24 April, 2016

Wafahamu madancer Albir Rojas na Sara Lopez wakali wa 'Kizomba dance'

Well! well! well!.. Leo nmepanda hapa MTOKAMBALI kivingine kabisa japo bado niko kule kule kwenye Burudani na Leo nitawapatia angalao Biography ya wakali hawa wa dance ulimwenguni. Linapotajwa jina la 'Kizomba' basi kila mmoja haachi kumfkiria Albir Rojas  na Sara Lopez maana wakali hawa ndio wenye KIZOMBA DANCE.

Nianze na Albir Rojas:-
Ni  dancer, choreographer, actor na ni professor.
 Alizaliwa mnamo 25th mwezi October 1979 huko PANAMA na mama yeke kumpatia jina la Albir ambalo hakutaka mwanae kuchakachua jina hilo kamwe, na mama yake aliamua hivyo sababu kuna siku mama yake huyo alikwenda nchini India nakumkuta mama mmoja akimwita mwanae wa kiume "Albir" kisha akamuuliza mama huyo wa kihindi jina hilo lina maana gani? basi mama yule wa kihindi akajibu "BRAVE" na ndipo mama yake dancer huyu akaamua kumpatia jina hilo.

Wakati akiwa mdogo wa umri mika 12, mama yake alikua akimfundisha dancing japokua wakati huo jamaa huyu alikua havutiwi na dancing na badala yake alikua akivutiwa na Video games na akaendelea na video games pamoja na dancing mpaka akiwa na umri wa miaka 14 wakati alipokuwa High school.
Akiwa high  school alialikwa kushiriki kwenye choreography na hapo ndipo Albir akaamua kuikubali DANCING na kuanza kuifanyia kazi. Akiwa na umri wa mika 16, alijiunnga na darasa ladance katika funky dance school na huko alikua akijifunza mambo mengi kuhusiana na choreography.
 Albir alimaliza high school akiwa na umri wa miaka 18 na lifanikiwa kutoka na Bachelor of Commerce degree (Accounting).

Baada ya kumaliza masomo yake alipata kazi akiwa kama accountant na huku alikua pia akisoma masomo yake ya shahada ya uzamivu katika maswala hayo hayo ya biashara. Albir alikua akiutesa mwili wake kwa kazi mno maana hasubuhi alikua akienda kazini na jioni alikua akihudhuria darasani na usiku alikua akifanya mazoezi ya dance jambo ambalo mwili wake kuna muda uluonekana kuchoka.
Licha ya hivyo jamaa huyo hakukata tamaa na aliamua kuacha kazi ofisini na kuamua Kuifanya sanaa kwa ujumla kipindi chote cha cha maisha yake.

Albir alikua katika dancing mwaka hadi mwaka na aliwahi kuonekana katika kazi kama Grease, the King and I, Fame, West Side Story na Fantastics, kote huko alikua kama Actor na dancer.
Aliamua kwenda  Madrid kwa ajili ya masomo yahusuyo Communication, Advertising, Film making and Sound Technician na alimaliza na akamua kuishi Madrid tangu mwaka 2001 mpaka leo.

Albir amekua akifundisha dancing styles kama cuban salsa, salsa in line, bachata dominicana, bachata madrid, hip hop, popping, KIZOMBA, TARRAXINHA, SEMBA and ballroom dances ambazo yeye ni MASTER wa Style hizo.
Albir anapenda anachokifanya na hua anapenda kushirikisha feelings zake kwa watu wapenda dancing mfano Mimi ( ha ha ha haa).

Nije kwa bibie Sara López:-
AlbirRojas2Mwana dada huyu ni mzaliwa  Madrid, Spain na alizaliwa mnamo mwaka 1986. Alianza dancing akiwa na umri mdogo wa miaka 5 na alitumia miaka 7 kujifunza dance katika ballet, contemporary dance, modern dance, hiphop. na akiwa na umri wa miaka 16 alinza na Latin dances, Salsa, Bachata pamoja na Kizomba.

Akiwa na umri wa mika 18 tuu, akawa amemaliza elimu yake ya  Sekondary na akaamua kwenda Madrid kwa ajili ya kujifunza classical ballet. Huko alikaa kwa muda wa mika mitatu zaidi akiwa akijifunza tena Latin rhythms.
Alipata dancing partner wake wa kwanza nchini humo aliyejulikana kama Ronald Jara ambaye alionekana nae katika mashindano ya dancing Madrid in Africadançar (Lisbon Ureno) mnamo mwaka 2012.
na baadae akatambulishwa kwa Mkali Albir ambaye walionekana kufanya kazi kwa pamoja hadi mwaka 2014 walipo achana.

Ikumbukwe kuwa Dancers hawa hawakuwahi kuwa wapenzi kamwe licha ya watu wengi ulimwenguni kufahamu kuwa walikua wapenzi. Nikupatie angalao video moja ya wakali hawa wakifanya vitu vyao katika KIZOMBA.

Mpaka hapo sina la ziada nikutakie siku njema na tukutane tena Juma lijalo hapa hapa MTOKAMBALI,







Mtokambali |

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...