09 September, 2016

Serena Williams atupwa nje kwenye michuano ya US Open

Serena Williams ameendelea kuharibu kwenye mashindano ya tennis baada ya hapo jana kuondolewa kwenye nusu fainali ya michuano ya US Open na mchezaji wa Jamhuri ya Czech, Karolina Pliskova.
381880bc00000578-0-image-a-4_1473382194216
Kwenye mchezo huo Karolina alifanikiwa kushinda kwa seti 6-2, 7-6 (3) katika mchezo uliofanyika kwa muda wa saa moja na dakika 26. Kwa sasa Pliskova atakutana na Kerber kwenye mchezo wa fainali siku ya Jumatatu.
38188a3e00000578-3780869-image-a-22_1473382710662
Mapema mwezi Agosti mwaka huu Serena na ndugu yake Venus Williams walitolewa kwenye raundi ya kwanza ya mchezo wa tennis wa wanawake wawili wawili kwenye michuano ya Olimpiki.
38187ad500000578-3780869-image-a-19_1473382609664
Serena alikuwa anatarajia kufikisha mataji 23 ya grand slam kwenye michuano hiyo na kuvunja rekodi ya Steffi Graf ya mataji 22 ambayo wanafanana kwa sasa.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...