09 May, 2016

Maajabu ya khanga!

  Na The Bitoz

 Hakuna mwanamke ambaye hajawahi kuvaa khanga, vilevile hakuna mwanaume ambaye hajawahi kufunikwa na khanga (utotoni si ulibebwa )....Yafuatayo ni maajabu ya khanga


1/Historia

Asili ya vazi hili ni pwani ya Afrika Mashariki kama sehemu za Mombasa nchini Kenya na visiwani Zanziba. Ndio walikuwa watu wa kwanza kulivaa vazi hili na kuliheshimu.Haijajulikana ilikuwa ni miaka gani. Kwahiyo historia inaonyesha vazi la khanga limeasisiwa na watu wa pwani ya Afrika Mashariki


2/Fahari ya Mwafrika

Khanga ni fahari kwa wanawake wa kiafrika , Ni vazi ambalo limetumiwa miaka kwa miaka, kizazi kwa kizazi.....ni utambulisho wa waafrika na halichuji !!


3/Linapendwa na rika zote

Khanga ndio vazi linalopendwa na wanawake wa aina zote, vijana kwa wazee, mjini kwa vijijini ....ni mwendo wa kutupia khanga !!


4/Matumizi kibao

Khanga ni vazi lenye matumizi mengi pengine kuliko yote, linatumika kubebea watoto, kufungia ngata,kama kamba.taulo n.k


5/Khanga moko ni shida

Wanawake wakitupia khanga moko mwanaume lazima utoe jicho , khanga moko uswahilini ni balaa hadi kwenye vigodoro....mwanamke khanga!!!


6/Vazi linalosema

Khanga huwakilisha hisia za mvaaji kupitia maneno yaliyoandikwa, kuna vijembe, busara,matusi, hekima n.k

 [​IMG]

Jionee mwenyewe maajabu haya .....

[​IMG]

Mwanamke khanga Babu weeee...


[​IMG] 

Je ungependa kupata Makala zetu kila ifikapo Week-End BURE? Basi Jiunge leo na Watu 3000 waliopenda kupata makala zetu.

* inahitajika

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...