07 March, 2016

Liverpool yapeta,Man U yachapwa


Ligi kuu ya England iliendelea tena mwisho wa wiki kwa michezo miwili kuchezwa.
Majogoo wa Anfield Liverpool wakicheza ugeni kwenye dimba la Selhurst Park waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Crystal Palace ndio walianza kuandika bao la kwanza kwa bao la Joe Ledley kisha Liverpool wakachomoa bao hilo kupitia kwa mshambuliaji wake Roberto Frimino, katika dakika za lala salama Christian Benteke akawapa ushindi kwa bao la mkwaju wa penati.
Nao Mashetani Wekundu wa Man United wakachapwa kwa bao 1-0 na West Bromwich Albion, bao hilo pekee likifungwa na Solomon Rondon, huku kiungo wa Juan Mata akitolewa nje kwa kadi nyekundu.

No comments:

Post a Comment

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...