07 March, 2016

Picha,Mpenzi mpya wa Baraka da Prince

baraka
Baada ya stori tofauti kusamba kwenye mitandao ya kijamii, imesemekana kuwa kwa sasa Baraka da Prince hayuko tena na msanii wa filamu Tanzania Nisher ila anatoka na msanii wa bongo Fleva Najma Aka Naj.
Haya ni maneno ya Barak Da Prince yaliyoambatana na Post ya kichwa cha mwanamke aliyelala naye.
bbk Screenshot_2016-03-06-13-43-24 Screenshot_2016-03-06-13-43-34

Liverpool yapeta,Man U yachapwa


Ligi kuu ya England iliendelea tena mwisho wa wiki kwa michezo miwili kuchezwa.
Majogoo wa Anfield Liverpool wakicheza ugeni kwenye dimba la Selhurst Park waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Crystal Palace ndio walianza kuandika bao la kwanza kwa bao la Joe Ledley kisha Liverpool wakachomoa bao hilo kupitia kwa mshambuliaji wake Roberto Frimino, katika dakika za lala salama Christian Benteke akawapa ushindi kwa bao la mkwaju wa penati.
Nao Mashetani Wekundu wa Man United wakachapwa kwa bao 1-0 na West Bromwich Albion, bao hilo pekee likifungwa na Solomon Rondon, huku kiungo wa Juan Mata akitolewa nje kwa kadi nyekundu.

Simba yaongoza ligi kuu Tanzania bara ni baada ya kuichapa Mbeya City bao 2-0

Wekundu wa Msimbazi Simba Sport Klabu wamechukua usukani wa ligi kuu Tanzania bara baada ya ushindi dhidi ya Mbeya City. Wekundu hao wa msimbazi walipa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wapinzani wao Mbeya City kwa mabao yaliyofungwa na Daniel Lyanga na Ibrahim Ajib. Simba wakiwa kileleni kwa alama 48 wakiwa wamecheza 21 wanafatiwa na wapinzani wao wa jadi Yanga walioko nafasi ya pili wakiwa na alama 47 kwa michezo 20 huku Azam akiwa katika nafasi ya tatu kwa alama 47 pia wakitofautiana na yanga kwa idada ya magoli. Ligi hiyo itaendelea tena hapo Jumanne kwa mchezo mmoja kupigwa ambapo Yanga, kushuka dimbani kwenye dimba la Taifa kukipiga na African Sports ya Tanga.

Maridhiano nchini Burundi ni Muhimu

Askofu mkuu wa Canterbury Justin Welby amemaliza ziara yake nchini Burundi na kufanikiwa kuwa na mazungumzo na Rais wa Taifa hilo Pierre Nkurunziza.
Mzungumzo hayo yameangazia umhimu wa kuwepo mazungumzo ya pamoja ili kuepusha mauaji yanayoendelea kufuatia vurugu zilizozuka kutokana na uamuazi wa Rais wa taifa hilo kuwania mhula mwingine wa Uongozi.
Mamia ya watu wameuawa kutokana na vurugu hizo huku maelfu wakilazimika kuikimbia nchi yao na kukimbilia nchi jirani.
Rais Pierre Nkurunziza Katika mazungumzo hayo na kiongozi huyu wa Kiroho,muda mwingi alionekana ni mwenye furaha na tabasamu mbele ya ambapo undani wa mazungumzo hayo ilikuwa ni kuhimiza ushiriki wa pande zote ili kuhakikisha kuwa amani ya kweli inafikiwa nchini humo.
Askofu Just Welby amesema kuwa suala la maridhiano nchini Burundi linahitaji watu kujitoa muhanga.
Hata hivyo amesisitiza hatua za msingi za kuzingatiwa ili kuweza kufikiwa kwa amani ya kweli nchini Burundi.
Taifa la Burundi lililopata Uhuru wake 1962 na kupitia katika vipindi mbalimbali vya machafuko limejikuta katika upotevu wa hali ya amani katika kipindi kingine kufuatia uamuzi wa Rais wa taifa hilo Pierre Nkurunziza kuamua kuwania muhula mwingine hatua inayopingwa na upinzani nchini humo.

Rais John Pombe Magufuli amteua katibu mkuu mpya


Mhandisi John William Kijazi ameteuliwa kuwa katibu mkuu kiongozi nchini
Kabla ya kuteuliwa leo Mhandisi Kijazi alikuwa anahudumu kama balozi wa Tanzania nchini India ambapo majuzi tu alitoa mchango mkubwa katika kuhakikisha wanafunzi raia wa Tanzania wanapata usalama kufuatia shambulizi dhidi ya mmoja wao.
Katika taarifa fupi kutoka kwa ikulu ya rais John Pombe Magufuli Balozi huyo anaanza kazi mara moja.
Mhandisi Kijazi anachukua nafasi iliyowachwa wazi baada ya kuondolewa Balozi Ombeni Sefue.
Haijulikani kwanini balozi Sefue ameondolewa katika wadhfa huo ila taarifa hiyo ya ikulu iliyotiwa sahihi na kaimu mkurugenzi wa mawasiliano Gerson Msigwa inasema kuwa Sefue atapewa majukumu mengine.

Magazeti ya Leo Jumatatu March 7

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...