27 April, 2016

Oliver Mtukudzi picha Halisi ya Muziki wa Kiafrica.


Linapotajwa jina la wimbo wa "Neria" basi kila mmoja wetu atakua na mawazo mawili tofauti ambayo yote humuongelea Nguli wa muziki wa Kiafrica na sio mwingine ni Oliver Mtukudzi kutoka kule Zimbabwe kwa mbabe Robert Mugabe.
Jina la utani huwa wanamuita "TUKU" ambapo jina hilo limetokana na jina Mtukudzi hivyo akaamua kufupisha jina lake hilo na kupata hiyo a..ka. amezaliwa mnamo 22 Septemba 1952 mjini Highfield, Harare) ni mwanamuziki wa Kizimbabwe. Oliver ni miongoni mwa wanamuziki walio maarufu kwa muda mrefu sana katika nchi hiyo ya Zimbabwe. Na alianza shughuli za muziki kunako miaka ya 1977 pale alipojiunga na bendi ya Wagon Wheels, ambayo pia alikuwemo na mwanamuziki wa zamani Bw. Thomas Mapfumo.

   Nyimbo ya kwanza ilikuwa "Dzandimomotera" iliyoheshimika sana, na hapo ndipo Tuku alipotoa albamu yake ya kwanza, nayo pia ilileta mafanikio makubwa kabisa. Mtukudzi nae pia ni mmoja wa wanakundi la Mahube, kundi la muziki la nchi za Afrika ya Kusini.

Oliver pia ni baba wa watoto watano na wajukuu wawili, wawili hao pia ni wanamuziki. Ana dada zake wanne na kaka mmoja ambaye tayari amekwisha fariki. Anafurahia kuogelea katika bwawa lake la kuogelea (swimming pool) ambalo lina umbo la gitaa. Oliver ametoa zaidi ya albamu 40 na amepata kushinda tuzo nyingi mno na hata zingine hawezi kuzikumbuka.
   
Filamu alizoshiriki:
  • Jit (mwong. Michael Raeburn , 1990)
  • Neria (mwong. Goodwin Mawuru, imetungwa na Tsitsi Dangarembga, 1993). Mtukudzi ndiyo alikuwa nyota wa filamu na yeye ndiye aliotengeneza nyimbo ya filamu.
  • Shanda (mwong. John na Louise Riber, 2002, rev. 2004)
 Tuzo alizowahi kushiriki na kushinda.
  • Tuzo ya KORA kwa ajili ya matayarisho mazuri ya nyimbo yake ya Ndakuwara mnamo mwaka wa 2002
  • Tuzo ya National Arts Merit (NAMA) mnamo mwaka wa 2002 na 2004 kama kundi bora la muziki/ mwanamuziki bora wa kiume
  • Tuzo ya KORA kama mwanamuziki bora wa kiume wa Africa na tuzo ya Lifetime Achievement mnamo mwezi Agosti wa mwaka wa 2003
  • Tuzo ya Reel kama lugha bora ya Kiafrica mnamo wamaka wa 2003
  • An honorary degree from the University of Zimbabwe in Desemba 2003
  • Tuzo za M-Net Best kama nyimbo bora ya filamu mnamo 1992, kwa ajili ya filamu ya Neria.

Tafadhali pitia na Hizi zifuatazo.
 1.Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'
 2. Sababu tano ni kwa nini Bongo flava ya Awali ilikuwa bora kuliko ya bongo 








No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...