipindi kirefu akiwa anafanya ngoma na wasanii wengine. Enjoy the Good Video From Shetta - Namjua

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...