18 April, 2016

Furaha ya kweli inaletwa na wewe mwenyewe.

Well well well! Karibu tena MTOKAMBALI, imekua kitambo sasa tangu nmeondoka hapa Mtokambali na leo nmerudi tena na nmekuja kukupatia kile ulichokikosa kutoka kwangu. Kwanza nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu aliye hai kwa kunifanya kuiona tena siku hii nikiwa na Afya na Amani Moyoni mwangu, sii kwa akili zangu ama kwa ujanja wangu kufikia hapa nilipo ila ni kwa NEEMA tuu. Nikushukuru ewe mpenzi msomaji wa blog hii kwa kuzidi kutupatia ushirikiano wako.

Leo nmekuja na somo hili linalohusu FURAHA! hivyo nikukaribishe mpenzi msomaji kuwa nami katika somo hili na kabla ya yote nikupatie mwongozo mzima wa somo hili:
Baada ya somo hili utajifunza vitu vifuatavyo:-
1. Maana kamili ya Furaha
2.Mambo yanayokuzuia kutopata Furaha maishani mwako
3.Nini kifanyike ili kurejesha Furaha iliyo potea.

Maana kamili ya Furaha
Furaha kamili ni amani ya Moyo wako. Unajua wanadamu wengi tunashindwa kuelewa maana kamili ya neno Furaha, na matokeo yake tunaposhindwa kuipata Furaha hiyo tunaishia kutafuta furaha hiyo pasipo kuipata popote kumbe dawa ya tatito hiyo tunayo Mioyoni mwetu.

Kuna tofauti kubwa kati ya RAHA na FURAHA, raha ni Tukizo la mwili kutoka kwenye taabu na ifahamike kua raha hudumu kwa muda mchache angali Furaha hudumu Daima. Raha hutokana na Furaha.

Wacha nikupatie story kidogo juu ya Maisha yangu ya hapo awali. Kipindi nikiwa natoka utotoni na kuelekea huku ujanani nilipata tabu mno kuelewa ni FURAHA ya maisha yangu na kiukweli ilinichukua muda mwingi kupata jibu kamili juu ya swala hilo. Niliamini yakua nikiwa napenda raha za ulimwengu huu basi hapo nitakua nmemaliza kila kitu. Kwa kweli mwisho wa siku nilijipata katika hali mbaya sana nafsini mwangu hali ambayo nilikua napata msongo mkubwa wa mawazo, sikua na amani kwa kweli maana vile vyote nilivyo tamani kufanya ili kupata Furaha ya kweli nilikua nikivikosa kutokana na hali ya Umasikini niliokuwa nao. Niliumia na Ujana vilivyo na mwishowe nilivyo tafuta amani ya moyo wangu ndipo maisha yangu yakawa na FURAHA mpaka leo licha ya matatizo niliyo nayo bado nina Furaha moyoni mwangu.

Kwa maana hiyo basi tuanalie mambo ambayo yana kuzuia kupata Furaha maishani mwako
Yapo mambo mengi ambayo kwa namna moja ama nyingine yanakuzuia kupata Furaha ya kweli maishani mwako na mbo hayo yanaweza kuwa yanasababishwa na WEWE mwenyewe ama MAZINGIRA yanayo kuzunguka na mabo hayo ni kama yafuatayo.

1.Kukosa amani moyoni mwako.
Jambo hili limekua likitesa wanadamu tulio wengi hasa vijana, na hii inatokana na mambo mengi mfano Umasikini/ufukara, mapenzi, unyonyaji na hata rushwa na kutokumjua MUNGU. Unapokua na amani kwenye moyo wako, ni wazi kwamba hata akili hufunguka nakufanya mambo makubwa zaidi ya kimaendeleo na kiuchumi na hivyo maisha kuwa Murua kabisa na unapokosa amani hiyo ni wazi kua akili huvurugika nakuishia pabaya katika maendeleo yako kiuchumi na kiimani. Na mwishoni unakosa Furaha ya kweli maisha yako.

2.Kutokumjua Mungu.
Rafiki yangu kama mpaka leo Huamini kuwa Mungu yupo na kuamini kuwa yeye ndiye kila kitu katika kazi za mikono yako na maisha yako kwa ujumla basi umekwisha potea mazima. Unajua hakuna jambo zuri kama kumjua Mungu hapa duniani, Unaweza kuwa na Mali nyingi mno hapa dunia lakini bila Kumjua Mungu ni bure kabisa, utakosa mambo mengi ya muhimu mno kuliko mali ulizo nazo na Furaha ya kweli utaisikia kwa wegine huko barabarani.

3.Imani za kishirikina.
Asikufiche mtu hapa duniani hakuna watu wanaoteseka kama washirikina. Wamekua wakitabasamu katika nyuso zao wakati wakiwa kwenye makutano ya watu wengi lakini mioyoni mwao hawana amani kabisa. We mwenyewe unajiuliza iko wapi Furaha? Hivyo basi, unapokua unaamini katika mambo hayo hakika utakua umeipoteza FURAHA YA KWELI maishani mwako.

4.Wivu na husda usio na Tija.
Kuna watu huwa hawapendagi kuona mtu amepata kitu jamani katika ulimwengu huuu wa Mnyezi Mungu, wamekua wakiteseka mioyoni mwao kila kukicha kwamba "kwa nini Fulani kapata hichi?". We jiulize mtu kama huyo atakua na Furaha kweli?

5.Dhiki na changamoto za masha.
Dhiki imekua miongoni mwa changamoto za kimaisha na wengi inawapata taabu kweli kweli hapa duniani. Maandiko ya Mnyezi Mungu yanasema "Ulimwengu mna dhiki lakini jipeni Moyo". Hakuna haja yakufikiri kila siku juu ya taabu na mateso tuliyo nayo.

Hayo ni baadhi ya Mambo ambayo hutufanya wanadamu kuikosa furaha ya kweli na sasa tupate kutizama nini kifanyike ili kuirejesha Furaha iliyopotea;-

Ukiweza kutambua sababu kuu ni kwa nini unakosa furaha ya kweli basi itakua ni rahisi kutatua tatizo lako mazima. Mpende Mungu, Jiamini, Tafuta kuwa na amani ya kweli moyoni mwako, acha mambo yakishirikina, punguza wivu na Husda, Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe, Jifunze kusamehe, shukuru kwa kila jambo.
Kwa kufanya mambo hayo yote basi utakua umejitengenezea FURAHA YA KWELI maishani mwako.

Basi ndugu zanu nimefikia mwisho wa somo langu, na nikushukuru wewe ulipendezwa na somo hili na kuamua kulipitia mwambo mwisho "Ubarikiwe Tena na Tena" nikuache na neno la Mungu kutoka katiaka kitabu kile cha Wafilipi sura ya 4 mstari wa 4 hadi ule wa 5 ambao unasema "Furahini katika Bwana tena nasema Furahini, Upole wenu na ujulikane na watu wote, Bwana yu karibu" 
Aksanteni na tukutane tena katika somo jingine hapa hapaMTOKAMBALI.



No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...