18 January, 2016

RONALDO NA BENZEMA KILA MMOJA AFUNGA MAWILI REAL MADRID YASHINDA 5-1 (Video)

Mshambuliaji Cristiano Ronaldo akikimbia kushangilia baada ya kuifungia mabao mawili Real Madrid katika ushindi wa 5-1 dhidi ya Sporting Gijon kwenye mchezo wa La Liga usiku huu Uwanja wa Bernabeu. Mabao mengine ya Real yamefungwa na Karim Benzema mawili na Gareth Bale moja, wakati la Gijon limefungwa na Isma Lopez Gareth Bale got Real Madrid on their way to victory with this perfectly timed header at Sporting Gijon's near post after just seven minutesKarim Benzema, on his 300th appearance for the club, blows a kiss to the Real Madrid fans after getting his first goal of the afternoonBale celebrated in trademark fashion and certainly looked to be enjoying himself having scored four goals in two games for Real Tazama Video ya magoli yote hapo chini

Mamlaka nchini Marekani zimesema zinajaribu kuwatafuta raia wa Marekani waliopotea mjini Baghdad nchini Iraq.


Watu watatu waliopotea wanahofiwa kutekwa nyara na wanamgambo, chombo cha habari cha al-Arabiya, kimenukuu vyanzo vyake.
''tuna taarifa kuhusu kupotea kwa raia wa Marekani nchini Iraq''. Maafisa wameeleza.
Msemaji wa Ubalozi wa Marekani nchini Iraq Scott Bolz amesema wanashirikiana na mamlaka za Iraq kuwatafuta.
Tukio hilo limetokea baada ya muda wa wiki moja paliposhuhudiwa kuzorota kwa hali usalama mjini Baghdad.
Wanamgambo wa Islamic state walikiri kutekeleza mashambulizi kadhaa mjini Baghdad na Dyala wiki iliyopita ambapo zaidi ya watu 50 walipoteza maisha.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu Ya Januari 18

Kutana na habari zilizoko katika magazeti pendwa hapa nchini leo Jumatatu

Mwandishi wa 'Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe' afariki

Mwandishi maarufu wa tamthilia na kitabu cha ‘Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe’, Edwin Semzaba amefariki jana.

Mbali na kuwa mwandishi maarufu, Semzaba alikuwa mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Pia, alikuwa mwenyekiti wa Umoja Wa Waandishi wa Vitabu Tanzania (UWAVITA).

Semzaba ambaye kitabu chake cha Ngoswe, Penzi Kitovu cha Uzembe kilimpatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya mipaka ya Tanzania, aliwahi kueleza kuwa alianza kuandika kitabu hicho akiwa anasoma kidato cha pili akiwa na umri wa miaka 16 tu.

Aliimalizia kazi yake hiyo nzuri baadae ambapo ilikubalika na kuanza kurushwa kupitia Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD) na baadae kuiweka katika kitabu kilichokubalika na kutumika kama kitabu cha kiada kwa shule za sekondari.

17 January, 2016

Rapa Rick Ross amaliza mkataba wake na Def Jam Records, sasa yuko Epic Records.

RozayRick Ross anafanya boss moves mwaka 2016, baada ya mkataba wake kuisha na lebel ya Def Jam Rozay amekataa kuongeza muda na lebel hio na moja kwa moja amejiunga na Epic Records.
Ijumaa ya Jan 15 picha ya Rozay akiwa na bosi wa Epic Records aliyewahi kuwa bosi wa Def Jam L.A Reid ilitolewa na kurasa za lebel hio ikiwa na ujumbe “Welcome @rickyrozay to the #EPIC family!”
Rozay alijiunga na Def Jam mwaka 2006 na ametoa album nane mpaka sasa yamwisho ikiwa Black Market iliyoshika namba 6 kwenye bilboard charts.
Rozay atakuwa lebel moja na wasanii kama Future, Diddy, Mariah Carey, Ciara, Travis Scott,na Fifth Harmony.

Wimbo mpya wa Tyga Ft Chris Brown ‘Rumorz’

foaf-raidersNi mwaka sasa umepita toka tumesikia wimbo mpya kati ya Chris Brown na Tyga kutoka kwneye album yao ya Fan of a Fan: The Album. Tyga na Chris wamekutana tena kwenye collabo ya wimbo wa Tyga “Rumorz” kutoka kwneye mixtape ya Rawwest Nigga Alive.

CHAN 2016:DRC yaichapa Ethiopia


Timu ya DRC imeanza kampeni yake ya kutaka kushinda kombe la Ubingwa wa Afrika kwa mara ya pili vyema baada ya kuicharaza Ethiopia 3-0 katika mechi ya ufunguzi wa kundi Ba.
DR Congo ilioshinda michuano ya CHAN mwaka 2009,ilitawala mechi hiyo iliochezwa katika mji wa Butare nchini Rwanda,huku Guy Lisadisu akiwaweka kifua mbele kunako dakika ya 44.
Baada ya mapumziko ,Chui hao wa DRC waliendeleza juhudi zao na kunako dakika ya 46 Heritier Luvumbu alifunga kupitia kichwa huku Mechack Elia akiongeza bao la tatu dakika tisa baadaye.Hatua hiyo ina maanisha kwamba timu ya Walia kutoka Ethiopia wanatafuta ushindi wao wa kwanza katika historia ya michuano hiyo.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...