05 August, 2015

KASEJA, TEGETE KUTUA MWADUI FC

TegeteAliyekuwa golikipa wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na vilabu vya Simba na Yanga Juma Kaseja na mshambuliaji wa zamani wa Yanga Jerryson Tegete huenda wakajiunga na klabu ya Mwadui FC kama mambo ya klabu hiyo yataenda kama yalivyopangwa.
Kocha mkuu wa klabu hiyo Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amesema pamoja na kukamilisha usajili wa wachezaji waliokuwa wanawahitaji, lakini bado nafasi ipo kwa ajili ya Juma Kaseja na Jerry Tegete kwani wakipewa nafasi wanaweza wakaonesha uwezo mkubwa.
“Mimi nimeshamaliza usajili, nimeshasajili wachezaji 26 wanatosha, wachezaji pekee ambao kama mipango yangu itaenda sawasawa basi kuna mpango wa kuwaongeza Juma Kaseja na Jerry Tegete. Kwasababu ni wachezaji ambao nimezungumza nao na wameniambia wanataka kucheza na hawakuweka mbele kipato, mimi wamenivutia kwasababu tunapokuwa na wachezaji kwenye timu tunataka tuwatumie kucheza ili tupate mafanikio kwenye ligi”.
juma-kaseja1“Lakini kunawachezaji ambao hawaperfom inabidi tuwatoe kwenye dirisha dogo la usajili, lakini ukiwa na wachezaji wazuri wenye kuonesha commitment ambao wanataka kucheza kuisaidia timu yao sioni kwanini nisiwachukue kwasababu namba bado inatosha”.
Kwa usajili wa wachezaji wa kigeni unaofanywa na baadhi ya vilabu vya ligi kuu hapa nhini Julio amesema yeye hatishwi na usajili huo kwani yeye ni Kocha mkubwa na anatambua uwezo wa wachezaji wengi na hata pale anapowaita wachezaji haoni kama ni wazee na anatambua kuwa ni wachezaji wenye uwezo mkubwa”.
“Mimi kwanza sitishiki na usajili wa Azam, Simba na Yanga, wao wamevutika na wachezaji wao wa nje kwasababu zao binafsi kwanza wanafedha,Yanga wanatarajia wakiwa na wachezaji wa kigeni watafanikiwa kwasababu wanacheza mashindano ya Afrika wanataka kuingia kwenye ‘Super eight’ ili wafanikiwe. Mimi sidhani kama hilo litafanikiwa”.
Lakini Azam hivyohivyo nao japokuwa juzi wamechukua ubingwa wamefanya vizuri nimeona timu yao sio mbaya sana, Simba wamepoteza ubingwa kwa takribani miaka mitatu kwahiyo wanategemea wakiwa na wachezaji wa nje basi wanaweza wakafanya kile kitu wanachokitarajia na watapata ubingwa lakini sioni kama itafanikiwa vilevile”.
Msikilize Julio hapa chini akieleza nia yake ya kuwasajili Kaseja na Tegete

WASHAMBULIAJI WATANO WANAOTEGEMEWA KUFANYA MAKUBWA EPL 2015/16

dara ya ushambuliaji inawezekana ndiyo idara muhimu sana na inayoangaliwa na watu wengi sana uwanjani, sina maaana kuwa soka linachezwa sehemu ya mbele pekee la hasha…., soka linachezwa klia kona ya uwanja ila wazungu hawakuwa wapuuzi waliposema “Striker life is in the goal scores”, wakiwa na maana kuwa maisha ya mshambuliaji yapo katika ufungaji, ukiwa mshambuliaji bila shaka assist ni kitu cha ziada ila kazi yako wewe ni kufunga tuu. Kutokana na hayo sio vibaya leo tukitazama baadhi ya wachezaji ambao baadhi ya mashabiki na wachambuzi mbalimbali wa soka wanategemea makubwa kutoka kwao kwenye idara ya kutikisa nyavu msimu ambao pazia lake tayari limefunguliwa juzi kwenye mchezo wa ngao hisani kwa “mbwatukaji” kupata kipigo kitakatifu kutoka kwa “Petit” Wenger. Naomba tuungane pamoja hapa chini kutazama washambuliaji watano ambao washabiki wanategemea kupata magoli Zaidi ya 19 kutoka kwao msimu ujao…….
5> Aleksandar Mitrovic
Mitrovic
Mashabiki wengi wa Epl wanatarajia mshambuliaji mpya wa Newcastle aliyesajiliwa kwa Euro 12M kutoka Anderlech ya Ubelgiji, Aleksandar Mitrovic kufanya makubwa kwenye ligi yenye ushindani barani Ulaya, matarajio haya yanakuja kutokana na kiwango alichokionyesha Mserbia huyu kwenye mechi ya Champion League msimu uliopita pale timu yake iliposawazisha magoli matatu dhidi ya Arsenal. Huyu jamaa alianza kupata uzoefu mapema kabisa tangu akiwa na umri wa miaka 20. Msimu uliopita alifunga magoli 20 katika ligi na kuwa mfungaji bora kwenye ligi ya ubelgiji. Pia katika mechi 69 alizocheza amefunga jumla ya magoli 36, ikiwa ni wastani wa karibu goli 1 katika mechi 2. Kutokana na kiwango chake, timu za Roma na Porto zilionyekana kuvutiwa naye sana ila mwisho wa siku alitua Saint James Park.
4> Harry Kane
Tottenham Hotspur's Harry Kane celebrates scoring his side's first goal of the game during the Barclays Premier League match at White Hart Lane, London.
clays Premier League match at White Hart Lane, London.
Hatimaye baada ya Roberto Soldado kuonekana kufanya vibaya katika idara ya ufungaji, Mauricio Pochettino aliamua kumpa nafasi kinda wa kiingereza Harry Kane na kufunga magoli 21 msimu uliopita na miongoni mwa magoli hayo ni yale aliyowafunga wapinzani wao wa London, Chelsea na Arsenal. Kutokana na kiwango chake msimu uliopita ni wazi tayari Kane ameshawafahamu mabeki wa Epl na jinsi ya kukabiliana nao. Idadi ya magoli inatarajiwa kuongezeka msimu ujao kwani utakuwa mnafiki kama ukiambiwa utaje wamaliziaji wazuri kwa sasa pale Epl alafu ukamuacha kinda huyu wa miaka 22. Tottenham itakuwa na ratiba nzuri kwani katika mechi 6 itakazo anza watakutana na timu moja pekee katika zile 8 zilizomaliza juu msimu uliopita. Hapa Kane ndo mahali ambapo anatarajiwa kuwaonea Mabeki wa timu hizi na kuanza kuweka akiba ya magoli mapema kabisa.
3> Wayne Rooney
rooney
Kuondoka kwa Robin Van Persie na Radamel Falcao, kunamfanya Wayne Rooney mpaka sasa kuwa tegemeo la Manchester United kule mbele hasa kutokana na United kutopata mshambuliaji wa kueleweka mpaka sasa japokuwa dirisha la usajii bado halijafungwa. Usajili wa viungo makini Schneiderlin na Schweinsteiger bila shaka utaimarisha idara ya kiungo na kumpa nafasi Rooney kucheza sana pale mbele na kuwa na uwanja mpana sana wa kufanya makubwa katika ufungaji. Tayari LVG ameshampa uhakika wa kuanza kila mechi kutokana na yeye kuwa nahodha wa timu. Kumbuka aliwahikufunga magoli 27 msimu wa 2011/12 na pia alitupia magoli 26 kwenye msimu wa 2009/10, misimu yote hiyo alipewa majukumu ya kucheza kama namba 9. Endapo LVG atafanya hivi ni wazi kuwa mfumo wowote atakao utumia na Rooney kucheza mbele bado atafanikiwa kupata magoli anayo yahitaji ili kuwa mshambuliaji wa pili kuwa na magoli mengi pale Epl.
2> Diego Costa
costa
Mshambuliaji hatari wa Ki Brazil anayecheza timu ya taifa ya Spain, Diego Costa”The governor”, anatarajiwa kumaliza msimu na magoli Zaidi ya 25 kama hatopata majeraha ya mara kwa mara kama msimu uliopita. Msimu uliopita alifunga magoli 20 katika mechi 26 kwenye msimu wake wa kwanza wa Epl, endapo kama sio Majeraha ni wazi hakuna mtu ambaye angemkamata Diego katika ufungaji wa EPL, kumbuka hakuwa na goli hata moja la penati katika magoli yake yote. Kutokana na support atakayo ipata kutoka kwa viungo wakabaji na washambuliaji ambao siku zote wapo nyuma yake, Oscar, Hazard na Willian ni wazi Diego ataendelea kupata huduma nzuri na kutupia nyavu mara kibao, pia assist za Cesc zitazidi kumuweka juu mchezaji huyu ambaye mpaka sasa hajafahamu lugha ya kiingreza licha ya kukaa takribani mwaka mzima pale London. Kumbuka Chelsea itakutana na Man City pamoja na Arsenal katika mechi 6 za mwanzo. Endapo diego atakuwa fiti bila majeraha naamini ataanza vizuri katika mechi hizi
1> Sergio Aguero
aguero
Hatutaweza kushangaa endapo Jamaa lenye nguvu na kasi kutoka Argentina, Sergio Aguero kuwa mfungaji bora wa ligi kwa mara nyingine tena. Amekuwa na mwendelezo mzuri wa kufunga kwenye michuano ya Copa America baada ya kufunga magoli 3 katika mechi 5, kumbuka msimu uliopita alimaliza na magoli 26 katika mechi 33 huku akitoa assist 10. Kutokana na kiwango chake ni wazi Aguero atakuwa na msimu mwingine mzuri hasa kutokana na kuwa mzoefu kwenye Epl kwa muda sasa, kingine pia huyu jamaa ndo mpiga penati za ndani ya uwanja hivo bado ana faida ya kuzidi kuongeza magoli hasa baada ya usajili wa Raheem ambaye anapenda ku drible hadi kwenye box za wapinzani.

Albamu Ya Dr.Dre Ya “Compton” Itatoka Kwa Mara Ya Kwanza Mtandaoni

Albamu ya “The Chronic” rapper Dr. Dre itatoka kwenye mtandao lakini haitakuwa halisi yenyewe lakini kupitia kwenye mitandao ndio itakuwa sehemu ya kwanza kusikiliza mzigo huo.

Albamu hiyo inayokuja ya “Compton” itapatikana kupitia Apple Music kuanzia saa 6pm-9pm PST siku ya Alhamisi Agosti 6, taarifa kupitia Beats 1 radio zimetengazwa na mtangazaji Zane Lowe.

“Listen to the premiere of @drdre new album, Compton,” (August 4). “Uncensored & exclusively on @AppleMusic.” Aliandika Lowe

Dr. Dre alitangaza albamu hiyo siku ya Jumamosi Agosti 1, kupitia kipindi chake cha “The Pharmacy” kupitia radio ya Beats 1, kwenye albamu hiyo ameshirikishwa Eminem, The Game, Kendrick Lamar, Jon Connor, Snoop Dogg, King Mez na wengine, albamu hiyo imepangwa kutoka Jumamosi Agosti 8.

Mwanzilishi huyo wa Aftermath alisema alivutiwa na filamu inayokuja ya N.W.A movie, Staright Outta Compton ndo maana akaamua atengeneza albamu yake ya kwanza baada ya zaidi ya miaka 10, filamu inatarajiwa kutoka Agosti 14.

Wapenda hip hop, movies get ready to hit the bottons na theaters….compton1

Kwenye StoriKubwa >>> Ya MAGUFULI, Rais JK.. Lowassa? mastaa waliokatwa YANGA …

222222MWANANCHI
Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk John Magufuli, na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan jana walichukua fomu kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), huku Rais Jakaya Kikwete akisema wapinzani wataisoma namba.
Ofisi ndogo za makao makuu ya CCM zilizoko Lumumba na za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), zilifurika mashabiki waliovalia nguo za rangi ya njano na kijani, ambazo hutumiwa na chama hicho, huku wakazi wengine wanaofanya kazi au kuishi maeneo jirani na barabara za Morogoro, Bibi Titi na Ohio, wakilazimika kusimamisha shughuli zao kwa muda kushuhudia msafara wa wagombea hao ukipita.
Walinzi  wa ofisi za NEC walilazimika kufanya kazi ya ziada kudhibiti wafuasi wa CCM waliosindikiza wagombea hao kutoka ofisi ndogo za CCM kabla ya msafara huo kuondoka baada ya wawili hao kuchukua fomu, kurejea Lumumba, ambako mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete aliupokea.
“Wakwere wanasema chihendo na mwene mwana, yaani shughuli na mwenye mtoto,” alisema Rais Kikwete mara baada ya msafara kuwasili akieleza sababu za yeye kuwapo eneo hilo kwa kutumia maneno ya shughuli za kitamaduni za jandoni, unyagoni na mkoleni za kabila la Wakwere.
“Nimekuja hapa kujiridhisha kama kweli fomu zimechukuliwa. Na kweli nimeziona. Baada ya hatua hii wale wanaodhani kuwa CCM ni chama cha mchezo mchezo, wataisoma namba.”
Huku akikatiza hotuba yake kwa kuitaka bendi ya TOT ya chama hicho kuimba wimbo wa “Shangilia Ushindi Unakuja”, Rais Kikwete alisema kwa kuwa yeye ni baba alilazimika kuja kuangalia kama mwanaye ametekeleza alichotuma.
Kikwete, ambaye alitumia mifano iliyovunja mbavu wafuasi hao, alirusha kijembe kwa wanachama walioihama CCM akisema ni tamaa na kuahidi kufanya mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni.
CCM shangilia ushindi unakuja, tena ushindi wa uhakika na si wa wasiwasi. Baada ya hapa kitakachofuata ni uzinduzi hapo Agosti 22 kwenye mkutano utakaotisha. Hatumwi mtoto siku hiyo, unakuja mwenyewe,” alisema.
“Watu wanasumbuliwa na tamaa na wakati mwingine ni tamaa iliyopitiliza kutaka madaraka.”
Magufuli alitoka ofisi ya CCM Lumumba akiwa amepanda gari aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa wazi juu akiwa na msafara wa magari yapatayo 10 kuelekea ofisi za NEC. Baada ya kufika eneo la makutano ya Barabara ya Ohio na Bibi Titi, alishuka na kupanda gari nyingine iliyokuwa wazi nyuma na kuamsha kelele za shangwe.
Aliwasili ofisi hizo saa 5.22 asubuhi na baada ya kuchukua fomu za kuwania urais, msafara wa kurejea ofisi za chama hicho zilizoko Lumumba ulianza tena na kufika ofisi hizo ndogo za CCM, ambako ulipokelewa na Rais Kikwete.
“Matatizo ya Watanzania nayajua na  ninaahidi kuwa nitakuwa mtumishi wenu mtiifu,” alisema Dk Magufuli baada ya Rais Kikwete kumuomba aketi ili azungumze na wafuasi wa chama hicho.
“Nafahamu kuwa Watanzania wanahitaji ajira na hawataki usumbufu kwenye biashara zao kama mamantilie, wana kero kwenye huduma mbalimbali. Ninawaahidi kuwa nitazishughulikia.
Napenda nimhakikishie mwenyekiti na wananchi mliokusanyika hapa kuwa CCM itashinda na wala simuoni mtu wa kutushinda. Nashukuru kwa moyo mliouonyesha wa kunisindikiza mimi pamoja na Samia. Mmetoa jasho na mmepoteza muda wenu. Napenda kuwahakikishia kuwa muda wenu hautapotea bure.”
Alirudia wito wake wa kuwataka wananchi kuendeleza mshikamano uliopo bila kujali itikadi zao wala makabila ili kuliletea Taifa maendeleo kwa kuondoa kero zinazowakabili.
MWANANCHI
Katibu Mkuu wa CUF na Makamu wa Kwanza Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad amesema ilikuwa kazi kubwa kumshawishi Juma Duni Haji kukiacha chama hicho na kujiunga Chadema ili awe mgombea mwenza wa Edward Lowassa.
Duni, ambaye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa CUF, alitangazwa kujiunga na Chadema jana, ikiwa ni makubaliano ya mkakati maalumu wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) wa kukabiliana na kikwazo cha kisheria cha kupata mgombea mwenza kutoka chama tofauti na kilichosimamisha mgombea urais.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inataka Makamu wa Rais kutoka chama kilichoshinda kiti cha urais na hivyo Duni amejiunga na Chadema akiwa mwakilishi wa Ukawa kwenye Serikali iwapo umoja huo, unaoundwa na CHADEMA, CUF, NLD na NCCR – Mageuzi utashinda Uchaguzi Mkuu.
Lakini kabla ya Duni kukubali ushauri huo, Maalim Seif alisema walikuwa na kibarua kigumu.
“Tulimwita Babu Duni, tukamwambia azma hii, akasema; ‘hivi kweli niende Chadema mie?’” alisema Maalim Seif akimnukuu Duni wakati akihutubia Mkutano Mkuu wa Chadema jana kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Nikamwambia kwa hili tunalotaka la mabadiliko, lazima uende Chadema.”
Maalim Seif, ambaye alikuwa mmoja wa wageni waalikwa waliopewa nafasi ya kuzungumza kwenye mkutano huo ambao ni chombo cha juu cha uamuzi cha Chadema, alisema kikubwa kinachotakiwa ni kuunganisha nguvu kuhakikisha kuwa upinzani unatwaa Dola katika uchaguzi ujao wa Rais, wabunge na madiwani.
Maalim Seif, ambaye alijitangazia ushindi wa kiti cha urais wa Zanzibar, pia alimtangaza Lowassa, ambaye pia aliondoka CCM na kujiunga na Chadema wiki iliyopita, kuwa ameshashinda mbio za urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mgombea mwenza na wanachosubiri sasa ni kuapishwa tu.
“Huu ni wakati wa kujiamini na kuamini kuwa tunaweza kuchukua dola,” alisema Maalim Seif ambaye pamoja na mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba waliiongoza CUF katika kupatikana kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar (SUK).
Wakati Maalim Seif akitangaza ushindi kwa Ukawa, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alionya kuwa kazi ya kuiondoa CCM si rahisi na kwamba nguvu ya Watanzania inahitajika kufanikisha azma hiyo.
HABARILEO
Mkuu wa Kitengo cha Kuzuia na Kupambana na Ujambazi Mkoa wa Morogoro, Elibariki Pallangyo , amepigwa risasi na kufa papo hapo nyumbani kwake eneo la Yombo jiji Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Andrew Satta alisema kuwa usiku wa kuamkia jana majira ya saa tisa usiku, kundi la watu zaidi ya kumi lilivamia nyumbani kwa Pallagyo eneo la Yombo kwa kuruka ukuta, kisha kuvunja mlango na kuingia ndani walikopora fedha na simu za mabinti wanne waliokuwa ndani kabla ya kufanya mauaji.
“Hili tukio ni la kusikitisha kwani watu hawa wanaonesha walikuwa na lengo la kumuua tu na si kupora mali, kwani wamechukua fedha Sh 130,000 pamoja na simu za mkononi 4 ambazo walikuwa nazo hawa wasichana waliowakuta sebuleni,Satta.
Alisema baada ya watu hao kupora simu na fedha kutoka kwa mabinti, waliekea kwenye chumba cha Pallangyo, wakampiga risasi moja kifuani na kumuua.
Wauaji hao walitokomea kusikojulikana huku wakisahau kifaa kinachotumika katika milipuko. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Temeke na utapelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kwa uchunguzi kabla ya maziko.
HABARILEO
Rais Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kufanya kampeni za kistaarabu, kwakuwa nchi ya Tanzania inayo sifa ya kuendesha mambo yake kwa njia ya amani na utulivu.
Alitoa kauli hiyo juzi jioni wakati akihutubia mamia ya wakazi kwenye hafla maalumu ya kuwaaga wananchi wa mkoa wa Tanga, iliyofanyika katika uwanja wa Mkwakwani jijini hapa.
Katika hafla hiyo, ambayo Rais Kikwete aliongozana na Mama Salma Kikwete alipata fursa ya kupokea zawadi za aina mbalimbali kutoka kwa wawakilishi wa wananchi kutoka wilaya za Tanga, Mkinga, Pangani, Muheza, Korogwe, Lushoto, Handeni na Kilindi ambazo zinaunda mkoa huo.
Alisema kwa kuwa kampeni za Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi wa Oktoba zitaanza rasmi Agosti 21 mwaka huu ni vyema wananchi kila mmoja kwa nafasi yake, wahakikishe zinafanyika kwa ustaarabu na utulivu ili kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo nchini.
“Tanzania ina sifa ya kuendesha vitu kwa amani na utulivu …naomba kampeni zitakazofanyika za kuwanadi wagombea wa udiwani, ubunge na urais ziwe za kistaarabu hakuna sababu ya kufanya vurugu bali kila mtu apewe nafasi ya kumwaga sera zake, asikilizwe kwa utulivu”, alisema.
Aidha, Rais Kikwete aliwashukuru wakazi wa Tanga kwa kuiunga mkono CCM sambamba na kumuunga mkono kwa kiwango kikubwa kwenye chaguzi zote, zilizomuweka madarakani mwaka 2005 na 2010, ikilinganishwa na baadhi ya mikoa mingine nchini.
“Wito wangu kwenu ichagueni CCM tu katika serikali inayokuja, chama hiki kitawajengea Chuo Kikuu cha Serikali kwa sababu hapa Tanga hamna… naomba wananchi tujiandae vizuri kwa ajili ya kushiriki uchaguzi huo mkuu,” alisema.
Awali, akizungumza kwa niaba ya wananchi, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Magalula Saidi Magalula alisema “Wananchi wa mkoa huu wameniagiza niwasilishe kwako maombi ya vitu vifuatavyo ujenzi wa daraja la Mligazi linalounganisha wilaya ya Handeni na Miono, pia ujenzi wa barabara ya Tanga- Pangani–Bagamoyo kwa kiwango cha lami, Bandari ya Tanga, kufufuliwa kwa viwanda mbalimbali vya uzalishaji na kufufuliwa kwa reli ya Tanga – Moshi hadi Musoma”.
HABARILEO
Mbunge wa Viti Maalumu Chadema, Chiku Abwao ndiye atakayepeperusha bendera ya ACT kuwania ubunge wa Jimbo la Iringa mjini katika uchaguzi mkuu ujao, huku akitamba kwamba atambwaga mbunge anayemaliza muda wake, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema).
Mbali na Abwao aliyejiunga na ACT Wazalendo hivi karibuni, Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chadema, Abuu Changawa naye ameiacha Chadema na kujiunga ACT Wazalendo, huku akitangaza kuwania udiwani katika Kata ya Mivinjeni, mjini hapa.
Abwao aliyewahi kuwa mbunge wa NCCRMageuzi, alisema; “Nimeondoka Chadema baada ya kubanwa kila kona na Mchungaji Msigwa akidhani kwamba mimi nilikuwa Chadema kwa sababu ya kutaka cheo.”
Alisema pamoja na kunusurika maisha yake wakati akipigania ushindi wa Mchungaji Msigwa 2010, mahusiano yao kisiasa yamekuwa mabaya kwa kipindi chote kwani kila alilokuwa akijaribu kulifanya kwa niaba ya chama hicho alitafsiriwa analenga kugombea ubunge jimbo la Iringa Mjini.
Alisema ili kumuonesha nguvu yake kisiasa na kwamba yeye sio mwanasiasa anayetaka tu uongozi lakini mwenye dhamira na maono ya dhati ya kusaidia kuleta mabadiliko nchini atagombea ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini kupitia ACT Wazalendo.
JAMBOLEO
Siku mbili baada ya mawaziri watano kushindwa katika kura za maoni ya ubunge ndani ya CCM, waziri mwingine, Gaudentia Kabaka anayeshughulikia Kazi na Ajira, naye amedondoshwa katika jimbo la Tarime Mjini.
Kabaka, kabla ya kujitosa katika siasa za majimbo, alikuwa mbunge wa muda mrefu wa viti maalumu. Aidha, katika kura hizo zilizofanyika kote nchini, zimewaacha katika hali mbaya wabunge wanne, baada ya kushindwa katika kura za maoni majimboni mwao.
Hao ni Nyambari Nyangwine, Gaudence Kayombo, John Lwanji na Salome Mwambu.
Matokeo ya Tarime Mjini na Tarime Vijijini ambako Nyangwine ameanguka, yamethibitishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Katibu Wazazi Wilaya ya Tarime, Mathias Lugola aliyetangaza rasmi matokeo ya majimbo hayo.
Awali, matokeo hayo ya kura za maoni yaliahirishwa kutangazwa kutokana na kuwepo kwa tuhuma za kuwapo kwa wizi wa kura. Kwa jimbo la Tarime Mjini, Lugola alifafanua kuwa Michael Kembaki ndiye aliyeibuka mshindi kwa kura 3,908 akifuatiwa na Kabaka aliyepata kura 2,411.
Katika Jimbo la Tarime Vijijini, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Christopher Kangoye ambaye amejaribu zaidi ya mara tatu kuusaka ubunge, lakini bila mafanikio aliibuka mshindi akivuna kura 15,928 dhidi ya 12,205 za John Gimunta ambaye ni Mweka Hazina wa CCM wilayani Tarime.
Nyangwine na Gimunta, baadaye walilalamikia matokeo hayo wakisema mchakato wa kura za maoni ulitawaliwa na hujuma.
Kayombo azidiwa Mbinga Katika Jimbo la Mbinga Vijijini, matokeo yaliyotangazwa saa 5:45 usiku baada ya mvutano wa kutangaza matokeo unaodaiwa kudumu kwa takribani saa 12, yameonesha kuwa mbunge wa jimbo hilo aliyekuwa amejitokeza kutetea kiti chake, Gaudence Kayombo ameshindwa katika kura za maoni ndani ya CCM.
Aliyeibuka mshindi ni Martin Msuha, aliyepata kura 13,354 dhidi ya 12,068 za Kayombo, ambaye pia kwa mwaka mmoja na nusu kati ya Januari 12, 2007 na Agosti 2, 2008 alikuwa Naibu Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji.
Wengine walioshiriki katika mchakato wa ubunge jimboni humo na kura zao kwenye mabano ni Humphrey Kisika (545), Dk Silverius Komba (1,289), Edesius Kinunda (2,355), Deodatus Mapunda (2,532), Benaya Kapinga (3,941) na Deodatus Ndunguru.
Wabunge Singida hoi MCHUANO wa makada mbalimbali wa CCM kuwania nafasi za ubunge katika mkoa wa Singida umekamilika, huku wabunge waliokuwa wakitetea nafasi zao na baadhi ya vigogo kwenye chama hicho wakiwa wamebwaga vibaya.
Kwa mujibu wa Kaimu Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Mary Maziku, wabunge wawili waliokuwa wakitetea nafasi zao hawakuweza kupata kura za kutosha kwenye kura za maoni. Nao ni Salome Mwambu wa Jimbo la Mkalama na John Lwanji wa Manyoni Magharibi.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai ambaye aligombea jimbo la Mkalama alifanikiwa kushika nafasi ya pili kwenye kinyang’anyiro hicho kwa kupata kura 3,908 nyuma ya Allan Kiula aliyezoa kura 5,823. Jimbo hilo lilikuwa na wagombea 16.
NIPASHE
Rais Jakaya Kikwete, amesaini miswada mitano ya sheria, iliyopitishwa na Bunge la 10 Julai, mwaka huu.
Imo iliyozua tafrani na kusababisha wabunge 45 wa Ukawa kutimuliwa bungeni na wengine kususia mkutano wa 20.
Katika tukio la kihistoria lililofanyika Ikulu, jana na kuhudhuriwa na mawaziri, watumishi wa wizara na wadau wa mafuta na gesi, Rais alisaini miswada hiyo baada ya mawaziri husika kuwasilisha maelezo ya miswada hiyo.
Miswada hiyo ni wa sheria ya mafuta, sheria uwazi na uwajibikaji katika rasilimali za madini, mafuta na gesi asilia, muswada wa sheria ya mapato yatokanayo na mafuta na gesi pamoja na muswada wa sheria ya Tume ya walimu.
Vile vile muswada wa sheria ya usimamizi wa masoko ya bidhaa yote ya mwaka 2015.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema tukio hilo ni la kihistoria kwa Tanzania kwa miswada mitano kusainiwa katika hadhara kubwa ya watu.
Alisema miswada ya sheria ya gesi na mafuta inaweka utaratibu mzuri wa kimfumo, kisheria na udhibiti mzuri wa kusimamia uchumi wa gesi na mafuta, kujibu kilio cha Watanzania kuwa rasilimali ziwanufaishe na kizazi kijacho.
Balozi Sefue alisema pia watanzania wataunganishwa na ulimwengu wa gesi kwa biashara watakazoanzisha na kutekeleza katika uchumi huo, ikiwa ni pamoja na kuwa na uchumi nyumbulifu katika kulinda mahitaji ya vizazi vijavyo na cha sasa.“Tunafanya walichofanya wengine duniani na kuepuka yaliyoleta matatizo katika nchi nyingine,” alisema Balozi Sefue.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene, alisema muswada wa sheria ya mafuta unalenga kuleta sheria mpya ya kusimamia sekta ndogo ya mafuta nchini kwenye masuala ya utafutaji; uendelezaji; uzalishaji; usafirishaji; uagizaji; uchakataji; uhifadhi na biashara ya mafuta na gesi asilia nchini.
“Malengo ya muswada wa sheria ni kuimarisha usimamizi wa sekta ili kuhakikisha maslahi ya nchi katika tasnia ya mafuta yanalindwa kikamilifu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo, kuweka mfumo madhubuti wa kisheria utakaoimarisha usimamizi wa shughuli za mafuta katika mkondo wa juu, wa kati na wa chini kupitia sheria moja,” alisema  na kuongeza:
“Masuala muhimu ni kuweka utaratibu ambao serikali ya Muungano na ya Mapinduzi ya Zanzibar zitashirikiana katika shughuli za utafutaji, uchimbaji na uendelezaji wa vitalu vya mafuta na gesi katika yaliyo kwenye maeneo yanayugusa pande zote mbili,” alibainisha.
Simbachawene alisema sheria hiyo itawezesha kuanzishwa kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (Pura) ambayo itasimamia shughuli zote za udhibiti katika masuala ya kiufundi na kibiashara katika mkondo wa juu.
NIPASHE
Mbunge wa Mkuranga mkoani Pwani, ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha,  Adam Malima, amesema kuwa kura za maoni zilizopigwa jimboni humo hazikuwa huru na haki kwa madai kwamba waliopiga kura walikuwa wachache lakini kura za matokeo zikawa nyingi.
Malima ambaye alisema kuwa hakuridhishwa na mwenendo mzima wa kura za maoni kwa vile umechukua siku tatu bila mawakala kusaini fomu za matokeo.
Matokeo ya kura za maoni katika jimbo hilo yalitangazwa juzi usiku, huku Malima akiwaambia wananchi na wapambe wake wasifanye fujo na kuwataka warudi nyumbani na kwamba vikao vya juu vya maamuzi vitatoa jina la nani apeperushe bendera ya chama.
“Mchakato uligubikwa na udanganyifu mkubwa, kura haziendani na uhalisia, pia mawakala hawakutia saini baada ya kumalizwa kwa upigaji kura katika vituo vyao, lakini ninaviachia vikao vya maamuzi vifanye kazi yake,” Malima.
Alisema kuwa ana nafasi nyingi ndani ya chama na miongoni mwa watu walioaminiwa na Rais Jakaya Kikwete kuandaa ilani ya uchaguzi, na kuwa anashangaa kusikia kuwa hawezi kuwaletea wananchi maendeleo katika jimbo hilo.
“Watu kama hao ni timu za wenzangu ambazo zinatumika kusema eti wataenda upinzani, siwezi kuzuia kambi zisiongee kitu chochote, lakini mimi sihami CCM ingawa kura hizi zina walakini,’” alisema.
Akitangaza matokeo hayo, Mkurugenzi wa  Uchaguzi ambaye pia ni Katibu wa CCM wa Wilaya hiyo, Hadija Kusaga, alisema kuwa waliojiandikisha kupiga kura walikuwa 46,904, kura zilizopigwa ni 26,949 na kwamba kura 904 ziliharibika.
Alisema kuwa katika matokeo ya kura hizo, mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, Abdallah Ulega, aliibuka na ushindi kwa kupata kura 16, 294 huku Malima akipata kura 8, 212.
NIPASHE
Mgombe urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Pombe Magufuli jana alichukua fomu za kuwania nafasi hiyo huku Mwenyeti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, akiwaasa wanachama wa chama hicho wasimpuuze adui yeyote katika uchaguzi mkuu mwaka huu na kutamba watafunga magori uwanjani huku wapinzani wakiwatazama.
Magufuli alichukua fomu hizo katika ofisi za Tume ya Taifa ya  Uchaguzi (Nec) kwa mbwembwe akiwa kwenye msafara wa magari, pikipiki, matarumbeta na muziki.
Akizungumza na wanachama wa CCM jana mchana katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam, Rais Kikwete aliwasihi wanachama wa chama hicho kutodharau adui yeyote watayepambana naye katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Licha ya Rais Kikwete kutofafanua kauli yake hiyo, katika uchaguzi mkuu ujao CCM inatarajia kupambana vikali na mgombea urais kupitia Ukawa, Edward Lowassa aliyehama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) hivi karibuni.
Lowassa alikihama CCM huku akisema kwamba ameamua kufanya hivyo kutokana na kubakwa kwa demokrasia ndani ya chama hicho kikongwe nchini.
Kikwete alisema katika uchaguzi wa mwaka huu, chama hicho kitafunga magori uwanjani huku upinzani ukitazama na kwamba kitapata ushindi wa kishindo na hilo hana wasiwasi nalo.
Rais Kikwete jana alionekana mwenye furaha muda wote huku akiomba kikundi cha kwaya cha TOT, kimuwekea wimbo wa ‘acha waseme CCM kina wenyewe, shangilia ushindi unakuja’.
Wakati wimbo huo ukipigwa, Kikwete aliamua kuucheza akiwa jukwaani huku akishangiliwa na wananchi waliokusanyika katika ofisi za CCM.
Hata hivyo, Rais Kikwete hakuzungumzia juu ya kuondoka  Lowassa ndani ya CCM, na kwenda kujiunga na Chadema kisha kuteuliwa kugombea urais kupitia umoja huo.
Alisema dunia nzima inajua maendeleo mazuri yaliyofikiwa kupitia utawala wake na kwamba katika kampeni watakwenda kuwaeleza wananchi mambo mazuri yaliyofanywa.
Alijivunia maendeleo makubwa yaliyopatikana katika utawala wake na kusisitiza kuwa anaondoka madarakani huku akiiacha nchi ikiwa na amani, umoja na mshikamano.
Wakati wa kwenda kuchukua fomu ya kugombea urais, Dk. Magufuli jana aliambatana na mgombea mwenza, Samia Suluhu Hassan kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), huku wakisindikizwa na viongozi mbalimbali waandamizi wa CCM.

04 August, 2015

For Men- The Jaeger A/W '15 Campaign

Among the best brands to follow and purchase from, is Jaeger. Their classic cloth lines includes the usage of the world's finest cashmere and even camel hair! I like their 1880's fabric and the consistency in their designs


For the Autumn/ Winter 2015 collection, Jaeger stocks its tweed blazers and their signature camel coat, among others
Clean cuts,amazing!
Tanzanian Designers on male clothes, be Inspired

For more, visit their site Jaeger.co.uk 

NEW AUDIO: MAYUNGA NICE COUPLE

RadekArtPhoto-5780Yule mshindi wa Airtel Trace Music Star Mayunga ametuletea audio yake iitwayo NICE COUPLE chukua time yako adhim kuidowload nakushare na wana DOWLOAD HAPA

Ripoti ya TFDA kuhusu idadi na thamani ya vipodozi vilivyoteketezwa 2014/15…(Audio)

fekiiii
Mmlaka ya chakula na Dawa TFDA imeatoa ripoti ya mwaka wa fedha kuhusu bidhaa mbalimbali zilizokamatwa na kuteketezwa kwa mujibu wa sheria na hatua zilizochukuliwa.
Mkurugenzi wa TFDA Hitti Sillo amesema  katika mwaka wa fedha wamekamata na kuteketeza vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku tani 16.61 ambazo thamani yake ni shilingi milioni 44.2.
‘Vipodozi ambavyo vimepigwa marufuku vilivyoingizwa tumekamata vikiwa vinaingizwa nchini na vingine vimekutwa katika soko vikiwa tayari vimeingizwa na vingine vikiwa njiani  kuingizwa nchini, mara nyingine tumekamata mabasi yakiwa na vipodozi vinavyoingizwa nchini  kinyume cha sheria vyote hivyo thamani yake kwa mwaka wa fedha uliopita ni shilingi milioni 44″ Sillo.
Amesema kazi hiyo ni endelevu kwa kuwa TFDA ipo sehemu mbalimbali nchini na wakaguzi wake wapo kuanzia bandarini na katika viwanja vya ndege ambapo ndipo hukamataa bidhaa nyingi.
Amesema miaka mitatu iliyopita udhibiti umeimarika sana ndio maana matukio mengi ya kukamatwa kwa watu ambao wanaingiza vipodozi hatari kinyume cha sheria wanakamatwa wakiwa mipakani.

Samsung kurejesha fedha kwa wanunuzi wa Note 7

KAMPUNI ya Vifaa vya Elektoriniki ya Samsung ya Afrika Mashariki (SEEA) itarejesha fedha kwa wateja wa simu za Note 7, ambao wataweza kuthib...