12 May, 2016
Download Music: Alikiba Ft. M.I - Aje

Alikikiba leo katuletea single yake mpya inayokwenda kwa jina la "AJE" akimshirikisha vyema Rapper M.I kutika kule Nigeria.
11 May, 2016
Acha kuogopa maisha, Thubutu kufanya...
“Kuzaliwa Masikini Sio Kosa Lako, ila Kufa Masikini ni Kosa Lako Kubwa Sana”Msingi wa kufanikiwa ni kuthubutu kufanya jambo fulani kwa mfano kufungua miradi, kufanya biashara, kusoma kwa bidii na mambo mengine kibao.
Ngoja nikuulize tena, maana najua utakua ushaulizwa hili swali mara
nying, Hivii unatamani kuishi au uwe kama nani ? wengi wetu mtasema
natamani kuishi maisha mazuri na bora.
Hii iko hivi unapozungumza na watu wote duniani kila mtu atakwambia kuwa
anataka kuwa na maisha mazuri ,huenda na ni vigumu kwa mtu wa kawaida
kusema anataka maisha yake yawe ya shida kila siku. Huyo atakua ana
lake.Wewe una stashahada una shahada na elimu nyingine nyingi, sijui
umeahudhulia workshop kama ishirini, ila ndugu yangu bado utaendelea
kuchapwa bakora na maisha kama hautakuwa makini na kuthubutu kufanya
mambo unayotamani kufanya.
Kusoma sana ama kidogo kuwa na marafiki
waliofanikiwa ama wasiofanikiwa,kwenda nje ya nchi ama au kuzaliwa
katika familia masikini au tajiri bado sio tiketi ya kukufanya uwe na
maisha bora .
Kuna watu kwa mfano unaweza kuona anakata tamaa eti kisa amezaliwa
katika familia maskini kitu ambacho sio sahihi.Bill Gates alisema
“Kuzaliwa Masikini Sio Kosa Lako, ila Kufa Masikini ni Kosa Lako Kubwa
Sana”
Yaani anamaanisha duniani kuna fursa nyingi sana ambazo unaweza kuzitumia na kuwa na maisha unayoyataka.
Kuwa na maisha bora ni kufanya kazi kwa bidii na kwa malengo zaidi
usiishi tuu ilimradi siku zinaenda mbele. Kwa chochote unachokifanya
kifanye kwa kutafakari na kuangalia faida na hasara yake.
Yapo mambo mengi ambayo yameweza kuzungumzwa ambayo yanaweza kukusababishia wewe kusonga mbele kimaisha lakini hata ukisoma mambo mengi yanayohusu mambo ya kimaisha bila kuthubutu kufanya kitu unachotaka kufanya ni kazi bure.
Inabidi kuwatathimini watu ambao wanakuzunguka, kuanzia marafiki,
majirani, na hata baadhi ya ndugu.Kuna wengine hata ukimwangalia
sura yake tu anaonekana wazi kuwa hana furaha unapomwambia kuwa mambo
yako yanakwenda vizuri kwa sababu watu wengi wanapenda kusikia kuwa
unaishi maisha ya shida ndio wengi walivyo na wakijua hivyo ndio
unaongeza uoga wa kuthubutu kufanya kazi. Sijui kwa nini hii inatokea,
lakini achana na hao wewe kazana kubuni miradi mingi ili uwe na
maendeleo bora maana wao kukasirika haikuzuii kufanya mambo yako.
Mafanikio yako yanatokana na akili yako ulionayo maana wengine
wamekuwa wakisema kuwa ugumu wa maisha ndio kipimo chako cha akili yako.
Katika jamii tunakoishi utakua ushasikia watu wanalalamika kuwa maisha
ni magumu,na hawajui wafanyaje lakini nikwambie kuwa kipimo cha maisha
unacho hapo wewe mwenyewe na akili yako. Kama unajua kusoma na kuandika
ni tosha kabisa kwa wewe kujiendeleza.
Kwaiyo jamani ni vizuri ukakaa na kutathimini unatamani maisha yako
yaweje au unataka kuishi vipi au maisha yako yakae katika level gani ya
kimaisha hapa duniani? Kipimo cha maisha ambayo unataka kuishi unacho
wewe mwenyewe pia uoga wako ndo umaskini wako yawezekana hapo ulipo kaa
una wasiwasi ,una uoga ,unawaza una tathimini wakati nguvu unazo, sababu
unazo, elimu unayo vifaa pia unavyo. Ila… kwa kumalizia Kitu kimoja tu
unahitaji ndugu yangu. “JITUME”.
Ukitaka kuelewa hii angalia wiki nzima iliyopita kama umefanya kitu
ambacho kinaendana na mambo ambayo unataka kufaninikiwa maishani mwako.
Kama kipo Good… kama hakipo, basi anza kujituma leo… yaani leo
namaanisha anza kupanga mikakati, kama serikali inavyoweka mipango na
mikakati ya miradi yake kwa wananchi na wewe kaa chini tengeneza
mikakati ya maisha yako.
Kumbuka Unapanga mikakati ya maisha YAKO! Sio
ya jirani yako ambae anakusema sema kila siku au mlie kosana nae juzi.
PITIA NA HIZI PIA
>>> Tuzungumze yanayo tusibu na Kupata suluhisho.>>> Viashiria 6 ni kwa nini unatakiwa kubadili Maisha yako Leo.
>>> Furaha ya kweli inaletwa na wewe mwenyewe.
09 May, 2016
Josee Chemelion ni nani?
Jina lake kamili anajulikana kama Joseph Mayanja na alizaliwa mnamo mwaka 1979 Huko nchini Uganda. Josee Chamelion alianza kazi za sanaa mnamo mika ya 1990 nakuendelea wakati akiwa sekondary na alianza kama Mc na Dj kwenye Night clubs..
Baadae alijiunga na Ogopa Djs nchini kenya na Ngoma yake ya kwanza kufanya ilikuwa ikijulikana kama "BAGEYA" mabayo alimsha Mkali mwingine kutoka kenye anaekwenda kwa jina la Red-son.
Aina ya muziki anayoimba Josee ni muunganiko wa ladha za muziki aina zouk, Rumba, na ragga na muziki kidogo kutoka pale Uganda kidogo.
Mpaka ilipo fika mwaka 2013 Chamelion alikuwa teyari ana album zipatazo 12 na album hizo ni Bageya-2000, “Mama Mia” - 2001, “Njo Karibu”- 2002, “The Golden Voice”- 2003, “Mambo Bado”-2004 “Kipepo” - 2005, "shida za dunia"-2006, "sivyo ndivyo"-2007, "Bayunga"-2009, "Vumilia"-2010, "Valu valu"-2012, Badilisha-2013.
Ni Raisi wa Ugandan Music label inayojulikana kwa jina la "Leone Island" ambayo ndani yake kuna wasanii kama Mosses Radio, Wheezle, AK 47 na wakali wengine wengi.
Ni member katika kundi la wasanii nchini Uganda ambalo wasanii hao hutumia majina yao na umaarufu wako kupinga na kupambana na umasikini pamoja na HIV/AIDS,
Tuzo alizo wahi kutwaa ni kama ifuatavyo:-
- Beffta Awards UK – Best International Act
- 2003 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year, Best Male Artist, Best Contemporary Artist & Song of the Year ("Mama Mia")
- 2004 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Artiste of the Year & Song of the Year ("Jamila")
- 2005 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group & Best Afro Beat Single ("Kipepeo")
- 2004 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Bei Kali")
- 2005 Tanzania Music Awards – Best East African Album ("Jamila")
- 2006 Pearl of Africa Music Awards (PAM Awards) – Best Afro Beat Artiste/Group
- 2006 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Mama Rhoda) & Best Ugandan Music Video (Mama Rhoda)
- 2007 Kisima Music Awards – Best Ugandan Song (Sivyo Ndiviyo with Professor Jay)
- 2011 Ugandan Radio Dotcom Music Awards – Artiste of The Year
- 2013 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Valu Valu"
- 2014 [Kilimanjaro Music Awards] – Best East African Song "Tubonge"
- 2014 HiPipo Music Awards – Song of the Year "Badilisha"
- 2014 HiPipo Music Awards – Best Male ZOUK Song "Badilisha"
- 2015 AFRIMA Awards - Africa Song Writer of the year 2015
Enjoy video mpya kutoka kwa Josee Chemelion inayokwenda kwa jina la Agatako.
Maajabu ya khanga!
Na The Bitoz
Hakuna mwanamke ambaye hajawahi kuvaa khanga, vilevile hakuna mwanaume ambaye hajawahi kufunikwa na khanga (utotoni si ulibebwa )....Yafuatayo ni maajabu ya khanga
1/Historia
Asili ya vazi hili ni pwani ya Afrika Mashariki kama sehemu za Mombasa nchini Kenya na visiwani Zanziba. Ndio walikuwa watu wa kwanza kulivaa vazi hili na kuliheshimu.Haijajulikana ilikuwa ni miaka gani. Kwahiyo historia inaonyesha vazi la khanga limeasisiwa na watu wa pwani ya Afrika Mashariki
2/Fahari ya Mwafrika
Khanga ni fahari kwa wanawake wa kiafrika , Ni vazi ambalo limetumiwa miaka kwa miaka, kizazi kwa kizazi.....ni utambulisho wa waafrika na halichuji !!
3/Linapendwa na rika zote
Khanga ndio vazi linalopendwa na wanawake wa aina zote, vijana kwa wazee, mjini kwa vijijini ....ni mwendo wa kutupia khanga !!
4/Matumizi kibao
Khanga ni vazi lenye matumizi mengi pengine kuliko yote, linatumika kubebea watoto, kufungia ngata,kama kamba.taulo n.k
5/Khanga moko ni shida
Wanawake wakitupia khanga moko mwanaume lazima utoe jicho , khanga moko uswahilini ni balaa hadi kwenye vigodoro....mwanamke khanga!!!
6/Vazi linalosema
Khanga huwakilisha hisia za mvaaji kupitia maneno yaliyoandikwa, kuna vijembe, busara,matusi, hekima n.k
Jionee mwenyewe maajabu haya .....
Mwanamke khanga Babu weeee...
Tuzungumze yanayo tusibu na Kupata suluhisho.
Mtu mmoja alipata kusema "Hasara roho, pesa makaratasi" na mimi nasema ni kweli kabisa.
Je una Amani ya moyo mwako? Je uhuru ulio nao unautumiaje? Je ukitazama ndani ya Fikra zako unaona Mafanikio yeyote? Je una imani juu ya ndoto zako? Je una mpango wowote juu ya Kuthubutu kuishi ndani ya Ndoto zako?.....
Leo nimepanda hapa MTOKAMBALI nikiuliza maswali hayo nikiwa na maana ya kwamba maswali hayo Yamekuwa chachu ya Mafanikio ya mtu yeyote hapa Ulimwenguni,,, Huwezi niambia ya kwamba utaweza kufanikiwa katika mambo yako angali Huna Amani Moyoni mwako wala kufanikiwa wakati umeshindwa kuutumia vyema Uhuru ulio nao ama Kufanikiwa angali hujawahi kuthubutu kufanya chochote juu ya ndoto zako...
Licha ya kuishi katika nchi yenye Uhuru lakini bado kuna vijana wenzangu hawana UHURU katika maisha yao. Wamekuwa wakiishi kama watumwa, wamekuwa wakipoteza hata matumaini yakuishi.. Hii yote inasababishwa na KIFUNGO CHA FIKRA.
Acha nikuambie rafiki yangu,
Hakuna jambo la muhimu na lenye nguvu katika maisha ya mwanadamu awaye yeyote hapa ulimwenguni litakalo weza kuishinda nguvu ya Fikra.(Weka kumbu-kumbu juu ya mstari huu tafadhali).
Kile ambacho unafikiri kwa Muda mrefu ndicho kitakachotokea katika maisha yako. Fikra zako zina nguvu ya uumbaji.. na zaidi ya yote fikra zako ndizo zitakazo kupatia Uhuru wa kweli katika maisha yako na mafanikio tele utayaona. Ila pale unapokuwa mtumwa wa fikra zako, hakika utatamani kuiona Ardhi inapasuka kisha Uingie ndani yake na kupotea katika ulimwengu huuu wenye dhiki tele.
Leo nitakupatia njia ambazo zitakufanya uondokane na Utumwa wa fikra zako na kisha kupata uhuru wa Fikra zako na kufanikiwa kuishi katika baadhi ya ndoto zako. Tambua yakwamba njia hizi nitakazo kupatia, ni njia ambazo nilizitumia mimi kipindi nikiwa Utumwani na hadi Leo nathubutu kusema "NIKO HURU".
Je uko teyari? lets move-on...
1. Jiamini unaweza
Katika maisha ya mwanadamu ni lazima kila mmoja ajiamini kwamba anaweza. Mwana harakati mmoja aliwahi kusema "Uoga wako ndio umasikini wako". Njia ya kwanza ya kutoka katika kifungo cha fikra zako ni kuamini kwamba unaweza kuleta mabadiliko yeyote katika maisha yako licha ya hali uliyo nayo. Amini kwamba utaweza kuboresha maisha yako yakawa bora zaidi kama tuu utaongeza bidii katika hilo.
2.Ondoa Mawazo hasi katika maisha yako.
Moja ya maadui wakubwa wa Uhuru wa fikra za mwanadamu na Maisha kwa ujumla ni Fikra hasi(potofu). Fikra hasi huwa na hulka ya kukua kidogo kidogo katika maisha ya mwanadamu awaye yote yule na mwishoni huleta maafa makubwa mno na majuto yale ya mjukuu. Ili kuepuka hali hii unapaswa kuchukulia mambo kwa upande wa chanya zaidi kuliko upande wa hasi... hii itakusaidia sana katika kufikiri kwenda mbele ya mafanikio yako. Fikra hasi hupoteza matumaini siku zote hivyo yakubidi kuziepuka.
3.Epuka kuchukulia mambo kwa ujumla
Kuna vijana wengi huchukulia mambo kirahisi kama yalivyo na mwisho wa siku wanajikuta katika hali ngumu mno katika maisha yao. Embu jaribu kuchambua jambo moja moja kwa kina kisha ainisha ni lipi jema na ni lipi baya katika huo ujumla ulio nayo. Kumbuka unapokuwa ukichukulia mambo kwa ujumla, hutopata changamoto yeyote ile ambayo itakufanya Kufikiri kwa kina.
4.Thubutu kufanya.
Njia nyingine ya kutoka katika utumwa na kuupata uhuru wako ni kuthubutu kufanya kile ulicho nacho katika fikra zako juu ya maendeleo yako. Natambua kila mmoja wetu hapa ana ndoto fulani kubwa katika maisha yake na kama( huna ndoto yeyote katika maisha yako jua una hali mbaya kupindukia..). Je uliwahi kujaribu kuifika hata nusu ya ndoto zako? kama jibu ni ndio basi endelea na safari maana bado kidogo utafika mpendwa na kama bado hujathubutu basi kwa nzia sasa thubutu.
5.Acha kufanya mambo mengi kwa mawazo yako.
Mwanadamu hajakamilika siku zote na kila mwanadamu ana mapungufu yake , hivyo mapungufu yako wenda ikawa mwenzako anaweza kuyatua na wewe pia unaweza kuyatatua, hivyo utaona ni kwa namna gani utakapo kuwa ukishirikiana na wenzako katika kutimiza mambo yako utafanikiwa zaidi kuliko kufanya peke yako..
6.Jali muda wako.
Nafahamu kwamba kwa asilimia kubwa mno vijana wengi wamekuwa wakipoteza muda wao katika mambo yasiyo na msingi na mwisho wa siku wanajikuta hawajafanya mambo yaliyo wapasa kufanya kwa wakati ule na kuanza kujuta ni kwa nini..... Embu kabla ya kupata majuto, jaribu kufanya mambo katika muda husika bila hata kupoteza sekunde moja katika Muda wako. "Majuto ni mjukuu"
Kwa kusema hayo, nammba nikwamie hapo na ni matumaini yangu kwamba nimekupatia kile unachokihitaji. Nimejfunza mengi mno katika maisha haya licha ya Umri wangu mdogo nilio nao. Likini kwa kuwa naamini katika ndoto zangu, sioni kama naumia bali nayaona maisha yangu katika Ulimwengu wa mafanikio.
Je umependa somo langu? Tafadhali niachie maoni yako hapo chini.
NINEPENDA PIA UPITIE NA HIZI:-
>>>> Viashiria 6 ni kwa nini unatakiwa kubadili Maisha yako Leo
>>>> Furaha ya kweli inaletwa na wewe mwenyewe.
>>>> Amani ya Moyoni mwako ndio Kunawiri kwa Uso wako.
08 May, 2016
Video: Shetta - Namjua
Tizama Video mpya ya Shetta inayokwenda kwa jina la Namjua. Mi wimbo wa kwanza wa Shetta alio fanya akiwa mwenyewe baada ya kipindi kirefu akiwa anafanya ngoma na wasanii wengine. Enjoy the Good Video From Shetta - Namjua
Subscribe to:
Posts (Atom)
Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7
KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...
-
Mpenzi msomaji wa safu hii ni siku nyingine tunakutana katika kujuzana,kukumbushana, na kuelimishana mila na desturi za makabila mbalimbal...
-
This is a song sang by a very gifted woman Adele, I sang it to show world that everyone appreciate and love to enjoy good music! Asa...
-
Mboga za majani na matunda zimekuwa zikisisitizwa kwa sana na wataalamu wa afya hasa kwa wanawake wajawaziti kwani zimekuwa zikiongeza Damu...


