07 March, 2016

Rais John Pombe Magufuli amteua katibu mkuu mpya


Mhandisi John William Kijazi ameteuliwa kuwa katibu mkuu kiongozi nchini
Kabla ya kuteuliwa leo Mhandisi Kijazi alikuwa anahudumu kama balozi wa Tanzania nchini India ambapo majuzi tu alitoa mchango mkubwa katika kuhakikisha wanafunzi raia wa Tanzania wanapata usalama kufuatia shambulizi dhidi ya mmoja wao.
Katika taarifa fupi kutoka kwa ikulu ya rais John Pombe Magufuli Balozi huyo anaanza kazi mara moja.
Mhandisi Kijazi anachukua nafasi iliyowachwa wazi baada ya kuondolewa Balozi Ombeni Sefue.
Haijulikani kwanini balozi Sefue ameondolewa katika wadhfa huo ila taarifa hiyo ya ikulu iliyotiwa sahihi na kaimu mkurugenzi wa mawasiliano Gerson Msigwa inasema kuwa Sefue atapewa majukumu mengine.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...